Alibaba

mardi 1 novembre 2016

Ripoti: Janet Jackson abadilisha dini kuwa muislamu

Janet Jackson, amedaiwa kubadilisha dini na kuwa muislamu, kumfuata mume wake, Wissam Al Mana, ambaye pamoja wanatarajia kupata mtoto wa kwanza.

Marafiki zake wanaamini kuwa muimbaji huyo mwenye umri wa miaka 50, amekuwa akijifunza dini hiyo na sasa ameslimu.

Chanzo kimoja kimeliambia gazeti la The Sun kuwa Janet anapoenda kuwasalimua ndugu wa mumewe, huenda bila make-up, bila nywele za bandia na huvaaa nguo za kiislamu.

“She feels like she has found a home with her new religion. She has spent a great deal of time studying it,”

kimeongeza chanzo.