Alibaba

samedi 31 décembre 2016

Alikiba ashinda tuzo Ufaransa, awabwaga Davido, Sarkodie, Yemi Alade na wengine

Fresh kutoka kushinda tuzo ya video bora ya mwaka (Aje) kwenye tuzo za Soundcity MVP za Nigeria, Alikiba ameongeza nyingine wikiendi hii.
Mkali huyo ameshinda tuzo ya Chaguo la Watu (Prix du Public) kwenye tuzo za Ufaransa za Wana Music Awards zilizotolewa Ijumaa hii.
“Hii ilikuwa ni tuzo pekee ambayo ilikuwa wazi kwa watu kupiga kura mwaka huu na msisimko uliozalishwa na tuzo hii umevuka matarajio yetu kwa kuwa na majadiliano zaidi ya 30,000 kwenye matangazo yetu kupitia mitandao ya kijamii,”

Kwa habari zaidi 👇  👇  👇
waandaji wa tuzo hizo Wana Corp wameandika kwenye tovuti yao.

“Mshindi, Alikiba wa Tanzania aliweza kujikusanyia jamii kubwa ya mashabiki, ‘mashabiki damu wa Alikiba’ kuweza kuuchukua ushindi. Mwaka huu umekuwa wa mafanikio kwa Alikiba akiwa na sahihi katika label kubwa ya Sony, kushinda tuzo ya kimataifa ya MTV Europe Music Awards kama ‘Best African Act’ na yote kwa yote kuwa na moja ya video bora za mwaka na Aje,” wameongeza.

“The main information of this “Public Prize” is to see that our small website created in France can have links with a country like Tanzania thanks to Alikiba. Just for that, we say thank you to all those fans who have mobilized: a new link between Paris and Dar-Es-Salaam has been formed,”

wamesisitiza.
Kwenye tuzo hiyo Alikiba alikuwa akichuana na Davido, Eddy Kenzo, Sarkodie, Serge Beynaud, Yemi Alade. Kulikuwa na jumla ya vipengele 14. Kundi la Sauti Sol nalo limeshinda kipengele cha kundi bora la mwaka.

vendredi 30 décembre 2016

Dully Sykes: Baada ya miaka 3 au 5 nitawapatanisha Alikiba na Diamond

Msanii mkongwe na mtayarishaji wa muziki nchini, Dully Sykes amedai kuwa baada ya miaka mitatu au mitano kupita atakuwa na uwezo wa kulimaliza bifu la Diamond na Alikiba.


Hitmaker huyo wa ‘Inde’ alikiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio Jumanne hii kuwa kuwapatanisha wasanii hao kwa sasa ni ngumu kwakuwa kila mmoja anataka sifa na kuwa juu zaidi ya mwingine.


“Kuwapatanisha inawezekana lakini si kwa sasa,” alisema. “Hii waliyofikia ni sifa kila mtu anataka sifa na kila mtu anataka kuwa mkubwa, kwahiyo mimi nitasubiri baadaye kidogo itakapofikia muda kama miaka mitano hivi mbele au mitatu Mungu akipenda na vuguvugu hili litakapokwisha mimi nina uwezo wa kuwakutanisha na kuwaambia ugomvi umekwisha. Lakini kwa ugomvi wao kupatana leo au kesho kwa sasa si kweli,” aliongeza.

Dully aliongeza kuwa kwa sasa ni ngumu kuwapatanisha wasanii hao kwa kuwa nyuma yao kuna watu wengi ambao wote kwa pamoja kuelewana kwa sasa itakuwa ni ngumu.

Nikikutana na Alikiba tunaongea na kucheka, ananiambia nafanya kazi nzuri – Rayvanny

Msanii wa muziki kutoka label ya WCB, Rayvanny amefunguka na kuzungumzia mahusiano yake na Alikiba ambaye ni mpinzani mkubwa wa boss wake Diamond Platnumz.
Muimbaji huyo ambaye bado anafanya vizuri na wimbo Salome alioshirikishwa na Diamond, amedai yeye hana tatizo na Alikiba na hata ikitokea nafasi ya kolabo atafanya naye.


“Alikiba huwa nikikutana naye huwa napiga naye stori, tunasalimiana tunacheka, ananiambia kuwa nafanya kazi nzuri, hatujawahi kuongea sana,” Rayvanny alikiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM.

Aliongeza,”Ikitokea siku naweza kufanya naye kolabo kwasababu ‘end of the day’ wote tunafanya muziki ni biashara pia, mashabiki wetu wanapenda kuona ‘combination’ za watu tofauti tofauti, hata nikikutana naye hatufungiani vioo,”

Diamond na Alikiba wamekuwa wenye bifu kwa muda mrefu huku mashabiki katika mitandao ya kijamii wakidaiwa kulichochea bifu hilo zaidi.


Ronaldo akataa mshahara wa £1.6m kwa wiki kutoka klabu ya China

Klabu ya Real Madrid ilipewa takriban pauni milioni 250 na klabu ya China ambayo haikutajwa jina ili kumnunua nyota wake Cristiano Ronaldo kulingana na ajenti wake Jorge Mendes.
Amesema kuwa nahodha huyo wa Portugal mwenye umri wa miaka 31 hana haja na mpango huo ambao ulishirikisha mshahara wa kila mwaka wa pauni milioni 85.
Ronaldo alisema kuwa anaweza kucheza kwa miaka mingine 10 mnamo mwezi Novemba baada ya kuandikisha mkataba mpya na Real Madrid hadi Juni 2021.


''Soko la China ni soko jipya.wanaweza kuwanunua wachezaji wengi, lakini haiwezekani kumnunua Ronaldo'', alisema Mendes.
''Cristiano ndio mchezaji bora duniani, ni kawaida kupata maombi'', aliongezea raia huyo wa Ureno.
Chini ya ombi hilo analodai Mendes, Ronaldo angepokea kitita cha pauni milioni 1.6 kwa wiki ikiwa ni mara tatu ya zaidi ya kitita cha uhamisho wa pauni milioni 89 zilizogharimu uhamisho wa Paul Pogba kutoka Juventus kuelekea Manchester United.
Mendes aliambia Sky Italia: Klabu ya China imetoa pauni milioni 257 kwa Real Madrid na zaidi ya Yuro milioni 100 kila mwaka kwa Ronaldo.
''Lakini fedha sio kila kitu.Klabu hiyo ya Uhispania ndio maisha yake''.
Hatua hiyo inajiri baada ya klabu ya Shanghai Shenhua kutoka China kuthibitisha kwamba imemsajili aliyekuwa mshambuliaji wa Manchester City Carlos Tevez kutoka klabu ya Boca Juniors.
Shanghai inayofunzwa na aliyekuwa mkufunzi wa Brighton Gus Poyet ,wameripotiwa kukubali uhamisho wa pauni milioni 40 mbali na mshahara wa zaidi ya pauni milioni 310,000 kwa wiki.

mardi 27 décembre 2016

Guardiola: Ni vigumu kwa Man City kuishika Chelsea

Mkufunzi wa klabu ya Manchester City Pep Guardiola anasema kuwa itakuwa vigumu kwa kikosi chake kushindana na viongozi wa ligi ya Uingereza Chelsea.
City ilipanda hadi nafasi ya pili katika jedwali baada ya kuicharaza Hull City 3-0 katika siku kuu ya Boxing Dei na kuweza kuwa nyuma ya Chelsea kwa pointi 7.
Kikosi hicho cha Antonio Conte awali kiliweka rekodi ya kushinda mara 12 katika ligi ya Uingereza baada ya kuichapa Bournemouth 3-0.
''Tumecheza mechi saba zaidi ya Chelsea ,ndio maana ni vigumu '',alisema Guradiola.

''Liverpool ilikaribia taji hilo mwaka mmoja uliopita kwa sababu walikuwa na mechi moja kwa wiki ,na ni hivyo ndivyo ilivyokuwa na Leicester.Mara hii Chelsea na Liverpool wana fursa''.

Liverpool na Chelsea zilishindwa kufuzu katika mashindano ya Ulaya baada ya kumaliza wa nane na 10 mtawalia katika ligi ya Uingereza mwaka uliopita.

lundi 26 décembre 2016

Roboti inayoweza kushiriki ngono kutengezwa

Je ungependelea kushiriki ngono na roboti? ungefunga ndoa na roboti? na Je roboti anaweza kuwa na haki ya kupinga ndoa hiyo?
Haya ni baadhi ya maswala machache yanayoulizwa katika mkutano wa pili wa kuwa na mpenzi wa roboti mbali na kushiriki naye ngono katika chuo kikuu cha Goldsmith mjini London baada ya serikali ya Malaysia ambayo ndio iliokuwa taifa la maandalizi ya mkutano huo kuupiga marufuku.

Hatua hiyo imezua utata sio tu kwa mataifa yenye maoni ya Kihafidhina .
Hakukuwepo na wawakilishi kutoka kwa sekta ya ngono wala roboti za ngono katika mkutano huo.
Kampuni ya Real Dolls inayotengeza wanaserere wa ngono ilidai kwamba itatengeza roboti wa ngono aliye na akili bandia mwaka ujao.
Uzinduzi huo iwapo utafanyika utakuwa ushahidi wa David Levy ambaye amekuwa akitabiri ujio wa roboti zinazofanana na binadamu zenye akili bandia.
Alitoa hotuba ya kufunga mkutano huo ambapo alipendekeza utengezaji wa roboti za ngono.

''Tuna roboti za urafiki na sasa roboti ambaye anaweza kuwa mpenzi ndio mtindo mpya''.
Katika kipindi cha miaka 10 ijayo, inawezakana kutengeza roboti ambayo watu wataihitaji kama mpenzi, ina upendo, inaaminika, inaheshima na hailalamiki alisema.
Wengi watapendelea uhusiano huo wa roboti na huenda wakataka kufunga ndoa nao.

Mpango huo wa mpenzi wa aina ya roboti huenda akazua maswali kadhaa ya kimaadili, hususana wakati ambapo sheria italazimika kutambua roboti kama binaadamu.

ZARI Afunguka :Hakuna Kitu Ninachokipenda Katika Maisha yangu Kama Kuzaa....

Wakati mabinti wengine wakijikita katika matumizi ya mikorogo na kukimbilia wanaume wenye pesa hali ni tofauti kwa mwanamama zari hassan (the boss lady ) ambaye amekiri wazi kuwa kitu anachopenda zaidi katika maisha yake ni kuzaa.

Zari ambaye ni mpenzi wa mwanamziki nyota Africa diamond platnumz amesema hayo ikiwa ni siku chache tangu apate mtoto wa kiume aliyezaa na diamond ambaye watu walimbeza kuwa anazaa bila mpangilio eti kiza tu alibeba ujauzito kabla ya mtoto wao wa kwanza tiffah hajatimiza mwaka mmoja.
Licha ya zari kuwa na watoto watano kwa sasa ameweka wazi kuwa kwa sasa yeye na diamond wana mpango wa kuzaa mtoto mwingine wa tatu na baada ya hapo hatozaa tena na badala yake watajikita zaidi katika kuwalea watoto wao.

Firmino akamatwa kwa kuendesha gari akiwa mlevi

Mchezaji wa Liverpool Roberto Firmino ameshtakiwa kwa kosa la kuendesha gari akiwa mlevi baada ya kukamatwa mkesha wa siku ya Krismasi.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 25 alikamatwa baada ya gari lake kusimamishwa katikati mwa Liverpool mapema siku ya Jumamosi ,polisi wamesema.


Mchezaji huyo wa Brazil anatarajiwa kufikishwa mbele ya hakimu wa Liverpool mnamo Januari 31.
Firmino atawasilishwa mahakamani siku ambayo timu yake itakabiliana na Chelsea katika uwanja wa Anfield.
Liverpool ilimsajili mchambuliaji huyo kutoka Hoffenheim kwa kandarasi ya miaka mitano iliogharimu kitita cha pauni milioni 29 mwezi Juni.

Alicheza katika ushindi wa wiki iliopita dhidi ya Everton katika uwanja wa Goodison Park.
Liverpool imesema kuwa haitazungumzia swala hilo hadi pale hatua hiyo ya kisheria itakapokamilika.

samedi 24 décembre 2016

HIZI NDIZO MBINU ZA KUMTONGOZA MWANAMKE YEYOTE NA HACHOMOKI.

Muda au Pesa Nyingi!"
Kutongoza ni sanaa ya ushawishi, ambayo lengo lake ni kuanzisha mahusiano ya karibu. Kuna sanaa zingine za ushawishi kama vile ushawishi wa kibiashara ambapo lengo ni kuuza bidhaa. Na kuna ushawishi wa kisiasa ambapo lengo ni kupata kura.
Wakati sanaa karibia zingine zote za ushawishi ni rahisi kujifunza, sanaa ya kutongoza watu wengi wanasema eti haifundishwi ... eti kila mwanaume anajua kutongoza.

Sio Kweli !!!

Sio kweli kwamba kila mwanaume anajua kutongoza, kwa sababu kuna mwanaume anaweza akongea na demu mpya leo na wakapatana leo leo, au akichelewa sana basi ndani ya wiki moja; wakati huo huo kuna wanaume wengine wanahangaika miezi au hata miaka 5. Au wengine wanatoboka sana mifukoni .... unakuta mtu anampangishia demu nyumba, au anamlipia ada ndio ale mzigo. Wakati huo huo kuna wengine wanakula hapo hapo bure, tena bila kunawa!

Je Unajua Njia Sahihi za Ku-handle Vikwazo vya Wanawake?
Wanawake ni watu wa vikwazo. Wenyewe wanasema wanaweka vikwazo ili kukupima kama una "mapenzi ya kweli". Unachotaka wewe ni kimoja. Kula mzigo. Maana inabidi ule mzigo kwanza, ndo ujue kama uendeleze mapenzi yawe ya kweli ... au upotezee. Au sio mzee?
Ila yeye atakuwekea vikwazo kibao kama vifuatavyo:
Niko kwenye period
Nina boyfriend / mume / mchumba
Ninaumwa (malaria/tumbo/kichwa/n.k.)
Mama yangu mgonjwa
Niko bize na kazi
Nimeokoka nampenda Yesu! Mwanaume wangu ni Yesu tu!
Wiki hii nina test (kwa wanavyuo)
Mi sitaki mambo hayo, mpaka nimalize masomo nipate na kazi
Mi bado mdogo
Sitaki!!
Nyumbani kwetu geti kali siwezi kutoka
Wewe sio mwanaume wa type yangu (mfupi sana/mweusi sana/mweupe sana/huna hela/n.k.)
Mi sitoki/siongei na watu nisiowajua (strangers)
Sijisikii kuwa na wewe / sikupendi!
na kadhalika
Je ni mara ngapi umekwamishwa na mojawapo ya vikwazo kama hivyo hapo juu?


Utajisikiaje nikikwambia kuwa vikwazo vya dizaini hiyo vingi ni geresha tu ... sio vikwazo kwa maana ya vikwazo bali ni fursa nzuri kwako kupata unachotaka?
Na bomba zaidi je unajua mbinu za kutumia ili kumfanya mwanamke asikupe kabisa vikwazo kama hivyo? Ukimtongoza mwanamke vibaya atakuwekea vikwazo vingi na hata kama utampata atakuwa ashakuzungusha sana na kukupotezea muda na pesa. Ukiwa na mbinu za kuzuia vikwazo maisha yako yatakuwa rahisi zaidi.
Sasa Mpango Mzima Uko Namna Hii...
Tuna wataalam wa kutongoza. Hao jamaa ni noma, we mwenyewe ukiwasikia sound zao, na ukiona swaga zao utawakubali.
Na uzuri zaidi sio sound na swaga tu, bali wanakula kweli mizigo fasta tena bure bure. Sio watu wa maneno miiiingi na resi kibao halafu mwisho wa siku wakaishia kunawa. La hasha, wanasoundisha na wanakula mzigo.
Kila wiki tunarekodi na kurusha kupitia email (au CD) "episode" kadhaa ambapo wataalam wanatokea mademu kwenye mazingira mbali mbali. Njiani, barabarani, vyuoni, kazini, stendi za daladala, kwenye daladala, club, beach, n.k.
Ukisikiliza hizi "episode" utapata darasa kamili la ujanja wa kumtongoza mwanamke yoyote yule, mahali popote.
Si rahisi kukupa picha kamili kwa maneno tu, inabidi ujiunge nasi uanze darasa ndipo utajionea mwenyewe.

Kwenye "episode" zetu utasikia staili mbali mbali za kutongoza, kama vile:
Tongoza ya kistaarabu (kiupole)
Tongoza ya ki-gangsta (yaani kigumu gumu)
Tongoza ya ki-mafia (yaani no kubembeleza)
Tongoza ya kizungu
Tongoza ya kihindi
Tongoza ya kiarabu
Tongoza ya kimya kimya
Tongoza ya mchanganyiko wa aina mbali mbali hapo juu
Kila tongoza ina mahali pake, utasikia na maelekezo ya ziada kuwa tongoza ipi itumike wapi ... ukichanganya umeharibu!
Na Si Hayo Tu...

Kwenye "episode" za kila wiki utapata sio tu kusikiliza laivu wanawake mbali mbali wanavyotongozwa mpaka kitandani, bali utapata na "track" za ziada ambapo mtaalam husika anaelezea na kufafanua kile alichokuwa anafanya na mahesabu aliyokuwa anapiga kichwani mwake wakati anamtongoza huyo mwanamke.

Kutongoza kunahitaji maandalizi makubwa nyuma ya pazia ... maandalizi ya kiakili, kimuonekano, kusoma mazingira, na kumsoma mwanamke.
Kwa hiyo utapata na maelezo ya ziada kwa nini mwanamke fulani katongozwa kwa staili fulani badala ya staili fulani. Hii itakusaidia kukujenga ndani na nje ili uwe "striker" hatari kuliko Emmanuel Okwi.

Mourinho: Sidhani kama Chelsea watapoteza kwa jinsi wanavyo paki basi

Kocha wa klabu ya Manchester United Jose Mourinho amekiri itakuwa vigumu mno kwa timu yake kushinda ubingwa wa ligi kuu msimu huu kwa sababu ya tabia ya Chelsea kupaki basi.
Man United ambayo ipo katika nafasi ya sita ipo nyuma ya Chelsea kwa jumla ya pointi 13, ambao wameshinda mechi zao 11 za mwisho na kuizidi Liverpool inayoshika nafasi ya pili kwa jumla ya pointi sita.

Mourinho amesema kuwa haitakuwa rahisi kwa klabu yake ya Man United kuzifikia alama ya klabu yake ya zamani, hasa ukizingatia Chelsea wanacheza mchezo wa kukaba zaidi.
“Ni vema kuwa mkweli na kusema kwamba ni ngumu sana (kutwaa ubingwa msimu huu). Si tofauti ya alama tu, bali pia falsafa ya Chelsea katika uchezaji. Hawajali nini watu wanasema, wala wanachofikiria watu. Wao wanataka kushinda tu. Na kwa sababu hiyo, sidhani kama watapoteza pointi.”

Mechi nne za mwisho kati ya sita walizoshinda Chelsea wamepata ushindi wa 1-0.

CAF yatangaza majina 3 ya wachezaji wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika

Shirikisho la mpira wa miguu Afrika (CAF) limetangaza majina ya wachezaji watatu ambao watawania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa mwaka huu.
Wachezaji waliotajwa kwenye orodha hiyo ni pamoja na Pierre-Emerick Aubameyang wa Gabon (Borussia Dortmund), Riyad Mahrez wa Algeria (Leicester City) na Sadio Mané wa Senegal (Liverpool).
Wachezaji wengine waliotajwa kuwania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa ligi za ndani kwa ligi za ndani ni golikipa wa Uganda Dennis Onyango na Khama Billiat wa Zimbabwe wote wanachezea klabu ya Mamelodi Sundowns na Rainford Kalaba kutoka Zambia na klabu ya TP Mazembe.

Tuzo hizo zinatarajiwa kutolewa Januari 5, mwakani jijini Abuja, Nigeria.

PSG ya kamilisha usajili wa kiungo Julian Draxler

Klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) ya Nchini Ufaransa, imetangaza kufanya usajili wa kiungo mshambuliaji ,Julian Draxler kutoka Wolfsburg kwa mkataba wa miaka minne na nusu kwa ada ambayo inasemekana kuwa ni pauni milioni £34m.
Mjerumani huyo,23, atajiunga rasmi na matajiri hao wa Ufaransa mwezi ujao katika dirisha dogo la usajili.

Souvenir France vs Portugal

#FRANCE - Ce moment où les larmes ont coulé...

Ronney en doute

Oui, c'est encore plus fou. 💸💸
800.000 euros de salaire par semaine offre des maîtres chinois guangzhou ever grande star le buteur anglais Wayne Rooney pour un changement. C'est ce que rapporte the mirror.
Oscar a changé hier de Chelsea à Shanghai sipg - et encaisse 415.000 euros nets par semaine.

vendredi 23 décembre 2016

GRANERO : "MOURINHO EST ADORABLE, FLORENTINO PÉREZ EST UN HOMME INSPIRANT"

Esteban Granero garde des bons souvenirs de son passage au Real Madrid et notamment de José Mourinho et Florentino Pérez.
Formé au Real Madrid, Esteban Granero a évolué avec l'équipe première des Merengue entre 2009 et 2012 avant de s'envoler vers d'autres cieux afin de trouver un peu plus de temps de jeu. Le milieu de terrain espagnol de 29 ans a connu une période dominée par le FC Barcelone mais a tout de même remporté la Liga avec son club formateur. Dans un entretien accordé à EFE Radio, il est revenu sur son passage au Real Madrid et a encensé José Mourinho qui selon lui n'est pas la même personne en réalité que face aux médias.

" José Mourinho est adorable, il crie quand il doit le faire. Il est très intelligent et utilise les médias comme filtre ou pour lancer des messages, toujours dans l'optique que ses joueurs et son équipe en soient bénéficiaires. Cela lui a causé beaucoup de problèmes, à lui, à sa famille et à son image. Florentino Pérez est un homme inspirant. Il ne s'arrête pas de travailler. Le président, qui a toujours été ici, est très apprécié. Beaucoup de présidents du Real Madrid sont passés et aucun n'est comme lui. De mon point de vue. J'ai toujours été pour le Real Madrid et il a procuré du plaisir. Pas seulement de la façon dont il fait son travail mais aussi comment il traite ses employés ", a déclaré Esteban Granero .

L'ancien milieu de terrain du Real Madrid a évoqué la domination du Barça à cette époque : " Le FC Barcelone a fait un grand saut avec Pep Guardiola et a formé cette équipe qui n'arrêtait pas de gagner. Jusqu'à ce qu'en 2011 nous gagnions la Liga. Cela a été comme le premier revers qu'a connu cette équipe. Nous avons remporté le championnat avec José Mourinho et avec 100 points. Nous avons mis le Real Madrid à sa place et Barcelone à la sienne".

Mke wa Mugabe aamrishwa kurudisha nyumba tatu

Jaji mmoja nchini Zimbawe amemwaagiza mke wa rais Robert Mugabe, Grace Mugabe, kurudisha nyumba tatu alizompokonya mfanyabiashara nmoja raia wa Lebanon, kufuatia zabuni ya pete ya almasi ya gharama ya dola milioni 1.35.
Kulingana na kesi iliyowasilishwa na mfanyabiashara huyo, Bi Mugabe alitaka kurudishiwa pesa baada ya pete hiyo ya almasi iliyonunuliwa mjini Dubai. ilipowasilishwa kwake baada ya kutengenezwa na mtu tofauti.

Wakati Jamal Ahmed alishindwa kulipa pesa hizo kwa akaunti mjini Dubai, na licha ya yeye kusema kuwa pesa hizo zilitumwa kupitia kwa benki moja ya Zimbabwe, Bi Mugabe alichukua kwa nguvu nyumba zake tatu mwezi Oktoba.
Jaji Clement Phiri alisema kuwa Bi Mugabe pia ni lazima ahakikishe kuwa wafanyakazi wote waliokuwa wakihudumu kwenye nyumba hizo wamerudishwa kazini.
Pete hiyo ilikuwa ni kama zawadi kwa mke wa rais Mugabe, Bi Grace, kuadhimisha miaka 20 ya ndoa.

Mshukiwa wa shambulizi la Berlin auawa Italia

Mtu aliyeendesha shambulizi kwenyr soko mjini Berlin Anis Amri, ameuawa kwa kupigwa risasi na polisi mjini Milan nchini Italia.
Mtu huyo alikuwa amewafyatulia polisi risasi walipomaka awaonyeshe kitambulisho chake walipokuwa wakipiga doria eneola Sesto San Giovani. mapema siku ya Ijumaa.
Polisi mmoja aliuawa wakati wa ufyatuaji huo wa risasi,

Ujerumani imekuwa kwenye tahadhari kubwa tangu lifanyike shambulizi lililowaua watu 49.
Wakati huo huo polisi wamewakamata watu wawili katika mji wa Oberhausen baada ya kushukiwa kupanga mashambulizi.

Alama za vidole za mtu aliyeuawa vinafanana na alama za mshukiwa raia wa Tunisia ambaye aliendesha shambulizi la bomu la lori mjini Berlin siku ya Jumatatu na kuwaua watu 12.

Diafra Sakho kukosa michuano ya mataifa bingwa barani Afrika

Mchezaji wa klabu ya West Ham na timu ya taifa ya Senegal, Diafra Sakho hatacheza katika mechi ya kuwania kombe la mataifa bingwa barani Afrika baada ya kuripotiwa kuwa hatacheza kwa kipindi cha wiki nane zaidi kutokana na jeraha.
Klabu ya West Ham ilitoa taarifa tarehe 30 mwezi Novemba kuwa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 26 hatacheza kwa wiki sita ikimaanisha kuwa hatarejea uwanjani hadi kati kati ya mwezi wa Januari.

Lakini koacha wa West Ham Slaven Bilic, amesema kuwa Sakho huenda asicheze kwa kipindi cha wiki nane na huenda sasa akarejea kati kati ya mwezi Februari.

Vanessa Mdee kubadili dini sababu ya Jux?

Iko wazi, kwamba wapenzi wengi wa dini tofauti, huamua kuchagua njia moja iwapo lengo lao ni kuja kufunga ndoa na kuwa mke na mume, kihalali.

Vipi kwa upande wa Vanessa Mdee ambaye ni mkrito, na Juma Jux ambaye ni muislamu, mustakabali wao ni upi iwapo wanakoelekea ndio huko ambako ndugu na jamaa zao wanapenda wafike yaani ndoani?
Nani yuko radhi kubadili dini yake? Swali hilo lilitupiwa kwa Vanessa Mdee na watangazaji wa kipindi cha The Base cha ITV.


“No, sina mipango yoyote ya kubadilisha dini,” jibu la Vee Money lilikuwa fupi kama hivyo.
There you have it!

Chelsea yathibitisha kumuuza Oscar kwenye ligi ya China

Klabu ya soka ya Chelsea ya Uingereza imethibitisha kumuuza kiungo wao Oscar dos Santos kwenye timu ya Shanghai SIPG ya China.
Kupitia mtandao wa Twitter wa klabu hiyo umeandika, “Thank you, @oscar8 and good luck for the future.”

Mchezaji huyo alikuwa anawindwa kwa muda mrefu na timu hiyo ambayo iliahidi kulipa ada ya uhamisho wa paundi milioni 52 na kumlipa mshahara wa paundi laki nne kwa wiki na kumfanya awe mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa zaidi duniani.


Naye mchezaji wa Boca Juniors ya Argentina anatazamiwa kujiunga na ligi hiyo ya China kwenye timu ya Shangahi Shenhua.


Leicester yashinda tuzo la klabu bora ya mwaka Uingereza

Klabu ya soka ya Leicester imeshinda tuzo ya timu bora ya mwaka kwa kuwashangaza wengi waliposhinda ligi ya Uingereza.
The Foxes kama inavyojiita ilishinda tuzo ya timu bora ya mwaka na mkufunzi wake Claudio Ranieri alitangazwa kuwa kocha bora baada ya kuisaidia timu hiyo kushinda taji hilo.
Leicester ilianza kampeni ya kushinda taji hilo bila wengi kutarajia baada ya kushushwa katika ligi ya Uingereza mwaka 2014-15.
Walipoteza mechi tatu pekee katika msimu wa 2015-16 na wamefuzu kucheza kombe la vilabu bingwa Ulaya na kuendelea hadi raundi za muondoano.
Mwanzoni mwa mwezi Aprili, Leicester ilikuwa pointi saba juu katika jedwali la ligi ya Uingereza .
Mwaka mmoja kabla ,walikuwa chini ya jedwali hilo pointi saba pekee juu ya timu ambazo zilishushwa daraja.
Mwogeleaji wa Marekani Michael Phelps alishinda tuzo la mwanariadha bora wa olimpiki baada ya kushinda medali 23 za dhahabu.

samedi 17 décembre 2016

Barua ya Mohammad Ali kwa Mandela yauzwa pauni 7,200

Barua iliyowekwa sahihi na mwanamasumbwi Mohammad Ali na kuandikiwa rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela, akitoa rambu ramba zake kufuatia kuawa kwa mtu aliyekuwa akipinga ubaguizi wa rangi imeuzwa kwa pauni 7,200.
Muuzaji wa barua hiyo Andrew Aldridge alisema, "ni vyema kuwa Mohammad Ali alikuwa mwanamichezo bora zaidi hukui naye Nelson Mandela akiwa mtu mashuhuri zaidi katika karne iliyopita.
Barua hiyo ilipiwa chapa cha msaidizi wa meneja wa hoteli ya Elangeni iliyo mjini Durban ambapo Ali alikuwa akiishi wakati huo.
Barua hiyo iliyouzwa kwa mnunuzi kutoka nchini Marekania ilitarajiwa kuuzwa kwa kati ya dola 6,000 na 8,000.

Muhammad Ali alikuwa nchini Afrika Kisini kwa kipindi kifupi mwezi Aprili mwaka 1993 baada ya kuwasili muda mfupi baada ya kuuliwa kwa Chris Hani tarehe 10 mwezi Aprili.
Hani alikuwq kamanda wa kundi la Umkhonto We Sizwe, kundi lililojihami la ANC.
Alikuwa mkosoaji mkubwa wa serikali ya ubaguzi wa rangi na aliuaw mkereketwa mmoja nje ya nyumba yake eneo la Boksburg.

Muhammad Ali's letter of condolence to Nelson Mandela up for sale


A signed letter from Muhammad Ali to Nelson Mandela offering his condolences on the death of an anti-apartheid leader will be sold at auction.
The letter, dated April 13 1993, is typed and signed by Ali on letter-headed Muhammad Ali in South Africa stationery.
It was typed by the personal assistant to the general manager of the Elangeni Hotel in Durban where Ali was staying at the time.
Ali requested the letter typed to express his condolences to Mandela on the loss of Chris Hani, who was assassinated on April 10 1993.
It will be sold at Henry Aldridge and Son in Devizes, Wiltshire, next Saturday and is expected to fetch between £6,000 and £8,000.
The letter reads:
"Dear Mr Mandela
"Allow me to extend to you and the A.N.C. my deepest regrets upon hearing of the death of Chris Hani. My prayers go out to Mr Hani's family and the people of South Africa during these difficult days.
"I am providing you the following information regarding my itinerary should you desire to contact me (prior to our scheduled meeting on 19 April 1993):-
"CAPE SUN - 13 TO 16 APRIL - TEL: 021 238844 FAX: 021 238875
"JOHANNESBURG GARDEN COURT - 16 TO 22 APRIL - TEL: 011 297011 FAX: 011 291515
"Inshallah, I pray that God keeps you safe"
A letter signed by the personal assistant who typed it includes: "Due to my nervous excitement about typing a letter of such historical importance I misspelt the name Muhammad replacing the last "a" with an "e".
"The letter was taken to Muhammad Ali and duly signed before someone noticed the error and returned it to me. I typed it again but kept the incorrect copy for posterity."
Auctioneer Andrew Aldridge said the letter was from one of the greatest sportsmen to one of the greatest men in history.

"It is a truly iconic cross collectable and will appeal to collectors of Ali memorabilia as well as those who collect Nelson Mandela material, items relating to apartheid, political history and collectors of iconic memorabilia," Mr Aldridge added.
"Muhammed Ali was only in South Africa for a short period in April 1993, arriving shortly after the assassination of Chris Hani on April 10.
"Hani was the chief of staff of Umkhonto We Sizwe, the armed wing of the African National Congress (ANC). He was a fierce opponent of the apartheid government and was murdered by a far right extremist outside of his home in Boksburg.
"Against that backdrop Ali arrived in South Africa at a time when the country stood on the edge of a precipice with civil war a possibility.
"He attended Hani's farewell at the FNB Stadium in Johannesburg on April 19th 1993, when he appeared to the crowd, they chanted "Ali! Ali!"."
Mr Aldridge said Mandela kept a photograph of himself with Ali on his desk and his favourite book, in his later years, was an autographed copy of Ali's biography.

Mwana FA asema wimbo ‘Muziki’ wa Darassa umerudisha heshima kwa wana hip hop

Msanii wa muziki wa hip hip, Mwana FA amesema hatua ya mafanikio ya wimbo ‘Muziki’ wa Darassa ni hatua ambayo wasanii wengi wa muziki wa hip hop walishindwa kuifikia kwa muda mrefu.

Rapa huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo wake ‘Dume Suruali’ amesema ni muda mrefu wasanii wa hip hop walikuwa wanashindwa kutoa ngoma ambazo zitaleta ushindani mkubwa na zawasanii wa kuimba.

“Kwanza I’m happy for rap music,” FA alikiambia kipindi cha FNL cha EATV. “Imekuwa muda mrefu hatujawahi kutengeneza nyimbo halafu zikatoka na nyimbo za waimbaji, halafu usisikie nyimbo za waimbaji na rap music ikawa vile,

Mwana FA amesema anapenda kuona Darassa akiendelea kufanikiwa zaidi katika muziki kwa kuwa ni msanii ambaye anaujua uwezo wake katika kile anachokifanya.

Wimbo ‘Muziki’ wa Darassa umeweza kufanya vizuri kwenye chart mbalimbali za muziki. Pia kupitia channel ya mtandao wa YouTbe video ya wimbo huo imeweza kuangaliwa mara 1,787,074 katika kipindi cha wiki tatu.

Mahakama ya Uganda yaamuru kukamatwa kwa Wizkid

Wizkid anakabiliwa na kifungo cha miaka 11 jela, baada ya mahakama ya Uganda kutoa hati ya kukamatwa kwake na meneja wake, Sunday Aare.
Wizkid alishindwa kutokea kwenye show iliyokuwa ifanyike December 3 mwaka huu mjini Kampala. Kampuni iliyomlipa, Face TV, kupitia mwanasheria wake, Fred Muwema, imepata kibali cha kumkamata muimbaji huyo kwa kuchukua dola $60,000 na kushindwa kutokea kwenye show. Gharama zingine walizotoa ni brokerage fee, $5,000 na per die, $3,000 kwa muda ambao Wizkid angekaa Uganda.
Muimbaji huyo alidaiwa kushindwa kusafiri na ndege toka Marekani kwenda nchini humo kwa show hiyo.
“Between 29th August 2016 and 29th November 2016, our client (Face TV) paid to Mr. Sunday Are, Wizkid’s manager the full performance fee of US$60,000, a brokerage fee of US$5,000 and US$3,000 being per diem for the days they were going to stay in Uganda,” yanasomeka maelezo ya mlalamikaji.
Zaidi ya watu 25,000 walikuwa wamenunua tiketi kwaajili ya show hiyo. Maelezo yaliyowasilishwa mahakamani yameeleza kuwa mwandaaji wa shiw hiyo amekula hasara ya zaidi ya $300,000 kutokana na maandalizi aliyofanya.
 

Ban Ki-moon kugombea urais Korea Kusini

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amedokeza kuwa huenda akawania urais nchini mwake, Korea Kusini.
Muhula wake Ban kama katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa unakamilika mwisho wa mwezi huu wa Disemba
Wakati wa mkutano wake wa mwisho na waandishi wa habari, Ban alisema kuwa baada ya kupata mapumziko anarudi nchini mwake Korea Kusini kuona vile ataisaidia nchi yake.
Uchaguzi wa uraia nchini Korea Kusini unatarajiwa kufanyika Desemba mwaka 2017


Lakini huenda uchaguzi huo ukafanyika katika muda wa miezi miwili baada ya bunge la nchi hiyo kupiga kura ya kumuondoa madarakani Rais Park Geun-hye, kutokana na sakata, ambapo analaumiwa kwa kumruhusu rafiki wake wa karibu kunufaika kifedha.
Ikiwa mahakama ya katiba itadumisha kura hiyo ya kumuondoa, atakuwa rais wa kwanza wa Korea Kusini aliye madarakani kuondelwa katika kipindi cha uhuru wa nchi hiyo.
Mahakama ya katiba ina siku 180 kutoa uamuzi wa mwisho.
Matamshi ya Ban yanakuja huku yakishuhudiwa maandamano kwenye mji mkuu wa Korea Kusini, Seol.

Oscar kuwazidi Messi na Ronaldo kwa kulipwa pesa nyingi

Mchezaji wa Chelsea Oscar anatarajiwa kuwa mchezaji soka anayelipwa pesa nyingi zaidi duniani atakapohamia Ligi Kuu ya Uchina mwezi Januari.
Shanghai SIPG wanatarajiwa kulipa £60m kumchukua kiungo huyo wa kati kutoka Brazil.
Akifanikiwa kuondoka, basi Oscar, 25, ataungana na meneja wa zamani wa Chelsea Andre Villas-Boas, ambaye kwa sasa ndiye mkufunzi wa Shanghai.
Taarifa zinasema atakuwa analipwa £400,000 kila wiki (£20.8m kila mwaka), ingawa huenda akapitwa haraka kwani kuna taarifa kwamba klabu za China zinajiandaa kulipa pesa nyingi kununua wachezaji wengine Januari. Mshahara wa Oscar ni sawa na £57,143 kila siku, au £2,381 kwa saa, au £39 kila dakika.
Kuna taarifa huenda Shanghai Shenhua ,ambao mkufunzi wao kwa sasa ni Gus Poyet aliyetoka Sunderland, wanapanga kumnunua nyota wa zamani wa Manchester United na Manchester City Carlos Tevez kutoka Boca Juniors. Tevez atakuwa analipwa £31.5m kila mwaka, sawa na £605,000 kila wiki.

France Football wanasema mshambuliaji wa Paris St-Germain na Uruguay Edinson Cavaninaye huenda akahamia Tianjin Quanjian, walio chini ya beki wa zamani wa Italia Fabio Cannavaro, kwa euro 50m (£41.79m) fambapo atakuwa akilipwa £16.7m kila mwaka.
Mwenzake kwenye klabu Javier Pastore kutoka Argentina pia huenda akahamia China.
Kiungo wa kati wa Arsenal Alexis Sanchez pia amehushishwa na kuhamia Hebei China Fortune, ambayo mkufunzi wake kwa sasa ni aliyekuwa meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini. Sanchez, anatarajiwa kulipwa £500,000 kila wiki iwapo atakubali kuhama.
Klabu ambazo zimetumia pesa nyingi zaidi karibuni nchini China ni Shanghai SIPG, Jiangsu Suning, mabingwa wa ligi Guangzhou Evergrande Taobao na Shanghai Shenhua.
Klabu za Ligi Kuu ya China zilitumia £200m kununua wachezaji kabla ya kuanza kwa ligi 2016.
Rekodi ya wachezaji ilivunjwa mara tatu kipindi cha siku 10. Jiangsu Suning walilipaShakhtar Donetsk £38.4mkumchukua Mbrazil Alex Teixeira baada ya kumchukua Ramires for £25m kutoka Chelsea siku chache awali.

Guangzhou Evergrande Taobao walimnunua nyota wa Colombia Jackson Martinez £31m kutoka Atletico Madrid.
Bei ya Teixeira hata hivyo ilipitwa na ya £46.1m (euro 55.8m) waliyolipa Shanghai SIPG kumchukua Mbrazil Hulk kutoka Zenit St Petersburg.

WACHEZAJI WANAOLIPWA PESA NYINGI ZAIDI DUNIANI
-------------------------

1) Oscar (Shanghai SIPG) £400,000 kila wiki £20.8m kila mwaka (kuanzia Januari)

2=) Cristiano Ronaldo (Real Madrid) £365,000 kila wiki £19m kila mwaka (kabla ya kutozwa kodi)

2= Lionel Messi (Barcelona) £365,000 kila wiki £19m kila mwaka(kabla ya kutozwa kodi)

4) Gareth Bale (Real Madrid) £346,000 kila wiki £18m kila mwaka(kabla ya kutozwa kodi)

5) Hulk (Shanghai SIPG) £317,000 kila wiki £16.5m kila mwaka

6) Paul Pogba (Manchester United) £290,000 kila wiki £15m kila mwaka

7) Neymar (Barcelona) £289,000 kila wiki £15m kila mwaka(kabla ya kutozwa kodi)

8=) Graziano Pelle (Shandong Luneng) £260,000 kila wiki £13.5m kila mwaka

8=) Wayne Rooney (Manchester United) £260,000 kila wiki £13.5m kila mwaka

10) Zlatan Ibrahimovic (Manchester United) £250,000 kila wiki £13m kila mwaka

jeudi 15 décembre 2016

Chapecoense wapangiwa mechi ya kwanza Brazil

Klabu ya Chapecoense itacheza mechi ya kwanza tangu kutokea kwa ajali ya ndege iliyoangamiza wengi wa wachezaji wake tarehe 29 Januari.

Maafisa katika klabu hiyo ya Brazil wameambia BBC kwamba klabu hiyo imepangiwa kucheza dhidi ya International de Lage nyumbani katika mechi ya ligi ya ubingwa wa jimbo.

Ndege iliyobeba wachezaji na maafisa wa timu hiyo iliishiwa na mafuta na kuanguka Medellin, Colombia mnamo 28 Novemba, na kuua watu 71, wakiwemo wachezaji na maafisa wa klabu hiyo.
Wachezaji watatu wa klabu hiyo walikuwa miongoni mwa manusura sita.

Wachezaji tisa hawakusafiri.

Wachezaji wawili kati ya walionusurika, beki Alan Ruschel na kipa Jakson Follmann, ambaye amekatwa mguu wake, walirejea Brazil Jumanne.

Wa tatu, neto, bado amelazwa hospitalini Colombia.

Vagner Mancini ameteuliwa meneja na kupewa jukumu la kuunda upya timu hiyo kutoka mji wa Chapeco, kusini mwa Brazil.

Klabu kubwa Brazil zimeahidi kuikopesha Chapecoense wachezaji bila malipo na pia zikaomba timu hiyo ilindwe dhidi ya kushushwa daraja misimu mitatu ijayo.

Mchezaji wa zamani wa Brazil na Barcelona Ronaldinho na nyota wa zamani wa Argentina Juan Roman Riquelme wanadaiwa kujitolea kuichezea klabu hiyo.

Mchezaji wa zamani wa Barca Eidur Gudjohnsen, pia yuko tayari kuchezea klabu hiyo.

mercredi 14 décembre 2016

Le Ballon d’or de Ronaldo déjà au musée !

Après avoir remporté son quatrième Ballon d’or, Cristiano Ronaldo l’a immédiatement exposé dans son musée de Madère, avec tous ses trophées.

Il n’a pas traîné ! Deux jours après la conquête de son quatrième Ballon d’or, Cristiano Ronaldo, actuellement au Japon pour disputer la Coupe du monde des clubs avec le Real Madrid, a déjà fait figurer l’iconique trophée dans le musée qui porte son nom, à Funchal, sa ville de naissance.
"Mon Ballon d’or est disponible dans mon musée de Madère", écrit-il en légende d’une photo où on peut apercevoir le trophée en bonne place dans le "Museu CR7", qui accueille 200 000 visiteurs par an.

Un musée, financé par la star portugaise, qui a récemment été agrandi "pour accueillir tous les nouveaux trophées de Ronaldo", avait déclaré son cousin l’été dernier. Bien vu.

Adabu kwa Chelsea na Manchester City wapigwa fain

Chelsea wamepigwa faini ya £100,000 na Manchester City wakapigwa faini ya £35,000 baada ya wachezaji wao kuhusika katika vurugu uwanjani wakati wa mechi ya Ligi ya Premia.
Hisia zilipanda na wachezaji wakakabiliana mechi hiyo iliyochezewa uwanjani Etihad ilipokaribia kumalizika baada ya Sergio Aguero wa City kufukuzwa uwanjani kwa kumchezea visivyo beki wa Chelsea David Luiz.
Fernandinho pia alifukuzwa uwanjani kwa kumkaba koo Cesc Fabregas wachezaji wa klabu hizo mbili walipokabiliana baada ya kisa hicho.
Chelsea walishinda 3-1.

Blues walikuwa awali wametahadharishwa kwamba wanaweza kupokonywa alama kwa utovu wa nidhamu.
Viongozi hao wa Ligi ya Premia wamepigwa faini mara sita tangu Februari 2015 kwa kushindwa kuwadhibiti wachezaji.

Lionel Messi akutana na kijana aliyevalia jezi ya karatasi Afghanistan

Mvulana kutoka nchini Afghanistan aliyepata umaarufu sana mtandaoni alipopigwa picha akiwa amevalia karatasi kama jezi ya Lionel Messi mechi amefanikiwa kukutana na shujaa huyo wake.
Picha ya Murtaza Ahmadi, mwenye miaka sita, akiwa amevalia karatasi hiyo iliyoandika nambari ya jezi ya Messi pamoja na jina lake ilivuma sana mwezi Januari mtandaoni.
Mwishowe, alipokea jezi halisi kutoka kwa mshambuliaji huyo wa Barcelona, ambayo pia ilikuwa imetiwa saini na mchezjai huyo.
Sasa, wawili hao wamekutana ana kwa ana mjini Doha, kwa mujibu wa kamati andalizi ya Kombe la Dunia la 2022 nchini Qatar.

Barcelona wamo nchini Qatar kucheza mechi ya kirafiki na Al Ahli Jumanne.
Ahmadi anatarajiwa kutembea kuingia uwanjani akiandamana na Messi.
"Ni picha ambayo ulimwengu ulitaka kuona," aliandika mkuu wa kamati hiyo Jumanne.
"Mvulana wa miaka sita akikutana na shujaa wake, #Messi, ndoto yake ikitimia."
Ahmadi, ambaye anatoka wilaya ya Jaghori, katika mkoa wa Ghazni mashariki mwa Afghanistan, alilazimika kukimbilia nchi jirani ya Pakistan mwezi Mei.
Murtaza alitambuliwa kama mvulana ambaye picha yake ilikuwa ikisambazwa mtandaoni baada ya mjomba wake Azim Ahmadi, raia wa Afghanistan anayeishi Australia, kuwaunganisha waandishi wa BBC Trending na nduguye, Arif - babake shabiki huyo mkubwa wa Messi.

Professor Jay amuandikia barua yenye ujumbe mzito Darassa

Ni ukweli kuwa kwa sasa Darassa ameyasogelea mafanikio aliyokuwa akiyatamani kwa muda mrefu. Rapper mkongwe wa muziki wa Hip Hop nchini, Professor Jay amemuandikia ujumbe hitmaker huyo wa Muziki wa kumpongeza kwa kazi nzuri anayoifanya na kumtaka kuendelea kukaza buti.

Kupitia mtandao wa Instagram, Jay ameandika:

Mdogo wangu @darassacmg Imani yako, Kutokukata tamaa na Struggle yako ya Usiku na Mchana ndio imekufanya ufikie hapo ulipofikia, Nakumbuka wakati unashoot Wimbo wako wa USIKATE TAMAA uliniambia unatamani ufikie level za juu kama zetu, Nami nilikwambia hakuna kinachoshindikana chini ya JUA Ukiset GOALS, kufanya kazi kwa bidii na SALA yote Yanawezekana, Naamini kwa style hii ya JIWE juu Ya JIWE, NDOTO yako inakwenda kuwa kweli, Cha MSINGI usiridhike na mafanikio haya..HUU ni mwanzo tuu na mafanikio makubwa zaidi yako at your DOOR, Keep your eyes open and Keep ya HEAD UP,
SKY IS THE LIMIT, GO GET DEM… BLESS
#ACHA MANENO WEKA MUZIKI
@darassacmg @darassacmg

Classement complet ballon d'or france football 2016

1. Cristiano Ronaldo (Real Madrid/Portugal) 745 points
2. Lionel Messi (FC Barcelone/Argentine) 316
3. Antoine Griezmann (Atlético Madrid/France) 198
4. Luis Suarez (FC Barcelone/Uruguay) 91
5. Neymar (FC Barcelone/Brésil) 68
6. Gareth Bale (Real Madrid/Pays de Galles) 60
7. Riyad Mahrez (Leicester/Algérie) 20
8. Jamie Vardy (Leicester/Angleterre) 11
9. Gianluigi Buffon (Juventus Turin/Italie) et Pepe (Real Madrid/Portugal) 8
11. Pierre-Emerick Aubameyang (Borussia Dortmund/Gabon) 7
12. Rui Patricio (Sporting CP/ Portugal) 6
13. Zlatan Ibrahimovic (Manchester United/Suède) 5
14. Paul Pogba (Manchester United/France) et Arturo Vidal (Bayern Munich/Chili)
16. Robert Lewandowski (Bayern Munich/Pologne) 3
17. Toni Kroos (Real Madrid/Allemagne), Luka Modric (Real Madrid/Croatie) et Dimitri Payet (West Ham/France) 1

Non-classés : Agüero, De Bruyne, Dybala, Godin, Higuain, Iniesta, Koke, Lloris, Müller, Neuer, Sergio Ramos.

Yaya Toure: Sikujua Coke ilikuwa imeongezwa pombe

Mchezaji nyota wa Ivory Coast Yaya Toure amesema hajapinga shtaka la kuendesha gari akiwa amelewa wiki mbili zilizopita.
Hata hivyo, amesema kwamba hakunywa pombe makusudi alipokamatwa akiendesha gari akiwa mlevi.
Ameandika kwenye Facebook kwamba "inafahamika wazi kwamba mimi ni Mwislamu na huwa sinywi pombe."

Hata hivyo, hajaelewa ni vipi alijipata akinywa pombe ama akajipata akiwa amelewa bila yeye kufahamu.
Gazeti la The Mirror la Uingereza linasema kwamba alidai alikunywa Diet Coke na hakujua kwamba kwenye jagi aliyokuwa akitumia kunywa palikuwa pameongezwa kilevi aina ya brandi.
Gazeti hilo linasema amepigwa marufuku kutoendesha gari kwa miezi 18 na kupigwa faini ya $68,000 (£54,000).

Mchezaji huyo wa Manchester City amesema: "Daima nimekuwa nikikataa pombe. Yeyote anayenifahamu na anayefuatilia uchezaji wangu atakuwa bila shaka ameniona nikikataa shampeni ya Mchezaji Bora wa Mechi kwa sababu ya kujitolea kwangu kuheshimu dini yangu."

"Ni muhimu kwangu kwamba niliiambia mahakama kwamba sikunywa pombe makusudi. Jaji akinihukumu mwenye alikubali kwamba sikuwa nimekunywa pombe makusudi."
Amesema kesi yake ilihitimishwa Jumatatu na kwamba alikubali shtaka.
"Kuendesha gari ukiwa mlevi ni kosa kubwa na ingawa sikunywa pombe makusudi, nakubali marufuku na faini na naomba radhi kwa yaliyotokea," aliongeza.

lundi 12 décembre 2016

Chelsea watapokonywa alama EPL?

Meneja wa Chelsea Antonio Conte amepuuzilia mbali pendekezo kwamba huenda viongozi hao wa Ligi Kuu ya Uingereza wakapokonywa alama kutokana na utovu wa nidhamu.
Chelsea na Manchester City wameshtakiwa kwa kukosa kuwadhibiti wachezaji wao wakati wa mechi kati ya klabu hizo mbili tarehe 3 Desemba.
Baada ya visa kadha awali, bodi ya rufaa ya Chama cha Soka England ilikuwa imeonya Chelsea mnamo Julai kwamba karibu utafika wakati ambapo "adhabu pekee itakayotosha ni kupokonywa alama".
Alipoulizwa kuhusu uwezekano wa hilo kutokea, Conte aliwaambia wanahabari: "Unafanya mzaha? Unatania?"

Chelsea wametozwa faini mara tano na FA kwa kukosa kuwadhibiti wachezai tangu Februari 2015.
Viongozi hao wa EPL awali walitozwa faini ya juu sana ya £375,000 kutokana na mashtaka matatu kutoka kwa mechi ambayo iliisha sare 2-2 wakicheza dhidi ya Tottenham uwanjani Stamford Bridge Mei.

Bodi ya rufaa ilipunguza faini hiyo hadi £290,000 lakini ikashutumu Chelsea kwa kuwa na rekodi mbaya ya kushindwa kuwadhibiti wachezaji.
Mara ya mwisho klabu kupokonywa alama kwa sababu ya utovu wa nidhamu ilikuwa Manchester United na Arsenal waliopokonywa alama kutokana na vurugu zilizotokea Old Trafford Oktoba 1990.

Wakati wa kuadhibu Chelsea kuhusu matukio ya Stamford mwezi Mei, tume ya FA ilisema ilitafakari uwezekano wa kupokonya alama Chelsea lakini wazo hilo likaondolewa kutokana na sababu kwamba Chelsea hawakuwa wamepewa onyo la mwisho.
Chelsea na Spurs walionywa kuhusu mienendo yao siku za usoni lakini FA haikugusia kamwe "onyo la mwisho".

vendredi 9 décembre 2016

Barcelona invite Chapecoense to play in pre-season friendly in bid to aid the 'reconstruction of the club'

Barcelona have invited tragedy-struck Chapecoense to play in a pre-season friendly next summer.
The Spanish champions have formally asked the Brazilian club if they wish to take part in the Joan Gamper Trophy, an annual match between Barcelona and an invited opponent at the Nou Camp.

Barcelona say they want to pay tribute and help with the "institutional and sporting reconstruction" of Chapecoense following last month's plane crash which killed 71 people, including 19 players.

"Barcelona has agreed to invite to the next edition of the Joan Gamper Trophy the Brazilian team Chapecoense, who were the victims of the tragic plane crash when on the way to play the final of the Copa Sudamericana in Colombia on 28 November," a statement read.

"Barcelona wants to pay tribute to the 71 people who died in the accident and their families, and will therefore make the 2017 Joan Gamper Trophy a great tribute to the world of football through various activities around this match which will become known as the date of this celebration approaches.

"Along with the invitation to Chapecoense to the 2017 Joan Gamper Trophy, Barcelona would like to collaborate on the institutional and sporting reconstruction of the club, and help to recover the competitive level that it had.

"Barcelona has today sent a formal letter of invitation to the current board of directors of Chapecoense."

The plane carrying the Chapecoense team, along with club officials and journalists, to Medellin for the Copa Sudamericana final against Colombian side Atletico Nacional came down late on Monday, November 28.

Just three of the team - defender Alan Luciano Ruschel, reserve goalkeeper Jackson Ragnar Follmann and centre-back Helio Hermito Zampier Neto - were named among only six survivors of the crash.

The South American Football Confederation (CONMEBOL) this week declared Chapecoense Copa Sudamericana champions 2016.

Barcelona kushiriki mechi ya kirafiki na Chapecoense mwaka 2017

Barcelona wameikarabisha klabu ya Brazil ya Chapecoense kwa mechi ya kirafiki kabla msimu wa kiangazi ujao.

Wachezaji 19 wa Chapecoense na wahudumu wa klabu hiyo walikuwa miongoni mwa watu 71 waliuawa katika ajali ya ndege iliyokuwa ikiwasafirisha kutoka Colombia kwa michuano ya fainali ya mkondo wa kwanza wa Sudamericana.
Mechi hiyo ya kirafiki itakuwa ya kuwania kombe la Joan Gamper, ambayo huandaliwa kila mwaka kati ya klabu ya Barcelona na timu alikwa.

Katika taarifa, Barcelona imesema walitaka ''kutoa heshima zao za mwisho'' kwa waathiriwa na kuisaidia timu ya Chapecoense kustawi tena.

Wachezaji watatu wa Chapecoense walikuwa miongoni mwa watu sita walinusurika katika mkasa huo.
Barcelona wamesema walitaka kulifanya kombe hilo la Joan Gamper kama 'heshima yao kubwa kwa ulimwengu wa soka kupitia shughuli mbalimbali zitakazo andaliwa kwenye mchuano huo.

''Licha ya kuialika timu hiyo ya Chapecoense kwa kombe la Joan Gamper mwaka 2017, Barcelona pia wamesema wangependa kushirikiana na klabu hiyo kwa ujenzi wa uwanja ili kuisaidia timu hiyo kujiendeleza katika kiwango cha ushindani waliokuwa nao hapo awali,''waliongezea Barcelona.
Barcelona leo hii imetuma barua rasmi ya mualiko kwa bodi ya wakurungezi wa klabu ya Chapecoense.

JINSI YA KUMPATA MSICHANA ANAEONEKANA MGUMU KUPATIKANA

MWANAMUME yeyote anapotaka kumtongoza mwanamke hulazimika kwanza kumwonesha – japo kwa matendo – kuwa anampenda, au kwamba amevutiwa naye, hata kama ni kimwili tu. Hatua hii ndiyo yenye changamoto kubwa zaidi kwa mwanamume, maana ndipo wakati anapokuwa anajaribu kufikisha ujumbe kwa mlengwa huku yeye mwenyewe akijihakikishia kuwa haharibu mambo.
Mwanamume anapokuwa anajaribu kufikisha ujumbe wa “nakupenda” kwa mwanamke, mapigo ya moyo yanaweza kumwenda mbio, hususan kama mwanamke mwenyewe anaonekana kuwa “maji marefu”. Hata hivyo, ni kazi ambayo kila mwanamume hulazimika kuifanya.
Kazi hii ya kufikisha ujumbe kwa mara ya kwanza huhitaji umakini. Bahati njema, shughuli yenyewe ina sayansi yake, ambayo ina misingi katika mahusiano ya kijamii. Ukifahamu sayansi hii inaweza kuwa rahisi zaidi kwako kufikisha ujumbe kwa mtarajiwa wako – na kufanikiwa.

1. KUKUTANISHA MACHO NI MUHIMU

Kawaida, mambo yote huanzia – na pengine kuishia – katika kukutanisha macho. Mwanamke atakapobaini kuwa hujajaribu kumwangalia japo kwa sekunde mbili mfululizo, ataondoa mawazo na hisia zake kwako hata kabla hujasema neno lolote.
Macho ndizo zana muhimu zaidi mtu anapokuwa anataka kufikisha ujumbe kwa mwenzake kuwa anampenda, au amevutiwa naye. Hii ni kwa sababu macho ndiyo vipitisho na visambazaji muhimu vya ishara baina ya mtu na mtu, hata kama si katika masuala yanayohusiana na mapenzi.
Kukutanisha macho na mtu wa jinsia nyingine unayevutiwa naye au anayevutiwa nawe ni jambo lenye nguvu za ajabu katika kuanzisha uhusiano. Kwa sababu hiyo, hata unapofanikiwa kumtazama moja kwa moja machoni mwenzako hutarajiwi kutumia zaidi ya sekunde mbili, kutokana na nguvu iliyomo katika mawasiliano haya.
Katika hili, wanaume mahiri hufahamu ni wakati gani wa kumwangalia mwanamke na ni wakati gani wa kutomwangalia. Mara nyingi, ni vizuri zaidi kumwangalia zaidi mwanamke wakati anapozungumza, huku ukikwepesha macho kidogo pale unapozungumza wewe.

2. UNATAKIWA UWIANO, UKWELI KATIKA MAZUNGUMZO

Ni jambo lisilopingika kwamba wanaume na wanawake wanatofautiana katika maana ya dhana ya mawasiliano. Hata hivyo, bado inawezekana kuendesha mazungumzo shirikishi na yenye kuburudisha ukiwa na mwanamke, bila kuonekana wa bandia.
Watu wa jinsia zote mbili wanaweza kutuhumiwa kwa kupindisha ukweli na kujaribu kuficha tabia na mienendo yao wanapozungumza na wapenzi watarajiwa. Naam, katika mazungumzo ya kwanza baina ya wapenzi au wachumba watarajiwa uwongo – ukiwemo ule usiotarajiwa – huwa mwingi.
Katika mazungumzo ya kwanza ni kawaida kwa mwanamume kubadilisha matendo yake na mtindo wake wa kuzungumza kwa maslahi ya kumpata mwanamke, jambo ambalo huifanya hulka yake ya wakati huo kuwa ya bandia. Lakini pia wasichana/wanawake husema “Nakupenda” bila kumaanisha, pengine kwa ajili ya kumfurahisha mwanamume, au kusikia mwanamume atasemaje.
Jambo la muhimu katika mazungumzo ya awali baina ya mwanamume na mwanamke ni kuepuka michezo ya kudanganyana na kukwepana, badala yake, yafanye mazungumzo kuwa rahisi na halisi. Hapo ndipo mwanamume hujitofautisha na wanaume wengine na kupendwa kwa sababu hiyo.

3. USIPUUZE NGUVU YA LUGHA YA MATENDO

Wakati mtu anapokuwa akijaribu kuwasilisha ujumbe wa “Nakupenda” kwa mwenzake, lugha ya matendo yake huzungumza kwa sauti kubwa zaidi kuliko maneno yake. Hili limeweza kuthibitishwa kwa nyakati mbalimbali kutokana na tafiti mbalimbali.
Katika muktadha wa kujaribu kufikisha ujumbe wa “Nakupenda” kwa mlengwa, lugha ya matendo ndiyo yenye nafasi kubwa zaidi. Kwa hakika, asilimia kubwa ya ujumbe unaowasilishwa kwa mlengwa huwasilishwa kwa njia ya matendo ya mwili na si maneno. Ni asilimia ndogo tu ya ujumbe inayowasilishwa kwa maneno – na wakati mwingine maneno huweza kuleta matatizo maana katika kuzungumza kuna kujikwaa kwingi, kwani ulimi hauna mfupa.
Ili uweze kufanikiwa katika kueleza nia yako kwa mwanamke, lazima ujue jinsi ya kutumia lugha ya matendo yako. Na pengine hutatumia nguvu, maana watu husema penzi kikohozi – kama unalo litaonekana tu machoni pa mlengwa.
Ukitafakari kwa makini utabaini kuwa huhitaji kusema sana ndipo uweze kupendwa, kwani maneno huchangia asilimia kidogo tu. La muhimu ni kuhakikisha kuwa mlengwa wako anakusoma na kukuelewa vizuri kwa kuangalia matendo ya mwili wako.

4. ACHA ASILI ICHUKUE MKONDO WAKE

Katika nadharia mbalimbali za kijamii na kidini ni jambo la kawaida kusikia kuwa binadamu wote ni sawa. Hata hivyo, katika muktadha wa kimapenzi, kila mtu mmoja mmoja anafahamu kabisa kuwa si kila mwanamume/mwanamke ni sawa na mwenzake.
Methali yenye asili ya kimagharibi husema “Uzuri wa mtu uko katika macho ya yule anayemtazama.” Hii ina maana pia kwamba, kila mtu anavyo vigezo vyake vya uzuri kwa kuzingatia maumbile yake. Pia jamii zinavyo vigezo vya uzuri, lakini hutangulia kwanza vigezo binafsi.
Unapokuwa umekaa na mwanamke ambaye anakuvutia kwa mwonekano wake, sauti yake na kadhalika, si rahisi sana kujizuia kuonesha kuwa anakuvutia. Hii ni kwa sababu si wewe, bali ni nafsi yako inayokusukuma. Na yeye mwenyewe atakusoma kwa kuangalia lugha ya matendo yako na kukwelewa, utakaobaki ni uamuzi wake tu.
Katika jamii kuna vigezo kuhusiana na kiuno, miguu, maziwa, makalio na kadhalika. Wengi wa wanajamii huvizingatia na kuongeza vyao. Huu ni ukweli wa kibiolojia ambao hauwezi kupingika. Mwanamke mwenye vigezo vinavyokubalika zaidi katika jamii yake atawavutia wanaume wengi zaidi. Hapa mwanamume hahitaji kutumia nguvu nyingi – asili ya maumbile itamsaidia humtambulisha mwanamke kuwa amempenda.

5. TUMIA CHANGAMOTO YA WALAKINI

Mara nyingi changamoto kubwa katika suala zima la mtu kubainisha nia yake kwa mwanamke hutokana na ukweli kwamba katika mchakato mzima huwa kuna wasiwasi na walakini. Kwa hakika, jambo hili ni la “pengine” au “labda” kutokana na kutoweza kufahamu kirahisi mwenzako anawaza nini.
Unapoonesha nia yako ya kumpenda mwanamke, ni kama unaamsha hisia zake kwako na ni kama vile unamuuliza: “Ungependa kuwa nami?” Kwa njia hii ni kama utakuwa unafungua mlango wa kupata jibu la “ndiyo” au “hapana” kwani huyo unayemwonesha kuwa unampenda na yeye ana matakwa yake na mapendeleo yake.
Kimsingi hakuna kanuni wala sheria rasmi unazopaswa kuzingatia wakati wote. La muhimu ni wewe mwenyewe kujiachia na kuingia katika maji usiyofahamu kina wala mwisho wake, bali wewe nenda na mkondo wake huku ukitarajia kuwa lolote linaweza kutokea. Hiyo ndiyo sehemu ya raha yake.

6. DHIBITI HISIA, MIHEMKO

Tofauti na mwanamke, mwanamume anayejaribu kuonesha nia yake hatakiwi kujiweka katika mkao wa mwanamitindo. Wanawake ndio hufahamika zaidi kwa mikao yao “ya kula” wanapokuwa katika mawindo (japo wengi hubisha), lakini si mwanamume. Wanawake ndio hutarajiwa kujieleza zaidi kwa njia ya matendo na mikao, lakini wanaume hutarajiwa kudhibiti hisia na mihemko yao .
Tofauti katika lugha ya matendo baina ya watu wa jinsia mbili hutokana na maumbile ya kujenetiki pamoja na utamaduni wa jamii husika. Yote yakizingatiwa, matakwa ya mwanamke ndiyo hupewa kipaumbele zaidi. Kwa ufupi, matendo ya kutongoza ya mwanamke huwa wazi zaidi, lakini mwanamume hulazimika kuficha hisia na mihemko yake.

IFAHAMU SAYANSI HII

Wajibu wa kufikisha ujumbe kwa mtu wa jinsia tofauti ni wa kila mmoja – mwanamume na mwanamke. Hata hivyo, wanaume ndio wenye jukumu kubwa zaidi la kuanzisha, kwa kuzingatia utamaduni wa jamii nyingi. Unaweza ukaona ugumu, lakini ipo sayansi itakayokusaidia. Kama una wasiwasi na uwezo wako, ni vizuri kuyazingatia yote yaliyobainishwa hapa.

FURIOUS 8: PAUL WALKER'S BROTHERS SUGGEST BRIAN O'CONNER MAY CAMEO

The Fast and the Furious 8 may feature an appearance by Paul Walker's character, Brian O'Conner, if recent comments by the late actor's brothers, Cody and Caleb, are any indication.

In an interview with ET , Caleb said he spoke with Vin Diesel about bringing O'Conner back for a future film. "I had a phone call with Vin for about an hour and we really discussed this a while back," he said.

"He wanted [our] blessing," Caleb continued, noting that Diesel wanted to check with them to see if it "would be acceptable to maybe bring Paul's character back… to really kind of let his fans know he's still out there."

Cody chimed in, adding, "Universal wants to make sure to be respectful of Paul and his image too, and his family."

The Fast and the Furious 8 is being directed by Straight Outta Compton's F. Gary Gray
and will open in theaters April 2017.

LE CHAPECOENSE CHANGE DE LOGO

Touché de plein fouet par un crash aérien qui a coûté la vie à 19 de ses 22 joueurs, le club de Chapecoense a décidé de changer son logo.
Après le terrible accident d'avion intervenu en Colombie le 28 novembre dernier qui a décimé l'équipe brésilienne de Chapecoense, le club a décidé de changer son logo.
Qualifiée pour la finale de la Copa Sudamericana, l'équipe devait affronter l'Atletico Nacional. La CONMEBOL a décidé d'attribuer le trophée aux Brésiliens. Les trois étoiles jaunes au-dessus de l’emblème ont laissé place à une étoile argentée représentant ce titre posthume.
"Symbole de la paix, pour nos éternels champions et la lumière qui nous guidera à partir de maintenant" , a confié le Chapecoense sur son twitter.

Nosso escudo ganhou novas estrelas. #VamosChape
19:00 - 8 Déc 2016
-------------------------------

 

LUKAKU : "JE N'AVAIS JAMAIS VU POGBA AUSSI HEUREUX QUE QUAND IL A SIGNÉ À MANCHESTER UNITED"

Romelu Lukaku, ami de Paul Pogba, a confié qu'il n'avait jamais vu le Français aussi heureux que lors de sa signature pour Manchester United.
Cet été, Paul Pogba a fait un choix crucial pour sa carrière. Après quatre saisons pleines et réussites à la Juventus, l'international français est revenu au bercail du côté de Manchester United. Le milieu de terrain a signé chez les Red Devils seulement quelques semaines après la défaite de la France en finale de l'Euro 2016. Dans la presse belge, Romelu Lukaku, ami de Paul Pogba, a affirmé ne jamais avoir vu le Français aussi heureux qu'au moment de son retour en Angleterre.

"J’étais là, à l’hôtel, quand Paul Pogba a signé pour Manchester United. Il y avait peut-être dix personnes autour de lui avec des serviettes et des contrats à l’intérieur. Je connais Paul depuis de nombreuses années mais je ne l’avais jamais vu afficher un tel visage, je ne l’avais jamais vu si heureux, une fois que tout a été signé, assure Lukaku. C’était un soulagement, un vrai bonheur pour lui" , a reconnu Romelu Lukaku .

"Durant les vacances, nous avons parlé une seule fois de foot. Autour de la piscine à Los Angeles, il me parlait de son rêve de revenir à Manchester United, poursuit l’international belge. J’ai compris ce que ça signifiait pour lui. Ce retour à Manchester United, ça n’a rien à voir avec l’argent" , a conclu l'attaquant d'Everton.

Nay wa Mitego: Biashara ya mimi na Mr T Touch ilishaisha

Nay wa Mitego anaweza akawa anamiss midundo ya producer wake wa zamani, Mr T Touch lakini hana mpango wa kufanya naye tena kazi.

Tangu waache kufanya kazi pamoja, rapper huyo amekuwa kimya kiasi na huenda akawa bado hajapata producer mwingine wa kuziba pengo lake. Akizungumza na mtangazaji wa Jembe FM, JJ, Nay amesema kuwa biashara yake na T Touch ilishakwisha.

“Katika suala ambazo huwa sipendi kuzungumzia ni suala la mimi na Mr T, tulishamalizina kama itakuja kutokea basi itakuja kutokea na kila kitu mtu ataona, nadhani hii biashara ya mimi na T ilishaisha,” alisema rapper huyo.

Kuhusu ukimya wake, Nay amesema ameamua kufanya hivyo makusudi ili kuwapa nafasi watu wengine. Amesema muda si mrefu atarejea tena akiwa na nguvu mpya baada ya kubaini kipi kinamiss kwenye muziki.

Vanessa Mdee adai wazo la wimbo ‘Cash Madame’ amelipata baada ya kuzinguliwa na promota

Msanii wa kike wa muziki, Vanessa Mdee amedai wazo la kuandika wimbo ‘Cash Madame’ alilipata baada ya kuzinguliwa malipo yake ya show ya promota.

Akiongea katika kipindi cha Mji Wa Burudani cha Choice FM wiki hii, Vanessa alisema “Promota alinizingua kwenye malipo hapo ndipo nilipopata wazo la kuandika wimbo wangu wa Cash Madame,”.

Pia muimbaji huyo amesema kwasasa ajipanga kufanya muziki mzuri zaidi huku akidai wakati wake wa kuwa na familia bado.

Katika hatua nyingine alisema ingawa amesomea sheria lakini kitu ambacho ameamua kukifanya katika maisha yake ni muziki.

“Ni kweli nimesomea sheria ila sijawahi kufanya kazi ya sheria na sio kwamba nilikuwa napenda sheria napenda muziki,” alisema Vanessa Mdee.

Cassper Nyovest apata shavu kutokea kwenye cover la Forbes Africa Life

Rapper wa Afrika Kusini, Cassper Nyovest amefanikiwa kutokea kwenye jarida la Forbes Africa Life.

Kupitia mtandao wa Twitter wa jarida hilo, wameandika, “@CassperNyovest started performing in front of a few people at school, 20 years later he’s filling up stadiums – @forbesafrica out NOW!.”

Naye Cassper ameonyesha furaha yake kwa kuandika kwenye mtandao wa Instagram, “Mama I made it!!! I made it on the Forbes Africa Life Cover!!!! All the glory to God!!! Black child , it’s possible!!! Go out there and do it for yourself!!! @forbesafrica out now!!!.”

Oktoba ya mwaka huu rapper huyo aliweka rekodi nyingine ya kuwa msanii wa kwanza wa Afrika kusini kuujaza mwenyewe uwanja wa mpira wa Orlando jijini Johannesburg kwenye show yake aliyoipa jina Fill Up Orlando Stadium.

Fifa kuanza kutumia Video michezoni

Mashindano ya FIFA ya Kombe la Dunia kwa Klabu yalianza hapo jana huko Japan na waamuzi wa Mechi hizo watapata msaada wa maamuzi yao kwa kutumia Video kutoka kwenye Mfumo wa Majaribio uitwao VARs, Video Assistant Referees.

Mfumo wa Video kusaidia maamuzi ya waamuzi wawapo Uwanjani umefanyiwa Majaribio rasmi ya FIFA kwa mara ya kwanza katika Mechi ya Kimataifa mwezi Septemba wakati Italy ilipocheza na Ufaransa huko Bari.

Kwenye Mfumo huo wa Video, mwamuzi Msaidizi anakuwepo pembeni mwa Uwanja na anakuwa na Mawasiliano na Refa wa Mechi wakati wote wa Mechi hiyo akipitia Video bila kusitisha Mechi.

VARs imekuwa ikitumika kwa Majaribio huko Marekani kwenye Ligi Daraja la 3 na sasa FIFA, ikishirikiana na IFAB, ambacho ndicho chombo pekee kinachoweza kubadili Sheria za Soka, vimeafika Majaribio hayo na sasa yameingia hatua mpya .

Mashindano hayo yanaanza Leo huko Yokohama kwa Wenyeji Kashima Antlers kucheza na Auckland City ya New Zealand.

mardi 6 décembre 2016

Ronaldinho a Chapecoense

#LEGENDE - Ronaldinho rejoint Chapecoense! Après avoir perdu 16 de leurs joueurs, les brésiliens accueillent la star brésilienne.

Sababu za kuanguka kwa ndege ya Brazil zatajwa

Ndege iliyokuwa imewabeba wachezaji wa timu ya mpira kutoka nchini Brazil ambayo ilipata ajali nchini Colombia inasemekana kwa muujibu wa taarifa zilizovuja ndege hiyo iliishiwa mafuta kutoka katika kifaa cha kurekodia mawasiliano.

Katika mnara wa mawasiliano ya ndege , rubani alisikika akirudia mara kadhaa akiomba ruhusa ya kutua kwa dharura kutokana na hitilafu ya umeme iliyokuwamo ndegeni pamoja na kuishiwa mafuta ya ndege.

Kabla hata mawasiliano hayo yaliyorekodiwa kufikia mwisho ,rubani alisikika akisema yuko angani umbali wa futi elfu tisa sawa na mita elfu mbili mia saba na arobaini na tatu.Taarifa za mawasiliano hayo zimekuwa gumzo katika mitandao kadhaa nchini Colombia na hata katika vyombo vya habari nchini humo, na hivyo kumekuwepo fununu za taarifa hizo kuwa huenda zikawa na chembe ya ukweli kwamba kuishiwa kwa mafuta ndiyo chanzo zha ajali ya ndege hiyo.

Wanajeshi wa Colombia waliliambia shirika la habari la AFP, kwamba pamoja na ndege hiyo kuanguka kuna shaka juu ya ajali hiyo kwani pamoja na ndege hiyo kuanguka hakukuwa na mlipuko wowote na kwamba huenda kulitumika nguvu ingine tofauti na nadharia ya kwisha kwa mafuta ndegeni.

Wadadisi wa mambo na wachunguzi bado hawako tayari kufungua mdomo na kuzungumzia juu ya chanzo chochote cha ajali hiyo na kwamba taarifa kamili ya uchunguzi itatolewa baada ya miezi kadhaa.

Wachezaji wa timu ya Chapecoense walikuwa safarini kuelekea nchini Colombian kwenye mji wa Medellin mahali kulikotarajiwa mechi kubwa ya mpira wa miguu ya kihistoria na badala yake wachezaji hao wameacha historia .Kufuatia vifo vya wachezaji wa timu hiyo, ulimwengu mzima umeungana kuomboleza vifo vyao.

Kwa muujibu wa taarifa zilizopatikana kutoka katika shirika la ndege la Lamia watu wanne waliokuwa wasafiri na ndege hiyo wameponea chupuchupu kuwa miongoni mwa waliokufa baada ya kukosa tiketi.

Mmoja wa manusura wa ajali hiyo ambaye ni fundi wa ndege Erwin Tumiri, ameeleza namna alivyokwepa kifo, kwamba yeye alifuata maelekezo yote ya namna ya kujiokoa ,anasema abiria wenzie , walio wengi walisimama na kuanza kupiga kelele nay eye aliamua kuweka sanduku lake la kusafiria kati kati ya miguu yake na kuamua kubaki hivyo.

Visanduku viwili vya mawasiliano vya ndege hiyo vyote vilipatikana na tayari vimeanza kufanyiwa uchunguzi na wataalamu wa masuala ya anga.

Wachunguzi wataalamu kutoka nchini Uingereza wanasaidiana na mamlaka za Amerika Kusini kwasababu ndege iliyopata ajali ilitengenezwa na wana anga wa Uingereza BAE nchini Uingereza.

Brazil imeanza siku tatu za maombolezo wakati maelfu ya watu na washabiki wa timu ya Chapecoense wako katika mji yaliko makao makuu ya timu hiyo Chapeco wanaendelea mkesha wa maombolezo wakati maandalizi ya kuchukua mabaki ya wachezaji hao inafanywa na jeshi kurejeshwa Brazil ili kuzikwa kwa pamoja katika uwanja wa Chapeco.
Nchi ya Bolivia tayari imekwisha tuma ndege ya kuchukua mabaki ya raia wake waliokufa katika ajali hiyo nchini Colombia.

Timu hiyo iliandika historia ya mafanikio katika soka kwa kuwa kileleni mwa ligi ya Brazil kwamara ya kwanza mwaka 2014.Kati ya watu 77 waliokuwa wameabiri ndege hiyo miongoni mwao ni watu sita tu ndiyo walionusurika .Abiria walio wengi walikuwa ni wachezaji wa timu ya Chapecoense na waandishi habari wapatao ishirini walikuwa miongoni mwa walipoteza maisha .