Alibaba

samedi 17 décembre 2016

Barua ya Mohammad Ali kwa Mandela yauzwa pauni 7,200

Barua iliyowekwa sahihi na mwanamasumbwi Mohammad Ali na kuandikiwa rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela, akitoa rambu ramba zake kufuatia kuawa kwa mtu aliyekuwa akipinga ubaguizi wa rangi imeuzwa kwa pauni 7,200.
Muuzaji wa barua hiyo Andrew Aldridge alisema, "ni vyema kuwa Mohammad Ali alikuwa mwanamichezo bora zaidi hukui naye Nelson Mandela akiwa mtu mashuhuri zaidi katika karne iliyopita.
Barua hiyo ilipiwa chapa cha msaidizi wa meneja wa hoteli ya Elangeni iliyo mjini Durban ambapo Ali alikuwa akiishi wakati huo.
Barua hiyo iliyouzwa kwa mnunuzi kutoka nchini Marekania ilitarajiwa kuuzwa kwa kati ya dola 6,000 na 8,000.

Muhammad Ali alikuwa nchini Afrika Kisini kwa kipindi kifupi mwezi Aprili mwaka 1993 baada ya kuwasili muda mfupi baada ya kuuliwa kwa Chris Hani tarehe 10 mwezi Aprili.
Hani alikuwq kamanda wa kundi la Umkhonto We Sizwe, kundi lililojihami la ANC.
Alikuwa mkosoaji mkubwa wa serikali ya ubaguzi wa rangi na aliuaw mkereketwa mmoja nje ya nyumba yake eneo la Boksburg.

Muhammad Ali's letter of condolence to Nelson Mandela up for sale


A signed letter from Muhammad Ali to Nelson Mandela offering his condolences on the death of an anti-apartheid leader will be sold at auction.
The letter, dated April 13 1993, is typed and signed by Ali on letter-headed Muhammad Ali in South Africa stationery.
It was typed by the personal assistant to the general manager of the Elangeni Hotel in Durban where Ali was staying at the time.
Ali requested the letter typed to express his condolences to Mandela on the loss of Chris Hani, who was assassinated on April 10 1993.
It will be sold at Henry Aldridge and Son in Devizes, Wiltshire, next Saturday and is expected to fetch between £6,000 and £8,000.
The letter reads:
"Dear Mr Mandela
"Allow me to extend to you and the A.N.C. my deepest regrets upon hearing of the death of Chris Hani. My prayers go out to Mr Hani's family and the people of South Africa during these difficult days.
"I am providing you the following information regarding my itinerary should you desire to contact me (prior to our scheduled meeting on 19 April 1993):-
"CAPE SUN - 13 TO 16 APRIL - TEL: 021 238844 FAX: 021 238875
"JOHANNESBURG GARDEN COURT - 16 TO 22 APRIL - TEL: 011 297011 FAX: 011 291515
"Inshallah, I pray that God keeps you safe"
A letter signed by the personal assistant who typed it includes: "Due to my nervous excitement about typing a letter of such historical importance I misspelt the name Muhammad replacing the last "a" with an "e".
"The letter was taken to Muhammad Ali and duly signed before someone noticed the error and returned it to me. I typed it again but kept the incorrect copy for posterity."
Auctioneer Andrew Aldridge said the letter was from one of the greatest sportsmen to one of the greatest men in history.

"It is a truly iconic cross collectable and will appeal to collectors of Ali memorabilia as well as those who collect Nelson Mandela material, items relating to apartheid, political history and collectors of iconic memorabilia," Mr Aldridge added.
"Muhammed Ali was only in South Africa for a short period in April 1993, arriving shortly after the assassination of Chris Hani on April 10.
"Hani was the chief of staff of Umkhonto We Sizwe, the armed wing of the African National Congress (ANC). He was a fierce opponent of the apartheid government and was murdered by a far right extremist outside of his home in Boksburg.
"Against that backdrop Ali arrived in South Africa at a time when the country stood on the edge of a precipice with civil war a possibility.
"He attended Hani's farewell at the FNB Stadium in Johannesburg on April 19th 1993, when he appeared to the crowd, they chanted "Ali! Ali!"."
Mr Aldridge said Mandela kept a photograph of himself with Ali on his desk and his favourite book, in his later years, was an autographed copy of Ali's biography.

