Alibaba

vendredi 2 décembre 2016

Soyinka airarua green card yake

Mshindi ya tuzo la Nobel raia wa Nigeria Wole Soyinka, ametimiza ahadi ya kuirarua green card yake kwa mujibu wa shirika la habari la AFP.

Mwezi uliopta mshindi huyo wa tuzo la fasihi alisema kuwa angeirarua green card, ambayo humpa mtu kibali cha kuishi nchini Marekanai ikiwa Dionald Trump angechaguliwa kuwa rais wa Marekani.

Aliliambia shirika la AFP mjini Johannesburg kuwa kutokana na vile Trump ameshinda, basi ametekeleza alichokisema
"Tayari nishafanya, nimetoka Marekani , nimefanya kile nilisema ningekifanya, nilitupa green card yangu , nimerudi penye ninastahili kuwa," alisema Soyinka.

Hata hivyo Soyinka hawashauri watu wengine kufuata mkondo huo.

Taasisi ya Drogba yafutiliwa makosa ya ufisadi

Uchunguzi dhidi ya shirika la kutoa msaada la mchezaji wa zamani wa Chelsea, Didier Drogba, haujapata ushahidi wa ufisadi au ulaghai,lakini umebaini shirika hilo ''liliwapotosha'' wafadhili.
Tume ya taasisi hiyo ya ufadhili iliyoanza uchuguzi wa madai ''makali ya udhibiti''katika shirika lake la Didier Drogba mwezi April.
Baadaye gazeti la Daily Mail liliripoti kwamba kati ya pauni milioni 1.7 za hisani ni pauni elfu 14,115 ndizo pesa pekee zilizotumika kusaidia barani Afrika.
Drogba , 38, amesema anataka kulipwa na kuombwa msamaha na gazeti hilo la Daily Mail.

Kamati hiyo iliyotumia mamlaka yake ili kuchunguza akaunti za shirika hilo, imesema imeridhika kwamba hakuna udanganyifu wowote.

Lakini ilikuwa vigumu kubaini ukweli kuhusu taasisi hiyo, ilivyogawanya mipango yake binafsi ya ili ya kutoa msaada Afrika.

Hilo nidhihirisho kamili kwa ufadili uliokuwa ukitoka Uingereza haukuwa unatumika kwa mahospitali au kwa makliniki, kama vile wafadhili walivyodhani, lakini pesa hizo zilikuwa zikiwekezwa kwenye akaunti za Uingereza.
''Wafadili walitarajia ufadhili wao ungetumika kwa madhumuni ya usaidizi, na sikuekeza kwenye akaunti za benki,''ripoti hiyo ilisema.

Wafadhili wa Uingereza labda yalidanganywa kuhusu miradi ya shirika hilo ambalo wamekuwa wakilifadhili.

Kamati hiyo imetoa ''mpango tekelezi'' kwa shirika la Didier Drogba kujiimarisha.

Charly na Nina ndani ya Buja

Charly na Nina waliyo mshirikisha msanii Big Fizzo kwenye pini 'indoro' watakuwa Town ifikapo tarehe 25/12/2016 usikosi basi...

Bob Junior ana mchango mkubwa kwenye maisha yangu – Diamond

Diamond hafanyi tena kazi na Bob Junior, lakini hawezi kusahau ukweli kuwa producer huyo wa Sharobaro Records ndiye aliyemfungulia njia ya mafanikio kimuziki.

Akizungumza kwenye kipindi cha Ngaz Kwa Ngaz Alhamis hii kupitia EATV, Diamond alikiri kuwa Bob Junior ana mchango mkubwa kwenye maisha yake.

“Kiukweli Bob Junior ana mchango mkubwa sana katika katika maisha yangu kwasababu ukiangalia nyimbo zangu zote zilizonitoa ni yeye ndiye alikuwa ametengeza,” alisema Diamond.

“Japokuwa hata kipindi ambacho nilikuwa nazitengeneza inawezekana watu walikuwa hawajamuona kama anaweza kuwa producer mzuri sana. Lakini mimi nilikuwa naona mbona huyu natoka naye, nakufa naye mimi yaani huyu natoa nyimbo na inahit,” aliongeza.

“Nakumbuka tulifanya nyimbo kama sita, Nenda Kamwambie, Mbagala, Nitarejea, Binadamu, nyimbo tofauti tofauti. Kila nyimbo alikuwa akinitengenezea akinipa beat nikifika nyumbani naandika vibaya sana. Na mpaka nakumbuka ilifika time niliweka kama chuki fulani kwa wasanii waliopo pale wakaona mbona unampendelea mtu fulani, yeye akasema mimi ni producer, natengeneza beat nikimpa msanii kaandikie kitu kikali, akasema huyu nikimpa analeta beat kali.”

Kwa upande mwingine staa huyo alidai kuwa Mbagala ni moja ya nyimbo zake anazozipenda sana kwakuwa aliuandika kwa ufanisi mkubwa.

Prince Harry akutana na Rihana Barbados

Prince Harry, mwanamfalme wa Uingereza amekutana na nyota wa muziki wa Pop Rihana mara mbili kwa siku katika warsha ya kuadhimisha miaka 50 ya uhuru wa Barbados.

Rihana ambaye muziki wake umebobea nchini Uingereea alisamama na kumsalimia Prince Harry.

Kisha wawili hao wakaketi pamoja jukwaani wakati ya sherehe.

Msaidizi mmoja alisema kuwa Prince Harry ambaye alivalia nguo rasmi za ufalme alisema kuwa Harrry alikuwa amejulishwa dakika 20 kabla awasili kwa warsha hiyo kuwa Rihana angehudhuria.

Baadaye Harry na Rihana tena waliketi pamoja kwenye jukwaa eneo la Kensington huko Bridgetown.

Umati wa watu 20,000 uliohudhuria ulimshangilia Prince Harry wakati jina lake lilipotajwa, Lakini kulikuwa na mbwembwe zaidi wakati jina la Rihana lilitajwa.