Alibaba

mardi 1 juillet 2014

hukumu ya kufunga siku ya ijumaa mosimosi pekee hatahata na inapo angukia ashuraaashuraa au arafaa


Swali LA KWANZA:

Assalamu Alaykum Warahmatullahi
Wabarakatu.
Shukran kwa kazi zenu munazofanya
kuelimisha umma.
Tumeelezewa kwamba haifai mtu kufunga
saum ya sita katika siku ya jumamosi, je hii
ni sawa. Je ikiwa nafunga saum ya 13, 14 &
15 ikiangukia jumamosi nifunge au vipi?
Shukran


SWALI LA PILI:
Eti kufungua Jumamosi haifai hata ikiwa ni
siku ya Arafa au Ashoora?


JIBU:


Sifa zote njema Anastahiki Allaah
(Subhaanahu wa Ta'ala) Aliyetukuka Mola
Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na
salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume
Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi
wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake
(Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu
wema mpaka Siku ya Mwisho.
Ahsante kwa ndugu zetu waliouliza
maswali hayo ambayo kwa nyakati za
karibuni limeleta utata sana baina ya
Masheikh na pia Waislamu wa kawaida.
Utata huu umesababishwa na kufahamika
Hadiyth hii kuwa ni ya makatazo katu, nayo
inasema:

Kutoka kwa 'Abdullaah bin Busr kutoka
kwa kaka yake kwamba Mtume (Swalla
Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)
kasema: ((Msifunge siku ya Jumamosi
isipokuwa ikiwa mmefaridhiwa na Allah
kwenu. Ikiwa mtu hakupata chochote cha
kula isipokuwa ganda la zabibu au gome la
mti, basi alitafune)) [at-Tirmidhy, Abu
Dawud, an-Nasaaiy, Ibn Maajah, Ahmad na
al-Haakim). Al-Haakim anasema kuwa hii ni
Hadiyth Sahihi kulingana na sharti za
Muslim na at-Tirmidhy akasema ni Hasan]
Wanaokataa kufunga kwa siku hiyo
wanategemea Hadiyth hiyo.

Wale wanaosema kuwa inawezekana
kufunga siku hiyo wanategemea Hadiyth
zifuatazo. Miongoni mwazo ni: Abu Dharr
(Radhiya Allahu 'anhu) amesema: "Mtume
wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi
wa sallam) alituamuru kufunga siku tatu
katika kila mwezi – yaani masiku meupe,
ambapo mwezi unakuwa umekamilika
(tarehe 13, 14, na 15 katika miezi ya
Kiislamu).

Na akasema kufanya hivyo ni
sawa na kufunga milele” (An-Nasaaiy na
Ibn Hibbaan, ambaye amesema ni Sahihi).
Wanachuoni wanasema kuwa hii ni kauli ya
kijumla katika kufunga siku hiyo na huenda
Jumamosi ikaangukia moja ya terehe hizo.
Na pia ipo Hadiyth ambayo inatupigia
mfano wa funga ya Mtume (Swalla Allahu
'alayhi wa aalihi wa sallam) katika suala
hilo. Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhiya
Allahu 'anhaa) amesema: “Mtume wa
Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa
sallam) alikuwa anafunga siku ya
Jumamosi, Jumapili na Jumatatu katika
mwezi mmoja na Jumanne, Jumatano na
Alkhamiys katika mwezi mwengine” (At-
Tirmidhiy).

Amesema ‘Abdullaah bin ‘Amr bin al-‘Aas
(Radhiya Allahu 'anhu) kuwa Mtume
(Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)
alimwambia: “Funga inayopendeza zaidi
kwa Allah ni funga ya Nabii Dawud …
alikuwa anafunga siku moja na anakula
siku moja” (Al-Bukhariy, Muslim na an-
Nasaaiy).

Hii ni Hadiyth ndefu ambayo inapatikana
katika Riyaadhus Swaalihiyn cha Imam an-
Nawawiy, Hadiyth Namba 150. Jambo
ambalo linaweza kupatikana katika kufuata
Sunnah hii ya funga ambayo ni bora kabisa
ni lazima baada ya kila wiki mbili utakuwa
ni mwenye kufunga siku ya Jumamosi. Na
ikiwa aina hii ya funga imeitwa ndiyo funga
bora na Mtume wa Allah (Swalla Allahu
'alayhi wa aalihi wa sallam) tutaweza
kuitekeleza namna gani?

Juawyriyah bint al-Haarith, Mama wa
Waumini anatuhadithia:
Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa
sallam) alinitembelea Ijumaa siku ambayo
ilikuwa nimefunga, akaniuliza: “Je, ulifunga
jana”. Nikasema: “Hapana”. Akauliza tena:
“Je, una nia ya kufunga kesho?” Nikasema:
“Hapana”. Akasema: “Basi fungua” . Katika
riwaya nyingine: “Alimuamuru afungue,
naye akafungua” (Al-Bukhaariy).
Na katika Hadiyth ya Jaabir (Radhiya
Allaahu 'anhu) amesema Mtume (Swalla
Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)
amesema: “Usifunge siku ya Ijumaa mpaka
uwe umefunga siku kabla yake au siku
inayofuata” (Al-Bukhaariy na Muslim).
Kwa hiyo hapa inaonesha kuwa siku
inayofuata baada ya Ijumaa ni Jumamosi.
Imepokewa kwa Abu Qataadah (Radhiya
Al

samedi 21 juin 2014

bili


Bili ilivyomchanganya Masawe;
Masawe
alienda na rafiki zake Bar
kunywa, baada ya
kumaliza kunywa bili ikaletwa
kama
ifuatavyo;
1). Manka = 35,000fr
2). Madona =20,000fr
3). Dine = 30,000fr
4). Abelle =15,000fr
5). Abuchf =10,000fr
TOTAL = 110,000fr
Masawe akaicheki bili akasema;
wote
nitawalipia, lakini huyo TOTAL
''mama wee'' simlipiyi
kabisa. Kwanza anamiliki station
kibao za
mafuta hapa Bujumbura....
na amekunywa nyingi kuliko wote,
alipe mwenyewe.

lundi 2 juin 2014

MAKAMUA: WAKALI KWANZA LIMEBAKI JINA TU

Makamua akihojiwa na Global TV Online.
MAKALA NA ANDREW CARLOS
WAKALI kwanza ni moja kati ya makundi ambayo yalitikisa sana katika muziki wa Bongo Fleva mwaka 2006-2009. Kundi hili lilibebwa na vichwa vyenye madini, Josline, Makamua na Q-Jay.
Mashabiki wengi walipenda nyimbo zao na miongoni mwa wimbo ambao ulitikisa sana ni pamoja na ule wa Natamani.
Makamua, mmoja kati ya vichwa vilivyokuwa vikiunda kundi hili juzikati alifanya mahojiano na Global TV Online, amewakumbushia vitu vingi, tujiunge naye:
Presenta wa Global TV Online, Erick Evarist akifanya mahojiano na Makamua.
ILIKUWAJE MKAUNDA WAKALI KWANZA?
Ni kama ‘oganaizesheni’ ambayo tuliianzisha  kwa kuona tunaweza kufanya hivyo kwa pamoja kama vijana sababu ya kuepuka vitu mbalimbali kupitia muziki.
Kundi lilianza nikiwa na Josline kipindi hicho alikuwa akitamba na wimbo wa Perfume aliorekodi katika Studio za Midman Records.
Mazoea ya kufika Studio za Midman ndiyo yalisababisha kukutana na Q-Jay, tukaona tunaweza kutengeneza kundi la pamoja.
Kulikuwa na majina tofauti ya kupendekeza kwa ajili ya kundi, mimi nikapendekeza jina la Wakali Kwanza likawa ‘lika-sound’ vizuri basi kila mtu akakubaliana nalo, tukalipitisha.
Mtu wa kwanza kusikiliza kazi zetu na kutukubali alikuwa ni Steven Mdoe ‘Dj Skillz’ akatukubali kinomanoma.
NGOMA GANI ILIWATAMBULISHA WAKALI KWANZA?
Tulianza kwa ‘project’ ya kila mtu kivyake. Nilianza kwa kurekodi wimbo wa Wanatamani kisha baadaye nikatoa wimbo wa Rudi Nyumbani nikimshirikisha Enika kipindi hicho Q-Jay alitoa wimbo wa Sifai, Josline alitoa Niite Basi na Mshikaji Mmoja.
Erick Evarist akizidi kulonga na Makamua.
Baadaye Josline alikuwa nje ya kundi lakini tuliendeleza love kwa kuwa naye kwenye wimbo wa Natamani.
Tukapotezana tena kila mmoja na mitikasi yake. Q-Jay akaingia kwenye nyimbo za Injili (akaokoka) Baada ya kimya kidogo nikatoka kivyangu na wimbo wa Don’t Cry nikimshirikisha  Sarah kutoka Sweden.
VIPI MNA MPANGO WA KURUDI TENA KAMA KUNDI?
Kutusikia wote watatu kwa kipindi hiki itakuwa ngumu. Kama nilivyokwambia Q-Jay ameokoka labda itokee nyimbo ya gospel ambayo itahamasisha watu wa dini ndio tunaweza kutoka watatu.
WEWE NA ENIKA MLIKUTANIA WAPI?
Mara ya kwanza tulikutana kwa marehemu Roy aliyekuwa studio za G records. Kwa sasa yupo anafanya sana adverts (matangazo) siwezi kueleza kwa nini labda kwake anapata benefit (faida) zaidi.
UNAMZUNGUMZIAJE DIAMOND NA TUZO ZA KILI?
Wanasema sometimes ukikaa nje ya mchezo unawea kuona mengi zaidi. Kwa maoni yangu naona kuwa amestahili kupata. Time imekuja vizuri kwake na ametumia muda vizuri na mchezo umeonekana kwenda vizuri kwake.
Joslin, Makamua wakipozi na Mwana hip hop, Kekuu.
Sema nimeona amekuwa katika category nyingi sana. Na kama mtu akichukua tuzo nyingi vile inaonekana kama watu hawajafanya kazi kabisa. Kuna watu kama Rich Mavoko, Ommy Dimpoz wamefanya kazi nzuri.
ULISHAWAHI KUSHIRIKI KWENYE TUZO ZOZOTE?
Mara ya kwanza kabisa nilitakiwa kuwa nomineted na sijui kwa nini sikuwekwa kwa sababu kipindi hicho nilitoa wimbo wa Rudi Nyumbani ambapo alichukuwa mwenzangu Q Jay lakini nikaona mzuka pia.
UNASHAURI KWA WAANDAAJI TUZO ZA KILI?
Kamati zikae chini na kucheki ‘countdown’ zote haijalishi ‘media’ ipi. Wajaribu pia kugawa category kutokana na ‘game’ ilivyotoka na wala sio kwa kukariri.
UKIMYA
Niko na nyimbo nyingi ila kwa sasa narudi na project yangu maalum. Nina wimbo unaitwa Nitakulinda nilioshirikiana na Josline nimeufanya Legendary Music pande za Kinondoni.

jeudi 24 avril 2014

CHID BENZ ALIVYOTAKA KUUA, DEMU AONGEA NA GLOBAL TV ONLINE, MCHEKI HAPA!

Stori:  Erick Evarist na Issa MnaLly
MAJANGA! Msanii wa Hip Hop anayetokea Ilala, Rashid Makwiro ‘Chid Benz’ amedaiwa kumpa kipigo kizito mpenzi wake wa zamani aliyefahamika kwa jina la Mwanaisha Kiboye.
Rashid Makwiro ‘Chid Benz’.
Tukio hilo lililokusanya umati wa watu lilijiri Jumapili iliyopita maeneo ya Buguruni (kwenye mafleti) jijini Dar ambapo Chid alikuwa kwenye mizunguko yake na mpenzi wake wa sasa ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja.
Mpenzi wa zamani  wa Chid Benz aliyefahamika kwa jina la Mwanaisha Kiboye.
ISHU ILIVYOKUWA
Kwa mujibu wa chanzo chetu, Chid na mpenzi wake huyo walifika katika baa moja maarufu iliyopo katika mafleti hayo na kumkuta Mwanaisha akiwa amekaa na rafiki zake. Demu huyo alimsalimia Chid na ndipo mtiti ukaibuka.
“Mwanaisha alipomuona Chid anakatiza na kwa kuwa aliwahi kuwa mpenzi wake, akaona siyo ishu bora ampe hai kwa mbali ndipo Chid alipomaindi na kumfuata huku akisema: unajifanya unanijua sana siyo? Ngoja nikuoneshe,” kilisema chanzo.
Mwanaisha Kiboye akiwa amelala nyumbani kwao.
AMZIMISHA
Chanzo hicho kilizidi kudai kuwa, baada ya Chid kusema hivyo alimshushia kipondo kikali hasa sehemu za usoni na kumsababisha Mwanaisha achanike mdomoni kabla ya kuzimia palepale na kuanza kupepewa na marafiki zake, Chid akatokomea kusikojulikana.
Imeelezwa kuwa, Mwanaisha alipozinduka baada ya kupepewa alikwenda kutoa taarifa katika Kituo cha Polisi Pangani, Ilala ambapo alipewa Fomu ya Polisi Nambari 3   (PF3) kisha kwenda kutibiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Kitabibu, Ilala - Amana.

CHID NAYE AKIMBILIA POLISI
Chanzo kimezidi kueleza kuwa, wakati Mwanaisha akianza kupewa matibabu hospitalini, Chid naye alishauriwa na marafiki zake kwenda kutoa taarifa katika kituo hicho cha polisi kama njia ya kujihami pasipo kujua kuwa  ameshawahiwa.
“Marafiki zake walioshuhudia tukio hilo walimshauri jamaa (Chid) akafungue mashitaka polisi kama njia ya kujihami, akakubali ndipo alipokwenda kutiwa nguvuni kwani tayari Mwanaisha alikuwa ameshamuwahi,” kilisema chanzo hicho.

ATUPWA MAHABUSU
Habari zimeeleza kuwa, Chid alipofika kituoni kwa ajili ya kutoa taarifa, alidakwa na kusokomezwa mahabusu kwa vile tayari alikuwa ameshafunguliwa mashitaka.
Chanzo kilichopo polisi hapo kimeliambia Amani kuwa, jamaa alipoambiwa avue mkanda ili atupwe sero alileta ubishi hivyo kusababisha polisi watumie nguvu ya ziada kumdhibiti kwa sababu alisema yeye ni mtu maarufu hivyo hawawezi kumtisha.

AKUTWA NA BANGI
Wakati msanii huyo anayesifika kwa  sauti nzito akitaka kuingizwa ndani, alisachiwa na kukutwa na misokoto miwili ya bangi hivyo kuandikishwa kesi nyingine ya madawa ya kulevya mbali na ile ya awali ya kujeruhi.

MWANAISHA ANASEMAJE?
Juzi Jumanne, Amani lililimsaka Mwanaisha ambapo lilifanikiwa kumkuta nyumbani kwao, maeneo ya Sharifu Shamba,  Ilala akiwa hawezi kutembea, kuongea vizuri akiwa hoi kitandani.
Akizungumza kwa shidashida, Mwanaisha alisema anasikitika kuona Chid amempiga bila kisa.
“Sijui hata kwa nini aliamua kunipiga, amenipiga vibaya, nimeshonwa nyuzi 12 na bado nasikia maumivu makali kichwani,” alisema.
Kwa mujibu wa dada wa Mwanaisha ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazetini, watafuatilia kwa karibu mwenendo wa kesi hiyo ili kuona mwisho wake kwani mbali na kumweka majeraha ndugu yake lakini bado hali ni mbaya na wanatakiwa kumfanyia Kipimo cha CT Scan.
“Hizi gharama zote tutakazohangaika kumtibu ndugu yetu lazima Chid azilipe maana amempiga ndugu yetu pasipo kufanya kosa lolote,” alisema dada wa Mwanaisha.

APANDISHWA KIZIMBANI
Kwa kuwa Jumapili na Jumatatu ilikuwa Sikukuu ya Pasaka, juzi Jumanne Chid alipandishwa katika Mahakama ya Mwanzo - Ilala na kusomewa mashitaka mawili; KUJERUHI na KUKUTWA NA BANGI.
Siku hiyo, mahakama ilimsomea mashitaka na kutakiwa kujibu kama ni kweli amefanya makosa hayo lakini mshitakiwa huyo alikanusha makosa yote mawili hivyo kesi hizo kuahirishwa.

KESI ZATOFAUTISHWA
Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika mahakama hiyo, kesi ya kujeruhi inatarajiwa kutajwa tena mahakamani hapo Aprili 24, mwaka huu (leo) huku ile ya kukutwa na bangi ikisogezwa mbele hadi Mei 6, mwaka huu.

APATA DHAMANA
Baada ya kuahirishwa kwa kesi hizo, mshitakiwa alipewa nafasi ya kupata dhamana kwa masharti ya kulipia shilingi 100,000 huku akidhaminiwa na watu wawili ambapo Chid alitimiza masharti hayo na kuachiwa huru kusubiri kesi zitajwe tena.
Kamanda wa Mkoa wa Polisi Ilala, ACP Marieta Minangi amekiri kutokea kwa tukio hilo.

Ahmed Bukhatir - Zawjati (My Wife) with English Subtitles

samedi 29 mars 2014

HIVI NDIVYO BONGO MOVIE WALIVYOSHEREHEKEA BETHIDEI YAO

Shilole katika picha ya pozi kwenye zulia jekundu ‘red carpet’.
Shamsa Ford akihojiwa kwenye zulia jekundu.
Baadhi ya wasanii wa Bongo Movie Unity wakiingia ukumbini.
Sandra (kushoto) na Eshe Buheti wakiwa kwenye zulia jekundu.
Wasanii na mashabiki wao wakicheza muziki.
Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Nyerere’ akizungumza machache mbele ya watu waliohudhuria.
Steve Nyerere akikata keki.
Jana ilikuwa ni siku ya furaha kwa wasanii wa Kundi la Bongo Movie Unity waliokuwa wakisherehekea kundi hilo kutimiza miaka mitatu tangu lilipoanzishwa.
Sherehe za kumbukumbu hiyo zilifanyika kwenye Ukumbi wa Arcade, Mikocheni jijini Dar ambapo wasanii walianza kwa kupiga picha kwenye zulia jekundu ‘red carpet’ na watu kibao waliohudhuria.
Kwa upande wa burudani ya muziki, wanamuziki Linex, Amini, Pendo wa Maisha Plus, Shilole, Bendi ya Fm Academia na Bendi ya BM walitoa burudani ya aina yake na kusababisha ukumbi wote kulipuka kwa shangwe.

J Moe / Juma Nature & Professor Jay - JWTZ 1


J Moe / Juma Nature & Professor Jay - JWTZ

Ni Director wa kwanza bongo wa Music Videoz kupata access ya vifaru,
ndege, helicopter pia sare za jeshi kufanyia music video

I believe kwa Kumtanguliza Mungu kila kitu kinawezekana

"After all, I believe that legends and myths are largely made of
'truth', and indeed present aspects of it that can only be received in
this mode; and long ago certain truths and modes of this kind were
discovered and must always reappear."

Directed, Edited By: Mike Mwakatundu as Director M

Under Williamz Visions Co Limited

All rights Reserved Under Copyright And Neighboring Right Act, only
for personal entertainment, not for sale or public performance.

Hope Ya'll going to have fun.

Like to share?

dimanche 23 mars 2014

Kifaransa

Siku moja kulikuwa na shule ya kifaransa nchini Tanzania jamaa umoja alisomea eko kisha akaja matembezini nchini Burundi aka enda kwenye kampun yake iliyoko Burundi akaona kazi haziendi sawa akataka awambie mkifaransa sababu warundi wanajua kifaransa Boss akawaza : fil mana yake ni uzi akisha marteau ni hummer oooh Boss: si vous me fil fil, je veux vous marteauner d'ici !

mercredi 22 janvier 2014

CHAN Orange 2014 – Groupe D, 3e J : Le Burundi a deux doigts d’une qualification historique

2014-01-16-Gabon-Burundi4
Ce soir, on connaîtra les deux derniers qualifiés pour le quart de finale du Championnat d’Afrique des Nations (CHAN Orange 2014) après les deux matchs prévus de la troisième journée de la poule D.
Le Burundi, le Gabon et la République Démocratique du Congo sont les trois concernés par les deux billets restants. Quant à la Mauritanie, les dès sont déjà jetés. Les Mourabitounes, derniers sans le moindre point, n’ont plus aucune chance de se hisser au deuxième tour. Mais le petit poucet de la compétition peut quand même offrir un dernier service au Burundi et à la RD Congo, avant de quitter le pays Nelson Mandela, en accrochant le Gabon. Les coéquipiers de Daniel Cousin, sont les mieux placés pour se qualifier, à condition de ne pas perdre.
Le second match est incontestablement le choc de cette poule. Les congolais doivent relever la tête après leur défaite face au Gabon. En face, le Burundi qu’on pensait être là juste pour compléter le nombre, est à deux doigts de l’exploit. Un match nul ou même une défaite conjuguée par une défaite avec le même score du Gabon leur permettra d’accompagner la RDC au quart de finale.
Programme :
RD Congo et Burundi se jouent le quart
  • 17h : RD Congo – Burundi
  • 17h : Gabon – Mauritanie

BURUNDI VS MAURITANIE: LES COMPOSITIONS D'éQUIPES

 
Burundi VS Mauritanie:  Les compositions d'équipes
veuillez cliquer ici pour les compositions d'equipes

lundi 6 janvier 2014

Diamond Platnumz Feat Davido Number One 'Remix' Official Video

Diamond Platnumz Feat Davido Number One 'Remix' Official Video



Dowload Sajna_-_Samahani

http://www.hulkshare.com/abuchief/sajna-samahani

Jackie Chan Police Story 2013 《Zheng Jiu》 MV Fast Version

STEVE NYERERE NDIYE MWENYEKITI MPYA BONGO MOVIE CLUB

Mwenyekiti mpya wa Bongo Movie Club, Steve Nyerere.
Dk. Cheni na Asha Baraka wakisalimiana kabla ya uchaguzi kuanza katika Viwanja vya Leaders Club.
Kutoka kushoto: Baba Khadji, Barafu na Libert wakisubiri mchakato wa kupiga kura kuanza.
Chiki (kushoto) na Rich wakiteta jambo kwenye Viwanja vya Leaders.
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Bongo Movie Club, Jimmy Mafufu.
Wasanii wakiwa tayari kuwachagua viongozi wao katika Viwanja vya Leaders Club.
Chiki (kushoto) akiwa na Makamu Mwenyekiti wa Bongo Movie Club, Dk. Cheni.

FAHAMU KISUKARI KATIKA MAFUNGU MATATU

Wengi wanapenda kujua ugonjwa wa kisukari unavyoanza kwa binadamu. Ugonjwa huu au kitaalamu huitwa Diabetes mellitus hutokea pale tezi kongosho au Pancrease inaposhindwa kutengeneza homoni au kichocheo aina ya Insulin, au pale mwili unaposhindwa kutumia vizuri kichocheo hicho na kusababisha kuongezeka kiwango cha sukari kwenye damu au kitaalamu huitwa Hyperglycemia.
Insulin ni kichocheo au homoni inayotengenezwa na kongosho ili kudhibiti sukari katika damu. Ugonjwa wa kisukari unaweza kusababishwa kuwa na kiwango kidogo cha Insulin mwilini, mwili kutosikia kichocheo hicho au yote mawili.
Ili kuelewa vyema ugonjwa wa kisukari ni muhimu kwanza kueleza namna chakula kinavyovunjwavunjwa na kutumiwa na mwili ili kuzalisha nguvu mwilini. Wakati chakula kinapoyeyushwa matukio kadhaa hutokea. Moja ni sukari inayoitwa Glucose ambayo ni chanzo cha nguvu mwilini huingia katika damu.
Tukio la pili ni kiungo kinachoitwa kongosho au kwa kitabibu Pancrease hutengeneza kichocheo cha Insulin ambayo kazi yake ni kuondoa Glucose katika damu na kuingiza katika misuli na seli za mafuta na ini, ambako hutumiwa kama nishati mwilini.
Watu wenye ugonjwa wa kisukari huwa na kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu kwa sababu miili yao haiwezi kupeleka sukari kwenye seli za mafuta, ini na misuli ili ihifadhiwe kwa ajili ya kuzalisha nguvu.
Hii ni kutokana na moja kongosho zao kushindwa kutengeneza Insulin ya kutosha  au seli za mwili wao haziathiriwi na Insulin kama inavyotakiwa au sababu zote hizo mbili.
MAFUNGU MATATU YA KISUKARI
Ugonjwa wa kisukari umegawanyika katika mafungu matatu, la kwanza ni kisukari aina ya kwanza  kitaalamu Type 1 Diabetes Mellitu ambayo wanaoathirika zaidi ni watoto na vijana.
 Ugonjwa huu hujitokeza iwapo seli maalumu zinazotengeneza homoni ya Insulin zinapokosekana katika tezi kongosho au zinapoharibika kutokana na sababu yoyote ile,  hivyo kusababisha ukosefu kabisa au upungufu wa kichocheo hicho kwenye damu mwilini.
Mambo yanayoweza kusababisha uharibifu wa seli hizi katika tezi kongosho ni pamoja na kushambuliwa tezi kongosho kunakoweza kufanywa na magonjwa ya kinga ya mwili ya mtu mwenyewe au Autoimmune diseases, au kushambuliwa na vyanzo visivyojulikana.
Kwa vile, uharibifu katika tezi kongosho husababisha kutokuwepo kabisa Insulin mwilini au Insulin kuzalishwa kwa kiwango kidogo sana, wagonjwa wa aina hii ya kisukari huhitaji kupewa dawa za Insulin kwa njia ya sindano au pampu kila siku za maisha yao ili waweze kuishi.
Kwa sababu hiyo aina hii ya kisukari huitwa pia kisukari kinachotegemea Insulin au Insulin Dependent Diabetes Mellitus (IDDM).
Aina ya pili ya kisukari  kitaalamu huitwa  Type 2 Diabetes Mellitus ni fungu la pili la maradhi haya na  huwapata watu  ukubwani na husababishwa na kupungua utendaji kazi wa homoni ya Insulin.

Itaendelea wiki ijayo.

jeudi 2 janvier 2014

Le PSG pas récompensé contre le Real Madrid

Le PSG s'est incliné face au Real Madrid (0-1), jeudi en amical. Pourtant, les Parisiens ont dominé, et auraient mérité mieux. Paris semble prêt pour la deuxième partie de saison.
 
Ibrahimovic et les Parisiens ont dominé le Real, jeudi à Doha. (L'Equipe)
 
Laurent Blanc ne prenait pas ce match à la légère. Pour affronter le Real Madrid en amical, jeudi à Doha, l’entraîneur parisien avait aligné son équipe-type, contrairement à son homologue et prédécesseur Carlo Ancelotti, qui avait beaucoup fait tourner. Et le PSG a dominé, assez largement, cette rencontre disputée sur un rythme élevé. Paris a perdu (0-1), comme en juillet dernier à Göteborg, mais c’est anecdotique : les Parisiens semblent prêts pour la suite de la saison.

Dès le début du match, les triplettes Verratti-Motta-Matuidi et Cavani-Ibrahimovic-Lavezzi se sont lancées sans complexe à l’assaut du but madrilène, faisant étalage de leur qualité technique et de leur capacité à varier le jeu. A la 16e minute, Cavani pouvait même se présenter seul face à Diego Lopez sur une superbe passe de volée de Matuidi, mais l’Uruguayen perdait son duel. Dans la foulée, le Real se procurait l’une de ses seules occasions, et Jesé trompait Sirigu sur sa droite grâce à un excellent service de Morata… Cruel pour un PSG qui est apparu très affûté à l’issue de son bref séjour au Qatar.
Jesé, félicité ici par ses partenaires, a inscrit le seul but de la victoire contre le PSG. (Reuters)

Verratti et Ibra régalent

Car la suite, c’est une pelletée d’occasions pour le PSG, dont les tentatives ont souvent frôlé les poteaux du Real. Alex (21e), Digne (22e), Matuidi (27e) et Cavani (35e) ont tous manqué le cadre de peu, avant qu’Ibrahimovic n’écrase trop sa frappe sur Diego Lopez à la 40e minute. Seul le jeune José Rodriguez, bien lancé par Ronaldo entre Alex et Van der Wiel, venait rappeler aux Parisiens la valeur de leur adversaire en trouvant le poteau de Sirigu avant la mi-temps. Comme souvent cette saison, Verratti rayonnait au milieu de terrain, distribuant le jeu et obtenant de précieux coups francs, alors que devant lui Ibrahimovic régalait de ses déviations pour Lavezzi et Cavani.

Les remplaçants au diapason

En seconde période, la domination des Parisiens s’est poursuivie et même accentuée en dépit des entrées en jeu, côté madrilène, de Benzema, Isco, Modric, Marcelo ou encore Di Maria à la pause. Benzema trouvait d’ailleurs la barre sur un bon service de Marcelo à la 53e, mais on assistait surtout à un festival de têtes au-dessus du but madrilène, signées Ibra (47e), Motta (58e) ou encore Rabiot, entré à l’heure de jeu (81e). Laurent Blanc pouvait aussi se satisfaire de la qualité et de l’engagement affichés par ses remplaçants, à l’image de Lucas, très vif et proche de l’égalisation sur une frappe au ras du poteau à la 90e, ou encore Kingsley Coman, qui a mis à mal la défense du Real. Ménez a également failli marquer, mais s’est montré moins incisif dans le jeu. La seule déception est venue de Javier Pastore, entré à la 62e à la place de Verratti et loin, très loin du rayonnement du petit italien… On ignore s'il sera encore là pour les échéances européennes du printemps prochain, mais ce jeudi, ses partenaires ont montré qu’ils ne faisaient aucun complexe face aux grosses écuries du continent. D’ici là, il faudra passer par Brest, dimanche, en 32es de finale de la Coupe de France. Et d’ailleurs, c’est bien en vue de ce match-là que les Parisiens « s’entraînaient », paraît-il…