Alibaba

lundi 28 novembre 2016

UKIYAONA HAYA JUA MWANAMKE ANA UCHI WENYE KINA KIREFU SANA

Dalili ni chache sana. Kuna watu wanasema mara nyingi mwanamke mwembamba ana uchi
wenye kina kirefu sana kwa hiyo wanawake wengi wa sampuli hiyo wamebarikiwa.

Lakini
wanene wamenyimwa zawadi ya kina kirefu.Piawengine wanadai kuwa ukiangalia mwanya
uliopo kati ya dole gumba la mguuni na kidole kinachofuatia,
utagundua kitu. Mwanamke
mwenye mwanya mkubwa ana uchi mpana na mwenye kina sana na mwenye mdogo ana uchi mdogo.
Tatu ni urefu wa kiganja pamoja na vidole vya mwanamke akivinyoosha.

Kama virefu sana jua basi na kina cha uchi wake ni kirefu sana. Lakinikama kiganja
na vidole vya mikononi ni vifupi, ujue kina ni kifupi pia!

Source;Chizika

HIZI NDIO ISHARA KUBWA TANO ZA MWANAMKE ALIYEKUZIMIA KISAWASAWA....soma hapa usipitwe !!!!

Ni muhimu sana kwako mwanaume kujua kwa uhakika kuwa mwanamke anakupeda kweli kweli,utajuaje kuwa mwanamke anakupenda? Zifuatazo ni ishara ambazo wewe kama mwanaume unapaswa uwe makini ili uweze kuziona na haraka kumtolea uvivu huyo mwanamke.

1*Mwanamke anaekupenda she apriciates the lito things you do hata kama sio cha maana sana na pia anapenda kushare nawe her time.....

2* Mwanamke anayekupenda atahangaika juu yako, atahangaika juu ya usalama wako,raha yako,heshima yako na maendeleo yako.Hii ni moja kati ya ishara kubwa kuwa mwanamke huyo anaupendo na wewe.

3* Mwanamke anayekupenda atakuonea wivu mara kadhaa,Wivu ni ishara kuwa anakupenda wewe na anataka akulinde usiibiwe au asije akakupoteza,anaogopa usije ukatoka katika maisha yake,au kwa maneno mengine usije ukamtoa moyoni mwako na nafasi yake ikachukuliwa.Japo wivu ukizidi sana pia inaweza kuleta tatizo.

4* Mwanamke anayekupenda atakapokuwa mbele ya marafiki zake au watu wengine atacheka nao lakini atakugeuzia ww macho/uso wake haraka sana. Kufanya hivi ni kuonyesha kuwa anakuhesabia ww kuwa utaweza kumletea furaha katika maisha yake,zaidi ya hilo ni kwamba anatumaini kuwa utamuona kuwa yeye ni mtu aliye rahisi kufurahishwa kwa kuwa yeye ni mtu wa furaha.

5* Mwanamke anayekupenda ataendelea kukuangalia usoni kwa muda mrefu kuliko ilivyo kawaida ya wanawake wengine,mara nyingi atakuangalia na kutabasamu vizuri. Hii huenda ni ishara moja muhimu sana ya kukuambia kimoyomoyo kuwa “NJOO NIKO KWAAJILI YAKO.”

Hivyo kama ulikuwa unahisi unamhitaji basi ni wakati mwafaka wa kumfuata na kumweleza ukweli na kirahisi nakuhakikishia unabeba mzigo kwani ni mtu tayari aliyekuwa anahisia kali za mahaba juu yako...

KUMBUKA: WASICHANA WANAAIBU SANA NA USITEGEMEE ATAKUFUATA NA ATAKWAMBIA KUWA ANAKUPENDA KWANI NI WACHACHE WENYE UJASIRI HUO... ILA UKIONA DALILI HIZO HAPO JUU USILAZE DAMU .. CHANGAMKA UTAMMILIKI KIULAINI

Njama 638 za mauaji alizoepuka Fidel Castro

Njama ya kutumia sigara kumuua Fidel Castro ambayo ilitibuka inajulikana sana, lakini njama nyengine 637 dhidi ya maisha yake ni zipi?

Shirika la kijasusi nchini Marekani CIA na watu waliotoroka Cuba wakati wa uongozi wa Castro walitumia nusu ya karne moja kufanya njama za kumuua kiongozi ambaye taifa lake lina athari kubwa kwa Marekani, kulingana na balozi wa Marekani nchini Cuba Wayne Smith.

Wakati mmoja kiongozi huyo wa Cuba alinukuliwa akisema, iwapo kuepuka majaribio ya mauaji kungekuwa miongoni mwa michezo ya Olimpiki ningejishindia medali ya dhahabu.

Hatahivyo baadhi ya njama hizo hazikutekelezwa ,kulingana na aliyekuwa mlinzi wa zamani wa Fidel Castro, Fabian Escalante.
Stakhabadhi zilizofichuliwa wakati wa utawala wa Bill Clinton zilionyesha kuwa CIA wakati mmoja walianza kuwafanyia utafiti konokono wa eneo la Carebean.

Njama, ilikuwa kutafuta konokono mmoja ambaye angemvutia Castro anayependa sana kuogelea na kumjaza vilipuzi ndani yake kabla ya kumlipua Castro atakapomshika
Mpango mwengine ulikuwa ule wa kutengeza boya la kuogelea ambalo huvaliwa kama shati na ambalo lingetiwa ugonjwa mbaya wa ngozi ili kumuathiri kiongozi huyo.

Mipango yote hiyo ilitupiliwa mbali.
Ajenti huyo alisikitika na akataka mpango mwengine ambao sio rahisi kuugundua,ripoti hiyo ilisema.

Mmoja ya wapenzi wa Castro wa zamani ,Marita Lorenz alisajiliwa.
Alipewa dawa zenye sumu ili kuweka katika kinywaji cha Castro.Lakini Castro aligundua jaribio hilo na anadaiwa kumpatia bunduki yake badala yake atumie kumuua.

''Huwezi kuniua. Hakuna anayeweza kuniua,"Bbi Lorenzo alisema Bw Castro alimwambia, alipokuwa anahojiwa na gazeti la New York daily.

Castro alidaiwa kutabasamu na kuendelea kuvuta sigara yake.''Nilijihisi nimetolewa pumzi kwa sababu alikuwa na uhakika juu yangu.Alinikumbatia na tukafanya mapenzi''.

Jaribio jingine lililokuwa maarufu dhidi ya maisha ya Castro ni lile la 2000, wakati ambapo mpango uliwekwa kuweka vilipuzi vingi katika jukwaa ambalo alitarajiwa kuhutubia nchini Panama.

Mpango huo ulitibuliwa na vikosi vya usalama vya Castro.

Watu wanne ikiwemo mtoro mmoja wa Cuba pamoja na ajenti wa CIA kwa jina Luis Posada walifungwa lakini baadaye wakaachiliwa.

Pia kulikuwa na mipango ya kumfanya Castro ambaye pia anajulikana '' The Beared'' aonekana kama chombo cha kukejeliwa badala ya kumuua.

Mpango mmoja ulikuwa kumwagia viatu vyake chumvi ya thallium wakati wa ziara yake ya ughaibuni kwa lengo kwamba anaposhika ndevu zake zingeweza kukatika.

Lakini mpango huo ulitibuliwa baada ya Castro kuahirisha ziara hiyo.Castro alichukua tahadhari ya hali ya juu ili kuwakwepa watu waliopanga mauaji yake.

Mwaka 1979 alipokuwa akielekea mjini New York ili kuhutubia mkutano wa Umoja wa Mataifa hakuweza kuwazuia wanahabari waliomuuliza iwapo alikuwa amevaa fulana ya ndani ambayo ina kinga dhidi ya risasi, alivua shati lake na kuwaonyesha kifua chake.

''Nimevaa fulana ya kawaida'',alisema.
Miongo kadhaa awali mwaka 1975, tume ya bunge la seneti nchini Marekani ilifichua maelezo ya njama nane dhidi ya maisha ya Castro kwa kutumia vifaa ambavyo tume hiyo inasema ''vinachosha akili''.

Njama moja iliopangwa na ambayo karibu ifaulu mara mbili ilikuwa ile ya kutuma dawa za sumu Cuba na kuwapeleka watu kumuua kiongozi huyo.

Ulikuwa wakati kama huo ambapo rais Kennedy, ambaye aliruhusu uvamizi wa kumuondoa madarakani rais Castro mwaka 1961 aliuawa, ambapo ajenti wa CIA alikuwa anatoa kalamu yenye sumu ilio na sindano kwa ajenti mmoja wa Cuba ili kumuua kiongozi huyo.

Davido aungana na wachezaji wa Chelsea kusherehekea ushindi

Davido ameonyesha yeye si mtu wa mchezo mchezo. Staa huyo aliungana na wachezaji wa Chelsea kusherehekea ushindi wa timu hiyo walioupata dhidi ya Tottenham Hospurs wa mabao 2-1, Jumamosi iliyopita.

Hitmaker huyo wa How Long alifanikiwa kupiga picha ya pamoja na baadhi ya wachezaji wa timu hiyo akiwemo Diego Costa, Eden Hazard, Victor Moses, David Luiz na César Azpilicueta.

Kupitia mtandao wa Instagram, muimbaji huyo ameandika, “GREAT
GAME!!@chelseafc ..”

Naye mchezaji wa timu hiyo Victor Moses ambaye ni raia wa Nigeria, ameandika kwenye mtandao wake wa Twitter, “What a feeling!So happy to get the win in such a big game.Thankful to score and help the team!Good to celebrate with @iam_davido too #CFC What a feeling!So happy to get the win in such a big game.Thankful to score and help the team!Good to celebrate with @iam_davido too #CFC.”

Hii ndio sababu ya timu ya Real Madrid kuvaa jezi za plastic dhidi ya Sporting Gijon

Klabu ya Real Madrid ya Hispania katika mchezo wao wa ligi kuu Hispania dhidi ya Sporting Gijon huku wakiwa wamevaa jezi zinazoangaza.

Jezi hizo zimetengenezwa na kampuni ya kijerumani ya Adidas, zimetengenezwa kwa kuyeyushwa plastiki laini iliyotokana na chupa zilizokuwa zimetupwa katika bahari ya Hindi, jezi moja inaripotiwa imetengenezwa kwa kutumia chupa 28.

Real Madrid na Adidas wametoa sababu ya kufanya hivyo huku wakishirikiana Parley ambao ni wanaharakati na utunzaji wa mazingira kama sehemu ya kuhamasisha utunzaji wa mazingira kwa kuacha kuharibu vyanzo vya maji.

samedi 26 novembre 2016

Ibrahimovic: Rooney anastahili heshima

Mshambuliaji wa Manchester united Zlatan Ibrahimovic, amesema Wayne Rooney''ni mchezaji bora'' na anastahili heshima zaidi, baada ya nahodha huyo wa Uingereza kuvunja rekodi ya ufungaji mabao.
Manchester United walifunga mabao 4-0 dhidi ya Feyenoord kwenye ligi ya Europa iliyochezwa siku ya Alhamisi.

Rooney, mwenye umri wa mika 31, alifunga goli la 39 barani Ulaya na kuifanya United kupata alama katika fainali ya hatua ya makundi dhidi ya Zorya Luhansk itakayowafikisha katika timu 32 bora katika ligi ya Europa.

Hii ni kutokana na mchango wa Rooney, ambaye amesalia na goli moja kufikia rekodi ya Sir Bobby Charlton ya magoli 249.

''Ni mtu mzuri , Ibrahimovic, aliyemsaidia Rooney kufunga bao la kwanza, aliambia BBC Sport. Nafurahi kwa kuwa amevunja rekodi. Lakini nitamsaidia kupata bao jingine. Lile ambalo litamfanya kuweka rekodi ya ukweli.''

Rooney aliomba radhi wiki iliyopita kwa picha ambazo ''hazifai'',alipohudhuria harusi katika hoteli walimokuwa ikilala timu ya taifa wakati wa mapumziko ya kimataifa.

Lakini Jumamosi alisema ripoti hizo ''zilikosa heshima'',akiongezea:Ni kama vyombo vya habari vinajaribu kuandika matangazo ya kifo change.

Alikasirika alipoulizwa tena swali kuhusiana na picha hizo baada ya ushindi dhidi ya Feyenoord, alisema: Kile kinachobuniwa na watu kama wewe unayeuliza maswali, kuyafanya mambo kuwa makubwa bila sababu yoyote.
''sikuhudhuria harusi hiyo,na ni aibu kuzungumzia kuhusu hilo usiku kama wa leo.''

Ibrahimovich alisema:'' Kwa mafikira yangu mtu akiwa na umaarufu kama hivyo, watu hutaka kujua zaidi kukuhusu.''
Tunastahili kumshukuru kwa kuwa michezaji jinsi alivyo, kwa kile alichokifanya. Siwaoni wachezaji wengi kutoka Uingereza walio na taaluma kama yake. Wanastahili kumpa heshima. Kila mtu hupenda kufanya jambo dogo kuwa kubwa.
Meneja Jose Mourinho alisema: Watu kama yeye hawastahili kujibu chochote tena , anastahili kufurahikia miaka michache iliyosalia katika taaluma yake na kucheza mchezo mzuri kadri ya uwezo wake.

L'ANCIEN MÉDECIN DE CHELSEA A REÇU DES MENACES DE MORT

Eva Carneiro a reconnu dans un entretien pour le Telegraph que la vie n'était pas la plus aisée pour elle depuis son départ de Chelsea.
Si elle a quitté Chelsea depuis septembre 2015 suite à un incident avec José Mourinho, technicien de l'époque, Eva Carneiro n'a pas pour autant oublié

Lors d'un entretien accordé au Telegraph, elle a reconnu avoir été victime de menaces de mort sur les résaux sociaux. "Même si je n'ai pas de présence sur les réseaux sociaux - je pense avoir fait un seul post dans ma vie - j'ai reçu des des menaces de violence sexuelle et de mort par ce biais-là. Ils [les agresseurs] semblent être des lâches sans visage et ils doivent être responsables devant la loi" , a-t-elle commenté.

Carneiro exerce désormais dans sa propre clinique à Londres comme le fait savoir l'Equipe.

Fifa: Argentina ndio bora duniani, Senegal yaongoza Afrika

Shirikisho la kandanda ulimwenguni (FIFA) limetoa orodha ya viwango bora vya soka ,ambapo mpaka sasa kwa upande wa bara la Ulaya Argentina bado ndio taifa bora duniani kwa mujibu wa viwango vya ubora duniani iliyotolewa Ijumaa.
Brazil, chini ya kocha wao mpya, inakuja moto na kuinyemelea kwa kasi.

Kwa upande wa Afrika Senegal ndio vinara na ipo nafasi ya 33 ulimwenguni , huku wakifuatwa na Ivory Coast katika nafasi ya pili ambapo wanafungana na Tunisia kwenye Nafasi hiyo na nafasi ya 36 ni Misri na wapo nafasi ya 34 ulimwenguni.

Nafasi kumi bora Argentina, Brazil, Ujerumani, Chile, Ubelgiji, Colombia, Ufaransa , Ureno, Uruguay, Hispania.
Orodha nyengine ya Fifa ya ubora duniani itatolewa Disemba 22.

Watu 80 wafariki katika shambulizi la Bomu lililowalenga washiha Iraq

Vyombo vya usalama vya Iraq vimesema kwamba zaidi ya watu themanini wameuawa kwa shambulizi la bomu lililowalenga madhehebu ya kiislamu ya kishia kusini mwa mji wa Baghdad.

Gari lililokuwa limebeba vilipuzi hivyo lililipuka karibu na kituo cha mafuta ambapo watu wengi wa dhehebu hilo walikuwa wameegesha magari yao.

Wengi wa watu waliofariki ni wananchi wa Iran na Afghanistan.
Walikuwa wakitoka kwenye moja ya tukio muhimu la kidini kwenye mji mtakatifu wa Karbala.

Askari wa kundi la kiislam wamekiri kuhusika na shambulizi hilo.
kundi hilo la wapiganaji la kiislam mara kwa mara hulenga madhehebu ya kishia na kuwatuhumu kwamba ni waongo.

jeudi 24 novembre 2016

Borussia Dortmund na Legia Warsaw wavunja rekodi

Klabu za Borussia Dortmund na Legia Warsaw zilivunja rekodi ya kufunga mabao mengi zaidi mechi ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya Jumanne, kwa kufungana jumla ya mabao 12.

Wajerumani hao chini ya Thomas Tuchel walishinda wapinzani wao kutoka Poland 8-4 mechi ya kusisimua iliyochezewa Ujerumani.
Walivunja rekodi iliyowekwa mabao 11 yalipofungwa mechi ambao Monaco waliwalaza Deportivo La Coruna 8-3 mwaka 2003.

Mabao saba yalifungwa dakika 22 za kipindi cha kwanza.
Legia ndiyo klabu ya kwanza kufunga mabao manne mechi ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya na bado kushindwa kwenye mechi.

Rekodi zilizovunjwa
---------------------

* Ni mara ya kwanza historia ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya wachezaji wanane kufunga mechi moja

* Dortmund ni klabu ya nne baada ya Liverpool, Monaco na Real Madrid kufunga mabao manane mechi moja Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya

* Ilikuwa mechi ya kwanza michuano ya ngazi ya juu Ulaya kufungwa magoli 12 tangu Ajax walipolaza Red Boys Differdange wa Luxemburg 14-0 michuano ya zamani ya Kombe la Uefa 3 Oktoba 1984.

* Ni mechi moja pekee historia ya Kombe la Ulaya na Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya ambapo mabao zaidi yalifungwa, Feyenoord ya Uholanzi ilipolaza KR ya Iceland 12-2 mnamo Septemba 1969.

* Dortmund sasa wamefunga mabao 14 dhidi ya Legia msimu huu, mabao mengi zaidi kufungwa dhidi ya mpinzani mmoja msimu mmoja wa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya

* Shinji Kagawa - ambaye wakati mmoja alichezea Manchester United - alifunga mabao mawili katika sekunde 76, mabao mawili ya kasi zaidi historia ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya

* Reus arejea kwa kishindo
Marco Reus wa Dortmund alirejea kwa kishindo baada ya kukaa nje kwa miezi sita kutokana na jeraha. Alikuwa na nahodha wa timu na alifunga mabao matatu.

"Nilifurahia kuwa hapo tangu mwanzo," alisema Reus ambaye alikosa Kombe la Dunia 2014 na Euro 2016 kutokana na jeraha.

Mambo yalivyokuwa
------------------

Moja - Legia wajiweka kifua mbele

Mbili - lakini hawaongozi muda mrefu

Tatu - Wajerumani wanaongoza

Nne - nakuongeza jingine

Tano - lakini Legia wanakomboa

Sita - sasa ni 4-2, wataendelea?

Saba - Reus anafanya mambo

Nane - na kisha anafunga jingine

Tisa - watajikwamua?

Kumi - tumefikisha mabao kumi!

11 - umekuwa usiku mrefu?

12- mambo yanamalizika 8-4

MAENEO FLANI ya KISHUA"


-Mshikaji alimuona demu mkali
anakatiza kitaa akamkubali akaamua amfuate amtemee cheche
MSHIKAJI- mambo dada?
DEMU- powa
MSHIKAJI-
umependezaa!!!
DEMU- asante.
MSHIKAJI- unaweza ukanisaidia namba yako ya simu.......
maana duh nmekukubali kinyama.
Demu baada ya kuambiwa vile akazama kwenye pochi lake akatoa noti ya 10000 akaandika namba yake kwenye noti akampa mshikaji.

Mshikaji kapokea ile noti akachana sehem iliyoandikwa namba halafu kamrudishia Demu noti yake..!!!

JE NANI ANA DHARAU

NA NANI JEURI..

DEMU AU MSHIKAJI??
🤒🤒🤒🤒🤒🤒🤒🤒

mercredi 23 novembre 2016

Alikiba ashinda tuzo mbili za The Nollywood & African Film Critics (NAFCA)/ISOME HAPA

Alikiba ameshinda vipengele viwili kwenye tuzo za heshima kubwa za The Nollywood & African Film Critics (NAFCA) ambazo hutolewa nchini Marekani.

Tuzo za mwaka huu zilitolewa Jumamosi ya November 19 kwenye ukumbi wa Alex Theatre of Glendale, huko California. Zilikuwa ni tuzo za 6 na zilionekana katika nchi mbalimbali duniani.
Alikiba ameshinda kipengele cha Favorite Artist of The Year na Favorite Song of The Year.
KUHUSU NAFCA

The Nollywood & African Film Critics’ Awards, commonly known as The NAFCA, are U.S. awards for achievements in the film industry and The NAFCA Honors are awarded to recognize outstanding individuals whose professional careers have been marked by extraordinary personal and professional accomplishments. Honorees and winners are awarded the NAFCA Trophies, officially the Award of Merit that is much better known by its nickname NAFCA. The awards, first presented in 2011 at the RTP Sheraton Imperial Hotel in Durham North Carolina, are overseen by the Nollywood Film Critics USA.

The NAFCA Special Honors were presented for the first time in 2011 to President Nelson Mandela. Recipients of this award in subsequent years include His Imperial Majesty Kabiyesi Alaiyeluwa Oba Okunade Sijuwade Olubuse II The Ooni of Ife, James Brown, Bobby Womack, President Paul Biya, President Yahya Jammeh of The Gambia, Dr. Folorunsho Alakija, Oscars’ award winner Louis Gossett Jr., Hollywood actors Glynn Thurman, Keith David, Marla Gibbs, Steven Williams and Lawrence Hilton Jacobs among others.

The NAFCA and The NAFCA Honors are presented yearly during the second weekend in September. The NAFCA is designed to globally promote African Cinema and culture. The prestigious NAFCA and The NAFCA Honors are awards of merit and are considered the highest African film and honorary awards.

samedi 19 novembre 2016

Conte na Hazard washinda tuzo ya mwezi Oktoba katika EPL

Mchezaji wa klabu ya Chelsea Eden Hazard ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Oktoba katika EPL, huku tuzo ya kocha bora mwezi Oktoba ikienda kwa kocha wa Chelsea, Antoine Conte ambaye ameshinda tuzo ya kocha bora wa EPL.

Chelsea imeshinda mechi zote 4 za ligi kuu katika mwezi huo, wakifunga magoli 11 na hawakuruhusu kufungwa goli hata moja, huku mchezaji Hazard akiwa amecheza mechi 4,akifunga goli 3 na kutoa Assist 1.

vendredi 18 novembre 2016

Mwili wa msichana anayetarajia 'kufufuliwa' kuhifadhiwa

Msichana ambaye alitaka mwili wake ugandishwe na kuhifadhiwa kwa matumaini kwamba anaweza kurejeshewa uhai wakati mmoja siku za usoni, alipata ushindi wa kihistoria saa chache baada ya kufariki dunia.

Msichana huyo alitaka mwili wake uhifadhiwe kwenye friji maalum baada ya kufa kwa matumaini kwamba anaweza kurejeshewa uhai, na hata ikiwezekana aponywe, baadaye. Mamake alimuunga mkono lakini babake alikuwa anapinga wazo hilo.

Msichana huyo mwenye umri wa miaka 14 alikuwa anaugua aina nadra sana ya saratani.

Jaji katika mahakama ya Uingereza aliamuru kuwa mama yake ndiye angekuwa na usemi wa mwisho kuhusu mwili wake.

Mwili wa msichana huyo, aliyefariki mwezi Oktoba, sasa umesafirishwa kwa ndege hadi Marekani kuhifadhiwa.

Msichana huyo alikuwa anaishi London na alitumia mtandao wa intaneti kusoma zaidi kuhusu teknolojia ya kuhifadhi miili ya cryonics miezi ya mwisho ya uhai wake.

Matumaini siku za usoni

Cryonics ni teknolojia inayotumia kuuhifadhi mwili kwa kuugandisha kwa matumaini kwamba huenda ikawezekana kuufufua au kupata tiba siku za usoni.

Msichana huyo alimwandikia jaji na kumwambia kwamba alitaka "kuishi muda mrefu" na hakutana "kuzikwa ardhini".
Aliandika: "Nafikiri kuhifadhiwa kwa teknolojia ya cryonic kutanipatia fursa ya kutibiwa na kuamshwa - hata kama ni baada ya miaka mia moja."

Jaji Justice Peter Jackson, alimtembelea msichana huyo hospitalini na anasema aliguswa sana na ujasiri ambao msichana huyo alikuwa nao katika kukabiliana na maradhi aliyokuwa anaugua.

Kwenye uamuzi wake, alisema, uamuzi huo haukuwa kuhusu usahihi au kutofaa kwa cyronics bali mzozo kati ya wazazi wa msichana huyo kuhusu hatima ya mwili wa binti yao.

Mwili kugandishwa

Cryonic ni shughuli ambayo imekuwa na utata mwingi na hakuna ajuaye iwapo inawezekana kufufua miili iliyogandishwa kufikia sasa.

Kuna vifaa Marekani na Urusi ambapo miili inaweza kuhifadhiwa kwenye madini ya naitorjeni kwenye baridi kali (chini ya nyozijoto -130C) - lakini huduma hiyo haipo Uingereza.

Gharama ya kugandisha mwili kwa muda usiojulikana inakadiriwa kuwa takriban £37,000.

------------------------------------------------------

Barua ya msichana kwa jaji

"Nimetakiwa kueleza ni kwa nini nataka jambo hili lisilo la kawaida lifanyike.

"Nina miaka 14 pekee na sitaki kufariki dunia lakini najua nitafariki dunia.

"Nafikiri kuhifadhiwa kwa njia hii ya cyronic kutanipa fursa ya kutibiwa na kuamshwa - hata kama ni miaka mia moja ijayo.

"Sitaki kuzikwa ardhini.
"Ninataka kuishi na niishi muda mrefu na nafikiri siku za usoni huenda kukapatikana tiba ya saratani ninayougua na kuniamsha.

"Ninataka kupata fursa hii.
"Hayo ndiyo mapenzi yangu.
Wazazi wa msichana huyo walitalakiana na msichana huyo hakuwa amekutana na babake kwa miaka sita kabla yake kuanza kuugua.

Mamake aliunga mkono mapenzi yake ya kutaka mwili wake uhifadhiwe kwa kugandishwa lakini babake alikuwa anapinga.

Babake alisema: "Hata kama itawezekana afufuliwe na atibiwe tuseme miaka 200 ijayo, huenda hatapata jamaa yeyote anayemjua na huenda asikumbuke mambo mengi. Atakuwa katika hali ya masikitiko ikizingatiwa kwamba ana miaka 14 na atakuwa Marekani."

Ingawa baadaye alibadili msimamo wake na kusema anaheshimu uamuzi wa bintiye, alitaka kuuona mwili wa bintiye baada ya kifo chake, jambo ambalo msichana huyo alikuwa amekataa.

Jaji alisema ombi la msichana huyo lilikuwa la kipekee kuwahi kuwasilishwa England na Wales, na labda kwingineko.

Kuhitajika kwa sheria

Jaji Jackson alisema kesi hiyo ni mfano wa matatizo mapya yanayoletwa na sayansi kwa wanasheria.
Msichana huyo alifariki Oktoba akifahamu kwamba mwili wake ungegandishwa, lakini jaji alisema kulikuwa na matatizo siku aliyofariki.

Wahudumu wa hospitali na wakuu wao walieleza wasiwasi kuhusu jinsi mwili wake uliandaliwa kwa ajili ya kuhifadhiwa.

Hilo lilifanywa na kundi la watu wa kujitolea Uingereza kabla ya mwili huo kupelekwa Marekani.
Amedokeza kwamba mawaziri wanafaa kutafakari uwezekano wa kutoa kanuni na sheria za kusimamia uhifadhi wa miili kwa kutumia teknolojia ya cyronic siku za usoni.

Shinzo Abe: Nina imani na Donald Trump

Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe amesema ana imani na Rais Mteule wa Marekani Donald Trump na kwamba wawili hao wanaweza kuaminiana.

Bw Abe ameeleza mkutano wa dakika 90 kati yake na Bw Trump katika jumba la Trump Tower, New York, kama wa uwazi na wa kirafiki.
Wakati wa kampeni, Bw Trump alitilia shaka manufaa ya urafiki kati ya Marekani na baadhi ya washirika wake wa muda mrefu, ikiwemo Japan.

Mkutano huo ulikuwa wa kwanza wa ana kwa ana kati ya Trump na kiongozi wa nchi nyingine duniani tangu ashinde urais.

Marekani na Japan zimekuwa washirika wakubwa tangu kumalizika kwa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia, ambapo Marekani iliisaidia Japan kufufua tena uchumi wake.

Trump ameahidi kufuta mktaba wa kibiashara kati ya Marekani na nchi za Pasifiki, ambapo Bw Abe amekuwa wakiuunga mkono sana kama njia ya kukabili ubabe wa kiuchumi wa China.

Mkataba huo uliidhinishwa na bunge la Japan, licha ya uwezekano kwamba huenda ukafutwa Bw Trump atakapoingia madarakani.
Bw Trump pia alisema Japan inafaa kulipia zaidi kwa ajili ya wanajeshi wa Marekani walio kwenye ardhi ya Japan kutoa ulinzi.

Aidha, ametoa pendekezo la Japan na Korea Kusini kustawisha silaha za nyuklia kukabili tishio kutoka kwa Korea Kaskazini.

Mkutano huo inadaiwa ulipangwa baada ya Bw Abe kumpigiakura Trump kumpongeza kwa kushinda uchaguzi wa urais, na kisha akamtajia kwamba angepitia New York akielekea Peru kuhudhuria mkutano wa kibiashara kati ya Asia na nchi za Pasifiki.

Akiongea baada ya mkutano huo, Bw Abe alisema: "Tulikuwa na mazungumzo ya kirafiki na ya kufana sana kwa kipindi kirefu. Yalikuwa mazingira ya kirafiki.
"Ninaamini kwamba bila kuaminiana kati ya nchi hizi mbili ushirikiano wetu hauwezi kufanya kazi siku zijazo na kama matokeo ya mazungumzo yetu leo, nimeshawishika kwamba Bw Trump ni kiongozi ambaye ninaweza kuwa na imani sana naye.

Kiongozi uyo wa Japan hakutoa maelezo mengi kuhusu mkutano huo lakini alisema watakutana tena kujadili kwa kina baadhi ya masuala muhimu.

Katika siku chache baada ya ushindi wake, Bw Trump amezungumza na viongozi kadha wa nchi mbalimbali kwa simu pamoja na baadhi ya watu anaotarajiwa kuwateua kuwa mawaziri katika jumba la Trump Tower.

Mengine yaliyotokea:

   #Luteni Jenerali Mstaafu Michael Flynn amepewa kazi ya kuwa mshauri mkuu wa usalama wa taifa, vyombo vya habari Marekani vimeripoti.

   #Waliomtembelea Trump Tower Alhamisi ni pamoja na waziri wa mambo ya nje wa zamani Henry Kissinger na gavana wa South Carolina Nikki Haley, mmoja wa wanaotarajiwa kupewa kazi ya waziri wa mambo ya nje

   #Mgombea urais wa zamani wa chama cha Republican Mitt Romney atakutana na Bw Trump wikendi hii, kwa mujibu wa vyombo vya habari Marekani

   #Bw Trump atazru majimbo ambayo alishinda kwa mikutano ya kusherehekea ushindi kwa mujibu wa mkurugenzi wake wa kampeni George Gigicos

Kwingineko, makamu wa rais mteule Mike Pence, ambaye pia anaongoza kundi la mpito la Bw Trump amesema ana imani utawala wa Trump utafanya kazi na wafuasi wa chama cha Democratic.

Hayo yakijiri, Rais Barack Obama amemhimiza mrithi wake kuikabili Urusi iwapo itakiuka maadili na sheria za kimataifa.

Baada ya kukutana na Kansela wa Ujerumani Angela Merkel mjini Berlin, Bw Obama amesema anatumai Bw Trump hatakuwa tu mtu wa kucheza siasa na maneno matupu na Urusi.

jeudi 17 novembre 2016

The Rock atajwa kuwa mwanaume mwenye mvuto zaidi 2016

Jarida la The People limemtangaza muigizaji Dwayne ‘The Rock’ Johnson kuwa mwanaume mwenye mvuto zaidi kwa mwaka 2016 (Sexiest Man Alive).

Baada ya kutangazwa na jarida hilo, The Rock kupitia mtandao wake wa Twitter aliandika, “He’s sweet, smart—and sculpted! Dwayne @TheRock Johnson is PEOPLE’s 2016 .”

Muigizaji huyo amechukuwa nafasi hiyo baada ya mchezaji mstaafu wa timu ya taifa ya Uingereza, David Beckham kutangazwa mwaka uliopita.

Fc Barcelona kupata wazamini wapya

Klabu ya Barcelona imeingia mkataba mpya na kampuni ya Rakuten ya Kijapan kwa ajili ya kudhamini timu hiyo kwa miaka minne.

Rakuten ni kampuni ya kuuza bidhaa kupitia mtandaoni wameingia mkataba na Barcelona wenye thamani ya pound milioni 200 ambazo ni zaidi ya bilioni 540 za kitanzania ni kampuni ya uuzaji wa vitu online kupitia tovuti yao na websites yao ni ya 11 kwa uingizaji mapato duniani, kwa jina jingine wanajiita kama “Japan’s Largest Internert Shopping Mall”.

Kuanzia msimu ujao, jezi za Barcelona zitakuwa na nembo ya Rakuten kifuani badala ya Qatar Airways ambalo ni shirika kubwa zaidi.

Raymond atuhumiwa kuiba baadhi ya mistari kwenye wimbo wa msanii wa Singeli

Msanii wa WCB, Raymond anatuhumiwa kutumia baadhi ya mistari ya wimbo wa msanii wa muziki wa Singeli, Manyo Lee kwenye wimbo wake mpya wa ‘Sugu’.

Akiongea na kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio, Manyo Lee amesema, “Mimi nilisikia kwa watu tu kuwa dogo kachukuwa mashairi yangu. Juzi kati lilifanyika tamasha kubwa tu nikaona akiimba yale mashairi lakini nikaona kawaida tu lakini hivi karibuni nimeona kaachia video kabisa nikaona kumbe dogo yupo serious kabisa.”

“Kama pochi ya dada naiminya kwapani, namuamini Mungu funga virago shetani. Joh Makini akiwa mweusi Barakah tumuite nani?,”
mistari ambayo Raymond anadaiwa kuchukua kwenye wimbo wa msanii huyo unaoitwa ‘Mwendo wa Pushapu’.

Naye Manyo Lee katika wimbo wake aliouachia mwezi Septemba mwaka huu ameimba,
“Kama pochi ya dada naiminya kwapani, namuamini Mungu virago funga shetani. Makini ajiite mweusi na Nigga ajiite nani?.”

Brazil kupanda hadi nafasi ya pili viwango vya Fifa mwezi huu

Timu ya soka ya wanaume ya Brazil inatarajiwa kupanda hadi kwenye nafasi ya pili kwenye viwango vipya vya mwezi huu kwenye shirikisho la soka duniani (Fifa) vinavyotarajiwa kutangazwa Novemba 24.

Viwango vya mwezi uliopita timu hiyo ilishika nafasi ya tatu huku nafasi ya pili ikishikiliwa na timu ya taifa ya Ujerumani na Argentina akiongoza orodha hiyo.

Hata hivyo imedaiwa kuwa timu hiyo ineweza kushika nafasi ya kwanza kwenye viwango hiyo endapo Argentina ingefungwa na timu ya taifa ya Colombia kwenye mchezo wa kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia Jumanne ya wiki hii.
Kwa sasa Brazil inaongoza kundi la timu za bara la Amerika ya Kusini zinazowania kufuzu kwenye kombe la dunia nchini Urusi mwaka 2018 ikiwa na pointi 27.

Mr T-Touch aeleza kwanini watayarishaji wa muziki hutoa beat bure kwa wasanii

Producer aliyetengeneza hits kibao, Mr T –Touch amefunguka kwa kuitaja sababu inayowafanya watayarishaji wengi wa muziki kuwapatia beat bure wasanii.

Mtayarishaji huyo amekiambia kipindi cha Ladha 3600 cha EFM, “Tunatoa beat bure ili tuweze kuaminiwa. Nimetoa beat za bure kwa takribani miaka mitatu.”

Touch ameongeza kuwa hakuna producer anayenufaika kupitia studio yake labda awe na kazi nyingine nje ya muziki. Kwa sasa Mr T anamiliki studio yake inayojulikana kwa jina la Touchez Sound aliyoifungua mwezi Julai mwaka huu.

Wayne Rooney ajutia kulewa kwenye sherehe ya harusi

Wayne Rooney amemuomba radhi kaimu meneja wa timu ya taifa ya Uingereza Gareth Southgate baada ya picha kutolewa zikimuonesha akiwa mlevi wakati wa sherehe ya harusi.

Nahodha huyo alihudhuria sherehe hiyo ya harusi katika hoteli ambayo timu hiyo ilikuwa inakaa wakicheza mechi ya kimataifa.

Nahodha huyo amesema kupitia taarifa kwamba picha hizo "hazifai".

Amesema ingawa picha hizo zilipigwa wakati wake wa kupumzika, "hazifai kwa mtu wa hadhi" yake.
Gazeti la The Sun la Uingereza lilichaisha picha hizo ambazo zinamuonesha Rooney, 31, akiwa kwenye sherehe usiku wa Jumamosi baada ya mechi ya England ya kufuzu kwa Kombe la Dunia dhidi ya Scotland.

England walishinda mechi hiyo.
Chama cha Soka cha England (FA) kimesema kitathmini upya sheria kuhusu mambo ambayo wachezaji wanaruhusiwa kufanya wakati wao wa kupumzika.

Gazeti la The Sun linadai FA imechukua hatua hiyo kwa sababu wachezaji 10 wa England walikaa kwenye kilabu cha usiku hadi saa 04:30 GMT Jumapili.

Rooney hakucheza mechi ambayo England walitoka sare 2-2 na Uhispania Jumanne kwa sababu ya jeraha ndogo kwenye goti.

mercredi 16 novembre 2016

Adhabu ya kifo dhidi ya Mohammed Morsi yatenguliwa

Mahakama ya juu nchini Misri imetengua adhabu ya hukumu ya kifo dhidi ya Rais wa zamani wa nchi hiyo aliyeondolewa madarakani Mohammed Morsi.
Morsi alihukumiwa adhabu ya kifo kwa ushiriki wake wa kuvunja gereza na wafungwa kutoroka kulikofanywa mwaka 2011 wakati wa vuguvugu la mabadiliko lililoikumba nchi hiyo.

Alichaguliwa kuwa Rais wa nchi hiyo mwaka 2012, lakini aliondolewa madarakani katika mapinduzi ya kijeshi dhidi ya utawala wake kufuatia maandamano makubwa yaliyofanyika nchini humo kuupinga utawala wake.

Kwa nyakati tofauti Morsi alihukumiwa kifungo cha maisha jela kwa makosa ya ugaidi na bado anakabiliwa na mashitaka mengine.

For more click :

Share on whatsapp

Lampard: Kuiaga klabu ya New York City

Kiungo wa kati wa zamani wa England na Chelsea, Frank Lampard amesema ataiaga ligi ya MLS ya New York City.

Lampard mwenye umri wa miaka ,38, ambaye mkataba wake utakamilika mwishoni mwa mwaka huu , amechapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram kwamba wakati wake katika klabu hiyo ''umefika kikomo.''

Amesema atatangaza hadharani ' hatma yake ya siku zijazo' hivi karibuni.''

Lampard amefunga mabao 15 katika mechi 31 alizoshiriki katika klabu ya New York ,kwa miaka miwili iliyokatizwa na mkopo kutoka Manchester City.

New York City walifungwa mabao 7 kwa nunge na klabu ya Toronto FC katika hatua za kwanza za mwezi.
Lampard alijiunga na klabu ya Chelsea mwaka 2014, na kuvunja rekodi ya mabao 211.

Mwenzake wa timu ya timu ya Uingereza na Liverpool Steven Gerrard pia anaweza kumaliza muda wake nchini Marekani
Gerrard, 36, amesema amekamilisha mkataba wake kwa akiichezea klabu ya LA Galaxy na amesema anaweza kuhudumu kama mkufunzi kwa klabu yake ya Liverpool.

Usain Bolt kujiunga na Borussia Dortmund

Klabu ya Ujerumani ya Borussia Dortmund imesema kuwa mwanariadha wa mbio fupi kutoka Jamaica Usain Bolt atashiriki mazoezi na klabu hiyo kwa siku chache.

Bolt amekuwa akisema kwamba angependa kucheza soka baada ya kustaafu katika riadha.

Lakini wakimkaribisha, maafisa wa klabu hiyo wamesema kuwa hakuna hakiksho kwamba mwanariadha huyo ataichezea klabu hiyo katika siku za usoni.

Messi na wenzake wagomea

Lionel Messi amewaongoza wachezaji wa timu ya taifa ya Argentina kususia kuongea na wanahabari baada ya uokosoaji kuhusu uchezaji duni wa timu hiyo.
Messi, 29, alitangaza mgomo huo baada yake kufunga bao wakati wa ushindi wao wa 3-0 mechi ya kufuzu kwa Kombe la Dunia dhidi ya Colombia.

Kituo kimoja cha redio kilikuwa kimeripoti kuwa mshambuliaji Ezequiel Lavezzi alivuta bangi baada ya kipindi cha mazoezi, tuhuma ambazo amekanusha.
"Tumepokwa tuhuma nyingi, kukosewa heshina na hatujasema lolote," messi alisema.

Messi na wenzake 25 waliondoka kutoka kwenye kikao na wanahabari bila kuzungumza nao baada ya mechi hiyo dhidi ya Colombia.

Taarifa zinasema Lavezzi atakishtaki kituo hicho cha redio.
"Tunajua wengi wenu ambao hamna heshima kwa mchezo huu, lakini kuingilia maisha ya kibinafsi ya mtu mmezidi," Messi aliongeza.
Argentina walikosolea sana baada yao kulazwa 3-0 na Brazil lakini ushindi wao dhidi ya Colombia umewawezesha kupaa hadi nambari tano na kwenye nafasi za kushindania kufuzu kwa Kombe la Dunia.

Mataifa manne yanaomaliza juu kanda ya Amerika Kusini hufuzu moja kwa moja. Nambari tano hukutana na mpinzani kutoka bara jingine kuamua mshindi.

Donald Trump kulipwa $1 kila mwaka

Rais mteule wa Marekani Donald Trump amesema hataki kulipwa mshahara wa rais wa $400,000 atakapochukua hatamu Januari mwakani. Badala yake atakuwa akilipwa $1 pekee kila mwaka.
Alifichua mpango wake huo wakati wa mahojiano na Lesley Stahl kipindi cha 60 Minutes cha CBS News.

Ingawa hakujua rais huwa analipwa pesa ngapi, Bw Trump alisema alidhani anahitaji kuchukua tu $1.
Baada ya Bi Stahl kumjulisha kwamba mshahara wa rais ni $400,000, alisema: "Hapana, sitaupokea mshahara huo. Sizichukui kamwe."

Rais huyo mteule anatimiza ahadi aliyoitoa wakati wa kampeni.
Aliambia waliohudhura mkutano wake Septemba kwamba mshahara wa rais si jambo kubwa kwake.

Kuna viongozi wengine walioukataa mshahara?

Bw Trump si kiongozi wa kwanza wa Marekani kukataa mshahara.

Herbert Hoover, aliyekuwa ametajirika kupitia biashara ya madini kabla ya kuingia madarakani, na John F Kennedy, aliyerithi utajiri mwili, wote walikataa kupokea mashahara na badala yake wakatoa pesa hizo zisaidie wasiojiweza katika jamii.
Meya wa zamani Michael Bloomberg, gavana wa zamani wa California Arnold Schwarzenegger na gavana wa zamani wa Massachusetts Mitt Romney pia walikataa kupokea mishahara yao.
Mark Zuckerberg, mwanzilishi wa mtandao wa kijamii wa Facebook, ndiye mfanyakazi anayelipwa mshahara wa chini zaidi katika kampuni hiyo.

Aidha, ni miongoni wa CEO (Afisa Mkuu Mtendaji) wengi ambao hulipwa mshahara wa $1 pekee.
Sergey Brin na Larry Page wa Google pia wamekuwa wakilipwa $1 kwa mwongo mmoja sasa.

Larry Ellison wa Oracle pia aliukataa mshahara wake kwa miaka kadha alipokuwa CEO. Afisa mkuu mtendaji wa Hewlett Packard Enterprise (HP) Meg Whitman apia alichukua hatua sawa.

Viongozi hawa hata hivyo hujipatia pesa kupitia njia nyingine. Wengi ni kupitia hisa wanazomiliki na wengine hulipwa kwa kutegemea matokeo au mapato ya kampuni.

Viongozi wa nchi nyingine hulipwa pesa ngapi?

Licha ya $400,000, anazolipwa rais wa Marekani, pia hupewa jumla ya $50,000 ambazo huwa hazitozwi ushuru, kwa mujibu wa sheria.
Waziri mkuu wa Canada alilipwa C$340,800 (£201,202) mwaka uliopita.

Kansela wa Ujerumani Angela Merkel alilipwa $242,000 (£193,976) naye Rais wa Ufaransa Francois Hollande akalipwa $198,700 (£158,000), kwa mujbiu wa taarifa ya CNN ya mwezi Agosti.

Bw Hollande alipunguza mashahara wake kwa 30% alipoingia madarakani mwaka 2012.
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May hulipwa $186,119 (£143,462) kila mwaka, ingawa thamani yake kwa dola imeshuka baada ya Uingereza kupiga kura kujiondoa EU.

Waziri mkuu wa zamani wa Uingereza David Cameron alishutumiwa sana alipoongeza mshahara wake kwa 10% mwaka 2015.

Hata hivyo alisema jambo la busara ni kulipwa "mshahara unaolingana na kazi".
Aliongeza kwamba kuongezewa mashahara kulimpa uwezo zaidi wa kutoa pesa za hisani na mambo mengine ya kusaidia jamii.

Wazo hili lilitoka wapi?

Mwanzilishi wa Apple Steve Jobs alivumisha wazo la mshahara wa $1 Silicon Valley baada yake kurejea katika kampuni hiyo 1997.

Wakuu wa kampuni mbalimbali wamekuwa wakikosa kupokea mishahara yao tangu Vita Vikuu vya Kwanza na vya Pili vya Dunia.
Wakuu wa kampuni, benki na viwanda mbali ambao walijitolea kutumikia nchi katika majukumu mbalimbali wakati wa Vita Vikuu vya Kwanza vya Dunia walifahamika kama "wanaume wa dola moja kila mwaka". Kwa kuwa sheria nchini Marekani huharamisha mtu kufanya kazi bila kulipwa, viongozi hao walipokea mshahara wa $1 kutimiza matakwa ya sheria kwamba walikuwa wanalipwa.

Wazo hilo lilirejea wakati wa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia ambapo wakuu wa kampuni kubwa kama vile Lockheed, Chrysler na Boeing walijitokeza kutumikia nchi kama uzalendo.

Donald Trump atapata pesa wapi?

Ana biashara nyingi ambazo zinampa pesa, ingawa kwa baadhi watu wameuliza maswali. Alitangaza majuzi kwamba wanawe - Donald Jr, Eric, na Ivanka - na mume wa Ivanka, Jared Kushner, watakuwa kwenye kamati inayosimamia mpito.

Bw Trump hatakiwi kuuza mali yake, ambayo thamani yake inafikia mabilioni, lakini amesema biashara zake zitasimamiwa na watoto wake.
Lakini kuhusika kwa watoto wake katika shughuli ya mpito kumewafanya baadhi kusema kutakuwa na mgongano wa maslahi.
Isitoshe, Bw Trump bado hajatoa taarifa zake za kodi na hakuna ajuaye iwapo kuna wato kutoka nje wanaomiliki sehemu ya hisa aktika biashara zake. Hilo linaweza kuathiri uhusiano wa Marekani na nchi za nje, hivyo kuibua suala la mgongano wa maslahi.

Jokate, Brown Mauzo, Abdu Kiba na wengine kuanza kuachia kazi chini ya label ya Alikiba ‘King’s Music’

Alikiba ametaja wasanii ambao wapo chini ya lebel yake ya ‘King’s Music”

Alikiba amewataja Jokate, Abdu Kiba, Delila, Abby Skills na Brown Mauzo wa Kenya kuwa ni baadhi ya wasanii ambao wapo chini ya label yake ambayo ameedai ipo tangu siku yingi lakini hakuitangaza tu.

“Mimi Record label ninayo muda mrefu,muda mrefu sana lakini sikufanya matangazo lakini nina wasanii ambao nilikuwa nawamiliki nikapumzika, sasa hivi nimerudi tena najipanga upya nao waendelee kufanya kazi, kama ambavyo unamuona Abby Skills anafanya kazi vizuri na bado ataendelea kufanya kazi, pia kuna Abdu Kiba” Alikiba alifunguka kwenye 255 ya Clouds Fm.

“Afu vilevile kuna msanii mwingine ambao watu hawajawahi kumsikia, Pia kuna wakiana Jokate, kina dalila na wengine wengi wapo chini ya label yangu, sijafanya rasmi lakini mtawasikia.”

lundi 14 novembre 2016

AFOTY: Wasifu wa Riyad Mahrez

"Utadhani ameweka gundi katika mguu wake kutokana na vile mpira unavyokwama''. Hayo yalikuwa maoni ya awali ya rafikiye mgombea wa taji la mchezaji bora wa mwaka 2016 barani Afrika Riyad Mahrez, Madjid.

''Tulikuwa tukipigana ili Riyadh ajumuishwe katika kikosi chetu," aliongezea, akikumbuka vile walivyotumia muda wao kucheza soka wakati walipokuwa watoto huko Beni Snous mji uliopo Kaskazini magharibi mwa Algeria.

''Sasa dunia nzima inafahamu uwezo wa Mahrez wa kuucheza mpira anavyotaka na sasa ni klabu kubwa duniani wala sio vijana wenzake wanaotaka ajiunge nao''.
Baada ya kuisaidia Leicester kushinda taji la ligi kuu nchini Uingereza mwaka 2016, katika kile kilichoonekana kuwa kisa cha kushangaza na cha kihistoria, klabu za Arsenal, Barcelona na Chelsea zilitaka kumsajili.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Algeria alikuwa ametangazwa kuwa mchezaji wa kulipwa wa mwaka, akiwa raia wa kwanza wa Afrika kupata taji hilo baada ya kuanzisha kampeni hiyo akicheza wingi ya kulia kwa kufunga mabao 17 kutoa usaidizi wa mabao mara 11 katika mechi 34 za ligi kuu.

Ulikuwa msimu ambapo Mahrez ambaye alijiunga na Leicester kutoka Le Havre kwa pauni 400,000 pekee mwaka 2014, aliimarika na kuisaidia timu yake pamoja na yeye mweyewe kufaidika zaidi ya ndoto yao.

Pengine siku iliyong'arisha nyota ya mchezaji huyo inayopaswa kuwekwa katika kumbukumbu ilikuwa Februari 6 nyumbani kwa mabingwa watetezi wa ligi ya Uingereza Manchester City wakati Mahrez alipougusa mpira na kumpita Nicolas Otamendi, akamchenga Martin Demichelis kabla ya kupiga mkwaju mkali katika lango la Man City ulioiweka Leicester kifua mbele 2-0.

Leicester ilishinda mechi hiyo 3-1 huku Mahrez akisaidia kupata mabao matatu katika mechi nyingine hatua ambayo iliisadia timu hiyo kuwa na ufanisi mkubwa na kushinda ligi.
Ni kwa sababu hiyo ndio maana hakuwashangaza wengi alipoanza kusakwa na klabu kubwa.

Timu zilianza kuitafuta saini ya mchezaji huyo mwembamba kwa maumbile, mchezaji ambaye umahiri wake umeleta hewa safi katika wingi na kuwafurahisha mashabiki na amekuwa tegemeo la wenzake.

Lakini mchezaji huyo amekataa kujiunga na klabu hizo kubwa na kusema kuwa alitaka kucheza katika klabu hiyo kwa msimu mwengine ili kuthibitisha uwezo wake.
Ameifungia Leicester mabao manne tayari msimu huu matatu kati yao yakitoka katika ligi ya vilabu bingwa ulaya.

Na amekuwa kiungo muhimu katika kuhakikisha kuwa Algeria inafuzu katika michuano ya kombe la mataifa bingwa Afrika itakayochezwa nchini Gabon.
''Riyad anaifanya timu yake ya taifa kuwa kubwa. Kila mtu anaijua Algeria kutokana na umaarufu wa Riyad." alisema mchezaji mwenza wa Algeria Mehdi Abied.
''Nchini Algeria tunajivunia sana Riyad. Sio rahisi kuwa mchezaji bora wa ligi ya Uingereza. Ni kitu kikubwa sana''.

"Kila mtu barani Afrika anampenda Riyad. Nakumbuka tulienda Ethiopia na Algeria na walikuwa wanamshabikia Riyad zaidi ya wachezaji wa timu yao''!

Piga kura hapa : bbc.com/africanfootball

Rooney amuahidi jezi kijana anayeugua saratani

Nyota wa timu ya soka ya Uingereza Wayne Rooney ameahidi kumpatia jezi yake mtoto anayeugua kufuatia ushindi dhidi Scotland England.

Kijana huyo amekuwa akifanyiwa kampeni katika mitandao ya kijamii.

Kasabian Newton-Smith mwenye umri wa miaka 8 kutoka Sheffield alipatikana na saratani alipokuwa mchanga na sasa ana uvimbe mara mbili katika kichwa chake.

Klabu za soka,wachezaji na watu binafsi wametakiwa kuchapisha ujumbe wa Twitter #1LastSmile4Kasabian.

Katika ujumbe wa kanda ya video,nahodha huyo wa Uingereza alisema kuwa wachezaji wenzake wanajivunia na ujasiri ulioonyeshwa na Kasabian.

samedi 12 novembre 2016

Alikiba akerwa na Watanzania wanaomtusi Wizkid

Alikiba ameelezea kusikitishwa kwake na Watanzania wanaomtukana staa wa Nigeria, Wizkid kwenye akaunti yake ya Instagram. Kiba amesema anaamini wale wanaomtukana si mashabiki wake kwakuwa mashabiki wake wa ukweli wanajua jinsi anavyomkubali Wiz.

Ali amesema yeye ni shabiki mkubwa wa Wizkid na amemsihi kuwapuuza watu hao wanaomtukana.

“I am not happy with what has been going on, on social media . I have a great appreciation for @wizkidayo as a fellow artist and as a fan . I am very disappointed and saddened by the insults and attacks directed at him, and I want to be very clear that I condemn this behaviour and I believe none of my true fans are part of this irrational silliness and stupidity as they know I have always had love for @wizkidayo,” ameandika Kiba.

“Drown out the noise from the haters bro, congratulations on your very successful year. Much love from my real fans and from Tanzania.”

Mambo yote hayo yamekuja baada ya MTV EMA kumnyang’anya tuzo Wizkid aliyokuwa ametangazwa kushinda na kumpa Alikiba.

vendredi 11 novembre 2016

VIRUS QUI SE PROPAGE SUR WHATSAPP : VOICI COMMENT S’EN PROTÉGER

ALERTE VIRUS – Si vous utilisez l’application de messagerie WhatsApp, soyez vigilant : un virus nommé WhatsEspião a déjà infecté des centaines de milliers d’utilisateurs. LCI vous explique comment s'en prémunir.

              

            Un virus dangereux nommé "WhatsEspião" (littéralement "espion" en portugais) se répand actuellement comme une traînée de poudre sur la très populaire messagerie WhatsApp. Si pendant longtemps les hackeurs ciblaient leurs victimes en passant par les sites pornographiques, aujourd’hui ils se cachent derrière le visage inoffensif de l’un de vos proches.

   Comment le virus se propage-t-il ?

Le principe est bien connu : un premier compte est piraté, il envoie ensuite à l'intégralité de son carnet d'adresse des messages contenant des liens. Si l'utilisateur clique dessus, il sera infecté à son tour instantanément et un petit virus s'installera discrètement sur son smartphone. Pas moins de 100.000 utilisateurs de l’application auraient été infectés, selon le site spécialisé PSafe, qui l’a repéré pour la première fois le 3 novembre dernier.

Soyez particulièrement vigilant, même si vous avez parfaitement confiance en la personne qui vous envoie ce message et que la proposition peut vous sembler attrayante.

Sais-tu qu'il est possible d'espionner les conversations de tes amis sur WhatsApp ? Va sur ce lien et télécharge cette application. Ça fonctionne réellement"
WhatsEspião

Que risque-t-on concrètement ?

Une fois que vous aurez cliqué sur le lien pour "espionner les conversations", les pirates qui se cachent derrière ce virus vous demanderont d'installer une application qui, évidemment, ne vous permettra pas d’y avoir accès. En vous poussant à cliquer sur ce lien, les pirates espèrent récupérer des informations personnelles vous concernant. Dans le but ensuite de les utiliser pour du phishing : en vous envoyant des factures bidons ou de fausses demandes de paiement, par exemple.

Toujours selon le site spécialisé PSafe, les pirates pourraient également ajouter des publicités sur votre écran pour gagner de l'argent. Nous avons contacté WhatsApp au sujet de ce virus et nous attendons un retour de leur part.

Que faire si vous avez cliqué ?
------------------------

Sur Android
----------

1 Allez dans les Paramètres
2 Cliquez sur l'onglet "Applications"
3 Sélectionnez WhatsApp
4 Cliquez sur "Effacer les données"

Sur l'iPhone
----------

1 Cliquez sur l'icône "Réglages" (en bas à droite)
2 Allez sur l'onglet "Discussions"
3 Cliquez sur "Supprimer toutes les discussions"

A NOTER : vous perdrez très probablement l'historique de vos conversations, mais le virus "WhatsEspião" aura disparu de votre téléphone !

Messenger, WhatsApp : une nouvelle cible pour les pirates

De manière générale si vous voulez protéger vos données et éviter que ce virus se propage sur WhatsApp, ne cliquez pas sur les liens que vous ne connaissez pas ni sur ceux qui peuvent vous sembler étranges. Et cela, quel que soit le réseau social : rappelons que début octobre, un virus prenant la forme d'une vidéo postée par une connaissance a infecté des milliers d'utilisateurs sur Messenger, l'application de messagerie instantanée de Facebook. Il se présentait lui aussi sous la forme d’un message contenant un lien vers une vidéo, qu’un ami aurait partagé avec vous via le chat de Facebook.

SHUHUDIA HAPA MASTAA SERENA NA VENUS WILLIAMS WANAVYO KUWA WAKIJIACHIA NA MABEBEZ WAO

Diamond na Millard Ayo washinda tuzo za #YouTubeSSA (YouTube Sub-Saharan Africa Creator)

Google wametangaza washindi 10 wa mwanzo wa tuzo za Sub-Saharan African YouTube [Awards].
Tuzo hizo zimekuwa zikifanyika kwenye mabara mengine tangu mwaka 2007 na zimekuwa zikiwapongeza watu wanaofanya vizuri kwenye Youtube. Jumla ya tuzo 24 zitatolewa ambapo zilizosalia zitatolewa leo, November 11.
Nominees walichaguliwa kutokana na idadi ya subscriber walionao.
Nchi zinashiriki kwenye tuzo za SSA ni Tanzania, Ghana, Uganda, South Africa, Zimbabwe, Kenya, Nigeria, na Senegal. Kuna channel zaidi ya 70 katika nchi za SSA ambazo zimefikisha zaidi ya subscribers, 100,000

Washindi 10 wa mwanzo ni:

Comic – Ramscomics / Supastrikas
Education – Retutpro – Photography and Photoshop Tutorials
Fitness – Six Pack Factory
Games – Slushy AJ
News and politics – Millard Ayo
Nonprofit – Jim Nduruchi
Pets and animals – Earth Touch
Top Subscribed Creator in Ghana – OfficialSarkodie
Top Subscribed Creator in Senegal – Prince Arts
Top Subscribed Creator in Tanzania –
Diamond Platnumz
Top Subscribed Creator in Zimbabwe – Mufti Menk

Top Subscribed Nollywood Channel – IbakaTV/Nollywood

jeudi 10 novembre 2016

Watakaoshindania tuzo ya soka ya BBC kutangazwa

Wachezaji watano nyota Afrika ambao watapigania tuzo ya BBC inayotolewa kwa Mwanakandanda Bora Afrika wa mwaka watatangazwa Jumamosi na upigaji kura kuanza.

Majina ya wachezaji hao watakaoshindania tuzo ya mwaka 2016 watatangazwa kwenye kipindi cha moja kwa moja BBC World TV na kwenye redio ya BBC World Service kuanzia saa 18:00 GMT.

Mashabiki wa soka ya Afrika kote duniani watapata fursa ya kupiga kura kwenye tovuti ya BBC African football kuanzia saa 18:50.

Upigaji kura utafungwa saa 18:00 Mnamo Jumatatu, 28 Novemba na mshindi atatangazwa moja kwa moja kupitia runinga ya Focus on Africa TV na pia kwenye redio Jumatatu 12 Desemba saa 17:35.

Wachezaji nyota wa zamani Afrika pamoja na wataalamu wa soka watahudhuria kipindi hicho maalum siku ya Jumamosi.

Kipindi hicho ambacho mtangazaji wake atakuwa Peter Okwoche, kitashirikisha mahojiano na mshindi mmoja wa zamani wa tuzo hiyo, majadiliano na watakaoshindania tuzo mwaka 2016 na utathmini wa soka ya Afrika mwaka huu.

Na kutakuwa pia na fursa ya kutazama video za matukio ya nyuma ya pazia tkwenye kurasa za Facebook za BBC Africa na BBC Sport na pia kwenye
Instagram.

BBC Sport pia wataandika ujumbe wa moja kwa moja kwenye Twitter uzinduzi utakapokuwa unafanyika, katika akaunti za Twitter za BBC Africa na BBC Sport.

Wanaotumia mitandao ya kijamii wanaweza kufuatilia matukio kupitia kitambulisha mada #BBCAFOTY.

Mshindi wa mwaka jana alikuwa Yaya Toure.

Washindi wa zamani wa Tuzo ya BBC ya Mwanakandanda Bora wa Afrika wa Mwaka:
-----------------------------------

2015: Yaya Toure (Manchester City & Ivory Coast

2014: Yacine Brahimi (Porto & Algeria)

2013: Yaya Toure (Manchester City & Ivory Coast)

2012: Chris Katongo (Henan Construction & Zambia)

2011: Andre Ayew (Marseille & Ghana)

2010: Asamoah Gyan (Sunderland & Ghana)

2009: Didier Drogba (Chelsea & Ivory Coast)

2008: Mohamed Aboutrika (Al Ahly & Egypt)

2007: Emmanuel Adebayor (Arsenal & Togo)

2006: Michael Essien (Chelsea & Ghana)

2005: Mohamed Barakat (Al Ahly & Egypt)

2004: Jay-Jay Okocha (Bolton & Nigeria)

2003: Jay-Jay Okocha (Bolton & Nigeria)

2002: El Hadji Diouf (Liverpool & Senegal)

2001: Sammy Kuffour (Bayern Munich & Ghana)

2000: Patrick Mboma (Parma & Cameroon)

Msomali achaguliwa katika bunge la Marekani

Ilhan Omar, mwenye umri wa miaka 34, ameweka historia kwa kuwa mbunge wa kwanza mwenye asili ya Kisomalia nchini Marekani.

Mwanamke huyo Muislamu mwenye asili ya Somali na Marekani ndio raia wa kwanza wa Kisomali kuchaguliwa katika wadhfa mkuu kama huo nchini Marekani.

Uchaguzi wake unajiri siku chache tu baada ya rais mteule Donald Trump kushtumu wahamiaji wa Kisomali mjini Minnesota kwa kueneza maoni ya itikadi kali.

Akisherehekea ushindi wake bi Omar amesema kuwa atakuwa sauti ya waliotengwa katika bunge la jimbo hilo.

''Nadhani nimeleta sauti ya akina mama vijana wanaotafuta fursa''.
Redio ya uma katika jimbo hilo ilimnukuu akisema kuwa alitoroka nchini Somalia na familia yake wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe wakati alipokuwa na umri wa miaka minane pekee.

Waliishi nchini Kenya kama wakimbizi kwa takriban miaka minne kabla ya kuelekea Marekani na kuishi katika jimbo lenye Wasomalia wengi la Minnesota.

Picha: Tattoo mpya ya Lionel Messi

Mchezaji wa klabu ya Barcelona na Argentina Lionel Messi, ameonyesha tattoo yake mpya mguuni wakati akiwa anafanya mazoezi na timu yake ya taifa.

Messi ambaye ni mshindi wa tuzo ya Ballon d’Or mara tano ameamua kuonyesha mguu wake wa kushoto ulivyokuwa umefunikwa na rangi nyeusi ya tattoo ambayo ina namba ya jezi yake namba 10.

Mashabiki msitengeneze bifu isiyo ya lazima kati ya Wizkid na Alikiba

Ushabiki ni mzuri kufurahia, ni mzuri kupongezana, lakini pale unapoingiza matusi, hakika matokeo yake ni mabaya siku zote.
Ama pengine ushabiki kimuziki tulionao Tanzania, ubaki kuwa wa kurushiana matusi tu ndani kwa ndani na usihusishe wasanii wa nje ambao timu zetu hazihusiani nao asilani.

Ninasikitishwa sana na ninachokiona kwenye ukurasa wa Instagram wa Wizkid baada ya kubainika kuwa tuzo ya MTV EMA aliyokuwa ameshinda awali itachukuliwa na atapewa Alikiba – ambaye kwa mujibu wa kura ndiye aliyestahili kushinda. Hiyo imekuwa habari njema kwa mashabiki wa Alikiba. Wanastahili kufurahia – actually, Watanzania wote bila kujali timu zilizopo tunapaswa kufurahia na kumpongeza Kiba kwa hatimaye kututoa kimasomaso.
Lakini kwanini Wizkid ambaye naye alipewa tu tuzo hiyo (si kama aliwawekea MTV EMA mtutu wa bunduki ili wampe) atukanwe? Kwanini mashabiki wanataka kutengeneza uadui si tu kati ya Wizkid na Alikiba, bali ni Nigeria na Tanzania?

Unadhani mashabiki wa Wizkid au Wanaijeria kwa ujumla wanapenda kuona msanii wao anatukanwa bila sababu? Kwanini hatuwezi tu kufurahia ushindi huu bila kumtusi, kumkejeli Wizkid ambaye kwa miaka yote amekuwa akiipenda sana nchi yetu? Isitoshe Alikiba amempongeza Wizkid kwa ushindi wake.

Sasa kwanini mashabiki wanashindwa kutambua kuwa msanii wanayempenda anahitaji kushirikiana na wasanii hawa na sio kutengenezewa tension baina yao isiyokuwa na faida! Nigeria ni sehemu muhimu Afrika kimuziki, si jambo la heri kwa msanii wa Tanzania kukimwagia mchanga kitumbua anachoweza kuhitaji kutoka huko siku za usoni.

Anachofanyiwa Wiz kwenye ukurasa wake ni aibu inayoirudia Tanzania. Watu wachache wanaharibu jina la nchi kwa kuendekeza ushabiki usiokuwa na afya. Na pengine ndio maana Wiz ametweet:
Too many dumb people in the world. God help us!

Ombi kwa baadhi ya mashabiki wa Alikiba ama tu wengine ambao wameamua kutumia nafasi hiyo kumharibia siku Wizkid: Tunajidhalilisha kwa tunachokifanya. Hakuna faida ya maneno tunayomwandikia msanii huyu kipenzi cha wengi Afrika na duniani kwa ujumla. Tufurahi kuwa tuzo inakuja Tanzania na tumpongeze Ali kwa ushindi huo, basi!

Caf yaongeza fedha za washindi katika mashindano yake

Shirikisho la soka barani Afrika Caf limeongeza kitita cha fedha zinazozawadiwa washindi katika michuano yote kuanzia mwaka 2017 kueleka 2020.

Washindi wa kombe la mataifa ya bara Afrika watapata dola milioni 4,wakati ambapo Ivory Coast ilizawadiwa dola milioni 1.5 iliposhinda taji hilo mwaka 2015.
Mshindi wa kombe la vilabu bingwa Afrika atajishindia dola milioni 2.5 badala ya dola milioni 1.5 ambazo Mamelodi Sundowns walijishindia mwezi uliopita.

Wakati huohuo fedha za mshindi wa kombe la mataifa ya bara Afrika upande wa wanawake zitaongezwa na kufikia 80,000 mwaka 2019 kutoka dola 50,000 mwaka huu.
Fedha hizo ni chache mno ikilinganishwa na zile inazopewa timu iliomaliza ya mwisho katika kombe la bara Afrika upande wa wanaume.

Uchaguzi Marekani 2016: Michelle Obama mwaka 2020?

Nani ameanza kufikiria kuhucu uchaguzi mkuu ujao nchini Marekani? Kunaye?
Naam, ingawa si wengi, kunao walioanza kufikiria kuhusu uchaguzi mkuu ujao nchini Marekani, sana wengi waliokuwa wanamuunga mkono Bi Hillary Clinton wa chama cha Democratic aliyeshindwa na Donald Trump wa Republican.
Uchaguzi mkuu hufanyika kila baada ya miaka minne, maana kwamba wanafikiria kuhusu Novemba 2020.

Aliyeanza kuzungumziwa sana ni mke wa Rais Obama, Michelle Obama, ambaye kando na kuwa mwanamke kama Bi Clinton, ameonyesha kuwa na sifa nzuri.

Ni mmoja wa waliotia juhudi sana siku za mwisho za kampeni upande wa Bi Clinton na alimshambulia sana Bw Trump.
Marekani kwa sasa ni taifa lililogawanyika kisiasa, lakini umaarufu wake unaonekana kuvuka mipaka.

Mamia tayari walijitokeza kwenye mitandao ya kijamii baada ya ushindi wa Trump kumhumiza Michelle awanie 2020.
"Mazingira mwafaka sana kwa Michelle Obama kushinda uchaguzi 2020," mmoja aliandika.
Mwingine alisema: "Michelle Obama 2020 tafadhali Michelle Obama 2020 tafadhali Michelle Obama 2020 tafadhali".

Kwa mujibu wa utafiti wa Gallup, Bi Obama anapendwa asilimia 64 na Wamarekani, kiwango kilicho juu ya Donald Trump, Hillary Clinton na hata mumewe.

Kuna tatizo moja hata hivyo, kwani Bi Obama mapema mwezi Machi alisema hana nia ya kuwania urais.
Lakini hata hivyo mambo mengi yamebadilika tangu wakati huo.

Bi Clinton, wakati wa hotuba yake baada ya kushindwa, alisema ingawa mwenyewe hakufanikiwa, anaamini siku sijazo kutakuwepo mwanamke atakayefanikiwa.

Donald Trump Story

Huyo ndio Trump.... Siyo mtu ana Vogue Tatu anajiita Bilionea... Haa haa haa...

DONALD TRUMP JOHN alizaliwa 14 Juni 1946 huko Jamaica Estates, Queens akiwa ni mtoto wa pili kwenye familia ya watoto wanne wa familia ya Mary na Fred Trump na kukulia katika Jiji la New York, Marekani.

Upande wa baba yake (Fred Trump aliyefariki mwaka 1981), alikuwa mzaliwa wa Ujerumani na mama yake (Mary) ni mzaliwa wa Scottish.
Trump alianza kusoma katika Chuo Kikuu cha Fordham kilichopo Bronx mwaka 1964, miaka miwili baadaye alihamishiwa katika Shule ya mambo ya fedha na Uchumi ya Wharton iliyopo Chuo Kikuu cha Pennsylvania ambako alihitimu shahada ya kwanza katika masuala ya uchumi mwaka 1968 kabla ya kujiunga na kufanya kazi kwenye kampuni ya familia yake iliyoitwa Elizabeth Trump & Son.

Mwaka 1971 Trump alikabidhiwa kuongoza makampuni na biashara za baba yake ambapo alipata mafanikio makubwa ndani ya muda mfupi ambayo mpaka sasa ndiye mkurugenzi wake mkuu.

Trump ambaye ni baba wa watoto watano, ni mfanyabiashara mkubwa na bilionea nchini Marekani, pia ni mtayarishaji wa vipindi vya televisheni.

Baadhi ya mali anazomiliki
---------------------

Trump Ocean Club International Hotel and Tower lililopo Panama City, Panama
Trump Tower lililopo Manhattan
Wollman Rink lililoko Central Park
Trump Taj Mahal lililoko Atlantic City, New Jersey
Turnberry Hotel, iliyoko Ayrshire, Scotland
Trump Hotel Las Vegas
Trump International Hotel & Tower ya New York
Trump International Hotel & Tower ya Chicago
Trump International Hotel ya Las Vegas
Trump International Hotel ya Waikiki Beach Walk
Trump SoHo ya New York
Trump International Hotel & Tower ya Toronto
Taasisi ya Donald J. Trump
Branding na licensing
Ndege kubwa ya Trump’s Boeing 757, maarufu kama “Trump Force One”.

Utajiri Mwaka huu (2016), Jarida maarufu la Forbes lilikadiria utajiri wa mali za Trump kuwa unafikia dola bilioni 3.7. Ameweka rekodi ya kuwa mwanasiasa mwenye utajiri mkubwa zaidi kwenye historia ya nchi hiyo.

Ikijumulishwa na thamani ya kampuni yake (brand), Trump anakadiliwa kuwa na utajiri sasa wa dola bilioni 10 na kuwa tajiri namba 324 wa dunia na wa 156 kwa nchi ya Marekani.

Trump ni Mwenyekiti na Rais wa Shirika Kibiashara la Trump (Trump Organization) lenye makao yake makuu katikati ya Mji wa Manhattan ambalo linamiliki majengo mengi marefu, hoteli, kasino, timu za gofu, ndege na miradi mbalimbali mikubwa ya maendeleo nchini Marekani na nje ya Marekani.

Ni mwanasiasa wa Chama cha Republican na anagombea urais wa Marekani kupitia chama hicho mwaka huu,
Na kwa sasa ndie aliechagulia kuwa Raisi wa 45 wa umarekani