Alibaba

jeudi 7 septembre 2017

Wanaume mpo tayari kwa nguo hii ya ndani?

Kumekuwa  na idadi kubwa ya wabunifu wa mavazi mbalimbali duniani, jopo la wabunifu wamekuja na aina mpya ya nguo ya ndani kwa upande wa wanaume. Je! wewe kama mwanaume upo tayari kutinga nguo hii kwa sasa.

Rick Ross na Briana Camille wapata mtoto wa kike

Rapper kutoka Maybach Music Group(MMG), Rick Ross amebahatika kupata mtoto wake wa kwanza na mwanamitindo Briana Camille.

Licha ya kuwa wawili hao hawakuwahi kutangaza kuwa katika mahusiano ya kimapenzi na wala hawakuwahi kuonekana pamoja ila wamebahatika kupata mtoto wa kike. Inaelezwa kuwa Camille alikuwa akimsapoti rapper huyo mara kwa mara na kupelekea watu kuhisi wapo katika mahusiano hayo.
Kwa sasa familia ya Boss wa MMG imekuwa na watoto watatu ambapo wawili ni wakeki na mmoja ni wa kiume, ambao ni Toie Roberts na William Roberts III.
wa mujibu wa vyanzo vya karibu vimeeleza kuwa mtoto huyo amezaliwa siku ya Labor Day wikiendi iliyopita na tayari ameshaanza kupokea zawadi kutoka kwa baba yake.

Wachezaji 47 wa Afrika wanaocheza Ligi Kuu England

Katika msimu wa 2017/2018 kutakuwa na wachezaji 47 kutoka nchi za Afrika wanaochezea klabu za Ligi Kuu ya England.

Hii ni kwa mujibu wa orodha ya wachezaji 25 wa kila timu ambao waliwafilishwa kwa Ligi ya Premia.
Wachezaji hao ni asilimia 9 ya wachezaji wote katika ligi hiyo, ambalo ni ongezeko ndogo ukilinganisha na msimu uliopita ambapo walikuwa 45.

Leicester City wanaongoza wakiwa na wachezaji saba, wakifuatwa na Crystal Palace, Newcastle United na West Ham ambao wana wachezaji wanne kutoka Afrika kila klabu.
Ni klabu moja pekee - Burnley - ambayo haina mchezaji wa kutoka Afrika msimu huu.
Senegal inaongoza kwa kuwa na wachezaji wengi zaidi, tisa, ikifuatwa na Nigeria iliyo na wachezaji sita.
DRC, Ghana na Ivory Coast zina wachezaji watano kila nchi.
Wachezaji kwa nchi (zenye wachezaji wengi):

Senegal
Pape Souare
Idrissa Gana Gueye
Oumar Niasse
Sadio Mane
Mohamed Diame
Henry Saivet
Mame Diram Diouf
Chekhou Kouyate
Diafra Sakho

Nigeria
Alex Iwobi
Ahmed Musa
Wilfred Ndidi
Kelechi Iheanacho
Isaac Success
Victor Moses

Ivory Coast
Wilfred Zaha
Yaya Toure
Eric Bailly
Wilfried Bony
Serge Aurier

Ghana
Jeffrey Schlupp
Daniel Amartey
Christian Atsu
Jordan Ayew
Andre Ayew

DRC
Benik Afobe
Yannick Bolasie
Elias Kachunga
Chancel Bemba
Arthur Masuaku

Wachezaji kwa klabu:

AFC Bournemouth
Benik Afobe (DRC)

Arsenal
Mohamed Elneny (Misri)
Alex Iwobi (Nigeria)

Brighton & Hove Albion
Gaetan Bong (Cameroon)

Chelsea
Victor Moses (Nigeria)
Crystal Palace
Bakary Sako (Mali)
Jeffrey Schlupp (Ghana)
Pape Souare (Senegal)
Wilfred Zaha (Ivory Coast)

Everton
Yannick Bolasie (DRC)
Idrissa Gana Gueye (Senegal)
Oumar Niasse (Senegal)
Huddersfield Town
Elias Kachunga (DRC)
Steve Mounie (Benin)

Leicester City
Daniel Amartey (Ghana)
Yohan Benalouane (Tunisia)
Riyad Mahrez (Algeria)
Ahmed Musa (Nigeria)
Wilfred Ndidi (Nigeria)
Kelechi Iheanacho (Nigeria)
Islam Slimani (Algeria)

Liverpool FC
Sadio Mane (Senegal)
Joel Matip (Cameroon)
Mohamed Salah (Misri)

Manchester City
Yaya Toure (Ivory Coast)

Manchester United
Eric Bailly (Ivory Coast)

Newcastle United
Mohamed Diame (Senegal)
Chancel Mbemba (DRC)
Christian Atsu (Ghana)
Henry Saivet (Senegal)

Southampton FC
Sofiane Boufal (Morocco )
Mario Lemina (Gabon)

Stoke City
Eric Choupo-Moting (Cameroon)
Mame Biram Diouf (Senegal)
Ramadan Sobhi (Egypt)

Swansea City
Jordan Ayew (Ghana)
Wilfried Bony (Ivory Coast)

Tottenham Hotspur
Serge Aurier (Ivory Coast)
Victor Wanyama (Kenya)

Watford FC
Isaac Success (Nigeria)
Molla Wague (Mali)
Brice Dja Djedje (Ivory Coast)

West Ham United
Andre Ayew (Ghana)
Chekhou Kouyate (Senegal)
Arthur Masuaku (DRC)
Diafra Sakho (Senegal)

West Bromwich Albion
Allan Nyom (Cameroon)
Ahmed Hegazi (Misri)