Alibaba

dimanche 29 décembre 2019

Fred na Manchester United

FREDINHO.🔥⚽️

Huyu Mwamba hatajwi sana ndani ya Manchester United lakini kwa mtazamo wangu mimi binafsi ndio amekuwa mchezaji bora wa Manchester United katika kipindi cha takribani miezi miwili 



United ashinde au afungwe mara zote huwa anaonesha kiwango cha juu sana, energy level ya juu, passing , defending, interceptions ( anakata sana pasi zinazopita njiani kwenda kwao ) lakini pia anaanzisha mashambulizi haraka sana 

Anahitaji wachezaji wenzake wawe na ‘ consistency ‘ nzuri ili kazi yake izidi kutoa matunda na jana dhidi ya Burnley alikuwa Bingwa tena katikati ya kiwanja akisaidiana na Matic ambaye alionesha uzoefu wake.

Erling Haaland kwenda BVB

Taarifa zaidi .....

Straika wa kimataifa wa Norway Erling Braut Haaland ametua ndani ya klabu ya Borussia Dortmund kutoka RB Salzburg kwa dau linaloripotiwa kufika kiasi cha Pauni Milioni 18 na mkataba mpaka mwaka 2024. 



Haaland alikuwa akiwindwa na Juventus, Manchester United na RB Leipzig lakini ni Dortmund ndio wamefanikiwa kumnasa na atajiunga na wenzake Januari 3. 

Haaland mwenye umri wa miaka 19 msimu huu ameweka kambani magoli 28 katika mechi 22 pamoja na yale 8 ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Future plan za CR7


Mreno mwenye myaka 33 na mchezaji nyota wa Juventus

Katangaza ya kwamba mchezo wa mpira wa miguu (Football) sio maisha yote
Bali kuna maisha mengine baada ya ku staff kucheza mpira wa miguu
Kasema : nataka kujiandaa kukisoma kingereza vizuri na kukielewa kiusawa, ili nikija Staff kucheza mpira niweze kuendeleya na mengine

Kasema : nataka niwe mchaza filamu