Alibaba

jeudi 28 avril 2016

Wanachuo jikingeni

WANACHUO...SOMA
UELIMIKE...
Nilikuwa nimemaliza zangu chuo Mzumbe pale, kozi ya BAF (bachellor of accountance and finance) na kufanikiwa kupata GPA nzuri tu ya 4.2. Nilikuwa na matumaini na ndoto nyingi za mbeleni juu ya maisha yangu. Nilipenda sana elimu na nilitegemea kupata nafasi ya TA (tutorial assistant) chuoni hapo. Wakati nangojea graduation ambayo huwa mwezi November, nilienda Dar es salaam kumtembelea dada yangu ambaye alikuwa akiishi huko, maeneo ya Tabata! Naye ndo kwanza alikuwa na mwaka mmoja kazini ila kwa bahati (nzuri?mbaya?…sijui) alipata ujauzito na mshkaji mmoja hivi walisoma naye chuo. Basi nikawa nakaa naye pale huku nikingojea siku zisonge. October 06, 2014 siku ya Jumanne: Siku hii alitakiwa kwenda clinic na kwa vile alikuwa karibu sana na kujifungua hakuweza kuendesha gari ikabidi nimsindikize kwenye zahanati moja pale Tabata nimeisahau jina. Basi wakati namngojea nikaenda kukaa kwenye mabenchi Fulani pembeni pale kuangalia TV. Karibu yangu alikuwa amekaa binti mmoja mrembo sana kwa kweli. Sikufahamu yupo pale kufanya nini. Nilidhani na yeye kaja kumsindikiza ndugu yake labda. Mimi bila hiyana nikaacha kuangalia TV nikaanza kupiga stori za hapa na pale. Tukakonekt vizuri na kuchangia changia mada iliyokuwa inaonyeshwa kwenye TV. Baada ya kama nusu saa dada naye akatoka ndani akaja tuondoke. Nikamwambia dada kama hutojali unipatie namba yako tuzidi kuwasiliana. Baada ya siku ile tuliendelea kuwasiliana sana tu. Tulikuwa tuna chat mpaka ma saa sita ya usiku na ukizingatia sikuwa na kazi. Aliniambia yupo chuo mwaka wa tatu anasoma Sheria. KAA NA MIMI….. Moyoni nilihisi hapa nimepata mtu lakini kama nilivyofundishwa sikuwa na papara ya kumtamkia hayo. Bado ninakumbuka maonyo niliyopewa juu ya jiji la Daslam! Baada ya wiki mbili hivi tulikutana for lunch posta..enzi hizo break point bado mpya kabisa. Tuliongea mengi about life. Wiki moja kabla ya graduation nilimwambia naenda zangu Morogoro wiki ijayo hivyo ningependa tuonane. Alikubali na kuja mpaka Tabata jioni. Tulikaa tukala na kupiga stori mpaka mida kama saa sita hivi ucku. Nikatumia mbinu za kimafia kumshawishi kwamba kwenda hostel kwao mida hiyo ingekuwa ngumu ilhali tungeweza kuchukua tu chumba hapo asubuhi arudi chuoni. Of course, strawberry whisky na contessa gin vilichangia kunisaidia kumfanya akumbali. Ila alikuwa amekataa sana mwanzoni.
Tulienda guest moja inaitwa MUNGU ANAKUONA GUEST HOUSE & RESTAURANT. Nikalipa pale tukaingia ndani. Kazi ikaanza kuomba game(sex) ila haikuwa ngumu saaaaana…….. Basi purukushani za hapa na pale za kujiandaa na game na mimi kwa kuwa nilichanganya Contessa gin, zansi na White horse nikasahau kabisaaa matumizi ya kinga. Poor me..!! Nikaenda zangu graduation November na kurudi. Nikawa nimempotezea kabisa Yule binti kama ilivyo kawaida yetu wanaume baada ya kupata tunda (baada ya kumchezesha ngololo)... April 15 / 2014 Jumanne: SMS iliingia : “Ndugu yangu, kama umenichunia sawa ila mbona hata sikuoni tena hospitali?” Nikashtuka hospitali? Si ikabidi nimpigie! Ananiambia: “Si pale Tabata sikuoni ukija tena kuchukua ARVs au umebadili kituo?” Kumbe benchi nililokuwa nimeenda kukalia ile siku lilikuwa la wagonjwa wa UKIMWI
nayeye alikuwa akisubiri kuchukua dawa. Mimi nikamwambia “acha kunidanganya mbona wewe unaishi hostel Kigamboni na ninajua hivyo..yani huko kote hakuna dispensary?” Akaniambia “wagonjwa wengi hawaendi kuchukulia dawa karibu na kwao kwa kuhofia kunyanyapaliwa hivyo alijua na mimi nipo kwenye foleni ya kuchukua dawa ndiyo maana hakuona umuhimu wa kunilazimisha kutumia kinga cku ile tulivyofuck” Nilishtuka…nikazimia…ndo nimeamka leo..
***** Mwisho ********

mercredi 27 avril 2016

THAMANI YA MWANAMKE

THAMANI YA MWANAMKE

Mwanamke, akilala na hali mumewe
amemkasirikia, basi hulaaniwa na Malaika
usikukucha.
🌼Lakini sikujuwa kua kuna na kinyume chake.
Ilitokea katika khutba ya Ijumaa, lilitokea
jambo ambalo si lakawaida, jamaa mmoja
alimshitaki mkewe kwa Shekhe wa msikiti
mbele ya watu. Shekhe akamjibu kua
mwanamke yuwabeba na yuwavumilia
mambo mengi kumshinda mwanamume
kwa mara zaidi ya mia na mia, na hata lau
angekua huyo mwanamume ana misiba au
matatizo mengi na akasubiri, lakini subira
za mwanamke ni kubwa zaidi.
Hapo hata sauti ya huyo Shekhe ilianza
kubadilika alipokuwa anamsemesha huyo
mwanamume alomshitaki mkewe na
kumwambia:
Mkeo amebeba mambo yako na ya
watoto wako, na anasimama kwa miguu
yake kuwatengezea chakula chenu. Na
Mtume (s.a.w.) ameshausia hivo.. Jee
kwani hana haki yeye ya kuheshimiwa? Na
ya kuthaminiwa? Bila ya kumpunguzia
chakula au kitu chochote anacho kihitaji?
Basi naapa Wallahi lau mwanamume
anamkasirisha mkewe, akamgeukia na
kumpa kishogo akatoka nyumba kumwacha
mkewe na huzuni, basi Mwenyezi-Mungu
anamlaani kwa kila khatwa anapokwenda,
na kumyimia rizki yake, na kumpunguzia
afiya yake, na kumuandikia kwa kila chozi
moja linalotoka machoni mwa mkewake
huyo, makaa ya moto elfu moja kila siku,
nusu yake duniyani, na nusu kesho
akheera.
Natamani maneno haya yawafikie wanaume
wengi walokwisha owa...
Machozi mangapi mengi yashamtoka
mke wako na wewe hata hujali kabisa, wala
huna hamu ya kitu chochote, wala hutaki
kujua habari yake..
Musiyawache maneno haya kubakia
moyoni mwenu tu, bali kila mtu awatumie
walokwisha owa. Na ambao hawaja owa
wahifadhi maneno haya msitari msitari
kama akiba ya kesho yake watakapo owa.
Amesema Amiir Talaal Ar-Rashiid,
Mungu amrehemu,:
(( Kama aliumbwa mwanamke kuwa ndege
angekuwa ni "Tausi", na kama aliumbwa
kuwa mnyama angekuwa ni
"Paa" (Ghazala),
na kama aliumbwa kuwa mdudu angekuwa
ni "Kipepeo" (Butterfly), lakini ameumbwa
kuwa mtu, kwa hivo yeye ndiye Mpenzi, na
ndiye Mke, na ndiye Mama bora, na ndiye
Neema nzuri kabisa ya mwanamume katika
duniya hii.
Na kama hangelikuwa mwanamke ni
kiumbe bora na kikubwa sana, Mungu
hangemfanya kuwa Huril-ayn na kutuzwa
watu Waloamini kesho Peponi.
Hakika nimependezewa na Mwanamke
kwa kuwa: "Ni kiumbe ambaye unaweza
kuishi naye kwa urahisi na vilevile kwa
vigumu kabisa, unaweza kumridhisha kwa
ua moja la waridi, na unaweza kumuuwa
kwa neno moja.
Jitahadhari ewe mwanamme ujue kuwa
mwanamke ameumbwa kwa mfupa wa
ubavu wako si kwa mguu wako hata
umkanyage...wala si kwa kichwa chako
hata umpandie juu ya kichwa chake, lakini
ameumbwa kwa mfupa wa mbavu zako ili
umueke ubavuni mwako, na ni kwa mfupa
ulioko karibu na moyo wako ili upate
kumpenda.
Mwanamke ni kiumbe bora kabisa...
Katika utoto wake humfungulia babake
mlango Peponi...
Na katika ujanajali wake humtimizia
mumewe dini yake...
Na anapokuwa mama, Pepo huwa chini
ya miguu yake...
Maneno mazuri kabisa.....
Nampa salamu na pongezi kila ambaye
ni Mwanamke.
Shukran kwa kila aloyaandika maneno
haya, na kila aloyatuma na akaingiza furaha
katika moyo wa kila msichana, na kila
ndugu wa kike, na kila mke, na kila mama.
🌷
Mola wetu tupe kutoka kwa wake zetu
watoto wenye kufurahisha macho na nyoyo
zetu...Aaamiin.
🌷🌷🌷🌷🌷🌷
Swala na Rehema za Mwenyeezi-Mungu
zimfikie Nabii wetu Mohammad, na ahli
zake na maswahaba zake wote.