Alibaba

jeudi 10 novembre 2016

Msomali achaguliwa katika bunge la Marekani

Ilhan Omar, mwenye umri wa miaka 34, ameweka historia kwa kuwa mbunge wa kwanza mwenye asili ya Kisomalia nchini Marekani.

Mwanamke huyo Muislamu mwenye asili ya Somali na Marekani ndio raia wa kwanza wa Kisomali kuchaguliwa katika wadhfa mkuu kama huo nchini Marekani.

Uchaguzi wake unajiri siku chache tu baada ya rais mteule Donald Trump kushtumu wahamiaji wa Kisomali mjini Minnesota kwa kueneza maoni ya itikadi kali.

Akisherehekea ushindi wake bi Omar amesema kuwa atakuwa sauti ya waliotengwa katika bunge la jimbo hilo.

''Nadhani nimeleta sauti ya akina mama vijana wanaotafuta fursa''.
Redio ya uma katika jimbo hilo ilimnukuu akisema kuwa alitoroka nchini Somalia na familia yake wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe wakati alipokuwa na umri wa miaka minane pekee.

Waliishi nchini Kenya kama wakimbizi kwa takriban miaka minne kabla ya kuelekea Marekani na kuishi katika jimbo lenye Wasomalia wengi la Minnesota.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire