Alibaba

mardi 25 octobre 2016

Ballon d'or 2016 wanao baki

Mshambuliaji wa timu ya Wales Gareth Bale na mwenzake wa Real Madrid Cristiano Ronaldo wameorodheshwa kuwania taji la mchezaji bora duniani mwaka 2016 Ballon d'Or.

Wachezaji wa Manchester City Sergio Aguerro na Kevin De Bruyne, pamoja na wachezaji wa Atletico Madrid Antoine Griezmann pia wako katika orodha hiyo.

Gazeti la soka la Ufaransa limebaini orodha ya wachezaji 30 katika makundi ya wachezaji watano kila baada ya saa mbili siku yote ya Jumatatu.

Tuzo hiyo hutolewa na Ufaransa kila mwaka tangu mwaka 1956, lakini kwa kipindi cha miaka sita iliopita tuzo hiyo ilibadilika na kuwa Fifa Ballon d'Or kwa ushirikiano na shirikisho la soka duniani Fifa.
Mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi alishinda tuzo hiyo mwaka uliopita kwa mara ya tano .

*Wachezaji waliorodheshwa ni:

Sergio Aguero (Manchester City),
Pierre-Emerick Aubameyang (Borussia Dortmund),
Gareth Bale (Real Madrid),
Gianluigi Buffon (Juventus),
Cristiano Ronaldo (Real Madrid),
Kevin de Bruyne (Manchester City),
Paulo Dybala (Juventus),
Diego Godin (Atletico Madrid),
Antoine Griezmann (Atletico Madrid),
Gonzalo Higuain (Juventus).

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire