Alibaba

jeudi 17 novembre 2016

Brazil kupanda hadi nafasi ya pili viwango vya Fifa mwezi huu

Timu ya soka ya wanaume ya Brazil inatarajiwa kupanda hadi kwenye nafasi ya pili kwenye viwango vipya vya mwezi huu kwenye shirikisho la soka duniani (Fifa) vinavyotarajiwa kutangazwa Novemba 24.

Viwango vya mwezi uliopita timu hiyo ilishika nafasi ya tatu huku nafasi ya pili ikishikiliwa na timu ya taifa ya Ujerumani na Argentina akiongoza orodha hiyo.

Hata hivyo imedaiwa kuwa timu hiyo ineweza kushika nafasi ya kwanza kwenye viwango hiyo endapo Argentina ingefungwa na timu ya taifa ya Colombia kwenye mchezo wa kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia Jumanne ya wiki hii.
Kwa sasa Brazil inaongoza kundi la timu za bara la Amerika ya Kusini zinazowania kufuzu kwenye kombe la dunia nchini Urusi mwaka 2018 ikiwa na pointi 27.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire