Alibaba

vendredi 3 février 2017

Haya ndio maamuzi ya Frank Lampard kuhusu soka

Mchezaji wa zamani wa vilabu vya West Ham, Manchester City, Chelsea, New York City na timu ya taifa ya Uingereza Frank Lampard ambaye anamiaka 38, ametangaza rasmi kustaafu kucheza soka na kusalia kuwa mtazamaji na kuchukua mafunzo ya Ukocha.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Lampard ametoa uamuzi huo kwa kuandika ujumbe huu.

Frank Lampard ameshinda mataji matatu ya EPL, Makombe manne ya FA, vikombe viwili vya kombe la Ligi, Taji moja la Klabu Bingwa Ulaya na Europa, na kumfanya atimize michezo 1039 na Magoli 302 kwa miaka 21 aliyoitumikia kama mchezaji kwenye vilabu mbalimbali na timu yake ya taifa.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire