Alibaba

samedi 26 novembre 2016

Ibrahimovic: Rooney anastahili heshima

Mshambuliaji wa Manchester united Zlatan Ibrahimovic, amesema Wayne Rooney''ni mchezaji bora'' na anastahili heshima zaidi, baada ya nahodha huyo wa Uingereza kuvunja rekodi ya ufungaji mabao.
Manchester United walifunga mabao 4-0 dhidi ya Feyenoord kwenye ligi ya Europa iliyochezwa siku ya Alhamisi.

Rooney, mwenye umri wa mika 31, alifunga goli la 39 barani Ulaya na kuifanya United kupata alama katika fainali ya hatua ya makundi dhidi ya Zorya Luhansk itakayowafikisha katika timu 32 bora katika ligi ya Europa.

Hii ni kutokana na mchango wa Rooney, ambaye amesalia na goli moja kufikia rekodi ya Sir Bobby Charlton ya magoli 249.

''Ni mtu mzuri , Ibrahimovic, aliyemsaidia Rooney kufunga bao la kwanza, aliambia BBC Sport. Nafurahi kwa kuwa amevunja rekodi. Lakini nitamsaidia kupata bao jingine. Lile ambalo litamfanya kuweka rekodi ya ukweli.''

Rooney aliomba radhi wiki iliyopita kwa picha ambazo ''hazifai'',alipohudhuria harusi katika hoteli walimokuwa ikilala timu ya taifa wakati wa mapumziko ya kimataifa.

Lakini Jumamosi alisema ripoti hizo ''zilikosa heshima'',akiongezea:Ni kama vyombo vya habari vinajaribu kuandika matangazo ya kifo change.

Alikasirika alipoulizwa tena swali kuhusiana na picha hizo baada ya ushindi dhidi ya Feyenoord, alisema: Kile kinachobuniwa na watu kama wewe unayeuliza maswali, kuyafanya mambo kuwa makubwa bila sababu yoyote.
''sikuhudhuria harusi hiyo,na ni aibu kuzungumzia kuhusu hilo usiku kama wa leo.''

Ibrahimovich alisema:'' Kwa mafikira yangu mtu akiwa na umaarufu kama hivyo, watu hutaka kujua zaidi kukuhusu.''
Tunastahili kumshukuru kwa kuwa michezaji jinsi alivyo, kwa kile alichokifanya. Siwaoni wachezaji wengi kutoka Uingereza walio na taaluma kama yake. Wanastahili kumpa heshima. Kila mtu hupenda kufanya jambo dogo kuwa kubwa.
Meneja Jose Mourinho alisema: Watu kama yeye hawastahili kujibu chochote tena , anastahili kufurahikia miaka michache iliyosalia katika taaluma yake na kucheza mchezo mzuri kadri ya uwezo wake.

L'ANCIEN MÉDECIN DE CHELSEA A REÇU DES MENACES DE MORT

Eva Carneiro a reconnu dans un entretien pour le Telegraph que la vie n'était pas la plus aisée pour elle depuis son départ de Chelsea.
Si elle a quitté Chelsea depuis septembre 2015 suite à un incident avec José Mourinho, technicien de l'époque, Eva Carneiro n'a pas pour autant oublié

Lors d'un entretien accordé au Telegraph, elle a reconnu avoir été victime de menaces de mort sur les résaux sociaux. "Même si je n'ai pas de présence sur les réseaux sociaux - je pense avoir fait un seul post dans ma vie - j'ai reçu des des menaces de violence sexuelle et de mort par ce biais-là. Ils [les agresseurs] semblent être des lâches sans visage et ils doivent être responsables devant la loi" , a-t-elle commenté.

Carneiro exerce désormais dans sa propre clinique à Londres comme le fait savoir l'Equipe.

Fifa: Argentina ndio bora duniani, Senegal yaongoza Afrika

Shirikisho la kandanda ulimwenguni (FIFA) limetoa orodha ya viwango bora vya soka ,ambapo mpaka sasa kwa upande wa bara la Ulaya Argentina bado ndio taifa bora duniani kwa mujibu wa viwango vya ubora duniani iliyotolewa Ijumaa.
Brazil, chini ya kocha wao mpya, inakuja moto na kuinyemelea kwa kasi.

Kwa upande wa Afrika Senegal ndio vinara na ipo nafasi ya 33 ulimwenguni , huku wakifuatwa na Ivory Coast katika nafasi ya pili ambapo wanafungana na Tunisia kwenye Nafasi hiyo na nafasi ya 36 ni Misri na wapo nafasi ya 34 ulimwenguni.

Nafasi kumi bora Argentina, Brazil, Ujerumani, Chile, Ubelgiji, Colombia, Ufaransa , Ureno, Uruguay, Hispania.
Orodha nyengine ya Fifa ya ubora duniani itatolewa Disemba 22.

Watu 80 wafariki katika shambulizi la Bomu lililowalenga washiha Iraq

Vyombo vya usalama vya Iraq vimesema kwamba zaidi ya watu themanini wameuawa kwa shambulizi la bomu lililowalenga madhehebu ya kiislamu ya kishia kusini mwa mji wa Baghdad.

Gari lililokuwa limebeba vilipuzi hivyo lililipuka karibu na kituo cha mafuta ambapo watu wengi wa dhehebu hilo walikuwa wameegesha magari yao.

Wengi wa watu waliofariki ni wananchi wa Iran na Afghanistan.
Walikuwa wakitoka kwenye moja ya tukio muhimu la kidini kwenye mji mtakatifu wa Karbala.

Askari wa kundi la kiislam wamekiri kuhusika na shambulizi hilo.
kundi hilo la wapiganaji la kiislam mara kwa mara hulenga madhehebu ya kishia na kuwatuhumu kwamba ni waongo.