Mwana FA asema wimbo ‘Muziki’ wa Darassa umerudisha heshima kwa wana hip hop

Msanii wa muziki wa hip hip, Mwana FA amesema hatua ya mafanikio ya wimbo ‘Muziki’ wa Darassa ni hatua ambayo wasanii wengi wa muziki wa hip hop walishindwa kuifikia kwa muda mrefu.

Rapa huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo wake ‘Dume Suruali’ amesema ni muda mrefu wasanii wa hip hop walikuwa wanashindwa kutoa ngoma ambazo zitaleta ushindani mkubwa na zawasanii wa kuimba.

“Kwanza I’m happy for rap music,” FA alikiambia kipindi cha FNL cha EATV. “Imekuwa muda mrefu hatujawahi kutengeneza nyimbo halafu zikatoka na nyimbo za waimbaji, halafu usisikie nyimbo za waimbaji na rap music ikawa vile,

Mwana FA amesema anapenda kuona Darassa akiendelea kufanikiwa zaidi katika muziki kwa kuwa ni msanii ambaye anaujua uwezo wake katika kile anachokifanya.

Wimbo ‘Muziki’ wa Darassa umeweza kufanya vizuri kwenye chart mbalimbali za muziki. Pia kupitia channel ya mtandao wa YouTbe video ya wimbo huo imeweza kuangaliwa mara 1,787,074 katika kipindi cha wiki tatu.

Mahakama ya Uganda yaamuru kukamatwa kwa Wizkid

Wizkid anakabiliwa na kifungo cha miaka 11 jela, baada ya mahakama ya Uganda kutoa hati ya kukamatwa kwake na meneja wake, Sunday Aare.
Wizkid alishindwa kutokea kwenye show iliyokuwa ifanyike December 3 mwaka huu mjini Kampala. Kampuni iliyomlipa, Face TV, kupitia mwanasheria wake, Fred Muwema, imepata kibali cha kumkamata muimbaji huyo kwa kuchukua dola $60,000 na kushindwa kutokea kwenye show. Gharama zingine walizotoa ni brokerage fee, $5,000 na per die, $3,000 kwa muda ambao Wizkid angekaa Uganda.
Muimbaji huyo alidaiwa kushindwa kusafiri na ndege toka Marekani kwenda nchini humo kwa show hiyo.
“Between 29th August 2016 and 29th November 2016, our client (Face TV) paid to Mr. Sunday Are, Wizkid’s manager the full performance fee of US$60,000, a brokerage fee of US$5,000 and US$3,000 being per diem for the days they were going to stay in Uganda,” yanasomeka maelezo ya mlalamikaji.
Zaidi ya watu 25,000 walikuwa wamenunua tiketi kwaajili ya show hiyo. Maelezo yaliyowasilishwa mahakamani yameeleza kuwa mwandaaji wa shiw hiyo amekula hasara ya zaidi ya $300,000 kutokana na maandalizi aliyofanya.
 

Ban Ki-moon kugombea urais Korea Kusini

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amedokeza kuwa huenda akawania urais nchini mwake, Korea Kusini.
Muhula wake Ban kama katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa unakamilika mwisho wa mwezi huu wa Disemba
Wakati wa mkutano wake wa mwisho na waandishi wa habari, Ban alisema kuwa baada ya kupata mapumziko anarudi nchini mwake Korea Kusini kuona vile ataisaidia nchi yake.
Uchaguzi wa uraia nchini Korea Kusini unatarajiwa kufanyika Desemba mwaka 2017


Lakini huenda uchaguzi huo ukafanyika katika muda wa miezi miwili baada ya bunge la nchi hiyo kupiga kura ya kumuondoa madarakani Rais Park Geun-hye, kutokana na sakata, ambapo analaumiwa kwa kumruhusu rafiki wake wa karibu kunufaika kifedha.
Ikiwa mahakama ya katiba itadumisha kura hiyo ya kumuondoa, atakuwa rais wa kwanza wa Korea Kusini aliye madarakani kuondelwa katika kipindi cha uhuru wa nchi hiyo.
Mahakama ya katiba ina siku 180 kutoa uamuzi wa mwisho.
Matamshi ya Ban yanakuja huku yakishuhudiwa maandamano kwenye mji mkuu wa Korea Kusini, Seol.

Oscar kuwazidi Messi na Ronaldo kwa kulipwa pesa nyingi

Mchezaji wa Chelsea Oscar anatarajiwa kuwa mchezaji soka anayelipwa pesa nyingi zaidi duniani atakapohamia Ligi Kuu ya Uchina mwezi Januari.
Shanghai SIPG wanatarajiwa kulipa £60m kumchukua kiungo huyo wa kati kutoka Brazil.
Akifanikiwa kuondoka, basi Oscar, 25, ataungana na meneja wa zamani wa Chelsea Andre Villas-Boas, ambaye kwa sasa ndiye mkufunzi wa Shanghai.
Taarifa zinasema atakuwa analipwa £400,000 kila wiki (£20.8m kila mwaka), ingawa huenda akapitwa haraka kwani kuna taarifa kwamba klabu za China zinajiandaa kulipa pesa nyingi kununua wachezaji wengine Januari. Mshahara wa Oscar ni sawa na £57,143 kila siku, au £2,381 kwa saa, au £39 kila dakika.
Kuna taarifa huenda Shanghai Shenhua ,ambao mkufunzi wao kwa sasa ni Gus Poyet aliyetoka Sunderland, wanapanga kumnunua nyota wa zamani wa Manchester United na Manchester City Carlos Tevez kutoka Boca Juniors. Tevez atakuwa analipwa £31.5m kila mwaka, sawa na £605,000 kila wiki.

France Football wanasema mshambuliaji wa Paris St-Germain na Uruguay Edinson Cavaninaye huenda akahamia Tianjin Quanjian, walio chini ya beki wa zamani wa Italia Fabio Cannavaro, kwa euro 50m (£41.79m) fambapo atakuwa akilipwa £16.7m kila mwaka.
Mwenzake kwenye klabu Javier Pastore kutoka Argentina pia huenda akahamia China.
Kiungo wa kati wa Arsenal Alexis Sanchez pia amehushishwa na kuhamia Hebei China Fortune, ambayo mkufunzi wake kwa sasa ni aliyekuwa meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini. Sanchez, anatarajiwa kulipwa £500,000 kila wiki iwapo atakubali kuhama.
Klabu ambazo zimetumia pesa nyingi zaidi karibuni nchini China ni Shanghai SIPG, Jiangsu Suning, mabingwa wa ligi Guangzhou Evergrande Taobao na Shanghai Shenhua.
Klabu za Ligi Kuu ya China zilitumia £200m kununua wachezaji kabla ya kuanza kwa ligi 2016.
Rekodi ya wachezaji ilivunjwa mara tatu kipindi cha siku 10. Jiangsu Suning walilipaShakhtar Donetsk £38.4mkumchukua Mbrazil Alex Teixeira baada ya kumchukua Ramires for £25m kutoka Chelsea siku chache awali.

Guangzhou Evergrande Taobao walimnunua nyota wa Colombia Jackson Martinez £31m kutoka Atletico Madrid.
Bei ya Teixeira hata hivyo ilipitwa na ya £46.1m (euro 55.8m) waliyolipa Shanghai SIPG kumchukua Mbrazil Hulk kutoka Zenit St Petersburg.

WACHEZAJI WANAOLIPWA PESA NYINGI ZAIDI DUNIANI
-------------------------

1) Oscar (Shanghai SIPG) £400,000 kila wiki £20.8m kila mwaka (kuanzia Januari)

2=) Cristiano Ronaldo (Real Madrid) £365,000 kila wiki £19m kila mwaka (kabla ya kutozwa kodi)

2= Lionel Messi (Barcelona) £365,000 kila wiki £19m kila mwaka(kabla ya kutozwa kodi)

4) Gareth Bale (Real Madrid) £346,000 kila wiki £18m kila mwaka(kabla ya kutozwa kodi)

5) Hulk (Shanghai SIPG) £317,000 kila wiki £16.5m kila mwaka

6) Paul Pogba (Manchester United) £290,000 kila wiki £15m kila mwaka

7) Neymar (Barcelona) £289,000 kila wiki £15m kila mwaka(kabla ya kutozwa kodi)

8=) Graziano Pelle (Shandong Luneng) £260,000 kila wiki £13.5m kila mwaka

8=) Wayne Rooney (Manchester United) £260,000 kila wiki £13.5m kila mwaka

10) Zlatan Ibrahimovic (Manchester United) £250,000 kila wiki £13m kila mwaka