Alibaba

dimanche 20 novembre 2022

Vivutio vikubwa Qatar kwa sasa ni Stadium 974

Moja kati ya vivutio vikubwa nchini Qatar ni uwanja wa 974 utakaotumiwa katika michezo ya Fainali za Kombe la Dunia 2022.


Upekee wa uwanja huo pamoja na mambo mengine ni kwamba baada ya Fainali za Kombe la Dunia 2022 utabomolewa na vifaa vyake kutolewa msaada kwa nchi zinazoendelea.


Uwanja huo umepewa jina la 974 kwa maana mbili kwanza ndio code ya kimataifa ya simu ya Qatar  pili umejengwa kwa idadi ya makontena 974 upo Doha Qatar na unachukua mashabiki 40,000, uwanja huu hauna AC kama vilivyo viwanja vingine.


Qatar world cup 2022