Alibaba

vendredi 3 février 2017

Michuano ya ligi kuu Uingereza wikendi hii

Chelsea wako kifua mbele katika ligi na alama 9 na wanaweza kujiimarisha kileleni wakati wakiipokea Arsenal ilio nafasi ya tatu.

Mechi hii kwa Chelsea ni fursa kujivua aibu baada ya kulambishwa sakafu na arsenal bao tatu kwa bila katika mechi ya awali.

Na baada ya hapo ndio ulikuwa mwanzo mzuri wa Chelsea kufululiza na matokeo mazuri .
Arsenal ambao jumanne walipokea kichapao cha Watford , wana wasiwasi mkubwa hasa baada ya kiungo wake Aron Ramsey kuumia mguu.

Pia watakosa huduma za Granit Xaka anayetumikia adhabu huku Mohamed Elneny akiwa michezo ya fainali za kombe la Afrika na timu yake ya Misr.

Ushindani pia ni kati ya washambuliaji wawili Diego Costa wa Chelsea na Alexis Sanchez ambao wanaongoza kama wafungaji bora na mabao 15.

Katika mechi nyingine hapo kesho Tottenham ilio nafasi ya pili wanaipokea Middlesbourg.

Nayo Liverpool itasaka ushindi wake wa kwanza mwaka huu wakiwa ni wageni wa Hull City .

Jumapili, Manchester City wanachuana na Swansea City huku Leicester City wakiikaribisha Man U

Nyumba ya Nicki Minaj yaporwa Marekani

Polisi kwenye jimbo la Los Angeles nchini Marekani wanachunguza wizi uliofanyika kwenye nyumba ya Nicki Minaj amabapo malia ya thamani ya dokl 175,000 iliibiwa.


Wizi huo ulitokea kwenye nyumba yake ya kifahari eneo la Beverly Hills lakini mwanamuziki huyo hakuwa nyumbani wakati huo.

Inaripotiwa kuwa nyumba hiyo ilivunjwa wakati wa uvamizi huo na baadhi ya nguo za Nicki Minaj kuibiwa.
Fanicha iliharibiwa huku picha na chupa za manukato zilivunjwa.
Bado haijulikani ni vipi waalifu waliingia nyumbani humo.

Waliiba vito vya thamani na bidhaa zingine zenye gharama ya dola 175,000.


Haya ndio maamuzi ya Frank Lampard kuhusu soka

Mchezaji wa zamani wa vilabu vya West Ham, Manchester City, Chelsea, New York City na timu ya taifa ya Uingereza Frank Lampard ambaye anamiaka 38, ametangaza rasmi kustaafu kucheza soka na kusalia kuwa mtazamaji na kuchukua mafunzo ya Ukocha.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Lampard ametoa uamuzi huo kwa kuandika ujumbe huu.

Frank Lampard ameshinda mataji matatu ya EPL, Makombe manne ya FA, vikombe viwili vya kombe la Ligi, Taji moja la Klabu Bingwa Ulaya na Europa, na kumfanya atimize michezo 1039 na Magoli 302 kwa miaka 21 aliyoitumikia kama mchezaji kwenye vilabu mbalimbali na timu yake ya taifa.