Alibaba

vendredi 4 novembre 2016

Huawei yazindua simu mpya ya Mate 9

Huawei imezindua simu mpya yenye skrini kubwa wakati huu ambapo simu ya Samsung Galaxy Note 7 inakumbwa na changamoto.

Simu hiyo kwa jina Mate 9, ni kati ya simu za kwanza zinazotumia teknolojia ya Android 7 na inakuja ikiwa katika aina mbili za kamera.
Kampuni hiyo ya China inasema kuwa imeshughulikia tatizo la simu hizo kupoteza mauzo baadaye.

Lakini mtaalamu mmoja anasema kuwa wateja bado wanazitilia shaka simu za kampuni hiyo.
Simu za Huawei hazijafikia viwango vya simu za Samsung na ndiyo sababu huwa inafanya ushirikiano na kampuni zingine kama Leica na Porsche kuboresha teknolojia yake ya Kamera.

Samsung ilitizisha uundaji wa simu ya Note 7 mwezi uliopita baada ya simu kadha kuwaka moto.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire