Alibaba

vendredi 3 février 2017

Nyumba ya Nicki Minaj yaporwa Marekani

Polisi kwenye jimbo la Los Angeles nchini Marekani wanachunguza wizi uliofanyika kwenye nyumba ya Nicki Minaj amabapo malia ya thamani ya dokl 175,000 iliibiwa.


Wizi huo ulitokea kwenye nyumba yake ya kifahari eneo la Beverly Hills lakini mwanamuziki huyo hakuwa nyumbani wakati huo.

Inaripotiwa kuwa nyumba hiyo ilivunjwa wakati wa uvamizi huo na baadhi ya nguo za Nicki Minaj kuibiwa.
Fanicha iliharibiwa huku picha na chupa za manukato zilivunjwa.
Bado haijulikani ni vipi waalifu waliingia nyumbani humo.

Waliiba vito vya thamani na bidhaa zingine zenye gharama ya dola 175,000.


Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire