Alibaba

jeudi 17 novembre 2016

Mr T-Touch aeleza kwanini watayarishaji wa muziki hutoa beat bure kwa wasanii

Producer aliyetengeneza hits kibao, Mr T –Touch amefunguka kwa kuitaja sababu inayowafanya watayarishaji wengi wa muziki kuwapatia beat bure wasanii.

Mtayarishaji huyo amekiambia kipindi cha Ladha 3600 cha EFM, “Tunatoa beat bure ili tuweze kuaminiwa. Nimetoa beat za bure kwa takribani miaka mitatu.”

Touch ameongeza kuwa hakuna producer anayenufaika kupitia studio yake labda awe na kazi nyingine nje ya muziki. Kwa sasa Mr T anamiliki studio yake inayojulikana kwa jina la Touchez Sound aliyoifungua mwezi Julai mwaka huu.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire