Alibaba

lundi 31 octobre 2016

Bondia maarufu nchini, Thomas Mashali afariki

#TANZIA Bondia maarufu nchini, Thomas Mashali, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kupigwa vibaya na watu wasiojulikana maeneo ya Kimara jijini Dar es salaam.


Rais wa Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO), Yassin Abdallah athibitisha.

Manchester City : l’agent de Yaya Touré détruit encore Guardiola !


Discret depuis un mois, Dimitri Seluk, l'agent de Yaya Touré, est de nouveau sorti du bois pour adresser un nouveau tacle à l'intention de Pep Guardiola.
  
Zlatan Ibrahimovic, José Mourinho, Franck Ribéry, Yaya Touré, la liste des "ennemis" de Pep Guardiola est longue. Mais l’ennemi numéro un de l’entraîneur de Manchester City se nomme Dimitri Seluk. Un nom qui est de plus en plus cité par les médias ces derniers mois puisqu’il s’agit de l’agent de Yaya Touré. Tout a commencé en février dernier quand le représentant de l’Ivoirien a confié au cours d’un entretien accordé au Sun : « Je pense que Yaya va quitter le club. Mais avant de partir, j’espère qu’il remportera le championnat et les coupes. Ce n’est pas en rapport avec Pep Guardiola, savoir s’il l’aime bien ou pas. C’est la vie. Pep peut très bien appeler Yaya et lui parler pour lui dire "je compte sur toi" ou "je ne compte pas sur toi". Mais le milieu de terrain est resté dans le nord de l’Angleterre malgré l’arrivée de Pep Guardiola avec lequel les relations n’étaient pas franchement cordiales.

Pendant que son poulain ne joue pas (1 match cette saison), Seluk lui enchaîne les sorties médiatiques à l’encontre de l’ancien coach du FC Barcelone. La dernière en date remonte d’ailleurs au 24 septembre sur la BBC . « Guardiola ne pense qu’à lui-même, il se prend pour Dieu. Il a gagné beaucoup de titres avec le Barça, mais Yaya a aussi gagné ces titres avec le Barça. Pep pense que, comme il a tout gagné, il peut faire tout ce qu’il veut. Mais je trouve étrange la situation à Manchester City, Yaya a joué là-bas depuis tellement de temps, pareil pour Hart, Kompany... Et là, un coach qui arrive à peine, décide que ces joueurs doivent être dehors, comme des chiens » . Depuis, l’agent de Yaya Touré s’était calmé et ne s’exprimait plus dans les médias. Mais il n’a tenu qu’un peu plus d’un mois.

Seluk donne la raison du conflit avec Guardiola
Dans un entretien accordé au Mirror , Dimitri Seluk a de nouveau démonté son meilleur ennemi. Il a évoqué son choix de ne pas s’excuser auprès de Guardiola, qui réclamait lui des excuses. Il précise toutefois lui avoir envoyé des messages afin d’échanger d’homme à homme : « Pourquoi devrais-je m’excuser quand ma seule faute a été de dire la vérité ? Lorsque Yaya a été sorti de l’équipe pour la Ligue des champions, j’ai appelé Pep. Je voulais lui demander des explications, mais il ne m’a pas rappelé (...) Il faut que tout le monde se rende compte que Pep ne cherche pas d’excuses. La question est plutôt de monter le cheikh Mansour (propriétaire du club) et les fans de City contre un joueur qui adore le club ».

Puis Seluk est revenu sur le mercato :

« J’ai demandé cet été à City s’ils voulaient que Yaya parte et il m’ont dit qu’il faisait partie du projet. Il est maintenant clair que ce n’était pas la vérité. Je pense que l’idée était d’humilier Yaya et tous les joueurs qui ont fait l’histoire de Manchester City ces six dernières années. Yaya n’est pas le seul. Joe Hart et Samir Nasri ont aussi payé car ils ont de grosses personnalités (..) Pep ne veut pas travailler avec des hommes. Il veut travailler avec des joueurs qui ne sont pas jeunes parce qu’il peut les contrôler comme des enfants » . L’agent de Yaya Touré donne enfin les raisons qui expliquent la mise à l’écart et les relations tendues entre son client et Guardiola : « Je sais quel est son problème. Quand Pep a forcé Yaya a quitté Barcelone, je l’ai critiqué. C’est sa revanche. C’est personnel et non professionnel » . La rupture est plus que jamais consommée entre Guardiola et le clan Touré.

samedi 29 octobre 2016

Cristiano Ronaldo: Ashley Cole ndio beki mgumu sana kumpita

Mchezaji wa kimataifa wa timu ya taifa ya Ureno anaye chezea klabu ya Real Madrid ya Hispania Cristiano Ronaldo baada ya kufanya mahojiano na jarida la Coach Magazine na kufunguka mambo kadhaa kuhusu soka, katika interview hiyo Ronaldo kazungumza alichojifunza katika soka na kamuongelea mpinzani wake Lionel Messi pamoja na beki Ashley Cole.

*Qn.* Kitu gani kikubwa ambacho mchezo wa mpira wa miguu umekufunza?

*Ans.* Kutumia mawazo hasi ya watu wanaokupiga kukuhamasisha, kiukweli nawahitaji haters kwa sababu wamenisaidia kufanikisha kila kitu nilichofanikiwa.

*Qn.* Kuhusu Lionel Messi?

*Ans.* Kuna heshima kubwa sana kati yangu na Lionel Messi, lakini vyombo vya habari vinapenda tuonekane kama tunaupinzani mkubwa sana lakini hatuna upinzani huo, haina maana kama sisi ni marafiki wa karibu sana lakini kuna heshima kubwa kati yetu

*Qn.* Ni beki gani mgumu ambaye amekuwa akikupa wakati mgumu

*Ans.* Ashley Cole ndio beki mgumu sana kumpita niliyewahi kukutana nae.
Cole na CR7 wameshakutana kuanzia kwenye ngazi ya taifa mpaka kwenye vilabu, wakati CR7 akiwa Old Trafford na Cole akiwa Gunners na baadae The Blues.

jeudi 27 octobre 2016

Mercato sur Wayne Rooney

#MERCATO - L'inter Milan serait prêt à batailler avec les clubs chinois afin de transféré Wayne Rooney en Janvier! Pensez-vous le club intériste capable de devancer la concurrence pour attirer le capitaine des Reds Devils ?

Ballon d'or 2016

Pacha wa Klopp aduwaza wengi kikosini Liverpool

                  KIUNGO wa Liverpool, Mbrazili Lucas Leiva alibaki kwenye mshangao kwa dakika kadhaa kitu ambacho kiliwashangaza pia mashabiki wa timu hiyo waliofurika uwanja wa Anfield, walipoona watu wawili wanaofanana kweli kweli kwenye benchi la timu hiyo.

Lucas aliitwa na kocha Jurgen Klopp kupewa maelekezo wakati Liverpool ilipomenyana na Tottenham Hotspur kwenye Kombe la Ligi, lakini kwenye benchi hilo alisimama kocha msaidizi, ambaye anafanana kweli kweli na Klopp.

Kitu hicho kiliwaduwaza pia mashabiki wa Liverpool. Kocha wa viungo, Andreas Kornmayer, anafanana sana na Klopp na jambo hilo limekuwa likiwapa shida wachezaji na mashabiki wakishindwa kuwatambua kutokana na kuonekana kama ma pacha.

Kornmayer alijiunga na Liverpool akitokea Bayern Munich kwenye dirisha lililopita la usajili na ndiye mtu anayehusika na soka la kasi linalochezwa na miamba hiyo ya Anfield kwa sasa. Kornmayer ni shabiki pia wa Klopp na ndiyo maana anajaribu kujifananisha na kocha huyo katika mazingira yote.

mercredi 26 octobre 2016

Nyimbo 5 za Bongo Flava zenye ujumbe ambao si rahisi msanii wa leo kuufikiria

Muziki ni sanaa, na sanaa ni ubunifu na upekee. Tasnia ya muziki wa Bongo flava ina miaka zaidi ya 20 sasa na kiukweli tasnia hii imepiga hatua kubwa sana kimaendeleo. Ndani ya kipindi chote hicho cha miaka zaidi ya 20 tumeshuhudia uwepo wa wasanii wengi wenye vipaji maridhawa na nyimbo zenye tija na ubunifu na upekee wa hali ya juu sana ambazo pengine kama wao wasingeimba basi zisingekuwepo kabisa.

Kwa mtazamo wangu, hizi ni nyimbo 5 za Bongo Flava zenye ubunifu usio rahisi kufanyika sasa

ALIKUFA KWA NGOMA – MWANA FA

Ni nyimbo ya pekee, ubunifu na utofauti ni wa hali juu. Meseji ya nyimbo hii ni tofauti sana na nyimbo nyingine zote zenye ujumbe kuhusiana na gonjwa hatari la UKIMWI. Wasanii wengi walioimba kuhusu UKIMWI walionesha kua starehe na uasherati ndio kama chanzo pekee cha gonjwa hili lakini Hamisi Mwinjuma ‘Mwana FA’ akasema hapana hata wacha Mungu na wafuasi wa maadili wanaweza kuathirika na gonjwa hili.

NDIYO MZEE NA SIYO MZEE – PROF JAY

Mbunge wa sasa wa jimbo la Mikumi, Mheshimiwa Joseph Haule alikuwa hashikiki enzi zake. Idea za siasa zilikuwa kichwani mwake muda mrefu. Nyimbo hizi mbili ni kama Part One na Part Two. Ndiyo mzee anaomba kura kwa wananchi ambao walimuamini na kumpa uongozi na Siyo Mzee ni kipindi kingine cha uchaguzi ambacho wananchi wanaonesha kumtosa baada ya kutotimiza ahadi zake za awali. Kwa ubunifu huu sioni kama kuna msanii mwingine angeweza kuimba hizi nyimbo kama Profesa Jay asingeimba.

NJE YA BOX -NICK WA PILI

‘Nje ya kumi na nane, nje nje nje ya box, nje ya kumi na nane’ hii ni chorus ya wimbo huu maridadi kabisa wa Hip hop ulioimbwa na kijana wa Hip Hop wa kizazi cha sasa Nick wa Pili akiwashirikisha members wenzake wa Kundi la Weus, kaka yake Joh Makini na G-Nako. 44

Kama ilivyo kwa jina la wimbo hata idea yake kweli ni nje ya box. Kikawaida kwa jamii yetu ya Tanzania na Afrika kwa ujumla wanaume wengi hupenda kuwa wanawake wanaowapenda katika shida na raha na si raha peke yake. Nick aliniacha hoi katika wimbo pale aliomba Mungu amjalie demu mpenda pesa ni kitu cha tofauti sana na ameenda na kinyume na mawazo ya wengi akiwepo Mr Blue aliyeimba ‘nipende kama nilivyo’. Kwa utofauti na ubunifu nisingetegemea kusikia idea hii kutoka kwa mwanamuziki mwingine kama Nick asingeimba.

JUA NA MVUA – JAY MOE

Anajiita Jay Moe Famous. Mimi hupenda kumuita mfalme wa Sinza. Wakati sisi wengine tukichukulia jua na mvua kama mabadiiko ya hali ya hewa tu ambayo ni matokeo ya dunia kulizunguka jua, Juma Mchopanga aliwaza mbali zaidi ya kaamua kuandika wimbo na kutuuliza kipi bora kati ya jua na mvua. Mpangilio wa mashairi ukielezea hasara na faida na kila kimoja kati ya jua na mvua naamini huu ni moja katika ya wimbo wa tofauti sana katika hili game.

MAMA KUMBENA -BANANA ZORRO

‘We mama kumbena, siamini nilichosikia.. Hutaki kumuoza binti, eti kisa umemzoea..’ haha it’s funny, inachekesha sana lakini Banana Zorro alifanya huu utunzi. Kwa jamii zetu za kiAfrika mtoto wa kike kupata mume wa kumuoa ni neema sana lakini mama Kumbena alimnyima mke Banana Zorro eti kisa amemzoea Kumbena. Siju kama ni true story au ni utunzi lakini ubunifu huu na utofauti ni ngumu kidogo kwa msanii mwingine kupata concept kama hii.

NYINGINEZO

Nyimbo zingine kwa haraka haraka ambazo naona utofauti na mawazo tofauti ambayo si rahisi kwa wasanii wengine kuimba endapo wasingeimba walioimba nyimbo hizo ni kama Usiniseme ya Alikiba, Pii Pii Ya Marlaw na Bado Nipo Nipo ya Mwana FA.

Guradiola: Nasubiri msamaha kutoka kwa Yaya Toure

Mkufunzi wa Manchester City Pep Guardiola anamuhitaji kiungo wa kati Yaya Toure lakini bado anasubiri kuombwa msamaha na ajenti wa mchezaji huyo.

Raia huyo wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 33,amecheza mara moja msimu huu,katika kombe la vilabu bingwa .

Baadaye aliwachwa nje katika kinyang'anyiro hicho.Dimitri Seluk alidai kuwa Toure amefedheheshwa na uamuzi huo.
Alipoulizwa iwapo Toure angecheza katika kombe la ligi katika uwanja wa Old Trafford ,Guardiola alisema: Unajua hali ilivyo.

Raia huyo wa Uhaspania alisema mnamo mwezi Septemba kwamba Seluk lazima aombe msamaha,iwapo Toure anahitaji kucheza katika kikosi cha kwanza ,lakini ajenti huyo aliambia BBC Sport wakati huo kwamba: Ni nini ninachofaa kukiombea msamaha?Anafaa kuongea na Yaya anayemfamnyia kazi yake''.

Na huku kukiwa hakuna msamaha uliotolewa ,hakuna mapatano kati ya mkufunzi huyo na mchezaji wake.

mardi 25 octobre 2016

Wenger: Tuna fursa nzuri ya kushinda ligi

Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger amesema kuwa ana fursa nzuri ya kushinda ligi ya Uingereza msimu huu kwa mara ya kwanza tangu washinde taji hilo bila kushindwa mwaka 2004.

Akizungumza katika mkutano wa kila mwaka wa klabu hiyo,Wenger mwenye umri wa miaka 67,alisema kuwa mshindi wa taji la ligi kuu atakuwa na kati ya pointi 82 na 86 mwaka huu.

Alisema: Hii leo tuko katika nafasi nzuri zaidi ya kuwania taji la ligi ya Uingereza ikilinganishwa na miaka mitano au sita iliopita.

Ninaamini tuna timu nzuri katika ligi yenye ushindani mkubwa.
Arsenal ni wa pili katika jedwali la ligi,ikiwa ni mojwapo ya timu tatu zenye pointi 20 na wako katika nafasi ya pili kutokana na tofauti ya mabao.

Wenger anasema kuwa anafikiri kwamba anahitaji pointi 62 kutoka kwa mechi 29 zilizosalia kushinda taji .

Leicester ndio mabingwa wa taji hilo msimu uliopita.
''Baada ya mechi 9 ,tuna pointi 20,ikimaanisha kwamba ubingwa huo utaamuliwa na kati ya pointi 82 na 86'',alisema.

Aliyekuwa beki wa Brazil Carlos Alberto afariki

Aliyekuwa mchezaji mashuhuri wa timu ya Brazil Carlos Alberto ,ambaye alikuwa nahodha wa kikosi kilichoshinda kombe la dunia mwaka 1970 amefariki akiwa na umri wa mika 72.

Alifunga mojawapo ya mabao mazuri zaidi duniani katika historia ya kombe la dunia katika mechi ya fainali dhidi ya Italy mwaka 1970,baada ya kuwachenga mabeki na kufunga kupitia mkwaju mkali.

Beki wa kulia Alberto alichezeshwa mara 53 na Brazil na kushinda mataji ya nyumbani dhidi ya Fluminense na Santos ambapo alishiriki mara 400.

Alifariki mjini Rio de Janeiro kufuatia mshtuko wa moyo.

Zamalek yasema "uchawi" uliwafanya kushindwa

Mwenyekiti wa Zamalek Mortada Mansour amelaumu "uchawi na bahati mbaya" kwa kushindwa kwa timu yake mikononi mwa timu ya Afrika Kusini ya Mamelodi Sundowns katika fainali ya ligi kuu barani Afrika.

"Kulikuwa na nafasi nyingi kwetu sisi katika mechi zote, lakini mpira ulikataa kutingiza nyavu" Mansour aliongeza, baada ya kushindwa mabao 3-1 kwa jumla ya mabao.
Pia aliunga mkono kwa kocha Moamen Soliman kusalia katika nafasi yake licha ya kupoteza.

"Tuna wakufunzi wazuri na sitawafuta kazi," amesema Mansour, mbaye aliwatumia wakufunzi sita mwaka huu.

"Kocha Moamen atasalia kama mkufunzi mkuu wa Zamalek, hadi mwisho wa msimu huu."

Ballon d'or 2016 wanao baki

Mshambuliaji wa timu ya Wales Gareth Bale na mwenzake wa Real Madrid Cristiano Ronaldo wameorodheshwa kuwania taji la mchezaji bora duniani mwaka 2016 Ballon d'Or.

Wachezaji wa Manchester City Sergio Aguerro na Kevin De Bruyne, pamoja na wachezaji wa Atletico Madrid Antoine Griezmann pia wako katika orodha hiyo.

Gazeti la soka la Ufaransa limebaini orodha ya wachezaji 30 katika makundi ya wachezaji watano kila baada ya saa mbili siku yote ya Jumatatu.

Tuzo hiyo hutolewa na Ufaransa kila mwaka tangu mwaka 1956, lakini kwa kipindi cha miaka sita iliopita tuzo hiyo ilibadilika na kuwa Fifa Ballon d'Or kwa ushirikiano na shirikisho la soka duniani Fifa.
Mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi alishinda tuzo hiyo mwaka uliopita kwa mara ya tano .

*Wachezaji waliorodheshwa ni:

Sergio Aguero (Manchester City),
Pierre-Emerick Aubameyang (Borussia Dortmund),
Gareth Bale (Real Madrid),
Gianluigi Buffon (Juventus),
Cristiano Ronaldo (Real Madrid),
Kevin de Bruyne (Manchester City),
Paulo Dybala (Juventus),
Diego Godin (Atletico Madrid),
Antoine Griezmann (Atletico Madrid),
Gonzalo Higuain (Juventus).

dimanche 23 octobre 2016

WINNERS: 2016 MTV Base Africa Music Awards MAMA

ARTIST OF THE YEAR

  *Black Coffee (South Africa)
  *Diamond (Tanzania)
  *Sauti Sol (Kenya)
  *Wizkid (Nigeria)*
  *Yemi Alade (Nigeria)

BEST FEMALE

  *Josey (Ivory Coast)
  *Mz Vee (Ghana)
  *Tiwa Savage (Nigeria)
  *Vanessa Mdee (Tanzania)
  *Yemi Alade (Nigeria)*♥
WINNER

BEST BREAKTHROUGH

  *Babes Wodumo (South Africa)
  *Emtee (South Africa)
  *Falz (Nigeria)
  *Franko (Cameroon)
  *Nasty C (South Africa)
  *Nathi (South Africa)
  *Raymond (Tanzania)
  *Simi (Nigeria)
  *Tekno (Nigeria)*

BEST FRANCOPHONE

  *Franko (Cameroon)
  *J-Rio (Gabon)
  *Magasco (Cameroon)
  *Serge Beynaud (Ivory Coast)*♥
  *Toofan (Togo)

LISTENER’S CHOICE

  *Adiouza (Senegal)
  *Bebe Cool (Uganda)
  *Burna Boy (Nigeria)
  *Den G (Liberia)
  *EL (Ghana)
  *Jah Prayzah (Zimbabwe)*
  *Jay Rox (Zambia)
  *Kansoul (Kenya)
  *Kiss Daniel (Nigeria)
  *Lij Michael (Ethiopia)
  *LXG (Sierra Leone)
  *Meddy (Rwanda)
  *Messias Marioca (Mozambique)
  *Prince Kaybee (South Africa)
  *Reda Taliani (Algeria)
  *Saad Lamjarred (Morocco)
  *Sabri Mosbah (Tunisia)
  *Sidiki Diabate (Mali)
  *Tamer Hosny (Egypt)
  *The Dogg (Namibia)
  *Yamoto Band (Tanzania)

SONG OF THE YEAR IN PARTNERSHIP WITH GOOGLE

  *“Shaktibobo” – Olamide (Nigeria)
  *“Reggae Blues” – Harrysongz feat Olamide, Kcee & Iyanya, Orezi (Nigeria)
  *“My Woman, My Everything” – Patoranking feat. Wande Coal (Nigeria)*
  *“Godwin” – Korede Bello (Nigeria)
  *“Ngud” – Kwesta feat. Cassper (South Africa)
  *“Roll Up Re-Up” – Emtee feat.       Wizkid and AKA (South Africa/Nigeria)
  *“Soweto Baby” – DJ Maphorisa feat. Wizkid (South Africa/Nigeria)
  *“Baddest” – AKA feat. Burna Boy, Khuli Chana, Yanga (South Africa/Nigeria)
  *“Wololo” – Babes Wodumo feat. Mampintsha (South Africa)
  *“Coller la Petite“ – Franko (Cameroon)
  *“Unconditionally bae” – Sauti Sol feat. Alikiba (Kenya/Tanzania)

VIDEO OF THE YEAR

  *“Jump” – Anatii & Cassper feat. Nasty C (South Africa); Director: Kyle Lewis
  *“Caviar Dreams” – AL Bairre & PhFAT (South Africa); Director: Daniel Levi
  *“If I Start to Talk” – Tiwa Savage feat. Dr Sid (South Africa); Director: Clarence Peters
  *“Kisasi Kumi” – Sheeba (Uganda) – Director: Sasha Vybz
  *“Niquer Ma Vie“ – Youssoupha (Congo) – Director: Antony Abdelli & Jose Eon*

BEST HIP HOP

  *Olamide (Nigeria)
  *Kiff No Beat(Ivory Coast)
  *Ycee(Nigeria)
  *Emtee(South Africa)*♥
  *Ricky Rick(South Africa)

BEST COLLABORATION

  *Patoranking ft. Sarkodie – No Kissing
  *Sauti Sol ft. Alikiba – Unconditionally Bae
  *AkA ft. Burna Boy,Khuli Chana & Yanga – Baddest
  *Dj Maphorsia ft. Wizkid & Dj Buckz – Soweto Baby*
  *Nasty c ft. Davido & Cassper Nyovest – Juice Back Remix

BEST INTERNATIONAL ACT

  *Drake WINNER*
  *Beyonce
  *Adele
  *Future
  *Rihanna

BEST LUSOPHONE

  *NGA
  *Nelson Freitas
  *C4 Pedro*♥
  *Lizha James
  *Petro Show

BEST MALE

  *Wizkid(Nigeria)*♥
  *AKA(South Africa)
  *Patoranking(Nigeria)
  *Black Coffee(South Africa)
  *Diamond Platnumz (Tanzania)

BEST LIVE ACT

  *Flavour(Nigeria)
  *Stonebwoy(Ghana)
  *Cassper Nyovest(South Africa) WINNER*
  *Eddy Kenzo
  *Mafikizolo(South Africa)

PERSONALITY OF THE YEAR

  *Linda Ikeji
  *Wizkid
  *Caster Semenya*
  *Pearl Thusi
  *Pierre Emerick Aubameyang

BEST GROUP

  *R2Bees(Ghana)
  *Sauti Sol(Kenya) WINNER*
  *Toofan(Togo)
  *Navy Kenzo (Tanzania)
  *Mi Casa (South Africa)

BEST POP

  *Tresor
  *TiMO ODV.
  *LCNVL
  *Desmond & The Tutus
  *kyle deutsch & shekhinah WINNER*♥

samedi 22 octobre 2016

Hat-trick imempa Messi rekodi

Lionel Messi amefunga hat-trick wakati Barcelona ikiaangamiza Manchester City kwenye mchezo wa Champions League wakati Pep Guardiola akirejea kwenye klabu yake ya zamani.

City walipambana kipindi cha kwanza lakini walifanya makosa mengi ya wazi dhidi ya kikosi cha Barcelona ambacho ndani yake kilikuwa na Messi aliye rejea kutoka majeruhi.

Fernandinho alianguka ndani ya box na kumpa nafasi Messi kupachika bao la pili kabla ya Kelvin de Bruyne kupoteza mpira na kumruhusu Iniesta kumtengenezea muargentina huyo kufunga bao la pili.

Hali ilikuwa mbaya zaidi kwa wageni ambapo golikipa wao Claudio Bravo alizawadiwa kadi nyekundu kwa kudaka mpira akiwa nje ya box kisha dakika moja baadaye Messi akapachika bao jingine.
Barcelona pia walibaki 10 uwanjani kwa dakika 15 za mwisho baada ya Jeremy Mathieu ambaye aliingia kuchukua nafasi ya Gerrard Pique kuoneshwa kadi ya pili ya njano kwa kumfanyia madhambi Raheem Sterling.

Willy Caballero aliokoa mchomo wa Neymar lakini nyota huyo wa Brazil akafunga goli dakika moja baadaye kukamilisha ushindi wa magoli 4-0 wa miamba hiyo ya La Liga.

Ushindi huo uaifanya Barcelona kuendeleza ushindi kwa 100% katika Kundi C na kuendelea kuongoza kwa tofauti ya pointi tano na Manchester City.
Hiki kilikuwa ni kipigo kingine kwa Guardiola akirejea Nou Camp. Akiwa kocha wa Barcelona, aliisaidia timu hiyo kutwaa jumla ya mataji 14 lakini sasa amepoteza mara mbili dhidi ya klabu hiyo ya Hispania. Alichezea kichapo cha magoli 3-0 kwenye mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya UEFA Champions Legue akiwa kocha wa Bayern Munich.

      *Lionel Messi amefunga magoli 15 katika mechi 13 za Champions League dhidi ya timu za England.
Manchester City wamechezea kipigo kikubwa zaidi kwenye michuano ya Champions League, kwa mara ya kwanza wamefungwa magoli manne.

      *Goli la kwanza la kwenye mchezo huo lilikuwa ni goli la 100 kwa safu ya MSN kwenye mashindano yote kwa mwaka 2016.

      *Messi kwa sasa anaongoza orodha ya wafungaji katika viwanja vya nyumbani kwenye michuano ya Ulaya akiwa mefunga magoli 50.
Pep Guardiola ameruhusu magoli 9 kwenye mechi tatu za Champions League dhidi ya Barcelona tangu alivyoondoka kwa miamba hiyo ya Catalan.

      *Barcelona wamekosa mikwaju 11 ya penati kati ya 27 ambayo wamepata katika michuano yote tangu kuanza kwa msimu wa 2015-16.

vendredi 21 octobre 2016

Patrice Evra amaliza ugomvi wake na Luis Suarez

Baada ya kudumu kwa zaidi ya miaka minne, bifu la Patrice Evra na Luis Suarez sasa limefika tamati. Evra amempongeza Suarez baada ya kukabidhiwa kiatu cha dhahabu (European Golden Shoe) kwa kuibuka mfungaji bora barani Ulaya msimu wa 2015/2016

Kupitia akaunti yake ya Instagram, Evra ameandika, “Kwenye Instagram kuna neno upendo tu na hakuna neno chuki !!! Luis, wewe ni mchezaji mkubwa na bora sana, wewe ni namba tisa bora, hongera sana Luis @ luissuarez9. Naupenda sana huu mchezo !!! hahahaah.”

Wawili hao waliingia kwenye ugomvi mzito wakati walipokuwa wakicheza kwenye ligi kuu ya Uingereza huku Evra akiwa Manchester United na Suarez akichezea timu ya Liverpool.

Ugomvi wao ulianza mwaka 2011 wakati wa mechi yao iliyochezwa kwenye uwanja wa Anfield ambapo Evra alidai Suarez alimkashfu kwa maneno ya kibaguzi kitendo ambacho kilisababisha FA kumuadhibu mchezaji huyo kutocheza mechi nane na kulipa faini ya £40,000.

Wachezaji hao walithibitisha kuwa ugomvi wao haushikiki mwaka 2012 wakati wa mechi yao iliyochezwa kwenye uwanja wa Old Traford ambapo Suarez aligoma kumpatia mkono Evra.

Mpango wa kuchezea Uefa Marekani

Rais wa shirikisho la soka la Ulaya (Uefa) amesema bado anafuatilia pendekezo lake la kutaka fainali ya Kombe la Klabu Bingwa Ulaya ichezewe nje ya bara Ulaya.

Aleksander Ceferin, kutoka Slovenia, amesema atafufua tena juhudi zake za kutaka miji iwe ikituma maombi ya kuwa mwenyeji wa fainali hizo.

Amesema anaunga mkono fainali kuchezewa New York.
"Linaweza kuwa wazo tu lakini ni sharti tulizungumzie," amesema Ceferin, ambaye aliteuliwa kuwa mkuu wa Uefa mwezi jana.

Fainali zote 61 zilizochezwa awali zilichezewa Ulaya, lakini Ceferin amesema haliwezi likawa tatizo kwa mashabiki wa soka kusafiri Marekani.
Aliongeza: "Kusafiri kutoka Ureno hadi Azerbaijan kwa mfano ni karibu sawa au ni sawa na kwenda New York."
"Hii ni michuano ya Ulaya kwa hivyo hebu tulifikirie hili."

Kunaweza kuwa na tatizo la nyakati hata hivyo, ikizingatiwa mabadiliko ya saa katika mabara mbalimbali.
Mkuu huyo wa Uefa hata hivyo hana mipango ya kubadilisha wakati wa kuanza kwa fainali, ambayo kawaida huchezwa saa 19:45 BST (20:45 GM).
Fainali zimekuwa zikichezwa Jumamosi tangu 2010.
"Ukiangalia kifedha, hilo haliwezi kufaa. Lakini lazima tufikirie kuhusu masoko mengine pia. China inavutia kama soko, na Marekani pia. Soka inaanza kupata umaarufu huko pia," anasema.

mercredi 19 octobre 2016

Mwanamfalme aliyekiri kuua akatwa shingo Saudi Arabia

Mwanamfalme mmoja nchini Saudi Arabia ameuawa kutokana na makosa ya kumuua mwanamume baada ya mzozo miaka mitatu iliyopita mjini Riyadh, wizara ya mambo ya ndani nchini humo imesema.

Hukumu ya kifo ilitekelezwa dhidi ya mwanamfalme huyo Turki bin Saud al-Kabir katika mji mkuu Riyadh.

Hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa kuhusu jinsi alivyouawa, lakini watu wengi waliohukumiwa kifo huuawa kwa kukatwa shingo.
Mwanamfalme huyo ndiye mtu wa 134 kuuawa baada ya kuhukumiwa kifo nchini humo, kwa mujibu wa orodha iliyoandaliwa na shirika la habari la AFP.

Lakini huwa nadra sana kwa watu wa familia ya kifamle kuuawa, wanahabari wanasema.
Mwanamfalme huyo alikiri kumuua raia huyo mwenzake, wizara ya mambo ya ndani imesema kupitia taarifa.
Wizara hiyo imewahakikishia raia kwamba serikali imejitolea "kudumisha usalama na kutekeleza haki".

Taarifa zinasema familia ya marehemu ilikataa malipo ya kifedha kama fidia ili kutoitisha hukumu ya kifo dhidi ya mwanamfalme huyo.
Kisa kinachofahamika zaidi cha mtu wa familia ya kifalme kuuawa ni cha Faisal bin Musaid al Saud, aliyemuua mjomba wake, Mfalme Faisal, mwaka 1975.

Wengi wa wanaouawa Saudi Arabia hupatikana na makosa ya mauaji au ulanguzi wa dawa.
Watu karibu 50 hata hivyo waliuawa siku moja Januari kwa tuhuma za ugaidi, akiwemo mhubiri maarufu wa Kishia Sheikh Nimr al-Nimr.

mardi 18 octobre 2016

Barça : Piqué ne reviendra pas sur sa décision..

Gerard Piqué a confirmé qu’il quittera bel et ben la sélection espagnole après le Mondial 2018 en Russie. Le défenseur central du FC Barcelone ne reviendra pas sur sa décision, c’est ce qu’il déclaré en conférence de presse ce mardi pour la veille du match contre Manchester City en Ligue des Champions.

Lors de la trêve internationale Pique avait annoncé qu’il prendrait sa retraite internationale, après qu’une polémique ait circulé autour des manches de son maillot qui auraient été coupées volontairement pour ne pas faire paraitre le drapeau espagnol, connu pour son attachement envers la Catalogne. Sauf que c’était faux.
« La décision est définitive. Peut-être que les choses se sont précipitées en Albanie. Je ne voulais pas communiquer à ce moment-là, mais c’est sorti à chaud à cause de cette info qui était fausse », a déclaré Pique.
« J’ai lu que je me suis fait virer par Marca , AS ou la marionnette de Florentino Perez, le OK Diario . Ce ne sont ni les journaux, ni Twitter qui m’ont fait quitter la sélection. C’est une décision que j’ai prise moi, que je mérite de prendre seul après 10 ans en sélection. Et je pense que ce sera le moment. C’est comme ça. Il faut faire un pas de côté et laisser les générations suivantes prendre la place. » Un choix donc bien réfléchi et définitif.

samedi 15 octobre 2016

Majina ya wanao wania Tuzo ya (CAF)

Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania anayechezea soka ya kulipwa Ubelgiji Mbwana Ally Samatta ni miongoni mwa wachezaji 30 walioteuliwa kushindania Tuzo ya shirikisho la soka barani Afrika (CAF) ya Mchezaji Bora wa Afrika.
Mkenya Victor Wanyama ambaye kwa sasa anachezea klabu ya Tottenham pia ameteuliwa.

Kutoka DR Congo kuna Yannick Bolasie anayechezea Everton.

Orodha kamili hii hapa:

1. Riyad Mahrez (Algeria & Leicester City)
2. El Arabi Hillel Soudani (Algeria & Dinamo Zagreb)
3. Islam Slimani (Algeria & Leicester City)
4. Samuel Eto'o (Cameroon & Antalyaspor)
5. Benjamin Mounkandjo (Cameroon & Lorient)
6. Serge Aurier (Cote d'Ivoire & PSG)
7. Eric Bailly (Cote d'Ivoire & Manchester United)
8. Yao Kouasi Gervais 'Gervinho' (Cote d'Ivoire & Hebei Fortune)
9. Mohamed Salah (Egypt & Roma)
10. Mohamed El Neny (Egypt & Arsenal)
11. Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon & Dortmund)
12. Andre Ayew (Ghana & West Ham)
13. Victor Wanyama (Kenya & Tottenham)
14. William Jebor (Liberia & Wydad Athletic Club)
15. Mehdi Benatia (Morocco & Juventus)
16. Hakim Ziyech (Morocco & Ajax)
17. John Mikel Obi (Nigeria & Chelsea)
18. Kelechi Iheanacho (Nigeria & Manchester City)
19. Ahmed Musa (Nigeria & Leicester City)
20. Cedric Bakambu (DR Congo & Villareal)
21. Yannick Bolasie (DR Congo & Everton)
22. Sadio Mane (Senegal & Liverpool)
23. Kalidou Koulibaly (Senegal & Napoli)
24. Keegan Dolly (South Africa & Mamelodi Sundowns)
25. Itumeleng Khune (South Africa & Kaizer Chiefs)
26. Mbwana Samatta (Tanzania & Genk)
27. Aymen Abdennour Tunisia & Valencia)
28. Wahbi Khazri (Tunisia & Sunderland)
29. Dennis Onyango (Uganda & Mamelodi Sundowns)
30. Khama Billiat (Zimbabwe & Mamelodi Sundowns)

mardi 11 octobre 2016

BUFFON REMPORTE LE GOLDEN FOOT

Le chevronné gardien italien, Gianluigi Buffon, vient de se faire attribuer le Golden Foot. Il devance au classement des votes, Cristiano Ronaldo.

A défaut du Ballon d'Or, qu'il a raté de justesse en 2006, Gianluigi Buffon va pouvoir déposer un Golden Foot sur sa cheminée. L'expérimenté portier italien a reçu ce prix ce mardi du côté de Monte-Carlo. Il devance la star portugaise Cristiano Ronaldo au nombre des voix récoltées.

Golden Foot est une récompense qui est décernée chaque année aux joueurs qui "s'illustrent par leurs réalisations athlétiques (à la fois comme individus et comme acteurs de l'équipe) et par leur personnalité". Le prix concerne seulement les joueurs actifs d'au moins 28 ans, et ne peut être gagné qu'une fois. La première édition a eu lieu en 2003.

b:1/SuivreJuventusFC✔‎@juventusfcTrophée@gianluigibuffonvince il#GoldenFootAward 2016. Super#G1G1, numero uno.Cercle blanc de taille moyenneCercle noir de taille moyenne#FinoAllaFine17:20 - 11 Oct 2016904904 Retweets1 3281 328 j'aime

JuventusFC:
@gianluigibuffon vince il
#GoldenFoot Award 2016. Super
#G1G1 , numero uno.
#FinoAllaFine

Buffon est le troisième représentant de la Juventus à remporter ce titre honorifique. Avant lui, Alessandro Del Piero et Pavel Nedved avaient connu le même honneur. Au palmarès, le capitaine de la Nazionale succède à Samuel Eto'o. En tant que vainqueur,
Buffon a dû laisser un moule permanent en bronze de ses empreintes sur "La Promenade des Champions", en bord de mer de la cité princière.

Rihanna awakejeli wapenzi wake aliowahi kutoka nao

Hitmaker wa wimbo ‘Work’, Rihanna amewakejeli waliokuwa wapenzi wake kupitia ujumbe aliouandioka kwenye mtandao wake wa Instagram.

Rihanna ameandika kwenye mtandao huo ujumbe unaodai kuwa hakuna hata ex-wake mmoja ambaye ameoa au kufurahia mahusiano yake.

Ujumbe huo umeonekana kumlenga moja kwa moja Chris Brown ambaye tangu wameachana tayari ameshakuwa kwenye mahusiano na wanawake kadhaa akiwemo Cydney Christine, Ammika Harris, Amy Shehab, Indya Marie, Blair Pena, na wengine.

Nay wa Mitego: Ya Barakah na Stan Bakora inaweza kuwa ni kiki, utajuaje?

Nay wa Mitego amedai kuwa kinachoendelea kati ya Barakah The Prince na Stan Bakora, kinaweza kuwa kitu cha kutengeneza.

Akiongea na mtangazaji wa Kings FM, Prince Ramalove, rapper huyo amewaita wawili hao wote watoto na kwamba umri wao unawaruhusu kufanya wwanachokifanya.

“Siwezi kusimama upande wowote, hao ni watoto, wote ni wadogo mimi ni wadogo zangu,” alisema.

“So inapofika time wanagombana wataelewana tu. Hatuwezi kujua labda ni kiki, haiwezi kuwa beef kiasi hicho, inawezekana labda kiki, watu mkachukulia serious kumbe wamekaa wametengeneza,” ameongeza Nay.

Barakah ameonekana kuchukizwa na parody aliyofanya Stan ya wimbo wake Nisamehe ambapo amejipaka masizi usoni kuwa mweusi kama muimbaji huyo.
Stan amejipatia umaarufu kwa kuigiza sauti ya Nay wa Mitego.

samedi 8 octobre 2016

Cheka Kidogo

Jamaa wawili waliiba Maembe kiroba kizima wakakimbilia mochwari chumba cha kuhifadhi maiti bila yamlinz kujua, wakati wanaingia wakaangusha Embe 2 mlangoni,

mlinz alipotoka usingizin akasikia jamaa wanagawana hii yako hii yangu..... Hii yako hii yangu.... Mlinzi akakimbia kumwita doctor
njoo usikie malaika na ibilisi wanagawana roho,

walipofika tu wakasimama mlangoni wakawasikia wanasema na zile mbili zilizoko mlangon twende tukazichukue, doct kusikia hvyo akadhan wanakuja kuchukua Roho zao docta na mlinzi wakatimua mbio.

Dokta na mlinzi sio watu wa mchezo mchezo 😀😀👆🏿

Powered by Chief pro

Neymar avunja rekodi Brazil kwa damu

Superstar wa Barcelona Neymar Jr ameendeleza rekodi yake ya kupachika mabao kwenye timu yake ya taifa wakati Brazil ikiichapa Bolivia kwa bao 5-0 kwenye mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia mwaka 2018 nchini Urusi.
Neymar alianza kufunga bao la kwanza dakika ya 11 na ku-assist magoli mengine mawili katika kikosi cha Tite.

Goli lake dhidi ya Bolivia lilivunja rekodi ya Zico na sasa amekuwa mchezaji wa nne mwenye magoli mengi kwenye historia ya timu ya taifa ya Brazil akiwa ameshafunga magoli 49.
Wachezaji watatu wa juu yake ni Romario (55), Ronaldo (62) na Pele (77).

Lakini mchezo huo haukumalizika salama kwa upande wa Neymar baada ya kupigwa kiwiko na mchezaji wa Bolivia Yasman Duk.
Neymar alijikuta akichezea ‘kipepsi’ wakati alipojaribu kumpiga ‘tobo’ Duk lakini beki huyo wa Bolivia akampiga kiwiko cha usoni nyota wa klabu ya Barcelona lakini mwamuzi hakuamua tukio hilo liwe ‘faulo’

Damu nyingi ilitoka usoni kwa Neymar ambaye alishindwa kuendelea na mchezo na kupelekea kupumzishwa halafu nafasi yake ikachukuliwa na kiungo mshambuliaji wa Chelsea Willian.

Rekodi za Argentina ikiwa na Messi na bila Messi kufuzu Kombe la Dunia

Miamba ya soka la bara la Amerika ya Kusini timu ya taifa ya Argentina ililazimishwa sare ya pili mfululizo na Peru kwa kufungana magoli 2-2 ikiwa imetoka kupata matokeo kama hayo mwezi uliopita dhidi ya Venezuela.
Wakati Lionel Messi akiwa nje ya uwanja akiuguza majeraha, kocha wa Argentina Edgardo Bauza aliwaita washambuliaji wanne kwenye kikosi chake wakiongozwa na Angel Di Maria, Sergio Aguero, Paulo Dybala pamoja na Gonzalo Higuain.
Licha ya kuwa na safu kali ya washambuliaji wenye vipaji, Argentina imeshindwa kutetea ushindi wake katika mechi mbili ambapo ililazimishwa sare licha ya kuwa mbele ya wapinzani wake kwa mabao. Kwa sasa inakamata nafasi ya tano kwenye kundi lake la kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia mwaka 2018.

Argentina ikiwa na Messi na bila Messi

Nyota huyo wa Barcelona mwenye miaka 29 alishawishiwa kurejea kwenye timu ya taifa baada ya kutangaza kustaafu kufatia kuchapwa kwa mara ya pili mfululizo kwenye fainali ya Copa America na timu ya taifa ya Chile.
Rekodi ya Argentina ikiwa na Messi na ikiwa bila Messi inaonesha kuna tofauti kubwa kwasababu katika mechi 6 za Argentina bila Messi imeweza kupata ushindi kwenye mchezo mmoja pekee wakati imeweza kupata ushindi kwenye mechi tatu ambazo Messi alicheza.

jeudi 6 octobre 2016

Guardiola apiga marufuku Internet Man City

SOKA maridadi linalochezwa na Pep Guardiola linaanzia mbali. Linaanzia katika masharti magumu ambayo yanawanyima raha wachezaji, lakini hawana budi kuyafuata. Ndio maagizo.

Na sasa imebainika kuwa kocha huyo Mhispaniola amepiga marufuku matumizi ya internet katika eneo la mazoezi ya klabu hiyo.
Guardiola ameruhusu maeneo machache kwenye uwanja wa mazoezi la Manchester City, The City Football Academy kupata internet, lakini amepiga marufuku na kukata mawasiliamo katika maeneo ya ndani kwa ajili ya kuwataka wachezaji wake wazingatie zaidi maelekezo yake.

Beki wa kimataifa wa Argentina, Pablo Zabaleta amedai kwamba Guardiola ameamua kuyafanya maisha yao kuwa magumu katika matumizi ya simu au vifaa vinginevyo vinavyotumia internet kwa ajili ya kuwafanya wazingatie zaidi anachowafundisha.

“Anatulazimisha kula chakula cha asubuhi na cha mchana pamoja klabuni. Internet imekatwa na tunakaa bila ya mawasiliano na watu wa nje. Hatuwezi kutumia 3G,” alisema beki huyo wa kimataifa wa Argentina, ambaye ameendelea kupata namba chini ya Guardiola.
Zabaleta, ambaye alinunuliwa na City mwaka 2008 akitokea Espanyol ya Hispania hata hivyo, amedai kwamba anafurahishwa na mbinu za kocha huyo wa zamani wa Barcelona na Bayern Munich, aliyetua klabuni hapo msimu huu.

“Siku zote unaota ndoto za kufanya mazoezi chini ya makocha bora na leo nimepata nafasi ya kufanya kazi na mmoja kati ya makocha bora. Kwa kweli unajifunza sana, ikiwa ni pamoja na jinsi ya kuishi. Zaidi ya ufahamu wake wa soka lakini pia mapenzi yake kwa soka,” aliongeza Zabaleta.

Hii ni mara ya pili kwa Guardiola kuonyesha makali yake katika kambi ya mazoezi ya City. Julai mwaka huu wakati City wakiwa katika mazoezi ya maandalizi ya msimu beki wa kushoto wa timu hiyo, Gael Clichy alidai Guardiola alikuwa amepiga marufuku baadhi ya vyakula kwa wachezaji wake.

“Uwanjani na nje ya uwanja kila kitu kinaangaliwa kwa umakini. Kwa mfano, utawasikia makocha wakisema afya ni muhimu. Kwa Guardiola, kama uzito wako ni mkubwa basi haufanyi mazoezi na kikosi cha kwanza.
“Ni kitu ambacho unakisikia sana lakini kwangu ni mara ya kwanza kwa kocha kufanya hivyo. Kwa hiyo kuna wachezaji wachache wa kikosi cha kwanza ambao hawafanyi mazoezi na sisi,” alisema Clichy.
“Kuna juisi ameziondoa katika orodha, Pizza na vyakula vizito.

Kuna watu huwa wanadhani ‘Hilo ni jambo la kawaida na lazima iwe hivyo’ lakini ukweli ni kwamba, sio mara zote mambo yanakuwa hivi. Nimekuwa katika mpira kwa muda mrefu na najua,” aliongeza beki huyo wa kimataifa wa Ufaransa.
Mmoja kati ya wachezaji ambao alirudi katika kambi ya City akiwa amezidisha uzito ni kiungo wa kimataifa wa Ufaransa, Samir Nasri, ambaye alipelekwa katika kikosi cha vijana kufanya mazoezi.

Rais wa Ufaransa aahidi kumsaidia Kim Kardashian kukamata watu waliomvamia na kumpora

Kim Kardashian amepata mshirika wa kumsaidia kuwawinda majambazi waliomvamia na kumshikilia kwa mtutu wa bunduki Jumatatu hii na kumuibia mali za thamani kubwa.

Si mwingine, bali ni Rais wa Ufaransa, François Hollande.

Watu waliokaribu na staa huyo, wanadai kuwa baada ya tukio hilo la Paris, Hollande yeye mwenyewe anahusika katika uchunguzi na ameahidi kutoa ulinzi wa ziada kwa Kim mara nyingine akiwa nchini humo, kwa mujibu wa Pagesix.
Kutokana na tukio hilo kuteka habari za wiki hii dunia, mamlaka za Ufaransa zitaabika iwapo zitashindwa kuwakamata watu hao watano waliokuwa wamefunika sura zao na Hollande anataka watu maarufu akiwemo Kardashian, kurejea na kujihisi wako salama Paris.

Wakati huo huo, kuna taarifa kuwa anatafutwa mtu anayefanana na Kim ili kumtumia kuchanganya watu na kumhakikisha usalama zaidi kila anapotoka nje.
Pia watoto wake, North na Saint, watakuwa na timu yao ya ulinzi kwakuwa Kim ana wasiwasi kuwa wao pia wanaweza kutekwa. Kutokana na tukio hilo Kanye anadaiwa kumuonya mke wake kutomuamini mtu yeyote ndani ya timu yake.

Ukinunua Iphone 7 nchini China huna kazi!

Kampuni kadhaa nchini China zimetangaza kuwafuta kazi wafanyakazi wake watakaoingia madukani kununua simu mpya za kampuni ya Apple ambazo ni Iphone 7.

Baadhi ya kampuni hizo zimedai kuwa zimeamua kuchukua maamuzi hayo kutokana na sababu za kizalendo huku nyingine zikisema zinataka kuwafundisha wafanyakazi wake kutopenda sana raha na anasa za dunia.

Mtandao mmoja umemnukuu msemaji wa kampuni ya Nanyang Yongkang Medicine, Liu akisema lengo la agizo hilo ni kuwahamasisha pia wafanyakazi kuangalia zaidi familia na kuachana na vitu vya starehe ambavyo si vya lazima.

Hata hivyo baadhi ya watu wamesema kuwa maamuzi ya makampuni hayo huenda kukawadhuru wachina wenyewe kwa kuwa uzalishaji wa simu za Apple hufanywa katika viwanda vya kampuni ya Foxconn nchini Uchina.
Simu hizo zinauzwa kwa kiasi cha $1,047 kwa nchi ya China.