Alibaba

mardi 24 janvier 2017

Huyu ndie mwamuzi atakae chezesha mechi ya Liverpool dhidi ya Chelsea

Mwamuzi Mark Clattenburg ameteuliwa kuchezesha mechi ya Chelsea dhidi ya Liverpool katika uwanja wa Anfield wiki ijayo.
Chelsea watasafiri hadi Anfield wiki ijayo siku ya Jumanne (Januari 31) wakiwa na pointi 10 dhidi ya timu ya Jurgen Klopp.

Clattenburg ana historia kadhaa anapo chezesha mechi za Chelsea, mechi ya mwisho msimu uliopita katika uwanja wa Stamford Bridge dhidi ya Tottenham Hotspur ikizua utata.

Kadi kumi na mbili za njano zilitolewa katika pambano hilo, na vitendo vya vurugu baina ya wachezaji katika sare ya 2-2.
Chelsea na Tottenham zilitozwa faini ya paundi 375,000 na 225,000 mwenyeji kuhusika katika kile kilichotokea, lakini Clattenburg hakuweza kutoa kadi nyekundu katika mechi hiyo.

Hii itakuwa mara ya pili kwa mwamuzi huyo kutoka County Durham kuchezesha mechi ya Chelsea msimu huu, baada ya kuchezesha Blues wakishinda 3-0 dhidi ya Burnley mwezi Agosti.

Mimi siwezi kuoa kwa sababu fulani kaoa – Chege

Msanii mkongwe wa muziki Chege Chigunda amedai hawezi kufuata mkumbo kuoa kwa sababu fulani kaoa.
Muimbaji huyo ambaye hivi karibuni ameachia wimbo mpya “Kelele za Chura” akiwa amemshirikisha Nandy, amedai suala la kuana linakuja kutoka kwa Mungu na sio kuigana.


“Mimi siwezi kuoa sijui kwa sababu nikienda kwenye interview nitaulizwa, mbona wewe haujaoa, mbona mwenzako kaoa, na siwezi kuoa kwa sababu Mh Temba kaoa,” Chege aliiambia Global TV. “Mimi nitaoa pindi tu mwenyezi Mungu atakaposema Chege oa lakini sio kwa sababu fulani kafanya hivyo,”
Muimbaji huyo ni msanii pekee wa Kundi la TMK Wanaume Halisi ambaye bado anafanya vizuri katika muziki.

Nimeanza kuupenda muonekano wangu, sitaki tena kuuharibu kwa sumu – Ray C

Msanii mkongwe wa muziki Ray C amedai ameupenda muonekano wake mpya huku akijipa mtihani wa kujizua kurudi katika mambo ambayo yalimpelekea kuupoteza muonekano wake mzuri wa mwili.

Ray C ndani ya muonekano mpya
Muimbaji huyo hivi karibuni amekuwa akipost picha zake mpya ambazo zinamuonyesha akiwa na muonekano mzuri hali ambayo imewafanya mashabiki wake katika mitandao ya kijamii kuona kweli mrembo huyo ana nia ya kubalika na kutoka katika matumizi ya Madawa ya kulevya.
Jumanne hii muimbaji huyo amepost picha yake katika mtandao na kuandika: Nimeanza kumpenda Huyu dada Ray C sitaki kumdhuru tena kwa sumu wala bunduki nataka Azidi kunivutia kila nimuonapo kiooni.

Kwa sasa muimbaji huyo anarekodi nyimbo zake katika studio ya Wanene Entertainment kufanya maandalizi ya ujio wake mpya