Alibaba

lundi 17 octobre 2022

Kuna Wachezaji mashoga EPL

Mwanasoka wa zamani wa England ambaye kwa sasa ni Mtangazaji wa michezo Gary Lineker (61), amedai kuwa anawajua wachezaji wawili wa Ligi ya England ambao ni mashoga na anatumani kuwa watajitokeza hivi karibuni.


”Huu ndio wakati mwafaka, wakati tunakaribia Kombe la Dunia,mjitokeze mtetee msimamo wenu ”

Akizungumza na gazeti la Daily Mirrow, Lineker alisema “Ninajua kwa uhakika kabisa kuwa hawa watu walikuwa karibu sana kujitokeza, ninawajua ni wapenzi wawili, lakini siwezi kuwataja,”

”Hofu ya Mashabiki na ukosoaji kutoka kwa wachezaji wenzao ndio unawafanya wengi wajifiche, na kubaki wakiishi maisha ya uwongo,”

”Ninajua ni ngumu sana, lakini nilikuwa natamani mjitokeze tu, sababu najua mpo, ni dhahiri kuna wachezaji wengi ambao wanalazimika kuishi kwa uwongo.”

Kombe la Dunia litafanyika mwezi ujao nchini Qatar ambako kutokana na sheria kali za Kiislamu mahusiano ya jinsia moja hayakubaliki na hukumu yake ni kifo.