Alibaba

samedi 29 mars 2014

HIVI NDIVYO BONGO MOVIE WALIVYOSHEREHEKEA BETHIDEI YAO

Shilole katika picha ya pozi kwenye zulia jekundu ‘red carpet’.
Shamsa Ford akihojiwa kwenye zulia jekundu.
Baadhi ya wasanii wa Bongo Movie Unity wakiingia ukumbini.
Sandra (kushoto) na Eshe Buheti wakiwa kwenye zulia jekundu.
Wasanii na mashabiki wao wakicheza muziki.
Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Nyerere’ akizungumza machache mbele ya watu waliohudhuria.
Steve Nyerere akikata keki.
Jana ilikuwa ni siku ya furaha kwa wasanii wa Kundi la Bongo Movie Unity waliokuwa wakisherehekea kundi hilo kutimiza miaka mitatu tangu lilipoanzishwa.
Sherehe za kumbukumbu hiyo zilifanyika kwenye Ukumbi wa Arcade, Mikocheni jijini Dar ambapo wasanii walianza kwa kupiga picha kwenye zulia jekundu ‘red carpet’ na watu kibao waliohudhuria.
Kwa upande wa burudani ya muziki, wanamuziki Linex, Amini, Pendo wa Maisha Plus, Shilole, Bendi ya Fm Academia na Bendi ya BM walitoa burudani ya aina yake na kusababisha ukumbi wote kulipuka kwa shangwe.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire