Alibaba

mercredi 9 novembre 2016

Hillary: Trump apewe fursa ya kuongoza

Mgombea wa urais aliyeshindwa katika uchaguzi mkuu wa Marekani Hillary Clinton amesema kuwa rais mteule Donald Trump anafaa kupewa nafasi ili kuongoza.

Akionekana kwa mara ya kwanza tangu kukiri kushindwa ,mgombea huyo wa chama cha Democrat amesema kuwa ana matumaini kwamba Trump atafanikiwa kuwa rais wa Wamarekani wote.

''Tumeona kwamba taifa letu limegawanyika sana zaidi ya nilivyodhania'',alisema bi Clinton.
Donald Trump atakuwa rais wa 45 wa Marekani baada ya ushindi mkubwa.

Atafanya mkutano wake wa kwanza wa mpito na rais Obama katika ikulu ya White House siku ya Alhamisi.
Bwana Obama alimpongeza mrithi wake katika mazungumzo ya simu mapema asubuhi akisema kwamba sio siri kwamba yeye na Trump wana tofauti kubwa kati yao.

''Hatahivyo tuko katika timu moja na watu wanafaa kujua kwamba sisi ni Wamarekani kwanza tunataka taifa hili kuboreka zaidi''.
Bi Clinton aliwaambia wafuasi wake akitaja kushindwa kwake katika uchaguzi huo katika hotubu yake huko New York.

''Bado hatujaafikia lengo letu .Lakini siku moja mtu ataafikia'', alisema Bi Clinton.

''Kwa wasichana wote wanaotazama hotuba hii...ondoeni shaka kwamba muna thamani tele na uwezo mkubwa na munapaswa kupewa kila fursa duniani'',alisema. Nawapa pole kwamba hatukushinda kutokana na thamani tulio nayo kati yetu na maono yetu tulionayo kwa taifa hili''.

Ahadi za Trump ndani ya siku 100 za kwanza madarakani

Ni kipi Donald Trump ameahidi kukifanya siku za kwanza 100 akiwa rais?

Hakujakuwa na mgombea wa urais katika historia ya Marekani kama mfanyabiashara tajiri Donald Trump.

Matamshi yake yenye utata na msimamo mkali kuhusu uhamiaji, vilileta msukosuko ndani ya chama chake na mgawanyiko nchini.

Lakini ahadi yake ya "kuiweka mbele nchi "iliwavutia mamilioni ya waamerika ambao wanahisi kuhujumiwa na mfumo wa sasa.
Kwa hivyo ni kipi tunatarajia kutoka kwa bwana Trump?

Baadhi ya ahadi zake ndani ya siku 100 za kwanza zilitolewa wakati wa hotuba yake mwezi uliopita mjini Gettysburg jimbo la Pennsylvania.
Ameapa kujenga ukuta kwenye mpaka kati ya Marekani na Mexico, mradi ambao utagharamiwa na Mexico.

Ahadi nyingine ambayo licha ya kutokuwepo kwenye hotuba ya Gettysburg ni kusaini upya mikataba ya biashara kati Marekani,Canada na Mexico.

Anasema kuwa mikataba hii inachangia katika kuwapokonya raia ajira zao.

Trump pia ameahidi kuboresha uhusiano na Raias wa Urusi Vladimir Putin, ambaye amemsifu na kumtaja kuwa kiongozi aliye imara.
Aidha ameapa kuondoa Marekani kutoka kwa mkataba kuhusu mpango wa nuklia wa Iran.