Alibaba

lundi 16 janvier 2023

super Cup d'Espagne 2022-2023

Barcelona 🏆
.Taji la kwanza la kocha Xavi Hernandez akiwa kocha wa Barcelona , katoa kichapo cha 3-1 dhidi ya Real Madrid ( fainali ya Spanish Super Cup ) 

.Bando langu limeenda kwa haki kabisa kushuhudia 

1: Pressing iliyoshiba ya Barcelona , mmoja akienda kwenye mpira wengine wanafunga njia za pasi kwamba yule mchezaji wa Real Madrid mwenye mpira anakosa options za kupasia 

2: Pedri ( 19 ) na Gavi ( 18 ) utasema wana miaka 29 na 30 wanacheza kwa maturity kubwa , Pasi zao , wanavyo control mchezo , energy na ukiangalia miili yao unaweza kudharau uimara wa mwili wapo imara sana 
.Hawa Real Madrid jinsi walivyo sasa wanahitaji kuamka haraka sana , ni kama vile mafanikio kwao yanatosha , kama yale matamanio ya kupambana yanapotea tangu mechi dhidi ya Villarreal 
.Angalau sasa presha inapungua kwa Xavi kutwaa taji lake la kwanza na sasa yupo kileleni mwa La Liga na bado Barca wapo Europa . Kwa Real Madrid wana Liverpool hatua ya 16 bora UCL