Alibaba

vendredi 23 décembre 2016

GRANERO : "MOURINHO EST ADORABLE, FLORENTINO PÉREZ EST UN HOMME INSPIRANT"

Esteban Granero garde des bons souvenirs de son passage au Real Madrid et notamment de José Mourinho et Florentino Pérez.
Formé au Real Madrid, Esteban Granero a évolué avec l'équipe première des Merengue entre 2009 et 2012 avant de s'envoler vers d'autres cieux afin de trouver un peu plus de temps de jeu. Le milieu de terrain espagnol de 29 ans a connu une période dominée par le FC Barcelone mais a tout de même remporté la Liga avec son club formateur. Dans un entretien accordé à EFE Radio, il est revenu sur son passage au Real Madrid et a encensé José Mourinho qui selon lui n'est pas la même personne en réalité que face aux médias.

" José Mourinho est adorable, il crie quand il doit le faire. Il est très intelligent et utilise les médias comme filtre ou pour lancer des messages, toujours dans l'optique que ses joueurs et son équipe en soient bénéficiaires. Cela lui a causé beaucoup de problèmes, à lui, à sa famille et à son image. Florentino Pérez est un homme inspirant. Il ne s'arrête pas de travailler. Le président, qui a toujours été ici, est très apprécié. Beaucoup de présidents du Real Madrid sont passés et aucun n'est comme lui. De mon point de vue. J'ai toujours été pour le Real Madrid et il a procuré du plaisir. Pas seulement de la façon dont il fait son travail mais aussi comment il traite ses employés ", a déclaré Esteban Granero .

L'ancien milieu de terrain du Real Madrid a évoqué la domination du Barça à cette époque : " Le FC Barcelone a fait un grand saut avec Pep Guardiola et a formé cette équipe qui n'arrêtait pas de gagner. Jusqu'à ce qu'en 2011 nous gagnions la Liga. Cela a été comme le premier revers qu'a connu cette équipe. Nous avons remporté le championnat avec José Mourinho et avec 100 points. Nous avons mis le Real Madrid à sa place et Barcelone à la sienne".

Mke wa Mugabe aamrishwa kurudisha nyumba tatu

Jaji mmoja nchini Zimbawe amemwaagiza mke wa rais Robert Mugabe, Grace Mugabe, kurudisha nyumba tatu alizompokonya mfanyabiashara nmoja raia wa Lebanon, kufuatia zabuni ya pete ya almasi ya gharama ya dola milioni 1.35.
Kulingana na kesi iliyowasilishwa na mfanyabiashara huyo, Bi Mugabe alitaka kurudishiwa pesa baada ya pete hiyo ya almasi iliyonunuliwa mjini Dubai. ilipowasilishwa kwake baada ya kutengenezwa na mtu tofauti.

Wakati Jamal Ahmed alishindwa kulipa pesa hizo kwa akaunti mjini Dubai, na licha ya yeye kusema kuwa pesa hizo zilitumwa kupitia kwa benki moja ya Zimbabwe, Bi Mugabe alichukua kwa nguvu nyumba zake tatu mwezi Oktoba.
Jaji Clement Phiri alisema kuwa Bi Mugabe pia ni lazima ahakikishe kuwa wafanyakazi wote waliokuwa wakihudumu kwenye nyumba hizo wamerudishwa kazini.
Pete hiyo ilikuwa ni kama zawadi kwa mke wa rais Mugabe, Bi Grace, kuadhimisha miaka 20 ya ndoa.

Mshukiwa wa shambulizi la Berlin auawa Italia

Mtu aliyeendesha shambulizi kwenyr soko mjini Berlin Anis Amri, ameuawa kwa kupigwa risasi na polisi mjini Milan nchini Italia.
Mtu huyo alikuwa amewafyatulia polisi risasi walipomaka awaonyeshe kitambulisho chake walipokuwa wakipiga doria eneola Sesto San Giovani. mapema siku ya Ijumaa.
Polisi mmoja aliuawa wakati wa ufyatuaji huo wa risasi,

Ujerumani imekuwa kwenye tahadhari kubwa tangu lifanyike shambulizi lililowaua watu 49.
Wakati huo huo polisi wamewakamata watu wawili katika mji wa Oberhausen baada ya kushukiwa kupanga mashambulizi.

Alama za vidole za mtu aliyeuawa vinafanana na alama za mshukiwa raia wa Tunisia ambaye aliendesha shambulizi la bomu la lori mjini Berlin siku ya Jumatatu na kuwaua watu 12.

Diafra Sakho kukosa michuano ya mataifa bingwa barani Afrika

Mchezaji wa klabu ya West Ham na timu ya taifa ya Senegal, Diafra Sakho hatacheza katika mechi ya kuwania kombe la mataifa bingwa barani Afrika baada ya kuripotiwa kuwa hatacheza kwa kipindi cha wiki nane zaidi kutokana na jeraha.
Klabu ya West Ham ilitoa taarifa tarehe 30 mwezi Novemba kuwa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 26 hatacheza kwa wiki sita ikimaanisha kuwa hatarejea uwanjani hadi kati kati ya mwezi wa Januari.

Lakini koacha wa West Ham Slaven Bilic, amesema kuwa Sakho huenda asicheze kwa kipindi cha wiki nane na huenda sasa akarejea kati kati ya mwezi Februari.

Vanessa Mdee kubadili dini sababu ya Jux?

Iko wazi, kwamba wapenzi wengi wa dini tofauti, huamua kuchagua njia moja iwapo lengo lao ni kuja kufunga ndoa na kuwa mke na mume, kihalali.

Vipi kwa upande wa Vanessa Mdee ambaye ni mkrito, na Juma Jux ambaye ni muislamu, mustakabali wao ni upi iwapo wanakoelekea ndio huko ambako ndugu na jamaa zao wanapenda wafike yaani ndoani?
Nani yuko radhi kubadili dini yake? Swali hilo lilitupiwa kwa Vanessa Mdee na watangazaji wa kipindi cha The Base cha ITV.


“No, sina mipango yoyote ya kubadilisha dini,” jibu la Vee Money lilikuwa fupi kama hivyo.
There you have it!

Chelsea yathibitisha kumuuza Oscar kwenye ligi ya China

Klabu ya soka ya Chelsea ya Uingereza imethibitisha kumuuza kiungo wao Oscar dos Santos kwenye timu ya Shanghai SIPG ya China.
Kupitia mtandao wa Twitter wa klabu hiyo umeandika, “Thank you, @oscar8 and good luck for the future.”

Mchezaji huyo alikuwa anawindwa kwa muda mrefu na timu hiyo ambayo iliahidi kulipa ada ya uhamisho wa paundi milioni 52 na kumlipa mshahara wa paundi laki nne kwa wiki na kumfanya awe mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa zaidi duniani.


Naye mchezaji wa Boca Juniors ya Argentina anatazamiwa kujiunga na ligi hiyo ya China kwenye timu ya Shangahi Shenhua.


Leicester yashinda tuzo la klabu bora ya mwaka Uingereza

Klabu ya soka ya Leicester imeshinda tuzo ya timu bora ya mwaka kwa kuwashangaza wengi waliposhinda ligi ya Uingereza.
The Foxes kama inavyojiita ilishinda tuzo ya timu bora ya mwaka na mkufunzi wake Claudio Ranieri alitangazwa kuwa kocha bora baada ya kuisaidia timu hiyo kushinda taji hilo.
Leicester ilianza kampeni ya kushinda taji hilo bila wengi kutarajia baada ya kushushwa katika ligi ya Uingereza mwaka 2014-15.
Walipoteza mechi tatu pekee katika msimu wa 2015-16 na wamefuzu kucheza kombe la vilabu bingwa Ulaya na kuendelea hadi raundi za muondoano.
Mwanzoni mwa mwezi Aprili, Leicester ilikuwa pointi saba juu katika jedwali la ligi ya Uingereza .
Mwaka mmoja kabla ,walikuwa chini ya jedwali hilo pointi saba pekee juu ya timu ambazo zilishushwa daraja.
Mwogeleaji wa Marekani Michael Phelps alishinda tuzo la mwanariadha bora wa olimpiki baada ya kushinda medali 23 za dhahabu.