Alibaba

vendredi 4 novembre 2016

UEFA Europa League TEAM OF THE WEEK

#UEFA Europa League TEAM OF THE WEEK
AS Roma's Edin Džeko , Athletic Club 's Aduriz and Fenerbahçe's Moussa Sow lead the attack!

ATLÉTICO MADRID, FERNANDO TORRES EN CHINE ?

En fin de contrat avec l'Atlético Madrid, Fernando Torres intéresserait le Guangzhou Evergrande. Le club chinois aimerait recruter l'attaquant espagnol dès cet hiver.

Adulé à Liverpool, Fernando Torres a peiné à s’imposer à Chelsea avant de se voir prêter à l’AC Milan pour un échec. De retour à l’Atlético Madrid, son club formateur, en janvier 2015, l’attaquant espagnol a réussi une saison convaincante en inscrivant 18 buts en 70 matches.

Simeone : "L"équipe a remercié Griezmann"

Prolongé d’une année supplémentaire, Fernando Torres connaît cependant un début de saison compliqué. Avec la confirmation d’Antoine Griezmann et de l’arrivée de Kevin Gameiro au club, l’international espagnol doit se cantonner à un simple rôle de remplaçant. Le joueur de 32 ans a seulement été titulaire 1 fois en 8 apparitions en Liga et a inscrit deux petits buts. En fin de contrat, l’ancien des Reds pourrait quitter l’ Atlético Madrid .

Selon les informations du média Mundo Deportivo, le Guangzhou Evergrande surveillerait la situation de Fernando Torres . Le club évoluant en Chinese Super League serait prêt à offrir un contrat en or pour s’attacher les services de l’attaquant dès ce mercato hivernal. Mais l’Espagnol détiendrait toujours une belle cote en Europe. La MLS serait également intéressée.

Mboga ya mchicha kugundua bomu

Wanasayansi wameweza kuifanya mboga ya aina ya Mchicha au 'Spinach' kugundua bomu.
Imearifiwa kwamba majani ya mchicha yanaweza kuhifadhi kemikali aina ya 'nitro-aromatics' ambazo hupatikana kwenye mabomu ya kutegwa arthini na silaha zinazozikwa arthini.

Siyo lazima mboga hii iwekwe nyaya yeyote ili kuweza kugundua bomu, bali mmoja anaweza kufahamu kwa kutizama au kwa taarifa maalum za simu.Utafiti huu umefanikishwa na Chuo Ki Kuu cha Massachusetts Institute of Technology-MIT.

Wanasayansi waliweka kemikali za carboni kwenye maji na kisha kufanya mizizi ya mboga kupitisha maji yale hadi kwenye matawi ya mchicha. Kisha wanasayansi wakapapasa majani ya mchicha na vyuma maalum.Majani yale yalianza kutoa chembechembe za moto ambazo zinaweza kuonekana kwa kompyuta.

Pia chembechembe hizo zinaweza kuonekana kwa simu ya mkononi. Wanasayansi sasa wanasema mboga ya mchicha pia inaweza kutumika kufahamu uwepo wa visima vya maji arthini, kemikali zilizovuja kutoka kwa silaha na madini ya nitro-aromatics. kwa sasa wananuia kuwezesha mboga hiyo kuweza kugundua bomu iliyotegwaa arthini kwa kwa mbali.

Mwanamke mwenye 'macho ya kushangaza' afungwa jela Pakistan

Mwanamke kutoka Afghanistan aliyepata umaarufu duniani picha yake ilipochapishwa kwenye ukurasa wa kwanza wa jarida la National Geographic mwaka 1985 alipokuwa msichana amehukumiwa kufungwa jela.

Sharbat Gula amepatikana na hatia ya kuishi Pakistan akiwa na stakabadhi bandia za utambulisho.
Amehukumiwa kufungwa jela siku 15 na pia akatozwa faini ya takriban dola elfu moja za Kimarekani.

Atarejeshwa Afghanistan baada yake kutumikia kifungo chake.

Muda wake wa kutumikia adhabu umeanza kuhesabiwa tangu siku alipokamatwa. Hii ina maana kwamba kuna uwezekano wake kuachiliwa kufikia Jumatatu.
Sharbat Gula alitoroka Afghanistan ilipokuwa chini ya utawala wa muungano wa Usovieti.
Picha yake kama mkimbizi, ambapo alionekana kuwa na macho makali, iliibuka kuwa kama nembo ya madhara ya vita Afghanistan.
Macho yake yalikuwa na rangi ya kijani, jambo lililomfanya kufahamika kwa jina 'Green-eyed Girl'.

Maafisa wanasema alikamatwa na Idara ya Uchunguzi ya Pakistan (FIA) baada ya uchunguzi wa miaka miwili Peshawar, karibu na mpaka wa nchi hiyo na Afghanistan.
Picha maarufu ya Bi Gula ilipigwa 1984 alipokuwa kambi ya wakimbizi kaskazini magharibi mwa Pakistan.
Wakati huo wanajeshi wa Muungano wa Usovieti walikuwa wameingia Afghanistan.

Mwaka 2002, mpiga picha Steve McCurry alimtafuta na kumpiga picha. Wakati huo alikuwa anaishi kijiji kimoja Afghanistan akiwa na mumewe na binti zao watatu.
Baada ya kutokea kwa habari za kukamatwa kwa Bi Gula, Bw McCurry alisema atafanya kila juhudi kumsaidia kifedha na kisheria.

Yaya Toure aomba msamaha Man City

Kiungo wa kati wa Manchester City amesalimu amri na kumuomba msamaha wasimamizi wa klabu hiyo baada ya kutochezeshwa kwa muda na meneja wa klabu hiyo Pep Guardiola.
Kupitia taarifa kwenye ukurasa wake wa Facebook, amesema: "Naomba radhi - kwa niaba yangu na watu wanaoniwakilisha - wasimamizi wa timu na wote wanaofanya kazi katika klabu hii kwa sababu ya suitafahamu zilizotokea awali.
"Matamshi hayo hayawakilishi msimamo wangu kuhusu klabu au watu wanaofanya kazi katika klabu hii."

Wiki iliyopita, Guardiola aliambia wanahabari kwamba anamuhitaji Toure lakini bado anasubiri kuombwa msamaha na ajenti wa mchezaji huyo Dimitry Seluk.

Toure, 33, ameshiriki katika mechi moja kati ya mechi nane walizozicheza Manchester City msimu huu.
Baada ya kuachwa nje ya Guardiola kikosi cha wachezaji watakaocheza Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya, Seluk alisema kuwa kiungo huyo wa kati ''alifedheheshwa'' na kwamba Gurdiola anafaa kumuomba msamaha iwapo City haitashinda kinyang'anyiro hicho.

Ni hapo ambapo Guardiola alijibu na kusema Toure hangecheza tena hadi ajenti huyo aombe msamaha.
''Sitakubali kama kocha kila ajenti, kwenda kwa vyombo vya habari kuwasilisha malalamiko yao iwapo mchezaji wake hajashirikishwa kwenye kikosi," Guardiola alisema.
Guardiol alikuwa kocha mkuu Barcelona Toure alipouzwa kwa Manchester City mwaka 2010.

Mourinho akerwa na wachezaji wa Manchester United

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho amesema wachezaji wa Manchester United walichukulia mechi dhidi ya Fenerbahce katika Europa League kana kwamba ilikuwa mechi ya kirafiki ya kujiandaa kwa msimu.

Red Devils walishuka hadi nambari tatu kwenye Kundi A ligi hiyo ndogo ya Ulaya baada ya kulazwa 2-1 na klabu hiyo ya Uturuki mjini Istanbul.

Manchester United sasa wameshinda mechi mbili pekee kati ya saba walizocheza mashindano yote karibuni.

"Timu inayofunga baada ya dakika mbili pekee ni timu ambayo haiko tayari, haijajiandaa kiakili, haina mwelekeo na haina umakinifu," amesema Mourinho.

United wamefunga mabao mawili pekee mechi zao nne walizocheza karibuni zaidi.

Aidha, walifungwa baada ya sekunde 30 pekee na Chelsea na sekunde 65 na Fenerbahce.
Mshambuliaji Moussa Sow alifunga kwa kombora la kushangaza la kupitishia mpira juu ya kichwa, naye Jeremain Lens akaongeza jingine kupitia frikiki kabla ya Wayne Rooney kufunga bao la kufutia machozi mechi ikikaribia kumalizika.

Bado lake hilo la dakika ya 89 limemuwezesha kufikia magoli 38 Ulaya na kufikia rekodi ya Ruud van Nistelrooy.

Hata hivyo, amefunga mabao mawili pekee katika mechi 17 alizocheza msimu wote.

Mourinho amesema: "Matatizo yetu yalianza na mtazamo wetu wa kiulimwengu. Walikuwa wanacheza fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya, tulikuwa tunacheza mechi ya kirafiki ya majira ya joto. Huo ndio uhalisia wa jinsi mechi ilianza.

"Walistahili kushinda, soka haihusu tu ubora, kuna kutia juhudi pia, kujitolea, kujituma na kujitolea kabisa. Lazima ucheze dakika zote 90 kwa hamu na umakinifu.

"Katika mazingira kama haya, kuwapa nafuu wapinzani wako (kwa kufungwa mapema), hapo ndipo wanataka kuwa. Kisha, tulituliza kasi ya uchezaji na kuanza kumshinikiza refa, kuigiza kwamba tumechezewa vibaya na hayo ndiyo makosa yetu."

Meneja huyo wa zamani wa Chelsea hata hivyo alikiri kuwa "moja ya mambo mazuri leo ni kwamba Rooney hatimaye amefunga bao."
Kati ya wachezaji walionunuliwa na Mourinho majira ya joto - Paul Pogba, Zlatan Ibrahimovic, Henrikh Mkhitaryan na Eric Bailly - ni Mfaransa Pogba pekee aliyeanza mechi.

Hata hivyo, aliondoka kabla ya kipindi cha kwanza kumalizika akionekana kuumia.
Ibrahimovic aliiingia nafasi yake.
Mkhitaryan naye alichezeshwa mara ya kwanza tangu 10 Septemba. Aliingia dakika ya 61 nafasi ya Marcus Rashford. Beki wao Bailly anatarajiwa kukaa nje miezi miwili kutokana na jeraha la goti.

Haijabainika jeraha la Pogba ni mbaya kiasi gani na iwapo ataweza kucheza dhidi ya Swansea Ligi ya Premia Jumapili.

Majeruhi United
-------------

Pogba, aliyetoka Juventus, amejiunga na orodha ya majeruhi wengi United amba wanajumuisha mabeki:

- Eric Bailly (kano za goti) - hatacheza hadi Desemba
- Antonio Valencia (mkono) - haijulikani atarejea lini
- Chris Smalling (mguu) - haijulikani atarejea lini

Magazeti Uingereza yalivyoandika baada ya United kuchapwa:

Huawei yazindua simu mpya ya Mate 9

Huawei imezindua simu mpya yenye skrini kubwa wakati huu ambapo simu ya Samsung Galaxy Note 7 inakumbwa na changamoto.

Simu hiyo kwa jina Mate 9, ni kati ya simu za kwanza zinazotumia teknolojia ya Android 7 na inakuja ikiwa katika aina mbili za kamera.
Kampuni hiyo ya China inasema kuwa imeshughulikia tatizo la simu hizo kupoteza mauzo baadaye.

Lakini mtaalamu mmoja anasema kuwa wateja bado wanazitilia shaka simu za kampuni hiyo.
Simu za Huawei hazijafikia viwango vya simu za Samsung na ndiyo sababu huwa inafanya ushirikiano na kampuni zingine kama Leica na Porsche kuboresha teknolojia yake ya Kamera.

Samsung ilitizisha uundaji wa simu ya Note 7 mwezi uliopita baada ya simu kadha kuwaka moto.