Alibaba

vendredi 30 décembre 2016

Dully Sykes: Baada ya miaka 3 au 5 nitawapatanisha Alikiba na Diamond

Msanii mkongwe na mtayarishaji wa muziki nchini, Dully Sykes amedai kuwa baada ya miaka mitatu au mitano kupita atakuwa na uwezo wa kulimaliza bifu la Diamond na Alikiba.


Hitmaker huyo wa ‘Inde’ alikiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio Jumanne hii kuwa kuwapatanisha wasanii hao kwa sasa ni ngumu kwakuwa kila mmoja anataka sifa na kuwa juu zaidi ya mwingine.


“Kuwapatanisha inawezekana lakini si kwa sasa,” alisema. “Hii waliyofikia ni sifa kila mtu anataka sifa na kila mtu anataka kuwa mkubwa, kwahiyo mimi nitasubiri baadaye kidogo itakapofikia muda kama miaka mitano hivi mbele au mitatu Mungu akipenda na vuguvugu hili litakapokwisha mimi nina uwezo wa kuwakutanisha na kuwaambia ugomvi umekwisha. Lakini kwa ugomvi wao kupatana leo au kesho kwa sasa si kweli,” aliongeza.

Dully aliongeza kuwa kwa sasa ni ngumu kuwapatanisha wasanii hao kwa kuwa nyuma yao kuna watu wengi ambao wote kwa pamoja kuelewana kwa sasa itakuwa ni ngumu.

Nikikutana na Alikiba tunaongea na kucheka, ananiambia nafanya kazi nzuri – Rayvanny

Msanii wa muziki kutoka label ya WCB, Rayvanny amefunguka na kuzungumzia mahusiano yake na Alikiba ambaye ni mpinzani mkubwa wa boss wake Diamond Platnumz.
Muimbaji huyo ambaye bado anafanya vizuri na wimbo Salome alioshirikishwa na Diamond, amedai yeye hana tatizo na Alikiba na hata ikitokea nafasi ya kolabo atafanya naye.


“Alikiba huwa nikikutana naye huwa napiga naye stori, tunasalimiana tunacheka, ananiambia kuwa nafanya kazi nzuri, hatujawahi kuongea sana,” Rayvanny alikiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM.

Aliongeza,”Ikitokea siku naweza kufanya naye kolabo kwasababu ‘end of the day’ wote tunafanya muziki ni biashara pia, mashabiki wetu wanapenda kuona ‘combination’ za watu tofauti tofauti, hata nikikutana naye hatufungiani vioo,”

Diamond na Alikiba wamekuwa wenye bifu kwa muda mrefu huku mashabiki katika mitandao ya kijamii wakidaiwa kulichochea bifu hilo zaidi.


Ronaldo akataa mshahara wa £1.6m kwa wiki kutoka klabu ya China

Klabu ya Real Madrid ilipewa takriban pauni milioni 250 na klabu ya China ambayo haikutajwa jina ili kumnunua nyota wake Cristiano Ronaldo kulingana na ajenti wake Jorge Mendes.
Amesema kuwa nahodha huyo wa Portugal mwenye umri wa miaka 31 hana haja na mpango huo ambao ulishirikisha mshahara wa kila mwaka wa pauni milioni 85.
Ronaldo alisema kuwa anaweza kucheza kwa miaka mingine 10 mnamo mwezi Novemba baada ya kuandikisha mkataba mpya na Real Madrid hadi Juni 2021.


''Soko la China ni soko jipya.wanaweza kuwanunua wachezaji wengi, lakini haiwezekani kumnunua Ronaldo'', alisema Mendes.
''Cristiano ndio mchezaji bora duniani, ni kawaida kupata maombi'', aliongezea raia huyo wa Ureno.
Chini ya ombi hilo analodai Mendes, Ronaldo angepokea kitita cha pauni milioni 1.6 kwa wiki ikiwa ni mara tatu ya zaidi ya kitita cha uhamisho wa pauni milioni 89 zilizogharimu uhamisho wa Paul Pogba kutoka Juventus kuelekea Manchester United.
Mendes aliambia Sky Italia: Klabu ya China imetoa pauni milioni 257 kwa Real Madrid na zaidi ya Yuro milioni 100 kila mwaka kwa Ronaldo.
''Lakini fedha sio kila kitu.Klabu hiyo ya Uhispania ndio maisha yake''.
Hatua hiyo inajiri baada ya klabu ya Shanghai Shenhua kutoka China kuthibitisha kwamba imemsajili aliyekuwa mshambuliaji wa Manchester City Carlos Tevez kutoka klabu ya Boca Juniors.
Shanghai inayofunzwa na aliyekuwa mkufunzi wa Brighton Gus Poyet ,wameripotiwa kukubali uhamisho wa pauni milioni 40 mbali na mshahara wa zaidi ya pauni milioni 310,000 kwa wiki.