Alibaba

samedi 28 janvier 2017

Video ya ‘Hela’ ya Madee yatoweka YouTube

Nini kimeikuta video ya wimbo wa ‘Hela’ ya Madee?
Video hiyo ambayo imetoka wiki iliyopita kwenye mtandao wa YouTube na kuanza kufanya vizuri kwenye vyombo mbalimbali vya habari kwa sasa imeonekana kufutika katika mtandao huo kwa mujibu wa meneja wa Tip Top Connection, Babu Tale.


Kupitia katika mtandao wa Instagra, Tale ameandika ujumbe kwa mashabiki unaosomeka, “Hii hatari sijui nini kimetokea mzigo umefutika kabisaa YouTube ila tuna pambana kuurudisha wadau mtuwie radhi tuta wapa taarifa kitakachojiri. @madeeali.”

Video hiyo ilifanikiwa hadi kushika namba moja ya video zilizo trend katika mtandao wa YouTube.

mardi 24 janvier 2017

Huyu ndie mwamuzi atakae chezesha mechi ya Liverpool dhidi ya Chelsea

Mwamuzi Mark Clattenburg ameteuliwa kuchezesha mechi ya Chelsea dhidi ya Liverpool katika uwanja wa Anfield wiki ijayo.
Chelsea watasafiri hadi Anfield wiki ijayo siku ya Jumanne (Januari 31) wakiwa na pointi 10 dhidi ya timu ya Jurgen Klopp.

Clattenburg ana historia kadhaa anapo chezesha mechi za Chelsea, mechi ya mwisho msimu uliopita katika uwanja wa Stamford Bridge dhidi ya Tottenham Hotspur ikizua utata.

Kadi kumi na mbili za njano zilitolewa katika pambano hilo, na vitendo vya vurugu baina ya wachezaji katika sare ya 2-2.
Chelsea na Tottenham zilitozwa faini ya paundi 375,000 na 225,000 mwenyeji kuhusika katika kile kilichotokea, lakini Clattenburg hakuweza kutoa kadi nyekundu katika mechi hiyo.

Hii itakuwa mara ya pili kwa mwamuzi huyo kutoka County Durham kuchezesha mechi ya Chelsea msimu huu, baada ya kuchezesha Blues wakishinda 3-0 dhidi ya Burnley mwezi Agosti.

Mimi siwezi kuoa kwa sababu fulani kaoa – Chege

Msanii mkongwe wa muziki Chege Chigunda amedai hawezi kufuata mkumbo kuoa kwa sababu fulani kaoa.
Muimbaji huyo ambaye hivi karibuni ameachia wimbo mpya “Kelele za Chura” akiwa amemshirikisha Nandy, amedai suala la kuana linakuja kutoka kwa Mungu na sio kuigana.


“Mimi siwezi kuoa sijui kwa sababu nikienda kwenye interview nitaulizwa, mbona wewe haujaoa, mbona mwenzako kaoa, na siwezi kuoa kwa sababu Mh Temba kaoa,” Chege aliiambia Global TV. “Mimi nitaoa pindi tu mwenyezi Mungu atakaposema Chege oa lakini sio kwa sababu fulani kafanya hivyo,”
Muimbaji huyo ni msanii pekee wa Kundi la TMK Wanaume Halisi ambaye bado anafanya vizuri katika muziki.

Nimeanza kuupenda muonekano wangu, sitaki tena kuuharibu kwa sumu – Ray C

Msanii mkongwe wa muziki Ray C amedai ameupenda muonekano wake mpya huku akijipa mtihani wa kujizua kurudi katika mambo ambayo yalimpelekea kuupoteza muonekano wake mzuri wa mwili.

Ray C ndani ya muonekano mpya
Muimbaji huyo hivi karibuni amekuwa akipost picha zake mpya ambazo zinamuonyesha akiwa na muonekano mzuri hali ambayo imewafanya mashabiki wake katika mitandao ya kijamii kuona kweli mrembo huyo ana nia ya kubalika na kutoka katika matumizi ya Madawa ya kulevya.
Jumanne hii muimbaji huyo amepost picha yake katika mtandao na kuandika: Nimeanza kumpenda Huyu dada Ray C sitaki kumdhuru tena kwa sumu wala bunduki nataka Azidi kunivutia kila nimuonapo kiooni.

Kwa sasa muimbaji huyo anarekodi nyimbo zake katika studio ya Wanene Entertainment kufanya maandalizi ya ujio wake mpya

jeudi 19 janvier 2017

Rais Bush na mkewe walazwa hospitalini


Rais mstaafu wa Marekani George HW Bush aliyekuwa amelazwa hospitalini huko mjini Texas tangu Jumamosi, amepelekwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.
Baada ya kutibiwa ugonjwa wa homa ya mapafu, Bush mwenye umri wa miaka 92 sasa anaendelea vizuri.
Mke wake Barbara, amelazwa katiaka hospitali hiyo hiyo kama tahadhari kwa sababu ya uchovu.

Kiungo wa zamani wa Misri Aboutrika atajwa kwenye listi ya magaidi wa nchini hiyo

Mamlaka za usalama za Egypt zimemweka mchezaji wa zamani wa soka wa timu ya taifa ya nchi hiyo, Mohamed Aboutrika katika ya magaidi baada ya kuhusishwa na kikundi cha waislam wa Brotherhood, amesema mwanasheria wa mchezaji huyo.


Mr Aboutrika anashutumiwa kuwasaidia kifedha kikundi cha Brotherhood, kikundi ambacho mamlaka za Misri kimewaeka kwenye kundi la magaidi.
Mnamo mwaka 2012, alimpigia kampeni ya urais Mohamed Morsi, ambaye ni mwanachama wa Brotherhood.
Jambo hilo lilipelekea kuwagawa mashabiki wa mchezaji bora wa mwaka wa BBC wa mwaka 2008.
Kwa sheria za Misri, mtu yoyote anayewekwa kwenye listi ya ugaidi, hufungiwa kusafiri na passport yake pamoja na mali zake hushikiliwa.
Mwanasheria wa Aboutrika, Mohamed Osman, alisema mteja wake hajatiwa hatiani wala hajapewa taarifa rasmi juu ya mashtaka wanayomtuhumi nayo. Pia ameahidi kukata rufaa juu ya tuhuma hizo kwa mteja wake.
Kiungo huyo wa zamani wa Al-Ahly na timu ya taifa ya Misri, alikuwa kipenzi cha wananchi wa Misri na walifikia hatua ya kumpa majina ya The Prince of Hearts, The Magician na The Saint wakati akicheza soka, lakini uamuzi wake wa kumsapoti Mohammed Morsi, ambaye alikaa madarakani kwa mwaka mmoja tu, uliwagawa mashabiki zake.
Mwaka 2015, mali zake nyingi ziliwekwa kizuiani, hisa zake kwenye makampuni tofauti zilishikiliwa na mamlaka za usalama za nchi hiyo.

FIFA kufanya mapinduzi ya soka, waweka wazi mpango wa kufuta offside na kubadili upigaji wa penati

Raisi mpya wa FIFA Gianni Infantino anaonekana kutaka kubadili soka kabisa.Infantino anaonekana kuondoa kila kitu cha Sepp Blatter na kuleta vyake.Baada ya kuongeza timu zitakazoshiriki kombe la dunia 2026 kufikia timu 48 sasa Infantino amekuja na mpya.Kwa kumtumia mkurugenzi wa mambo ya ufundi wa FIFA Marco Van Basten amependekeza baadhi ya sheria mpya katika soka.


Akihojiwa na gazeti la Ujerumani liitwalo Bild,Van Basten amesema wanawaza kuondoa mchezo wa kuzidi katika soka.
“sipati picha soka isipokuwa na ofside,washambuliaji watapata nafasi nyingi sana za kufunga”.Van Basten alisema mpira wa miguu utakuwa wakuvutia sana kama offside itaondolewa na anaamini jambo hilo litawafurahisha mashabiko na washambuliaji.
Kubadili upigaji wa penati.Van Basten pia anaona kuna haja kubwa kwa FIFA kubadili aina ya upigaji wa penati.Kwa sasa adhabu ya penati mchezaji anauweka mpira mita kadhaa karibu na goli ma kuupiga.Lakini Van Basten anaona penati ibadilishwe.Anataka mpiga penati auweke mpira mita 25 kabla ya goli na kama anaweza atembee nao kuelekea golini kwa muda usiozidi sekunde nane.Aina hii ya upigaji penati sio ngeni kwani mwaka 1999 ilishafanyiwa majaribio nchini Marekani.
Kupunguza adhabu mipira ya kushika.Van Basten anaona kama adhabu ya kadi nyekundu ni kali mno kwa tukio hilo.Na analiona kama tukio dogo lisilohitaji kadi nyekundu na anazani inapaswa ipunguzwe adhabu hiyo.Kusitolewe kadi nyekundu mpira ukishikwa.Adhabu kam ile ya tukio la Luis Suarez mwaka 2010 wakicheza dhidi ya Ghana aliposhika mpira wakati ukiingia golini Van Basten anataka kadi iwe ya njano.
Kapteni awe mtu pekee kuongea na mwamuzi.Kama katika Rugby ni kapteni tu anayeongea na mwamuzi,asiruhusiwe mtu yeyote,mchezaji yeyote kuongea na mwamuzi.
Style ya faulu ya mchezo wa kikapu.Katika mchezo wa kikapu pale mchezaji anapocheza faulu tano anatakiwa atoke uwanjani.Na sasa Van Basten anaamini staili hiyo inapaswa kuletwa katika soka.
Kupunguza idadi ya mechi.Hii itafurahiwa sana na makocha wageni Uingereza.Alianza Van Gaal akaja Jurgen Klopp walilalamikia idadi ya mechi kuwa nyingi Epl.Van Basten anataka idadi ya mechi zipunguzwe kutoka mechi 80 kwa msimu hadi 50 kwa msimu.
Kuongeza idadi ya Substitution.Van Basten anatamani kuongeza idadi ya wachezaji wa sub kuanzia 5-7,kwa muda mrefu wadau wa soka wamekuwa wakizungumzia kuhusu suala la kuongeza wachezaji wa akiba na sasa FIFA inatarajia kuliangalia suala hili.
Kuzifanya dakika 10 za mwisho kutumika ipasavyo.”Tunajua kutokana na kuongeza idadi ya wachezaji wa akiba pamoja na aina ya upigaji penati vitachukua mda mrefu uwanjani na itatubidi kuhakikisha dakika 10 za mwisho zinatumika kiuhakika” Van Basten alisema watahakikisha hakuna upotezaji muda katika dakika zamwisho za mchezo.
Hayo ni mapendekezo tu kutoka kwa mkurugenzi wa ufundi wa FIFA, na sasa atawasilisha mapendekezo hayo katika kamati ya FIFA yaweze kujadiliwa.

Shukran by The Light of Peace (Nuuru Salaam)

Twamtukuza Rabaana


New Kaswida Colaboration of Group
 The Light of Peace (Nuuru Salaam), Madrasatul Firdaus & Wana Karori

samedi 14 janvier 2017

Harusi za kifahari zapigwa marufuku Somalia


Mji mmoja nchini Somalia umepiga marufuku harusi za gharama ya juu ili kuwashinikiza vijana zaidi kuoa.

Kamishna wa wilaya Mohamud Hayd Osman wa Bula Hawa karibu na mpaka wa Kenya waliambia BBC kwamba ni mbuzi wasiozidi watatu ndio wanaofaa kuchinjwa pekee ili kuwalisha wageni na kwamba sherehe katika hoteli hazitaruhusiwa.
Amesema kuwa mahari itakuwa chini ya dola 150 pekee.
Uamuzi huo unajiri baada ya maafisa kubaini kwamba takriban watoto 150 walizaliwa nje ya ndoa hivi karibuni.

Kamishna huyo ameongezea kwamba gharama ya harusi, ukosefu wa ajira na kiangazi ndio maswala yanayowafanya watu kulihama eneo hilo.
Waandishi wanasema sio kawaida kwa familia ya bwana harusi kutumia takriban dola 5000 katika harusi nchini Somalia.

"Mafunzo ya kiislamu yanasema kuwa ndoa inafaa kuwa ya gharama ya chini, alisema Osman.
Hatua ya kupunguza matumizi kuhusu sherehe za kifahari pamoja na matumizi mengine baada ya ya maafisa kugundua kwamba ni kwa nini watoto 150 walizaliwa nje ya ndoa mjini humo.
Wasichana walikuwa wanakataa kuolewa hadi pale kitita cha pesa kitakapotumika kwa dhahabu pamoja na fanicha, alisema.

AFCON: Matukio sita makuu historia ya Kombe la Mataifa Afrika

Michuano ya Kombe la Mataifa Afrika, makala ya 31, itang'oa nanga Jumamosi 14 Januari pale wenyeji watakapokabiliana na Guinea-Bissau ambao wanashiriki fainali hizo kwa mara ya kwanza.
Kwa baadhi ya mashabiki, hii ni michuano tu ya kawaida ya soka.

Lakini AFCON kwa sasa ni michuano yenye ushindani mkali na yenye wachezaji nyota kama vile Riyad Mahrez, Sadio Mane na Pierre-Emerick Aubameyang.

Michuano hii inapong'oa nanga, tunaangalia matukio muhimu ya furaha na ya kusikitisha pia ambayo hayasahauliki katika historia ya AFCON.

1994: Zambia yajikwamua baada ya mauti

 Mnamo 27 Aprili 1993, timu ya taifa ya Zambia ilikuwa safarini mechi ya kufuzu Kombe la Dunia nchini Senegal ndege iliyowabeba ilipoanguka na kutumbukia baharini mita 500 kutoka mji wa Libreville, Gabon.
Abiria wote 25 waliangamia pamoja na wahudumu watano.
Mwaka mmoja baadaye, Zambia ilijijenga na kufana sana michuano ya Kombe la Mataifa Bingwa Afrika 1994. Walifika fainali ingawa walishindwa na Nigeria 2-1.

2012: Herve Renard asaidia Zambia kutwaa kombe


Herve Renard and Zambia win the Africa Cup of Nations in 2012Getty Images
Zambia walikosa ushindi fainali 1994 lakini walifanikiwa 2012 chini ya kocha wao Mfaransa Herve Renard ambapo walikabiliana na Ivory Coast fainali.
Kwenye mechi hiyo, kulipigwa mikwaju 18 ya penalti, na Zambia wakashinda 8-7.

2015: Morocco yajiondoa kwa sababu ya Ebola

 

 

Kutokana na kuenea kwa ugonjwa wa Ebola Afrika Magharibi, wenyeji waliopangiwa kuandaa michuano ya 2015 Morocco walijiondoa wakihofia michuano hiyo ingefikisha ugonjwa huo nchini mwao.

CAF ilikataa ombi la kujiondoa, na baada ya Morocco kusisitiza timu yake ikafurushwa kutoka kwa michuano hiyo.
Mataifa matano yalikataa kuwa mwenyeji kabla ya Equatorial Guinea kukubali. Ivory Coast waliibuka washindi kwa kulaza Ghana 9-8 kupitia mikwaju ya penalti.

2010: Basi la Togo lashambuliwa

Basi la timu ya Togo lilishambuliwa na watu wenye silaha timu hiyo ilipokuwa ikirejea kambini Angola.
Kundi moja la waasi kutoka eneo la Cabinda lilikiri kuhusika

Watu watatu waliuawa na wengine tisa kujeruhiwa. Nyota wa zamani wa Arsenal na Manchester City Emmanuel Adebayor ni miongoni mwa waliokuwa kwenye basi hilo.
Togo ilijiondoa kutoka kwa michuano hiyo.

2006 & 2012: Drogba ashindia amani Ivory Coast

Mshambuliaji wa Ivory Coast Didier Drogba alikuwa stadi sana uwanjani kwa taifa na Chelsea na pia alitumia hadhi yake kufanikisha amani nchini mwake.
Wakati wa vita kati ya 2002 na 2007, alipiga magoti moja kwa moja kwenye runinga akiwa na wachezaji wenzake 20045 kuwahimiza waliokuwa wanapigana kuweka chini silaha.

Kipindi cha amani kilifuata. Mwaka 2008, alisisitiza mechi ya kufuzu Kombe la Taifa Bingwa Afrika dhidi ya Madagascar ichezewe ngome ya zamani ya waasi Bouake kama wito kwa raia kuungana.
Mwaka 2006 na 2012, Drogba alisaidia taifa lake kufika fainali za Kombe la Mataifa Bingwa Afrika lakini wakashindwa kwa mikwaju ya penalti.
Hata hivyo, hakufanikiwa kushinda.

2002 & 2004: Jezi za Cameroon

Cameroon walishinda michuano ya Kombe la Mataifa Bingwa Afrika 2002 kwa kulaza Senegal kupitia mikwaju ya penalti kwenye fainali.

Lakini kinachokumbukwa sana ni jezi za Simba Wasioshindwa ambazo zilikuwa hazina mikono.
Fifa hata hivyo waliwazuia kuzivalia wakati wa Kombe la Dunia 2002.
Mwaka 2004 walikuwa na jipya tena. Walivalia jezi moja iliyoshikana - fulana na kaptura nchini Tunisia.
Fifa hawakufurahia, na ikizingatiwa kwamba walikiuka ahadi ya awali ya kuzitumia kucheza mechi za makundi pekee,
Fifa waliwapiga faini kwa kucheza mechi ya robofainali ambayo walishindwa na Nigeria.

El Salvador yafurahia kumaliza siku bila mauaji

Polisi nchini El Salvador wanasema taifa hilo la Amerika ya Kati limemaliza siku moja bila mauaji yoyote kuripotiwa, jambo ambalo ni nadra sana katika taifa hilo.
El Salvador, taifa ambalo limeathiriwa sana na mapigano ya magenge ya wahalifu, ina mojawapo ya viwango vya juu zaidi vya mauaji duniani kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.
Watu 10 walikuwa wameuawa, mmoja kila siku mwaka huu nchini humo hadi kulipotokea Jumatano yenye utulivu wiki hii.
Mengi ya mauaji hutekelezwa na magenge ya uhalifu, ambayo hufahamika sana kama maras, ambayo huendesha shughuli zake maeneo mengi ya Amerika ya Kati.


Polisi hawajatoa maelezo yoyote kuhusu nini labda kilisababisha kutotokea kwa mauaji siku hiyo ya Jumatano.
Lakini serikali imekanusha madai kwamba imeamua kuanza kufanya mazungumzo ya kusitisha vurugu na magenge hayo.

Magenge hayo ya uhalifu mwanzoni yaliundwa kwenye barabara za mji wa Los Angeles miaka ya 1980 na watoto wa wahamiaji kutoka El Salvado waliokuwa wametoroka vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Vita vilipomalizika mwaka 1992, wengi wao walirejea nyumbani na utamaduni huo wa uhalifu.

mardi 10 janvier 2017

Droo ya Kombe la FA

Mabingwa watetezi wa Kombe la FA, Manchester United watapambana na washindi wa mwaka 2013 katika raundi ya nne ya kombe hilo.
Mabingwa wa England Leicester City watakumbana na Derby County, huku Chelsea wakicheza na Brentford.
Raundi ya nne inashirikisha timu 32, na mechi hizi zitachezwa Januari 27-30.

Droo kamili ni kama ifuatavyo:

Tottenham Hotspur v Wycombe Wanderers
Derby County v Leicester City
Oxford United v Newcastle United au Birmingham City
AFC Wimbledon au Sutton United v Cambridge United au Leeds United
Plymouth Argyle or Liverpool v Wolverhampton Wanderers
Southampton au Norwich City v Arsenal
Lincoln au Ipswich v Brighton
Chelsea v Brentford
Manchester United v Wigan Athletic
Millwall v Watford
Rochdale v Huddersfield Town
Burnley or Sunderland v Fleetwood Town au Bristol City
Blackburn Rovers v Barnsley au Blackpool
Fulham v Hull City
Middlesbrough v Accrington Stanley
Crystal Palace au Bolton v Manchester City.

Usiya na Elimika

Dada mmoja akiwa ofisini alipigiwa simu kuwa mwanae amepata ajali wakati anatoka shule, alikuwa ameumia sana. Kwa harakaharaka yule dada aliwasha gari na kuanza safari kuelekea hospitali ili kumuona mwanae.

Akiwa njiani katika mistari ya Zebra huku akiwa na mawazo alitaka kumgonga Kaka mmoja ambaye alikuwa akivuka barabara kwa kukimbia. Katika kumkwepa gari iligonga ukingo wa barabara na kukwaruizika kidogo.

Kwa hasira yule dada alishuka na kuanza kumtukana yule kijana kuwa kamsababishia ajali na kumchelewesha. Alimtukana sana, hali iliyowafanya watu kujaa. Watu walipofika walianza kuuliza nini ndipo yule dada kwa uoga alidanganya kuwa yule kaka alitaka kumuibia.

Watu walianza kumpiga Kaka wa watu kama mwizi, kuona vile yule dada aliingia kwenye gari na kuelekea hospitalini kumuona mwanae. Huku nyuma Polisi walikuja na kumuokoa yule kijana lakini akiwa ameumizwa sana.

Alifika hospitalini na kumkuta binti yake akiwa katika hali mbaya, alikuwa akitakiwa kufanyiwa upasuaji wa haraka ili kuokoa maisha yake, manesi walishamuandaa mtoto na alikuwa akisubiriwa Daktari ambaye alipigiwa simu na alikuwa njiani.

Wakati wakimsubiri Daktari, Nesi alikuja na kuwamabia kuwa, wampeleke hospitali nyingine kwani Daktari waliyekuwa wakimsubiri asingeweza kumfanyia upasuaji mtoto wao kwani alikuwa amepigwa na wananchi wakati akija hospitalini wakimuita mwizi.

Dada na mumewe walichanganyikiwa, mtoto kutokana na hali yake mbaya alichukuliwa harakaharaka na gari la wagonjwa ili kuhamishwiwa hospitalini nyingine. Wakati wanatoka kuelekea kwenye gari kulikuwa na gari ya Polisi inaingia.

Kijana mmoja akiwa hoi alishushwa, yule Dada alimtambua ni yule kijana ambaye alimuitia mwizi kule barabarani. Kwa hasira yule Dada allimuambia Mume wake.
“Huyu Kaka namfahamu ni kibaka tu alitaka kuniibia, ndiyo amenichelewesha kufika huku hospitalini!”
Nesi ambaye alikuwa akimsaidia kumpandisha mtoto katika gari la wagonjwa alimkatisha na kusema.
“Hapana Dada huyu kaka si kibaka, ni Daktari ambaye alipaswa kumfanyia upasuaji mwanao. Amepigwa wakati akikimbia kuja hospitalini, mimi ndiyo nimempigia simu kuja…”

Dada wawatu nguvu zilimuishia ilibidi anyamaze, walifika hospitali nyingine, mtoto alikuwa katika hali mbaya. Aliandaliwa na kuingizwa katika chumba cha upasuaji lakini kabla hajafanyiwa chochote yule mtoto alifariki.

Baada ya uchunguzi ilionekana damu ilishaingia kwenye ubongo. Wangeweza kuokoa maisha yake kama angefanyiwa upasuaji katika hospitali ya mwanzo, kule kusafirishwa tena na kurushwa rushwa barabarani kulisababisha damu kuendelea kuvuja kwa kasi ndani.

Yule dada alizimia baada ya kupata habari zile, maneno yake yalisababisha kuondoa maisha ya mwanae.

FUNZO

Usimdharau mtu kutokana na hali yake kwani hujui ni kitu gani anaweza kukusaidia.

lundi 9 janvier 2017

RONALDO CROWNED FIFA'S BEST PLAYER IN THE WORLD

The Real Madrid superstar enjoyed a staggering 2016 and has now been awarded the title of the best player in the world, beating Lionel Messi and Antoine Griezmann
Cristiano Ronaldo has been crowned the world’s best player at FIFA’s annual awards gala in Zurich.

The Real Madrid superstar enjoyed a fantastic 2016, and has now beaten his perennial rival Lionel Messi and Atletico Madrid’s Antoine Griezmann to the prize.

"It's a great feeling, as I mentioned many times last year was a dream year, no doubt about that," the striker said at the ceremony shortly before receiving the prize.

"Real Madrid win the Champions League and the national team won the Euros for the first time in history. Unbelievable season. I'm so proud and happy.

"I have to say thank you to my team-mates of Real Madrid, and team-mates of Portugal and the coaches. It was an amazing year."
Ronaldo scored a total of 59 goals for both club and country throughout the 12 months, as his career reached new heights.

The Portugal international, despite suffering an injury in the final, guided his country to Euro 2016 glory, scoring three goals and cajoling his team-mates from the sidelines after being stretchered off.

Eder’s late goal ensured that Ronaldo lifted the trophy in France, with Griezmann – the player to outscore him in the tournament - on the losing side in the showpiece.


Ronaldo also scored the winning penalty in the Champions League final, as Real defeated Griezmann’s Atletico at San Siro in Milan, and was rewarded with a staggering new deal until 2021.
The 31-year-old’s incredible year – which also saw him named the world’s highest paid sports star – was capped in December, when he was awarded his fourth Ballon d’Or award.

While Messi, the man who has forever threatened to overshadow Ronaldo during an era of individual footballing dominance, scored a sensational 55 goals throughout 2016, he was topped by four goals by Ronaldo, though he did guide Barcelona to La Liga glory.

Ronaldo was recently linked with a mind-boggling move to China, with a £257 million bid mooted, but the former Manchester United star appears set to continue his battle for supremacy with Messi and Griezmann in La Liga.

RONALDO CROWNED FIFA'S BEST PLAYER IN THE WORLD

The Real Madrid superstar enjoyed a staggering 2016 and has now been awarded the title of the best player in the world, beating Lionel Messi and Antoine Griezmann
Cristiano Ronaldo has been crowned the world’s best player at FIFA’s annual awards gala in Zurich.

The Real Madrid superstar enjoyed a fantastic 2016, and has now beaten his perennial rival Lionel Messi and Atletico Madrid’s Antoine Griezmann to the prize.

"It's a great feeling, as I mentioned many times last year was a dream year, no doubt about that," the striker said at the ceremony shortly before receiving the prize.

"Real Madrid win the Champions League and the national team won the Euros for the first time in history. Unbelievable season. I'm so proud and happy.

"I have to say thank you to my team-mates of Real Madrid, and team-mates of Portugal and the coaches. It was an amazing year."
Ronaldo scored a total of 59 goals for both club and country throughout the 12 months, as his career reached new heights.

The Portugal international, despite suffering an injury in the final, guided his country to Euro 2016 glory, scoring three goals and cajoling his team-mates from the sidelines after being stretchered off.

Eder’s late goal ensured that Ronaldo lifted the trophy in France, with Griezmann – the player to outscore him in the tournament - on the losing side in the showpiece.

Ronaldo also scored the winning penalty in the Champions League final, as Real defeated Griezmann’s Atletico at San Siro in Milan, and was rewarded with a staggering new deal until 2021.
The 31-year-old’s incredible year – which also saw him named the world’s highest paid sports star – was capped in December, when he was awarded his fourth Ballon d’Or award.

While Messi, the man who has forever threatened to overshadow Ronaldo during an era of individual footballing dominance, scored a sensational 55 goals throughout 2016, he was topped by four goals by Ronaldo, though he did guide Barcelona to La Liga glory.

Ronaldo was recently linked with a mind-boggling move to China, with a £257 million bid mooted, but the former Manchester United star appears set to continue his battle for supremacy with Messi and Griezmann in La Liga.

FIFA Women's Player of 2016!

FIFA Football Awards
Carli Lloyd has been voted
#TheBest FIFA Women's Player of 2016!
Congrats, Carli!
U.S. Soccer

The Best FIFA Men's Player of 2016!

FIFA Football Awards
Cristiano Ronaldo has been voted
#TheBest FIFA Men's Player of 2016!
Congrats, Cristiano!

The FIFA Fair Play Award 2016

The FIFA Fair Play Award has been presented to Club Atlético Nacional Oficial , for their remarkable display of humility following the tragic events of December

Colombian side Atletico Nacional,
Associação Chapecoense de Futebol ’s planned opponents in the continental final, in a remarkable display of humility, sent a request to CONMEBOL to award Chapecoense the title, with the South American governing body duly obliging.

Coach of The year 2016

Claudio Ranieri has been voted
#TheBest FIFA Men's Coach of 2016!
Congrats, Claudio!

Here is the FIFA FIFPro World11 for 2016!

🏆FIFA FIFPro World 11🌟

As part The Best FIFA Football Awards, the FIFA FIFPro World 11 has been chosen.

🔰 Goalkeeper

Manuel Neuer (FC Bayern Munich)

🔰 Defenders

Dani Alves (Juventus)

Sergio Ramos (Real Madrid)

Gerard Pique (FC Barcelona)

Marcelo (Real Madrid)

🔰 Midfielders

Andres Iniesta (FC Barcelona)

Luka Modric (Real Madrid)

Toni Kroos (Real Madrid)

🔰 Forwards

Lionel Messi (FC Barcelona)

Luis Suarez (FC Barcelona)

Cristiano Ronaldo (Real Madrid)

Type 👍 to like t

Picha za utambulishaj wa ndege mpya ya Arsenal

Arsenal imetambulisha ndege mpya ambayo itakuwa inaitumia kusafiria kwenda kwenye mechi zake za ugenini za Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Ndege hiyo ni ya kifahari na ina kila kitu kinachohitajika ndani. Klabu hiyo iliionyesha ndege hiyo kwenye Instagram wiki iliyopita, aina ya Emirates Airbus A380 nje ikiwa imepambwa na picha za mastaa watano wa timu hiyo; Hector Bellerin, Olivier Giroud, Santi Cazorla, Alexis Sanchez na Mesut Ozil.

Ndani ya ndege hiyo, kila mchezaji ana kitanda chake huku wakiwa wamewekewa anasa kibao, zikiwemo chaneli za televisheni 2,500 na kila mchezaji ana TV yake.
Ndani kuna baa ya kisasa yenye vinywaji vya kila aina, vyoo na mabafu lakini pia mazingira mazuri ya kukaa.

The Gunners wataipanda ndege hiyo kwa mara ya kwanza watakaposafiri kuifuata Bayern Munich mwezi ujao. 
Angalia picha.

Goli la Mkhitaryan ndio bao bora la mwezi Desemba, mwaka jana

Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), mwanzoni mwa mwezi huu, lilitangaza bao la kiungo mshambulizi wa Manchester United, Henrikh Mkhitaryan ndiyo bao bora la mwezi Desemba, mwaka jana.
Bao hilo lililofungwa Jumatatu ya Desemba 26, 2016 mashabiki mbalimbali duniani walipiga kura na likaibuka na ushindi wa asilimia 39.9.
Bao la Alexis Sanchez wa Arsenal ambalo lililofungwa Desemba 3, wakati Arsenal ikiifunga West Ham kwa mabao 5-1 lilikamata nafasi ya pili.

HAYA NDIO MABAO YALIYOSHINDANISHWA:

Henrikh Mkhitaryan (Manchester United 3-0 Sunderland, Mon 26 Dec) – 39.9%
Alexis Sanchez (West Ham 1-5 Arsenal, Sat 3 Dec) – 29.6%
Jeff Hendrick (Burnley 1-0 Bournemouth, Sat 10 Dec) – 16.1%
Hal Robson Kanu (Southampton 1-2 West Brom, Sat 31 Dec) – 6.4%
Wilfried Zaha (Hull 1-2 Crystal Palace, Sat 10 Dec) – 2.9%
Steve Cook (Bournemouth 3-3 Liverpool, Sun 4 Dec) – 1.9%
Marc Muniesa (Stoke 2-0 Burnley, Sat 3 Dec) – 1.8%
Sofiane Boufal (Southampton 1-0 Middlesbrough, Sun 11 Dec) – 1.4%


MABAO YALIYOPIGIWA KURA MTANDAONI

Caster Semenya afunga pingu za maisha

Mshindi wa nishani ya dhahabu katika mashindano ya olimpiki raia wa Afrika Kusini Caster Semenya amefunga ndoa na mpenzi wake mwishoni mwa wiki.
Bingwa huyo wa mbio za akina dada za mita 800 ambaye amekuwa akikumbwa na mzozo kuhusi jinsia yake, alimuoa Violet Raseboya aliyevalia gauni nyeupe.

Semenya alitaja harusi kuwa siku muhimu kwao na kusambaza picha zake kwenye mitandao ya kijamii.