Alibaba

jeudi 5 janvier 2017

Mwana wa Osama bin Laden asakwa na Marekani

Marekani imesema kuwa imemuorodhesha mwana wa mwisho wa Osama Bin laden Hamza katika orodha ya magaidi wanaosakwa na taifa hilo.

Idara ya maswala ya kigeni imesema kuwa hamza Bin Laden ameanza kushiriki katika maswala ya kundi la al Qaeda ,kundi la jihad lililofadhiliwa na babake.
Amesema kuwa atalipiza kisasi mauaji ya babake yaliotekelezwa na kikosi maalum cha Marekani kwa kutekeleza mashambulizi dhidi ya Wamarekani.

Sasa atapigwa marufuku kwa kufanya biashara na raia wa Marekani huku mali yake ikipigwa tanji.

Mkuu wa kitengo cha usalama cha kundi la al-Qaeda Ibrahim al-Banna pia ameongezwa katika orodha hiyo .

Marekani imetoa kitita cha dola milioni 5 kwa mtu yeyote atakayemkamata al-Banna.

FA kuitupilia mbali kadi nyenkundu ya West Ham

Chama cha Soka cha England FA kimeitupilia mbali kadi nyekundu aliyooneshwa kiungo wa West Ham Soufiane Feghouli kwenye mchezo dhidi ya Manchester United. West Ham wakicheza pungufu ya mchezaji mmoja kwa dakika 75 walipoteza mchezo huo 2-0. Mwamuzi Mike Dean aliomtoa Feghouli kwa madai ya kumchezea rafu Phil Jones wa Man Utd.