Alibaba

lundi 26 décembre 2016

Roboti inayoweza kushiriki ngono kutengezwa

Je ungependelea kushiriki ngono na roboti? ungefunga ndoa na roboti? na Je roboti anaweza kuwa na haki ya kupinga ndoa hiyo?
Haya ni baadhi ya maswala machache yanayoulizwa katika mkutano wa pili wa kuwa na mpenzi wa roboti mbali na kushiriki naye ngono katika chuo kikuu cha Goldsmith mjini London baada ya serikali ya Malaysia ambayo ndio iliokuwa taifa la maandalizi ya mkutano huo kuupiga marufuku.

Hatua hiyo imezua utata sio tu kwa mataifa yenye maoni ya Kihafidhina .
Hakukuwepo na wawakilishi kutoka kwa sekta ya ngono wala roboti za ngono katika mkutano huo.
Kampuni ya Real Dolls inayotengeza wanaserere wa ngono ilidai kwamba itatengeza roboti wa ngono aliye na akili bandia mwaka ujao.
Uzinduzi huo iwapo utafanyika utakuwa ushahidi wa David Levy ambaye amekuwa akitabiri ujio wa roboti zinazofanana na binadamu zenye akili bandia.
Alitoa hotuba ya kufunga mkutano huo ambapo alipendekeza utengezaji wa roboti za ngono.

''Tuna roboti za urafiki na sasa roboti ambaye anaweza kuwa mpenzi ndio mtindo mpya''.
Katika kipindi cha miaka 10 ijayo, inawezakana kutengeza roboti ambayo watu wataihitaji kama mpenzi, ina upendo, inaaminika, inaheshima na hailalamiki alisema.
Wengi watapendelea uhusiano huo wa roboti na huenda wakataka kufunga ndoa nao.

Mpango huo wa mpenzi wa aina ya roboti huenda akazua maswali kadhaa ya kimaadili, hususana wakati ambapo sheria italazimika kutambua roboti kama binaadamu.

ZARI Afunguka :Hakuna Kitu Ninachokipenda Katika Maisha yangu Kama Kuzaa....

Wakati mabinti wengine wakijikita katika matumizi ya mikorogo na kukimbilia wanaume wenye pesa hali ni tofauti kwa mwanamama zari hassan (the boss lady ) ambaye amekiri wazi kuwa kitu anachopenda zaidi katika maisha yake ni kuzaa.

Zari ambaye ni mpenzi wa mwanamziki nyota Africa diamond platnumz amesema hayo ikiwa ni siku chache tangu apate mtoto wa kiume aliyezaa na diamond ambaye watu walimbeza kuwa anazaa bila mpangilio eti kiza tu alibeba ujauzito kabla ya mtoto wao wa kwanza tiffah hajatimiza mwaka mmoja.
Licha ya zari kuwa na watoto watano kwa sasa ameweka wazi kuwa kwa sasa yeye na diamond wana mpango wa kuzaa mtoto mwingine wa tatu na baada ya hapo hatozaa tena na badala yake watajikita zaidi katika kuwalea watoto wao.

Firmino akamatwa kwa kuendesha gari akiwa mlevi

Mchezaji wa Liverpool Roberto Firmino ameshtakiwa kwa kosa la kuendesha gari akiwa mlevi baada ya kukamatwa mkesha wa siku ya Krismasi.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 25 alikamatwa baada ya gari lake kusimamishwa katikati mwa Liverpool mapema siku ya Jumamosi ,polisi wamesema.


Mchezaji huyo wa Brazil anatarajiwa kufikishwa mbele ya hakimu wa Liverpool mnamo Januari 31.
Firmino atawasilishwa mahakamani siku ambayo timu yake itakabiliana na Chelsea katika uwanja wa Anfield.
Liverpool ilimsajili mchambuliaji huyo kutoka Hoffenheim kwa kandarasi ya miaka mitano iliogharimu kitita cha pauni milioni 29 mwezi Juni.

Alicheza katika ushindi wa wiki iliopita dhidi ya Everton katika uwanja wa Goodison Park.
Liverpool imesema kuwa haitazungumzia swala hilo hadi pale hatua hiyo ya kisheria itakapokamilika.