Alibaba

lundi 19 septembre 2016

LES NOUVELLES RÈGLES POUR LE BALLON D'OR CONNUES

L'hebdomadaire France Football vient de divulguer une partie des nouvelles règles qui vont être appliquées pour l'élection du Ballon d'Or.

Le divorce entre France Football et la FIFA est consommé. Après cinq ans de collaboration pour l'élection du Ballon d'Or , les deux entités se sont séparées. La plus prestigieuse des récompenses individuelles redevient la propriété exclusive du célèbre hebdomadaire français. Un retour aux sources qui s'étend jusqu'aux règles qui sont adoptées dans les votes et l'annonce des nominés et du lauréat.

Il n'y aura pas de trio final de nominés

Comme c'était le cas avant 2010, FF vient d'annoncer que c'est uniquement le collège des journalistes, choisis un peu partout dans le monde, qui va procéder au vote. Les capitaines et sélectionneurs des différents pays affilés à la FIFA ne seront plus sollicités. Les journalistes retenus auront à établir un classement en choisissant entre non pas parmi 23 nominés, mais 30.

Par ailleurs, pour ce 61e Ballon d'Or, le choix a été fait de supprimer l'étape intermédiaire qui consiste à dévoiler les trois derniers nominés à quelques semaines du verdict. Enfin, l'heureux élu sera connu non pas au début de la prochaine année civile, mais dès le mois de décembre.

En revanche, une cérémonie sera toujours organisée pour couronner et dévoiler le lauréat au public. Des changements qui ont de quoi ravir les nostalgiques de la vieille formule.

PASTA Ajitia Kitanzi Baada ya Kutumia Waumini Picha zake Akiwa Uchi

Pasta mmoja Afrika Kusini alijitia kitanzi baada ya kutumia waumini picha yake akiwa uchi kwenye mtandao wa WhatsApp

– Pasta huyo ambaye ameoa alitaka kumjulisha mpenzi wake wa pembeni kwamba mkewe hakuwa nyumbani, lakini akaishia kuwatumia waumini wake ujumbe huo

Pasta Letsego aliye na kanisa lake Afrika Kusini alijitoa uhai baada ya kusemekana kuwa aliwatumia waumini picha ya uume wake kwenye mtandao wa Whatsapp wa kanisa hilo.

Ripoti zasema pasta Letsego ambaye ameoa alituma picha hiyo kimakosa kwa kikundi cha kanisa hilo kwenye Whatsapp, na kwamba alinuia kumtumia mpenzi wake wa pembeni.

“Mke hayupo, hii ni yako yote usiku wa leo,”pasta huyo akasema katika maelezo yaliyoandamana na picha hiyo.

Dakika chache baada ya kutuma picha hizo, waumini walianza kumshambulia vikali na akalazimika kujiondoa katika kikundi hicho cha Whatsapp.

Siku iliyofuata pasta huyo alipatikana amefariki, akining’inia kwa kamba shingoni katika nyumba yake aliyokodishiwa na kanisa.
Pasta Letsego ni mmoja wa wachungaji wa kanisa la Christ Embassy Church. Waumini wake walisema kuwa wamekuwa wakishuku kuwepo kwa uhusiano wa kimapenzi baina yake na mwanadada aliyenuiwa kupokea picha hizo.

“Vitendo vya pasta kwa muda mrefu vilikuwa vya kutiliwa shaka,” alisema mmoja wa waumini wa kanisa hilo.
“Mara kwa mara alionekana na mmoja wa mashemasi kwa jina Miriam na tulishuku kuwa walikuwa na uhusiano zaidi ya urafiki. Mkewe na waumini walipomwuliza alipuuza madai yoyote na kusema kuwa, kama pasta yeye ni baba kwa kila mtu na kwamba Miriam alikuwa binti yake mpendwa.”

MOURINHO Awajia Juu Wachezaji Walioiponza Man United, Awataja, Atoa Sababu 3 Za Kufungwa

Baada ya kipigo cha tatu mfululizo, Kocha wa Manchester United, Jose Mourinho ameonyesha kuwa na hasira na kutofurahishwa na aina ya ukabaji wa beki wake wa kushoto, Luke Shaw katika mchezo wa jana Jumapili dhidi ya Watford.

Man United ilifungwa mabao 3-1 na wapinzani wao hao katika Premier League.

Mourinho amenukuliwa akisema: "Bao la kwanza tulilofungwa na Man City na lile la pili la Watford linaweza kuwa na uhusiano,
bao la Man City (Aleksandar) Kolarov alikuwa na mpira na mchezaji wangu badala ya kwenda kumkata alimpa nafasi ya kufanya maamuzi.”
Katika kosa hilo, Mourinho alikuwa akimzungumzia kiungo wake, Henrikh Mkhitaryan.

Mourinho akaendelea kusema: "Hili la pili nalo, (Nordin) Amrabat alikuwa na mpira kisha beki wetu wa kushoto alikuwa umbali wa mita 25 kutoka alipo mpinzani badala ya kuw amita tano. Lakini hata unapokuwa katika kita 25 unatakiwa kumfuata na kumdhibiti, lakini yeye alisimama akimsubiri.
"Hili ni kosa la kiufundi lakini linahitajia uelewe wa kisaikolojia.

"Naweza kugawa vipigo hivyo katika sehemu tatu, kwanza ni makosa ya waamuzi, ambayo yapo nje ya uwezo wangu.
"Lakini katika mechi ya Man City unajua kilichotokea katika dakika ya 55 (kipa wa City Claudio Bravo alipomkwatua Wayne Rooney). Kilichotokea pia katika mechi ya Feyenoord walipofunga bao wakati kuna mtu alikuwa ameotea.

"Pili, kumekuwa na kukosa bahati na hiyo ni sehemu ya mchezo.

"Tatu ni suala lililopo mkononi mwangu, kuboresha kikosi.”

Premier League 5th day

Michael Schumacher hatoweza kutembea tena – mwanasheria wake

Mwanasheria wa bingwa wa zamani wa mbio za magari, Michael Schumacher, amedai kuwa hatoweza kutembea tena.

Felix Damm alikuwa akiongea kwenye mahakama ya huko Ujerumani kwa niaba ya familia Schumacher, wanaolishtaki jarida moja ambalo liliandika habari kuwa dereva huyo mwenye maika 47 ataweza kutembea tena.

Schumacher, aliyewahi kuwa bingwa wa mashindano ya Formula 1 mara saba, aliumia vibaya wakati akicheza michezo ya kwenye barafu huko Ufaransa mwaka 2013.

Jarida la Bunte la Ujerumani lilidai kuwa Schumacher anaweza kutembea tena, lakini Damm alikanusha vikali kuwa nyota huyo hajapona kiasi hicho. Kwa mujibu wa Mirror, Damm alisema Schumacher hawezi kutembea wala kusimama.

Pogba awapa moyo mashabiki wake wa Manchester United

Mchezaji ghali zaidi duniani kwa sasa Paul Pogba wa Manchester United amelazimika kuwapa moyo mashabiki wake baada ya timu yake kupoteza mechi mbili mfululizo.

Jumapili, Septemba 18 ilishuka dimbani kucheza mchezo wake wa tano wa ligi kuu ya England dhidi ya Watford na kufungwa magoli 3-1. Kiungo huyo wa Ufaransa ambaye hadi kwa sasa hajafanya vizuri kama wengi walivyokuwa wana matarajio akiwa na Man United toka avunje rekodi ya usajili.
Kupitia Instagram, Pogba ameandika: Asante kwa mashabiki wote kuwa pamoja na sisi matokeo bado sio mazuri kwa upande wetu, lakini tunaendelea kupambana, Man United tunaweza.”

Guardiola: ''Ni Messi pekee anayemshinda Kevin de Bryne''

Mkufunzi wa Klabu ya Manchester City Pep Guardiola anasema kuwa anamthamini mchezaji wake Kevin de Bryne kuwa katika kiwango cha juu kama mchezaji mwengine yeyote yule isopokuwa Lionel Messi wa Barcelona.
Raia huyo wa Ubelgiji aliifungia City bao la Kwanza katika ushindi wa bao 4-0 dhidi ya Bournemouth siku ya Jumamosi.

Kwa sasa mchezaji huyo ana magoli 18 na usaidi wa pasi 16 katika mechi 48 alizochezea The Blues ambao wameanza msimu huu kuweka rekodi ya mechi nane bila kushindwa katika michuano yote.

Guardiola: Messi ni mchezaji wa kiwango cha kivyake.Hakuna anayemfika baada yake Kevin anamfuata.

Katika kipindi cha kazi yake Guardiola amefanikiwa kuwafunza wachezaji bora dunia akiowemo,Xavi na Andres Iniesta akiwa Barcelona na Arjen Robben na Thomas Muller akiwa Bayern Munich.

Real Madrid wafikia rekodi ya Barca La Liga

Real Madrid wamecharaza Espanyol 2-0 na kufikia rekodi ya Barcelona ya kushinda mechi 16 mfululizo katika ligi kuu ya Uhispania, La Liga.
Ushindi wao mechi hiyo ya Jumapili umewaweka alama tatu mbele kileleni mwa ligi hiyo.
Mabao kutoka kwa James Rodriguez na Karim Benzema yaliwawezesha kufikia rekodi hiyo iliyowekwa na Barcelona walipokuwa chini ya Pep Guardiola msimu wa 2010-11.
Real, walicheza bila nyota wao Gareth Bale na Cristiano Ronaldo ugenini uwanja wa Cornella-El Prat lakini hilo halikuwazuia kuandikisha ushindi wao wa nne kutoka kwa mechi nne walizocheza msimu huu.
Barcelona wanashikilia nafasi ya pili ligini kwa sasa wakiwa na alama tisa, sawa na Las Palmas. Madrid wana alama 12.