Alibaba

mardi 31 décembre 2013

le coq de retour dans le bon sens sur le maillot des Bleus pour le Brésil

Un bon présage?

Image promotionnelle pour le nouveau maillot des Bleus
LU SUR...
OUTILS
> taille du texte
Mercredi 20 novembre, au lendemain de la belle qualification de l'équipe de France de football pour la Coupe du monde au Brésil, son équipementier Nike a présenté le maillot avec lequel les Bleus vont défendre les couleurs de la France l'été prochain. Après avoir sévèrement critiqué des joueurs trop payés et pas assez motivés à la suite de la défaite 2-0 au match aller face à l'Ukraine, le pays était dans l'euphorie générale et l'annonce est passée quelque peu inaperçue.
On a tout de même eu le droit à quelques articles évaluant les qualités esthétiques de la nouvelle tenue, comme la bonne idée d'un retour à la combinaison traditionnelle maillot bleu-short blanc-chaussettes rouges, ou regrettant son prix excessif (120 euros)  et sa coupe trop moulante. Eurosport a fait son travail d'attaché de presse de journaliste en soulignant que «les designers de Nike se sont inspirés de l'histoire de la ville de Nîmes, surnommée "la Rome française" et qui est le berceau du "denim"» et ont «étudié la cartographie des points de tension des joueurs pendant les matches en analysant les endroits où ces sportifs sollicitaient le plus leurs tenues».
publicité
Mais un détail primordial, qui avait jusqu'ici échappé à tous, vient d'être rélevé par le blog «Panthéon foot» de L'Express, plus d'un mois après la sortie de la tunique: l'orientation du célèbre coq gaulois, symbole de l'équipe de France depuis toujours ou presque, a changé. Et le détail n'a rien d'anodin.
Du début du siècle jusqu'en 2006 inclus, période qui contient incontestablement les plus belles heures du foot français avec les victoires aux Championnats d'Europe de 1984 et 2000 et celle à la Coupe du monde 1998, le coq était orienté vers l'intérieur (ou vers la droite pour le joueur).

Zinedine Zidane devant Junior Baiano lors de la finale de la Coupe du monde de football France-Brésil le 12 juillet 1998 au Stade de France à Saint-Denis, REUTERS/Paulo Whitaker
Puis, après la défaite en finale du mondial 2006, le coq a mystérieusement changé d'orientation pour regarder vers l'extérieur (ou vers la gauche pour le joueur), changement correspondant à une période sombre de l'équipe de France: deux élimination en phase de poule à l'Euro 2008 et au Mondial 2010 et des polémiques à la pelle sur le comportement des joueurs, de l'épisode du bus de Knysna à celui des insultes de Nasri en 2012 (pour un aperçu de tous les maillots portés par les Bleus depuis 50 ans, c'est par ici).

Thierry Henrry lors de France-Afrique du Sud à Bloemfontein, en Afrique du Sud, le 22 juin 2010 , REUTERS/Adnan Abidi
Les superstitieux ne manqueront pas de voir dans ce retour à l'orientation de coq gagnante un bon signe pour l'aventure brésilienne des Bleus l'été prochain.

lundi 30 décembre 2013

KUMBUKUMBU YA SAJUKI... BONGO MOVIE WAMFANYIA MBAYA WASTARA


Wastara Juma akiwa na simanzi wakati wa dua maalum ya kumbukumbu na kumuombea mumewe.
Stori: Brighton Masalu na Deogratius Mongela
DUA maalum ya kumbukumbu na kumuombea aliyekuwa msanii wa filamu Bongo, Marehemu Juma Issa Kilowoko ‘Sajuki’ imezua minong’ono mingi kufuatia wasanii wengi wanaounda Kundi la Bongo Movie kudaiwa kumfanyia mbaya mkewe, Wastara Juma kwa kutohudhuria, Ijumaa Wikienda lilikuwepo.
Kaburi la marehemu Sajuki.
Dua hiyo ya ilifanyika Jumamosi iliyopita nyumbani kwa marehemu Tabata-Bima, Dar na kumalizikia kaburini kwake Kisutu.
Katika tukio hilo, wadau mbalimbali wa filamu na burudani, walionekana kushangazwa na kitendo cha wasanii wengi wa Bongo Movie kutokuwepo licha ya marehemu Sajuki kushirikiana nao kwa karibu enzi za uhai wake.
Aidha, wengine walifika mbali kwa kuhoji kulikoni wafanye hivyo, maswali ambayo yalimuongezea uchungu mkubwa Wastara aliyekuwa akibubujikwa machozi mara kwa mara.
Wastara akilia wakati wa kumbukumbu ya mumewe.
Kwa upande wake, Wastara alisema anamshukuru Mungu kwa kufanikisha shughuli hiyo na kuwaombea kwa Mungu wote waliojitokeza kumuunga mkono kwenye dua hiyo.
“Nawashukuru wote waliojitokeza, wamenifariji sana,” alisema Wastara kwa simanzi.
Wasanii wa filamu waliohudhuria dua hiyo, ni pamoja na Denis Sweya ‘Dino’, Ahmed Olotu ‘Mzee Chilo’, Flora Mvungi, Hamis Ramadhan ‘H. Baba’ na Suleiman Bin Sinan ‘Bond’.
Mwenyekiti wa Bongo Movie, Vincent Kigosi ‘Ray’ alipotafutwa, simu iliita bila kupokelewa.
Sajuki alifariki dunia Januari 2, 2012 na katika kutimiza mwaka mmoja kaburini misa nyingine itafanyika nyumbani kwa wazazi wake mkoani Songea Januari 2, 2014.

samedi 28 décembre 2013

swahili love sms


Uzuri wa usiku si giza lifunikalo dunia wala si kimya kinachotawala mazingira bali ni njozi njema zenye maono na matarajio yenye mafanikio. Nakutakia ucku mwema
*°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
Naituma  sauti yangu"" izunguke"" moyo"" wako kwa""upendo"" iuguse"" uso"" wako""kwa"" busu""na"" mwisho""ikunong'oneze"" sikioni"" taratiiiiibu"" Gd9t
    *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
mpnz wangu ninavyo jua mm huwezi kutupa mawe kwenye mti usiokuwa na matunda mazuri maana hivyo basi tambua ww ni mrembo xanandani ya moyo wangu usiniache pekeyangu kwani na kupenda xana tabua hilo mpnz wangu
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
Niseme nini ujue nakupenda? Nifanye nini ujue nakupenda? Nikuite jina gani ujue ni wewe peke yako upo moyoni mwangu? Hakika hakuna ila moyo wangu ndio naosema kuwa nakupenda, niamini mpenzi!
       *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
nina mambo saba ya kukuambia ,lakini kwa sasa nakumbuka 6tu,bila shaka matano ndio muhimu kwa leo ,ila unayopaswa kujua ni manne kwa sasa ,oooh usijali nitakuambia ma3 tu,ila kwa jinsi ulivyo naona nianze na ma2 muhimu,ila yatakugusa sana na kwa kuwa sipendi kukuumiza naomba niseme moja tu .mchana mwema dia
       *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
kwa hakika inzi hufia kidondoni,shujaa vitani ,mtaliii mbugani ,je mwenye penzi la dhati hufia kwa ampendaye?
       *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
upendo sio tigo eti ongea kwa nusu shilingi wala sio voda kazi ni kwako, pia sio airtel jisikie huru bali upendo ni zawadi pekee sana mungu aliyoiweka ndani ya mioyo yetu.hili ni la kuzingatia dear nakupenda sana
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
yakumbuke haya sana katika maisha yako wahurumie wenye kukupenda hasa mwenye pendo la dhati kama langu,wapende wanaokupenda japo kwa chembe ya upendo,thamini pendo la akupendae kwa kila mara japo sekunde moja.     
       *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
nalia ukiwa mbali, nachukia nisipo kuona ,najuta ninapo kuudhi ,naumia unapo nitenga , nateseka ukiwa kimya ,nafurahi ukinikumbuka, nakupnda mpz
   ●´¯`´¯`●♥¡¡♥●´¯`´¯`●♥
utamu wa penzi hunogeshwa na pendo la dhati pia utamu wa penzi ni uwepo wangu na wako,ladha yake ni zaidi ya nazi kwenye wali au royco kwenye mchuzi au pilipili kwenye kachumbari, utamu wake ni zaidi ya asali au jam kwenye mkate ,blueband kwenye uji.penzi tamu halina kifan
 *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
nimegundua dawa ya maisha ukinichukia nakupenda,ukiniudhi nakufurahisha,ukinisahau nakukumbuka,ukikaa kimya nakusalimia,na ukinisahau kuniombea kwa ALLAH nitakukumbusha.
          *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°
najua mimi sio wa kwanza kukuombea mema ,ila napenda kuwa ni mmoja kati ya  wanaokutakia asubuhi njema.
           *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°

unaweza ukafunga macho kwa usilolitaka kuliona lakini hauwez kufunga moyo wako kwa Unalo Lipenda. Nakupenda Mpenzi

        *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
upepo wangu wakupuliza wewe kutokana na joto kali usijaribu kwa kuvaa sweta ukapunguza ukali ninachotaka mi nikuwa na wewe naomb unielewe .
        *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
Uzuni ,upole,ukarimu wanakusalimia. Furahana unyenyekevu wapo njiani wanakujakwako .ila taabu nashida hawatakuja kwasababu wote wanaumwa.mawazo mashakana kukata tamaa wapo jela.ushindi utajiri na amani wapo njiani wanakuja gday
         *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 rafiki mwaminifu ni mlinzi mahiri na aliyempata amepata hazina isiyokuwa na kifani,ahsante kwa kuwa rafiki mwaminifu.
         *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
     usiku huu tulivu nikiwa nimejilaza kitandani natamani nisikie sauti yako ambayo hunikosha na kunikosesha raha nisipoisikia.uwembamba Wa Sauti Yako Hupenya Kwenye Ngoma Ya Masikio Yangu Hunitekenya Na Kuniacha Nikifurahi. Nakupend Wangu Kipenzi
         *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
   maumivu ya kulipoteza penzi lako ni kubwa,lakini ni makubwa zaidi baada ya kugundua haukuwa yule nileyedhani. inaniuma sana
         *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
     maneno million  haliwez kulirudisha pendo lako najua kwasababu nimejaribu,pia machozi million haliwez kulirudisha najua kwasababu nimelia.
        *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
Kuna miezi 12 katika mwaka…siku 30 katika mwezi…siku 7 katika wiki, masaa 24 katika siku…dakika 60 katika saa……lakini wewe ni mmoja tu maishani mwangu.
        *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*

Kuna vitu viwili zinavyoniamsha asubuhi na mapema: Alamu ya saa yangu na wewe

        *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
Bongo zenye fikra kali huwa na mawazo, suluhu na sababu; ubongo wa kisayansi huwa na kanuni, nadharia na takwimu; wangu una wewe tu!
        *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
Penzi linaweza kuelezewa kwa namna nyingi. Namna moja niijuayo nikumtumia mapenzi hayo mtu asomaye meseji hii.
        *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
Kama ningeweza kubadili herufi, ningeweka yangu na yako kuwa pamoja
        *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
Umewekwa usiku ili tuweze tuukubali mchana, huzuni ili tuikubali furaha, ubaya ili tuukubali uzuri, wewe ili niyakunali mapenzi.
        *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
Mapenzi ni nini? Wale wasiopenda huita majukumu, wale wanaoyachezea huita mchezo, wale wasiokuwa nayo huita ndoto, na wale wanaoelewa huyaita mwisho wa safari, na mimi, mwisho wangu ni wewe.
        *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
Ni mapenzi gani yanayofanya simu yako ilie kila nitumapo meseji?
        *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
Unaonekana kung’ara leo nilijuaje…….ni kwasababu unaonekana hivyo kila siku
        *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
Kama mapenzi huweza kukimbiwa kwa kufumba macho yetu tu, basi nisingefunika macho kabisa. Sitaki sekunde ipite bila kukupenda wewe.
        *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
Nilikuwa nikifiria kwamba ndoto haziwezi kuwa kweli, lakini nilibadili mawazo yangu pale tu nilipokuona wewe.
         *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
Baadhi ya watu huzaliwa na vipaji. Huweza kufanya mambo mazuri kwa ujuzi wao, lakini hamna anayekufikia wewe, kwani ukinisogelea tu kila kitu huwa kizuri.
         *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
Mwanamke ni yule amfanyaye mwanamme auhisi uanaume wake, wewe ni mwanamke mwenye sifa hizo.
         *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
Kukusahau wewe ni ngumu lakini kunisahau mimi ni juu yako. Usinisahau kamwe, unaweza kuisahau meseji hii, lakini si mtumaji.
         *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*

DIAMOND, WEMA WATANGAZA NDOA

Stori: Shakoor Jongo na Imelda Mtema
HUKU mchumba’ke, Penniel Mungilwa ‘Penny’ akifungasha virago kurejea kwao, mzee mzima Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ametangaza kumuoa Miss Tanzania 2006, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’.
Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’(kushoto) na Penniel Mungilwa ‘Penny’ wakiongea jambo enzi za mapenzi yao.
Ishu hiyo ilijiri ndani ya Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar ambapo mkali huyo wa Bongo Fleva alikuwa akikamua kwenye sherehe ya Krismasi aliyoiandaa mwenyewe.
Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ baada ya kupanda jukwaani katika viwanja vya leaders.
TANGAZO LA AWALI
Awali kabla ya kufikia eneo la kutangaza kuoana, Diamond aliweka wazi jukwaani kwamba yeye na Wema wamerudiana.
Diamond Platnumz akiongea jambo baada ya Wema Isaac Sepetu ‘Madam’  kupanda jukwaani.
MTIRIRIKO ULIVYOKUWA
Diamond, akiwa ameshika kipaza sauti alikatisha kuimba na kuwauliza mashabiki wake, hasa watoto waliohudhuria kwa wingi tamasha hilo, je, wanataka kumuona shemeji yao?
“Itakuwa si vizuri mkaondoka bila kumuona shemeji yenu, nikuleteeni mumuone?” aliuliza  Diamond. Swali hilohilo akalirudia tena ambapo lilipokelewa kwa shangwe huku mashabiki wakilitaja jina la Wema.
                                        Diamond Platnumz na Wema Isaac Sepetu wakijiachia.
WEMA APANDISHWA JUKWAANI
Kufuatia kelele za mashabiki, Diamond alimuomba Disco Joker (DJ) wake amuwekee Wimbo wa Ukimwona ambao ulisindikiza ujio wa Wema jukwaani akifuatana na wapambe wa Diamond.
“DJ acha huo, nipigie Wimbo wa Ukimwona watu wangu wa nguvu wamwone shemeji yao kwani tangu nilivyokwenda naye China walikuwa wakisumbuliwa na maneno tofautitofauti kutoka kwenye mitandao ya kijamii,” alisikika Diamond.
Diamond, akiwa ameshika kipaza sauti akiima Wimbo wa Ukimwona na Wema akiwa amemkumatia.
JUKWAA SASA
Hali haikuwa ya kawaida jukwaani kwani kilichofuata hapo ni Wema kuonesha kwa vitendo mambo yaliyoashiria kuwa, wawili hao sasa ni mwendo mdundo.
Wema alishuhudiwa akimzungushia mikono Diamond kwenye kiuno jambo ambalo liliwafanya baadhi ya mashabiki wa mastaa hao kutoa machozi ya furaha kuona penzi la wawili hao limerudi upya, wengine walimwambia Diamond amuoe Wema.
“Diamond muoe Wema, mnapendezana sana,” walisikika mashabiki.
Wema Isaac Sepetu ‘Madam’akimuaga Diamond Platnumz kwa kumkumatia.
MAWIFI WADAI KUHARIBIWA SIKU NA KAKA YAO
Hata hivyo, kitendo cha Diamond kumwita Wema jukwaani kilionekana kuharibu furaha ya sikukuu kwa ndugu zake kwani bila ya kuuma midomo dada zake staa huyo wakiongozwa na Esma Khan walinuna na kuanza kuondoka.
“Yaani siku yangu imeshaharibika, nilikuja nina furaha sasa imepotea, tuondokeni ndugu zanguni,” alisema Esma akiwaambia Mwanaisha Abdul ‘Queen Darleen’ na Halima Haroun ‘Kimwana’.

Diamond Platnumz na Penny wakiwa pamoja enzi za mapenzi yao.
MAMA DIAMOND ASHANGAA
Kitendo cha ndugu hao kukasirika hakikupokelewa vizuri na bi mkubwa wao yaani mama Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’ ambaye aliwajia juu akiwashangaa.
“Wajinga nini? Sasa walitaka Diamond… (tusi) wao, mtu ameshaamua kupenda wamwache, mi’ mwenyewe nimeshajifunza, sitaki kuingilia penzi lake,” alisema mwanamke huyo ambaye mjini anazungukia usafiri aina ya Altezza.
Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’  na Penniel Mungilwa ‘Penny’.
Baada ya shoo hiyo iliyomalizika saa moja usiku, paparazi wetu alimfuata Diamond akiwa amesimama na Wema na kuwauliza kama kweli wana nia ya kufunga ndoa.
“Hilo mwana mbona lipo wazi, nataka kumuoa staa na nataka kuzaa na staa,” alisema Diamond huku Wema akiwa hapingi.

MAMA WEMA ATANGAZA VITA  NA DIAMOND
Wakati Dimaond akitambia ndoa na Wema, siku hiyohiyo ya Krismasi, mama wa Wema, Mariam Sepetu alidaiwa kutangaza vita na mwanamuziki huyo baada ya kusikia tetesi kuwa amerudiana na mwanaye.
Kwa mujibu wa rafiki wa karibu wa mama Wema (jina tunalo) mama wa staa huyo alichukizwa na kitendo cha Diamond kurudiana na mwanaye kwani anaamini anamchezea tu.
Mama wa Wema, Mariam Sepetu.
Rafiki huyo alizidi kudai kuwa, taarifa hizo zimemuweka  mama huyo kwenye wakati mgumu na kudai kuwa popote atakapokutana na mwanamziki huyo atampopoa mawe au machungwa hata ikiwa siku ya ndoa yao.
“Mama Wema amesema hampendi Diamond, popote atakapomuona itakuwa vita ya wawili, kama kuna jiwe atamrushia, hata machungwa kama yapo yatakuwa halali yake,” alisema rafiki huyo.

WOSIA WA MZEE SEPETU
Mpashaji huyo wetu alizidi kufunguka kuwa, mama Wema ana wosia mkononi ambao aliuacha marehemu mumewe, mzee Isaac Abraham Sepetu.
Alisema katika wosia huo, mzee huyo alisema hataki Diamond amuoe Wema na kama mrembo huyo atakiuka  wosia huo atapatwa na laana mbaya katika maisha yake.
“Kinachomuumiza zaidi mama Wema ni huo wosia, mzee Sepetu alisema hataki mtoto wake aolewe na Diamond, kama atakataa kuna kitu kibaya kitamkuta katika maisha yake,” alisema rafiki huyo.

MAMA WEMA ASAKWA
Baada ya kupata habari hizo, gazeti hili lilimvutia waya mama Wema ili kuweza kuthibitisha madai hayo ambapo alisema kuwa, hayuko tayari kuzungumzia jambo hilo kwa wakati huo mpaka atapoamua akisisitiza muda si mrefu.
“Jamani nina mambo mengi sana ya kufanya na sijatulia kabisa siko tayari kuzungumza chochote kwa sasa nikiwa tayari nitawaambia kila kitu,” alisema mama Wema.

mardi 24 décembre 2013

Kalachnikov, inventeur du fusil le plus vendu au monde, meurt à 94 ans

Mikhaïl Kalachnikov, l'inventeur du légendaire fusil d'assaut soviétique AK-47, vendu à des millions d'exemplaires dans le monde, est mort lundi à l'âge de 94 ans.
"Le légendaire concepteur d?armes russe Mikhaïl Kalachnikov est décédé", a indiqué la société de fabrication d?armes Kalachnikov dans un communiqué, en déplorant une "perte irréparable".
Le président russe Vladimir Poutine a exprimé ses "profondes condoléances" aux proches de celui qui avait mis au point, sans en tirer aucun revenu à la hauteur du succès de son invention, l'arme automatique la plus répandue sur la planète, utilisée aussi bien par les armées régulières que par les guérillas.
Kalachnikov est mort des suites d'"une longue maladie" à Ijevsk, la capitale de la région d'Oudmourtie, à 1.300 kilomètres à l'est de Moscou, a précisé à l'AFP Viktor Tchoulkov, porte-parole des autorités de cette région de l'Oural.
Une commission des autorités locales doit se réunir mardi pour préparer l'organisation de ses funérailles, selon la même source.
"L'un des patriotes russes les plus brillants, les plus talentueux, les plus cohérents, qui a consacré toute sa vie à sa patrie, a perdu la vie", a déclaré le président d'Oudmourtie, Alexandre Volkov.
Né le 10 novembre 1919 dans un village de Sibérie, Mikhaïl Kalachnikov avait été hospitalisé à de nombreuses reprises ces derniers mois. En novembre, il avait été placé en réanimation dans une clinique d'Ijevsk après un malaise.
Il n'avait arrêté de travailler qu'en 2012 en raison de problèmes de santé, notamment cardiaques.
Petit homme soigné amateur de pêche, il fut l'un des Russes les plus connus du monde et les plus décorés dans son pays. Il avait toujours répété sa fierté pour l'arme meurtrière conçue en 1947 et dont il vantait la simplicité.
Arme la plus répandue de la planète, le fusil AK-47 aurait été vendu, selon certaines estimations, à 100 millions d'exemplaires.
Mais de l'aveu même de son inventeur, la majorité des kalachnikovs produites sont fabriquées en contrebande et leur vente échappe à tout contrôle.
Utilisée par plus de 80 armées
Mikhaïl Kalachnikov a commencé à mettre au point le fusil d'assaut AK-47, tandis qu'il se remettait d'une blessure reçue pendant la Deuxième guerre mondiale. L'arme a ensuite été déclinée en de multiples modèles.
"J'ai fabriqué des armes dans le but de défendre notre société", avait-il souligné lors de son 90e anniversaire en 2009, tout en reconnaissant que "ce n'est pas agréable de voir que toutes sortes de criminels tirent avec mes armes".
"Bien sûr que j'ai des regrets, comme tout le monde. Mais je peux vous dire une chose : si c'était à refaire, je ne vivrais pas autrement", avait-il conclu.
Le ministre russe de la Défense, Sergueï Choïgou, a salué en lui un "exemple éclatant de dévouement sans réserve à sa patrie". "Le nom de Kalachnikov constitue depuis des décennies l'une des marques les plus célèbres et demandées sur le marché mondial des armes", a-t-il déclaré.
C'était "un spécialiste remarquable des armes, comme il en naît un tous les 100 ans", a commenté pour l'AFP Igor Korotchenko, directeur du Centre d'analyse du commerce mondial d'armes dont le siège est à Moscou.
Mikhaïl Kalachnikov n'a jamais touché d'argent sur la vente des millions de fusils portant son nom et utilisés par les armées de plus de 80 pays.
La kalachnikov est devenue le symbole de la lutte armée pour l'indépendance, et orne de nombreux drapeaux, dont celui du Mozambique et celui du mouvement chiite libanais Hezbollah.
La célèbre arme automatique est produite par l'ex-usine d'Ijmach, dans la ville d'Ijevsk.
Critiquée par son inventeur pour sa mauvaise gestion et ses bas salaires, elle a depuis été reprise par la holding publique Rostec et renommée "société Kalachnikov" cette année en l'honneur de son plus célèbre employé.
Déporté avec sa famille à l'âge de 11 ans pendant les répressions staliniennes, le militaire était devenu délégué aux congrès du Parti communiste de l'URSS.
Il avait confié en 2000 à l'AFP être très affecté par la disparition de l'Union soviétique et n'hésitait pas à défendre le système communiste "où tout n'était pas si mauvais".
Le chef du parti libéral-démocrate russe, l'ultra-nationaliste Vladimir Jirinovski, a regretté sur Twitter la disparition d'une "légende", "symbole de la fierté du pays".

lundi 23 décembre 2013

DIAMOND,PENNY WAMWAGANA!


Stori: shakoor jongo na mayasa mariwata.
NDIYO habari ya ‘mujini’ kwa sasa, kwamba staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul Juma ‘Diamond Platnumz’ na mwandani wake, mtangazaji wa kituo cha runinga cha DTV, Penniel Mungilwa ‘Penny’ wamemwagana, Risasi Jumamosi limemwagiwa upupu.
Penniel Mungilwa ‘Penny’ na Nasibu Abdul Juma ‘Diamond Platnumz’ wakiwa pamoja katika pozi.
KAMA UTANI, WEMA ATAJWA
Kwa sharti la kutotajwa mahali popote, ‘mtonyaji’ wetu ambaye ni mtu wa karibu wa wawili hao aliliambia gazeti hili kuwa chanzo cha Diamond na Penny kuingia kwenye listi ya ‘zilipendwa’ kilianza kama utani.
Awali ilidaiwa kuwa kila mmoja amekuwa akijiona mwenye thamani mbele ya mwenzake huku Wema Sepetu naye akidaiwa kuwa chanzo.
                                Nasibu Abdul Juma ‘Diamond Platnumz’ akiwa na Wema Sepetu.
“Hakuna penzi tena kati yao, wameachana na kila mmoja yuko kivyake.
“Walianza kama utani, unajua wale kila mmoja anajiona yuko juu kuliko mwenzake, lakini kitendo cha Diamond kuripotiwa kutoka na wanawake tofauti mara kwa mara hasa Wema, kimemchosha Penny ndiyo maana ameamua kujiweka pembeni kuepuka msongamano.
“Kupangwa kama mafungu ya nyanya inahusu?” alihoji ‘kikulacho’ huyo ambaye ni rafiki wa Diamond.

RISASI MZIGONI
Baada ya kutojiridhisha moja kwa moja na taarifa za awali kutoka kwa rafiki huyo, timu ya gazeti hili kwa kuwatumia ‘wahangaikaji’ wake maalum, iliingia mzigoni kupeleleza ukweli juu ya tetesi hizo.
Watu kadhaa walio chini ya Wasafi Classic Baby (WCB) ambayo rais wake ni Diamond walihojiwa ambapo majibu yalikuwa yaleyale kwamba, kwa sasa Diamond na Penny imebaki stori!

 SHAKA ILIPOANZIA
Wakati timu yetu ikiendelea na uchunguzi wake makini juu ya uvumi huo, hivi karibuni Diamond alionekana ‘singo’ kwenye pati ya kusherehekea siku ya kuzaliwa ya ‘dada wa mjini’, Halima Haroun ‘ Halima Kimwana’ ambayo aliiandaa Diamond.
Minong’ono ya kuhoji kutoonekana kwa Penny ilisikika ndani ya Ukumbi wa Business Park, Kijitonyama jijini Dar ilikofanyikia pati hiyo iliyojaa vitendo vya ufuska.
“Haiwezekani leo rais (Diamond) akajiachia peke yake bila Penny. Si kawaida ya Diamond.
“Kwa vyovyote watakuwa wameshamwagana kwa sababu kwenye pati zote huwa wanakuwa pamoja tangu walipoanza uhusiano wa kimapenzi,” alisikika mmoja wa waalikwa katika sherehe hiyo.
Katika tukio hilo, Penny alipigiwa simu na paparazi wetu na kujibu kwa kifupi: “Naumwa. Halafu si lazima nije kwani kila mtu ana ratiba zake.”
                                                                Penniel Mungilwa ‘Penny’.
PENNY KIZIMBANI TENA
Baada ya kukamilisha udadisi huo kupitia kwa watu wao wa karibu, gazeti hili lilianza na Penny kwa kumuuliza undani juu ya habari hiyo lakini alionekana kuwa ‘mzito’ kwa kutoingia ndani kulizungumzia sakata hilo huku akiahidi kulifungukia muda wowote kuanzia sasa.
“Kwa sasa sina cha kuzungumza juu ya hilo, nitalizungumzia muda wowote tena si siku nyingi zijazo, lakini si leo, tafadhali sana,” alijibu Penny kwa kifupi na sauti ya chini iliyojaa uchovu.
Paparazi: “Hebu nisaidie, mko wote au hamko wote?”
Penny: “Nimesema sitoweza kusema lolote kwa leo, subirini.”
                                               Nasibu Abdul Juma ‘Diamond Platnumz’.
DIAMOND KIMYA
Alipotafutwa Diamond kwa njia ya simu yake ya kiganjani, hakupokea licha ya kupigiwa mara kadhaa kwa namba zake zote. Akatumiwa meseji yenye maelezo yote, hakujibu.

MAMA DIAMOND
Ili kujiridhisha na madai hayo, waandishi wetu walimtafuta mama mzazi wa Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’ ambaye alisema hajui na hana taarifa hizo.

NDUGU WA KARIBU SANA
Baada ya mama Diamond, paparazi wetu alimpigia simu ndugu wa karibu sana na Diamond, sikiliza:
Paparazi: “Kumbe Diamond na Penny wamemwagana we huniambii. Sasa wifi yako mpya ni nani?”
Ndugu: “Aka! Sikwambii. Kwanza mi nipo mbali, sipo Dar.

WADAU WANAJUA
Haikuishia hapo, timu yetu ilizungumza na wadau mbalimbali ambao walionesha kusikitika huku baadhi yao wakisema walitabiri tangu awali.
“Duh! Penny ameachia ngazi mwenyewe. Sisi tulijua hawawezi kufika mbali, maana penzi lenyewe lilikuwa na mbwembwe nyingi,” alisema mwanamke mmoja anayejua kila kitu.

TUJIKUMBUSHE
Siku za hivi karibuni Diamond alifanya mahojiano kwa njia ya mtandao mmoja wa kijamii ambapo moja kati ya maswali aliyoulizwa ni pamoja na mpango wa kuoa ambapo alisema kuwa hana mpango huo kwa sasa na hatarajii kumuoa yeyote kati ya wanawake wanaotajwa kwa sana midomoni mwa watu (akiwemo Penny).
Wema alipigiwa simu juzi, lakini simu yake ilikuwa ikiita ‘weee’ mpaka inakatika, inaita ‘weee’ mpaka inakatika.

DAYNA: SITAKI MALUMBANO NA DIAMOND

Na Gladness Mallya
MWANADADA anayetamba na kibao cha Mimi na Wewe, Mwanaisha Said Nyange ‘Dayna’ amefunguka kuwa hataki kabisa kumzungumzia msanii mwenzake, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Mwanaisha Said Nyange ‘Dayna’.
Dayna aliyasema hayo hivi karibuni alipoulizwa kuhusiana na bifu lake na Diamond lililotokana na kumwibia wimbo wake ambapo alisema hataki kumzungumzia kabisa Diamond kwa sababu hataki malumbano kwani hivi karibuni amezungumza maneno mbofumbofu kwenye vyombo vya habari.
Nasibu Abdul ‘Diamond’.
“Mimi sitaki malumbano na Diamond  kwa sababu amekuwa akizungumza mengi sana kwenye vyombo vya habari mengine ya kuniponda na mengine ya kawaida hivyo sitaki malumbano kabisa mimi niko kikazi zaidi yeye aendelee tu”, alisema Dayna.