Alibaba

mercredi 25 mai 2016

Mola tusameh New Kaswida Coming soon

New kaswida by The Light Of Peace (Nuuru Salaaam)
Mola tusameh
Coming soon !!!

http://youtu.be/NW_0MJ6rOCU?a

mardi 17 mai 2016

Katazo La Kujizuilia Kulala [Kustarehe] Na Mume Anapomuhitaji

Katazo La Kujizuilia Kulala [Kustarehe] Na Mume Anapomuhitaji

Huu dada yangu katika iymaan ni uwanja wenye hatari kubwa, na wengi miongoni mwa wanawake kwa visingizio visivyokuwa na misingi wameuingia na kugaragara ndani yake; hivyo imewawajibikia kwa hilo laana ya Malaika wa ar-Rahmaan kwa kuwa waume zao hawakuridhika nao bali walighadhibika nao.

Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu 'anhu) kwamba Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mume atakapomwita mkewe kwenye kitanda chake [kwa tendo la ndoa] na yule mke akakataa kumuitika, Malaika humlaani mpaka kupambazuke” [Imepokelewa na Al-Bukhaariy, kitabu cha Nikaah, mlango wa atakapolala mwanamke hali ya kuwa amekihama kitanda cha mumewe. Hadiyth namba 4821 na namba 4822; Muslim, kitabu cha Nikaah, mlango uharamu wa mwanamke kujizuilia [kujitenga] na kitanda cha mumewe, Hadiyth namba 2602 na Hadiyth namba 2603 na 2604.]

Hadiyth hii na nyengine kama hii dada yangu katika iymaan inabainisha na kuthibitisha kuwa mume ana haki kwa mkewe kama alivyo na haki mke kwa mumewe; na miongoni mwa hizo haki ni hii haki ya kustarehe na mkewe, na ni haramu kwa mke kujizuilia kutekeleza haki za mumewe ikiwemo hii haki ya kustarehe nae; hivyo wakati wowote ule mke akijizuilia kustarehe na mumewe hujiwajibishia laana ya Malaika [dua ya kumuombea maangamizo ya kufukuzwa kutoka kwenye Rahmah ya Allaah].

Vipi utakuwa ikiwa Malaika wa ar-Rahmaan watakuapiza? Vipi itakuwa hali yako wakati umesimama mbele ya Jabbaar Siku ya Qiyaamah, unahesabiwa amali zako na katika amali zako mbovu na chafu imo hii ya kujizuilia kustarehe na mumeo?

Mke huruhusika kujizuilia kustarehe na mumewe kama atakuwa mgonjwa au ana udhuru wenye kukubalika kishari’ah, kama vile yuko katika siku zake au amefunga Swawm ya waajib, na humuwajibikia kumuitika mumewe kama atamuhitaji wakati wowote ule utakapotoweka udhuru.

Katazo La Kufunga Sawm Ya Sunnah Bila Idhini Ya Mume

Wanawake wengi huwa wanapendelea kufunga Swawm za Sunnah; na wakati mwingine kwa pupa zao za upendaji wao wa mambo ya kheri na kutaka kujikumbia fadhila zilizofungamana na Swawm za Sunnah utawaona wanakimbilia kutekeleza Swawm za Sunnah au hata kutaka kuzitanguliza kabla ya kutimiza za waajib; wakisahau kuwa Swawm ya wajibu [fardhi] ni deni na isipotekelezwa huwa ni kosa kinyume na utekelezaji wa Swawm ya Sunnah ambayo ni jambo la mtu kujipendekeza kwa Muumba wake. 

Kwa hali hii huwapelekea wengi miongoni mwa dada zangu katika iymaan kujifungia Swawm ya Sunnah kwa kutafuta fadhila na kujikurubisha kwa Allaah bila ya kuelewa kuwa huyo wanayetaka kujikurubisha Kwake na kwa kuwapatia Fadhila Zake, Amewataka kwa kupitia Mjumbe Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wawe na hadhari ya kutofunga Swawm yoyote ile ya Sunnah bila idhini ya waume zao.

Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu 'anhu) kwamba Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Asifunge mwanamke [Swawm ya Sunnah] na huku mumewe yuko pamoja nae isipokuwa kwa idhini yake huyo mume na wala asimruhusu mtu katika nyumba ikiwa mumewe yuko isipokuwa kwa idhini yake huyo mume” [Imepokelewa na Al-Bukhaariy, kitabu cha Nikaah, mlango wa Swamw ya Sunnah ya mwanamke kwa idhini ya mumewe, Hadiyth namba 4820; na katika Kitabu cha Tafsiri Qur aan, Suuratul Qul A’uwdhu birabbil Falaq, Hadiyth namba 4823; na Muslim, katika Kitabu cha Zakaah, mlango wa atachotoa mtumishi katika mali ya tajiri wake, Hadiyth namba 1710].

Imaam An-Nawawiy amesema: Hii inakusudiwa Swawm ya Sunnah na Swawm zote zisizokuwa za nyakati maalumu, na hili katazo la uharamu liko wazi, na sababu yake ni kuwa mume ana haki ya kustarehe na mkewe katika siku zote za wiki, na haki hii ni waajib ulio wa haraka; hivyo haiwezi ikaondoka [ikaporomoka] au kudondoshwa kwa Sunnah wala kwa jambo la waajib lisilo la haraka.

Na kauli yake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): “... na huku mumewe yuko pamoja nae” na maana kama kama mume atakuwa safarini na mke yuko nyumbani, mke huyo atakuwa huru kufunga Swawm yak

lundi 16 mai 2016

Je nini hukmu ya mtu aliyefungulia funga ya Ramadhan kwa kuzini

*📘SWALI LA " 1137"📘*

*✍Je nini hukmu ya mtu aliyefungulia funga ya Ramadhan kwa kuzini❓ Je inampasa kutoa kafara❓*
🌷 🌷 🌷 🌷 🌷 🌷 🌷 🌷 🌷

         *📘 JAWABU 📘*

➡ Ni ubaya ulioje kwa mja muovu mwenye kukosa haya na heshima kwa Mola wake *ﷻ.*

➡ Vipi afungue saumu ya siku yake nzima hiyo kwa maasi makubwa na machafu kama hayo❓

➡Nini faida na malengo ya funga yake ikiwa amefanya jambo hilo❓

➡Ikiwa amefanya jambo hilo atapata dhambi kubwa,  na atakuwa ameharibu amali yake hiyo ya saumu ya siku hiyo.

➡ Na ikiwa amefanya zinaa hiyo baada ya kuwa muda wa saumu umemaliza kwa kuingia tayari wakati wa magharibi, hapo kuna ikhtilafu baina ya maulamaa kuhusu kuharibika saumu yake kwa maasi hayo.

➡ Na kuharibika saumu ya siku hiyo ni kauli yenye nguvu zaidi,  kwa kuwa ALLAAH ﷻ amekataza kuharibu amali zetu kwa maasi ya aina yoyote.

*➡ Amesema ALLAAHUﷻ,*

(يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا أَطِيعُوا اللَّهَ وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ وَلَا تُبْطِلُوا أَعْمَالَكُمْ)
[Surat Muhammad 33]

Enyi mlio amini! Mt'iini Mwenyezi Mungu, na mt'iini Mtume, wala msiviharibu vitendo vyenu.

➡ Na hata maneno ya kusimbulia pia yanaharibu malipo ya sadaka ya mja.

*Amesema ALLAAHU ﷻ*

(يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُبْطِلُوا صَدَقَاتِكُمْ بِالْمَنِّ وَالْأَذَىٰ كَالَّذِي يُنْفِقُ مَالَهُ رِئَاءَ النَّاسِ وَلَا يُؤْمِنُ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ ۖ فَمَثَلُهُ كَمَثَلِ صَفْوَانٍ عَلَيْهِ تُرَابٌ فَأَصَابَهُ وَابِلٌ فَتَرَكَهُ صَلْدًا ۖ لَا يَقْدِرُونَ عَلَىٰ شَيْءٍ مِمَّا كَسَبُوا ۗ وَاللَّهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْكَافِرِينَ)
[Surat Al-Baqara 264]

Enyi mlio amini! Msiharibu sadaka zenu kwa masimbulizi na maudhi, kama anaye toa mali yake kwa kuwaonyesha watu, wala hamuamini Mwenyezi Mungu wala Siku ya Mwisho. Basi mfano wake ni kama mfano wa jabali ambalo juu yake pana udongo, kisha likapigwa na mvua kubwa, ikaliacha tupu. Basi hawatakuwa na uweza wowote kwa walivyo chuma. Na Mwenyezi Mungu hawaongoi watu makafiri.

➡ Ikiwa kauli inaharibu sadaka,  vipi itakuwa hali katika jambo chafu zaidi kulikoni yote hayo❓❗

➡Na ALLAAH ﷻ  akakubali matendo ya waja wema tu wenye uchamungu.

➡ Amesema ALLAAHU ﷻ  baada ya kutaja kisa cha watoto wawili wa Nabii Adam A.S, ambao mmoja wao alimuua mwenzake :

(وَاتْلُ عَلَيْهِمْ نَبَأَ ابْنَيْ آدَمَ بِالْحَقِّ إِذْ قَرَّبَا قُرْبَانًا فَتُقُبِّلَ مِنْ أَحَدِهِمَا وَلَمْ يُتَقَبَّلْ مِنَ الْآخَرِ قَالَ لَأَقْتُلَنَّكَ ۖ قَالَ إِنَّمَا يَتَقَبَّلُ اللَّهُ مِنَ الْمُتَّقِينَ)
[Surat Al-Maeda 27]

Na wasomee khabari za wana wawili wa Adam kwa kweli. Walipo toa mhanga, ukakubaliwa wa mmoja wao, na wa mwengine haukukubaliwa. Akasema: Nitakuuwa. Akasema mwengine: Mwenyezi Mungu huwapokelea wachamngu.

➡ Anatakiwa kwa wajibu mtu huyo afanye yafuatayo:

1⃣Atubie kwa ALLAAHﷻ toba ya kweli.

2⃣Arudie kufunga siku hiyo kwa salama ya dini yake.

3⃣Hakuna kafara yoyote ya kutoa ikiwa amefanya zinaa hiyo baada ya kuzama jua na kuwa ni wakati wa halali kula kwa aliekuwa amefunga.

➡ Na Nakumbusha pia kuwa : " Ni haramu kisheria kwa muisilamu yoyote kufungulia saumu yake kwa kutumia kitu chochote kilicho haramishwa na ALLAAH ﷻ"

➡ Hata ikiwa atafungua kwa kuvuta sigara au kunywa pombe / ulevi,  au kumbusu mwanamke alie haramu kwake kumbusu,  au kutazama picha za Uchi,  au kutukana na mfano wa hayo.

*➡ TUNAMUOMBA ALLAAH S.W ATUFUNDISHE YALIYO NA MANUFAA NA ATUNUFAISHE KWAYO.*

📘 ALLAAHU AALAMU.

*📘JAWABU KUTOKA KWA:*
   *U / SHAABAN ALBATTAASHY.*
🌷 🌷 🌷 🌷 🌷 🌷 🌷 🌷 🌷

*👉"Ukikosa haya kwa Mola basi fanya utakayo uone atakayo kufanyia Mola"*