Alibaba

vendredi 24 mars 2017

Arsenal imesitisha mazungumzo na Sanchez na Ozil

Kocha wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amesema klabu hiyo imesitisha kwa muda mazungumzo kuhusu mikataba ya Alexis Sanchez na Mesut Ozil hadi mwisho wa msimu.

Sanchez na Ozil mikataba yao katika klabu ya Arsenal inamalizika mwezi juni mwakani na wamekuwa wakisusua kusaini mikataba mipya ya kuendelea kuitumika timu hiyo.
Mfaransa huyo amesema hayo wakati akihojiwa na kituo cha BeiN Sports huku akikataa kuweka wazi mustabali wake klabuni hapo.
Arsenal wameshuka hadi nambari sita Ligi ya Premia baada ya kushindwa mechi nne kati ya tano walizocheza karibuni zaidi.
Kuhusu mustakabali wake, Wenger alisema: “Bila kujali nitasalia katika klabu hii muda gani bado nitabaki kujitolea na kuangazia kabisa (majukumu yangu) muda wote nitakaokuwa katika klabu hii.”
Gunners watarejea uwanjani Ligi ya Premia Jumapili tarehe 2 Aprili watakapokuwa wenyeji wa Manchester City.

Buffon kutengeneza rekodi nyingine timu ya taifa leo

Kipa wa klabu ya Juventus na timu ya taifa ya Italia, Gianluigi Buffon akizungumza na waandishi wa habari jana kuelekea mchezo wake 1,000 wakati timu yake ya taifa, Italia itakapoikaribisha Albania leo mjini Palermo katika mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia.
Amesema “Najiona ni mwenye furaha sana kufukisha mechi 1000 kwa taifa langu”, alisema Buffon ambaye alionekana kuwa ni mwenye furaha.

Buffon alicheza mechi yake ya kwanza Parma akiwa ana umri wa miaka 17 mwaka 1995, kabla ya kuhamia Juventus mwaka 2001 na kipa huyo ameichezea Italia kwa miaka zaidi ya 19 tangu Oktoba 29, mwaka 1997 akiwa ana umri wa miaka 19.

Harusi by The Light of Peace ( Nuuru Salaam ) official video



Abuchief.Com