Alibaba

mercredi 19 avril 2017

UEFA: Real Madrid yailaza Bayern Munich 4-2 Ligi ya Mabingwa Ulaya

Cristiano Ronaldo alifunga mabao matatu na kuwawezesha mabingwa watetezi wa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya Real Madrid kuwatimua Bayern Munich kutoka kwenye michuano ya msimu huu katika hatua ya robofainali.
Mechi hiyo iliyomalizika 4-2 hata hivyo ilijaa utata na mshindi alipatikana katika muda wa ziada.

Kiungo wa kati wa Bayern Munich Arturo Vidal alitimuliwa uwanjani dakika ya 84 jambo ambalo lilionekana kuathiri mwelekeo wa mechi hiyo.
Ronaldo naye alionekana kuwa alikuwa ameotea alipokuwa anafunga bao la pili la Real muda wa ziada.
Bayern, ambao walihitaji mabao mawili kusonga, alikuwa wameongoza kupitia penalti iliyofungwa na Robert Lewandowski.

Madrid walitatizika kutamba kwenye mechi hiyo iliyochezewa Bernabeu kabla ya Ronaldo kufunga kwa kichwa kutokana na krosi ya Casemiro.
Bayern walijibu sekunde 36 baadaye Sergio Ramos alipojifunga na kulazimisha mechi hiyo kuingia muda wa ziada.
Ni hapo ambapo Ronaldo alifunga bao la utata la Madrid.
Nahodha huyo wa Ureno kisha alifunga la tatu - lake la 100 katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya. Marco Asensio aliwakamilishia ushindi kwa kuongeza la tatu.

Madrid watamfahamu mpinzani wao nusufainali wakati wa droo Ijumaa.
Majirani wao Madrid Atletico Madrid walisonga kwa kuwaondoa Leicester City.
Kwenye robofainali hizo nyingine, Barcelona wanakutana na Juventus nao Monaco wakutane na Borussia Dortmund baadaye Jumatano.

Mashabiki wamrushia panya mchezaji nchini Denmark

Mechi ya ligi kuu ya Denmark kati ya Brondby na FC Copenhagen ilitibuka baada ya mashabiki kuwarushia panya waliokufa uwanjani.
Mashabiki wa Brondby walimrushia panya mlinzi wa Copenhagen Ludwig Augustinsson alipokwenda kupiga kona.

Copenhagen ilishinda mechi hiyo 1 - 0 na sasa ni wa kwanza huku ikiishindia timu ya pili ambayo ni Brondby kwa alama 13.
"Sio vyema kuwa na baadhi ya wageni ambao hawawezi kuwa na tabia njema," alisema mkurugenzi wa michezo wa Brondby, Troels Bech.

Video iliyorekodi yaliyotokea uwanjani inaonyesha mchezaji wa Slovenia Benjamin Verbic akimsaidia mwenzake Augustinsson kuwatoa angalau panya wawili kutoka uwanja huo wa Brondby ambao unaweza kubeba mashabiki elfu 28.
Brondby ni mabingwa mara 10 wa Denmark na FC Copenhagen inayosimamiwa na aliyekuwa meneja wa Wolverhampton Wanderers Zamani Solbakken, wameweza kunyakua ushindi mara 11