Alibaba

mercredi 14 décembre 2016

Le Ballon d’or de Ronaldo déjà au musée !

Après avoir remporté son quatrième Ballon d’or, Cristiano Ronaldo l’a immédiatement exposé dans son musée de Madère, avec tous ses trophées.

Il n’a pas traîné ! Deux jours après la conquête de son quatrième Ballon d’or, Cristiano Ronaldo, actuellement au Japon pour disputer la Coupe du monde des clubs avec le Real Madrid, a déjà fait figurer l’iconique trophée dans le musée qui porte son nom, à Funchal, sa ville de naissance.
"Mon Ballon d’or est disponible dans mon musée de Madère", écrit-il en légende d’une photo où on peut apercevoir le trophée en bonne place dans le "Museu CR7", qui accueille 200 000 visiteurs par an.

Un musée, financé par la star portugaise, qui a récemment été agrandi "pour accueillir tous les nouveaux trophées de Ronaldo", avait déclaré son cousin l’été dernier. Bien vu.

Adabu kwa Chelsea na Manchester City wapigwa fain

Chelsea wamepigwa faini ya £100,000 na Manchester City wakapigwa faini ya £35,000 baada ya wachezaji wao kuhusika katika vurugu uwanjani wakati wa mechi ya Ligi ya Premia.
Hisia zilipanda na wachezaji wakakabiliana mechi hiyo iliyochezewa uwanjani Etihad ilipokaribia kumalizika baada ya Sergio Aguero wa City kufukuzwa uwanjani kwa kumchezea visivyo beki wa Chelsea David Luiz.
Fernandinho pia alifukuzwa uwanjani kwa kumkaba koo Cesc Fabregas wachezaji wa klabu hizo mbili walipokabiliana baada ya kisa hicho.
Chelsea walishinda 3-1.

Blues walikuwa awali wametahadharishwa kwamba wanaweza kupokonywa alama kwa utovu wa nidhamu.
Viongozi hao wa Ligi ya Premia wamepigwa faini mara sita tangu Februari 2015 kwa kushindwa kuwadhibiti wachezaji.

Lionel Messi akutana na kijana aliyevalia jezi ya karatasi Afghanistan

Mvulana kutoka nchini Afghanistan aliyepata umaarufu sana mtandaoni alipopigwa picha akiwa amevalia karatasi kama jezi ya Lionel Messi mechi amefanikiwa kukutana na shujaa huyo wake.
Picha ya Murtaza Ahmadi, mwenye miaka sita, akiwa amevalia karatasi hiyo iliyoandika nambari ya jezi ya Messi pamoja na jina lake ilivuma sana mwezi Januari mtandaoni.
Mwishowe, alipokea jezi halisi kutoka kwa mshambuliaji huyo wa Barcelona, ambayo pia ilikuwa imetiwa saini na mchezjai huyo.
Sasa, wawili hao wamekutana ana kwa ana mjini Doha, kwa mujibu wa kamati andalizi ya Kombe la Dunia la 2022 nchini Qatar.

Barcelona wamo nchini Qatar kucheza mechi ya kirafiki na Al Ahli Jumanne.
Ahmadi anatarajiwa kutembea kuingia uwanjani akiandamana na Messi.
"Ni picha ambayo ulimwengu ulitaka kuona," aliandika mkuu wa kamati hiyo Jumanne.
"Mvulana wa miaka sita akikutana na shujaa wake, #Messi, ndoto yake ikitimia."
Ahmadi, ambaye anatoka wilaya ya Jaghori, katika mkoa wa Ghazni mashariki mwa Afghanistan, alilazimika kukimbilia nchi jirani ya Pakistan mwezi Mei.
Murtaza alitambuliwa kama mvulana ambaye picha yake ilikuwa ikisambazwa mtandaoni baada ya mjomba wake Azim Ahmadi, raia wa Afghanistan anayeishi Australia, kuwaunganisha waandishi wa BBC Trending na nduguye, Arif - babake shabiki huyo mkubwa wa Messi.

Professor Jay amuandikia barua yenye ujumbe mzito Darassa

Ni ukweli kuwa kwa sasa Darassa ameyasogelea mafanikio aliyokuwa akiyatamani kwa muda mrefu. Rapper mkongwe wa muziki wa Hip Hop nchini, Professor Jay amemuandikia ujumbe hitmaker huyo wa Muziki wa kumpongeza kwa kazi nzuri anayoifanya na kumtaka kuendelea kukaza buti.

Kupitia mtandao wa Instagram, Jay ameandika:

Mdogo wangu @darassacmg Imani yako, Kutokukata tamaa na Struggle yako ya Usiku na Mchana ndio imekufanya ufikie hapo ulipofikia, Nakumbuka wakati unashoot Wimbo wako wa USIKATE TAMAA uliniambia unatamani ufikie level za juu kama zetu, Nami nilikwambia hakuna kinachoshindikana chini ya JUA Ukiset GOALS, kufanya kazi kwa bidii na SALA yote Yanawezekana, Naamini kwa style hii ya JIWE juu Ya JIWE, NDOTO yako inakwenda kuwa kweli, Cha MSINGI usiridhike na mafanikio haya..HUU ni mwanzo tuu na mafanikio makubwa zaidi yako at your DOOR, Keep your eyes open and Keep ya HEAD UP,
SKY IS THE LIMIT, GO GET DEM… BLESS
#ACHA MANENO WEKA MUZIKI
@darassacmg @darassacmg

Classement complet ballon d'or france football 2016

1. Cristiano Ronaldo (Real Madrid/Portugal) 745 points
2. Lionel Messi (FC Barcelone/Argentine) 316
3. Antoine Griezmann (Atlético Madrid/France) 198
4. Luis Suarez (FC Barcelone/Uruguay) 91
5. Neymar (FC Barcelone/Brésil) 68
6. Gareth Bale (Real Madrid/Pays de Galles) 60
7. Riyad Mahrez (Leicester/Algérie) 20
8. Jamie Vardy (Leicester/Angleterre) 11
9. Gianluigi Buffon (Juventus Turin/Italie) et Pepe (Real Madrid/Portugal) 8
11. Pierre-Emerick Aubameyang (Borussia Dortmund/Gabon) 7
12. Rui Patricio (Sporting CP/ Portugal) 6
13. Zlatan Ibrahimovic (Manchester United/Suède) 5
14. Paul Pogba (Manchester United/France) et Arturo Vidal (Bayern Munich/Chili)
16. Robert Lewandowski (Bayern Munich/Pologne) 3
17. Toni Kroos (Real Madrid/Allemagne), Luka Modric (Real Madrid/Croatie) et Dimitri Payet (West Ham/France) 1

Non-classés : Agüero, De Bruyne, Dybala, Godin, Higuain, Iniesta, Koke, Lloris, Müller, Neuer, Sergio Ramos.

Yaya Toure: Sikujua Coke ilikuwa imeongezwa pombe

Mchezaji nyota wa Ivory Coast Yaya Toure amesema hajapinga shtaka la kuendesha gari akiwa amelewa wiki mbili zilizopita.
Hata hivyo, amesema kwamba hakunywa pombe makusudi alipokamatwa akiendesha gari akiwa mlevi.
Ameandika kwenye Facebook kwamba "inafahamika wazi kwamba mimi ni Mwislamu na huwa sinywi pombe."

Hata hivyo, hajaelewa ni vipi alijipata akinywa pombe ama akajipata akiwa amelewa bila yeye kufahamu.
Gazeti la The Mirror la Uingereza linasema kwamba alidai alikunywa Diet Coke na hakujua kwamba kwenye jagi aliyokuwa akitumia kunywa palikuwa pameongezwa kilevi aina ya brandi.
Gazeti hilo linasema amepigwa marufuku kutoendesha gari kwa miezi 18 na kupigwa faini ya $68,000 (£54,000).

Mchezaji huyo wa Manchester City amesema: "Daima nimekuwa nikikataa pombe. Yeyote anayenifahamu na anayefuatilia uchezaji wangu atakuwa bila shaka ameniona nikikataa shampeni ya Mchezaji Bora wa Mechi kwa sababu ya kujitolea kwangu kuheshimu dini yangu."

"Ni muhimu kwangu kwamba niliiambia mahakama kwamba sikunywa pombe makusudi. Jaji akinihukumu mwenye alikubali kwamba sikuwa nimekunywa pombe makusudi."
Amesema kesi yake ilihitimishwa Jumatatu na kwamba alikubali shtaka.
"Kuendesha gari ukiwa mlevi ni kosa kubwa na ingawa sikunywa pombe makusudi, nakubali marufuku na faini na naomba radhi kwa yaliyotokea," aliongeza.