Alibaba

mardi 1 mars 2022

BOSI WA GSM, GHALIB AFIWA NA BABA YAKE MZAZI


Mfanyabiashara Ghalib Said Mohamed (GSM) amefiwa na Baba yake, Mzee Said Mohamed ambaye amefariki dunia alfajiri ya leo March 1 2022 na atazikwa leo saa kumi jioni kwenye makaburi ya kisutu Dar es salaam.


Marehemu Mzee Said ni Mfanyabiashara wa muda mrefu Tanzania ambapo alianzisha biashara ya kwanza mwaka 1955 kwa kuuza bidhaa ndogondogo Tanga lakini baadae alihamia kuuza nguo na kuhama kutoka Tanga hadi Songea ambako alijitanua katika kilimo cha korosho ambacho Familia yake imekiendeleza hadi leo.


Inna lillahi wa inna ilayhi rajuun

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire