Alibaba

mercredi 31 juillet 2013

Des femmes déshabillées par la garde républicaine à Brazzaville


 
Depuis lundi, ces images créent l’indignation au Congo-Brazzaville : dans une forêt du centre-ville des femmes sont humiliées par des éléments de la garde républicaine, qui les forcent à se déshabiller tout en les filmant hilares. Selon nos Observateurs, ce corps d’élite congolais bénéficierait d’une totale impunité.
 
D’après plusieurs témoignages recoupés par FRANCE 24, la scène se serait déroulée le 23 juillet dans la forêt Patte d’Oie, un lieu réputé pour abriter essentiellement des prostituéesoriginaires de la République démocratique du Congo. La forêt est située à quelques mètres du Palais du Parlement où s’ouvrait le même jour le Forum économique Forbes consacré à l’émergence des classes moyennes en Afrique.
 
Cinq femmes présentes dans la forêt sont forcées par les gardes de se déshabiller entièrement.
 
Sur la vidéo publiée par le site Brazzanews, les cinq femmes sont forcées de se déshabiller devant une patrouille d’éléments de la garde républicaine, reconnaissables à leurs bérets violets traditionnels. La vidéo est prise d’un téléphone portable par un des gardes assistant à la scène. À plusieurs reprises un des gardes installés dans une voiture ordonne "Madame, enlevez tout, rapidement !". Une fois qu’elles sont totalement nues, on leur lance "vous voyez à quoi vous ressemblez, vous n’avez pas honte". Puis elles sont forcées de marcher dans de grandes herbes urticantes. À la fin de la vidéo, les cinq femmes sont autorisées à se rhabiller et reçoivent l’ordre de ne plus jamais revenir dans cette forêt.
 
Postée sur Youtube puis Dailymotion, la vidéo a depuis été censurée par les deux sites de partage de vidéo. FRANCE 24, qui a récupéré les images, a choisi de n’en diffuser que des captures d’écran.
 
Les gardes républicains leurs demandent ensuite de passer par les grandes herbes urticantes en guise de punition.
 
Contacté par FRANCE 24, le délégué en charge de la presse de la présidence du Congo-Brazzaville, André Ondélé, a affirmé que la présidence n’avait pas eu connaissance de cette scène. FRANCE 24 lui a transmis les images et publiera la réaction lorsque celle-ci nous parviendra.
 
Les femmes sont autorisées à se rhabiller avant d'être invitées à quitter les lieux par les gardes. 

"Ces femmes sont probablement des prostituées de RDC (…) la garde a voulu leur dire qu’elle ne sont pas les bienvenues"

lundi 22 juillet 2013

WEMA AJINAJISI MWEZI MTUKUFU

Stori: Shakoor Jongo na Musa Mateja
WAKATI zilipendwa wake Nasibu Abdul ‘Diamond’ akifuturisha kila kukicha, Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu ametupiwa madongo mazito akiambiwa amejinajisi Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kufuatia picha zake  zisizopendeza kipindi cha mfungo kutumbukizwa mtandaoni, Ijumaa Wikienda linakupa habari kamili.
Moja ya picha alizotupia Wema Sepetu.
Julai 19, mwaka huu (Chungu cha Kumi) picha za Wema ambaye ni staa wa filamu za Bongo na Miss Tanzania mwaka 2006/07 ziliingizwwa mtandaoni akiwa katika mapozi mbalimbali yenye ‘kuuchefua’ mwezi kama mtu atakumbana nazo.
Picha moja ilimuonesha mrembo huyo akiwa ‘klozidi’ na meneja wake, Martin Kadinda. Wanaonekana wamekumbatiana.
Picha nyingine inamuonesha Wema akipiga mbizi kwenye swimming pool moja ambayo haikufafanuliwa ni wapi nchini Tanzania.
Mbali na picha hizo mbili, nyingine ilimuonesha mlimbwende huyo akiwa katika gauni jepesi kiasi cha kuweza kuonesha ‘nido’ zake.
Diamond (wa pili kulia) akifuturu na watu mbalimbali wakiwemo mastaa wa Bongo.
WACHANGIAJI SASA
“Dah! Nimemshangaa sana Wema, amekubali vipi kuweka picha zake kwenye neti katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, maana hazistahili kabisa,” alisema mmoja wa wasomaji wetu ambaye  alibahatika kuziona picha hizo.
Msomaji huyo aliendelea kusema kwamba kwa uzoefu wake kipindi hiki cha mfungo ‘blogi’ nyingi (akimaanisha mitandao) zinaweka picha za watu wakifuturu, wengine wakifuturisha, alimshangaa Wema ni Muislamu safi lakini kumbe si mfuataji wa maadili ya imani.
“Wema amejinajisi tu kwa Mwezi wa Ramadhani, picha zilizoko kwenye mtandao siyo kabisa, ikiwezekana azitoe ataziweka tena baada ya mfungo kwisha,” alimalizia kusema mtu huyo.
Wachangiaji wengine hawakuwa mbali sana na wa kwanza, nao walionesha kukerwa kwao na jinsi picha hizo zilivyotupiwa mtandaoni katika kipindi hiki cha toba na kusema funga ya Wema ni bure.
Diamond katika vazi la kanzu.
AWALI YA YOTE
Kabla ya kumsaka Wema, Ijumaa Wikienda lilijiridhisha kwamba, mtandao uliotumika kutupiwa picha hizo zilizowakera baadhi ya watu si wa Wema, bali ni wa meneja wake, Martin  Kadinda.
 
WIKIENDA LAANZA NA WEMA
Licha ya kutambua hilo, Jumamosi iliyopita, Ijumaa Wikienda lilianza kwa kumsaka Wema kwa njia ya simu ya kiganjani ili kumuuliza kama ana amani moyoni kufuatia picha zake zilizotafsiriwa kuwa ni za kuinajisi swaumu yake kutumbukizwa mtandaoni, lakini simu yake haikupatikana hewani.
Wema katika vazi la hijabu.
KADINDA APATIKANA, HEBU MSIKIE
Baada ya kumkosa Wema ndipo Ijumaa Wikienda lilipomsaka Kadinda ili kuisikia kauli yake hasa ikizingatiwa kuwa, mtandao uliotumika ni wa kwake.
“Hivi ngoja nikuulize, mtu akifunga haruhusiwi kuingiza, kuangalia picha mtandaoni au haruhusiwi kuogelea? Isitoshe picha hizo zilipigwa kabla ya Mwezi wa Ramadhani ilikuwa siku ya vunja jungu, siku moja kabla ya kuanza kwa Ramadhani,” alisema Kadinda.
Wikienda: Lakini hata kama ilikuwa vunja jungu, sasa ni kwa nini umeziweka picha zile kipindi hiki?
Kadinda: Kwani kuna tatizo?
Wikienda: Wee huoni kama umeinajisi funga ya mwenzako katika mwezi huu?
Kadinda: Mimi sijaona tatizo.
Wikienda: Kwa nini usingesubiri mfungo ukaisha ndipo utupie zile picha? Maana kwa sasa wengi wanatupia picha za kufuturu au kufuturisha.
Kadinda: Tatizo liko wapi kwani?
Ijumaa Wikienda liliamini Kadinda hakuwa tayari kukiri, likaachana naye.

MASTAA WAGOMBEA FUTARI KWA DIAMOND
Wakati Wema yakimkuta hayo, naye Diamond, Ijumaa iliyopita aliendelea na kufanya suna kwa kufuturisha watu mbalimbali wakiwemo mastaa wa Bongo.
Wengine walioalikwa kufuturu ni watoto yatima kutoka vituo vinne vya jijini Dar.
Diamond alilifanya zoezi hilo nyumbani kwake, Sinza-Mori, Dar ambako anaishi na mama yake mzazi, Sanura Kasim ‘Sandra’.
Baadhi ya mastaa waliohudhuria mwaliko huo wa futari walionekana kugombea kutokana na watu kuwa wengi huku futari ikiwa kidogo kuliko wafungaji.
“Watu ni wengi lakini kwa mtazamo wangu naona kama futari yenyewe ni ndogo,” alisema memba wa Tip Top Connection, Hamad Ally ‘Madee’.

DIAMOND AGAWA ‘WEKUNDU’
Baada ya kumaliza kufuturu na watu kutoa shukurani zao kwa Diamond huku wengine wakimpongeza kwa hatua hiyo, ghafla msanii huyo aligeuka pedeshee kwa kutoa noti za shilingi elfu kumikumi ‘wekundu’ kwa kila mtoto yatima aliyehudhuria futari hiyo.
“Unajua kwenye hii futari ukiacha marafiki, ndugu na jamaa, kuna watoto yatima kutoka vituo vinne na kila kituo wamekuja watoto kumi na ndiyo hao peke yao nimewapa fedha kama sadaka yangu,” alisema Diamond alipoulizwa na waandishi mara baada ya kumaliza zoezi hilo.

APONDWA, ADAIWA SI MSAFI SANA
Licha ya futari hiyo ya kuwepo yatima, lakini wapo watu waliosema msanii huyo si msafi sana kwa vile siku kadhaa nyuma, alipiga picha akifuturu na demu wake (hawara), Peniel Mungilwa ‘Penny’ jambo walilolisema halina baraka Kiislamu kwa kuwa si mke wake wa ndoa.

APINGWA KUMWAGA PESA HADHARANI
Wakati wengine wakiponda usafi wa msanii huyo kwa kufuturu na kimada, wapo waliohoji kama Kuran inakubaliana mtu kutoa sadaka ya fedha kwa wasiojiweza huku wengine wakishuhudia (kama alivyofanya kwa yatima).
“Uislamu hausemi hivi. Uislamu unasema hivi, ukiwa unatoa sadaka kwa yatima au wasiojiweza, mtu mwingine asione ndiyo baraka zako zipo hapo,” alisikika akisema mwalikwa mmoja.

vendredi 19 juillet 2013

DEMU WA PREZZO ACHANWA KWA KUTUMIA PICHA ZA UTUPU KUTAFUTA UMAARUFU !


Na Mwandishi Wetu
MDADA wa Kenya anayetajwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamuziki Jackson Makini ‘Prezzo’, Huddah Monroe ‘The Boss Lady’ amechanwa kuwa anatumia nguvu kubwa kujipatia umaarufu kwa kupiga picha chafu kisha kuzisambaza mtandaoni.
Huddah Monroe ‘The Boss Lady’ katika pozi la utupu.
Mtandao mmoja wa nchini humo umeeleza kuwa, kuna watu wengi akiwemo Huddah ambao badala ya kufanya mambo yenye faida kwa jamii na hatimaye kuwa maarufu, wao hutumia njia batili ikiwemo hiyo ya kupiga picha za utupu.
Huddah katika pozi nyinine tata.
“Miaka ya nyuma ili mtu ajulikane zaidi kwenye jamii lazima afanye kazi nzuri lakini kipindi hiki ni tofauti. Wengi hasa wadada wanajipatia umaarufu kwa kuposti picha zao wakiwa watupu kwenye mitandao ya kijamii. Mfano Huddah na wengine kama vile Kim Kardashian wa Marekani,” uliandika mtandao huo.
Huddah akiwa na Prezzo.

WEMA JELA INAMUITA !

Na Waandishi Wetu
KUNA kila dalili kwamba mrembo anayetamba kwenye filamu za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ au Madam jela inamwita na anatakiwa kufanya maombi ili kukwepa kifungo maishani mwake.
Hali hiyo inafuatia staa huyo kupandishwa kizimbani kwa mara nyingine tena Jumatano iliyopita, pale alipopanda katika Mahakama ya Mwanzo ya Kawe jijini Dar kwa kosa la kumpiga na kumtukana matusi ya nguoni meneja wa hoteli moja iliyopo Kawe Beach jijini Dar, Godluck Kayumbu.
Kabla ya  kupandishwa  kwa ‘pilato’,  staa huyo anayemiliki Kampuni ya Endless Fame alikuwa akisakwa na askari kwa siku kadhaa na kufanikiwa kuwapiga chenga za hapa na pale.

ANASWA AKIFUTURU
Hata hivyo, mbio zake ziliishia ukingoni Julai 16, mwaka huu, alipokamatwa saa mbili usiku akiwa anafuturu na wageni wake nyumbani kwake, Kijitonyama Dar.
MTITI KIDOGO
Askari saba walifika nyumbani kwake wakiwa ndani ya Land Rover ‘difenda’ kwa ajili ya kumkamata, hata hivyo walipata upinzani kidogo kutoka kwa mlinzi wa staa huyo ambaye alikuwa akizuia bosi wake asikamatwe ambapo ilibidi askari hao wakaze msuli na kutuliza mtiti uliokuwa ukitaka kutokea.
WEMA AGEUKA MBOGO, ALALA SELO
Baada askari kumfikia staa huyo, walimtaka kwenda naye kituo cha polisi kwa kutumia difenda walilofika nalo ambapo Wema alipinga na kugeuka mbogo kwa kudai kwamba hawezi kupanda difenda kutokana na hadhi yake.
Pamoja na askari kutaka kumpandisha kwa nguvu, staa huyo alipinga na ikakubaliwa apande gari lake aina ya Audi Q7 huku akiwa chini ya ulinzi wa askari.
Safari ikaishia Kituo cha Polisi cha Kawe ambako staa huyo aliandikisha maelezo na baada ya zoezi hilo akatupwa selo.

WEMA HAUOZI
Kama lilivyo jina lake, wema hauozi, staa huyo alipata dhamana saa 5 za usiku baada ya kudhaminiwa na msanii  mwenzake wa filamu, Kajala Masanja.
Kajala aliwahi kutolewa katika mdomo wa jela na Wema siku za nyuma baada ya kukutwa na hatia na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar alipotakiwa kulipa faini ya shilingi milioni 13 au kwenda jela, Wema alimlipia kiasi hicho cha fedha.
WAPAMBE FULL SHANGWE
Wapambe wa Wema waliokuwa wamejazana nje ya kituo hicho cha polisi, walilipuka kwa shangwe baada ya bosi wao kuchomolewa kutoka selo. Staa huyo aliondoka na gari lake lililokuwa likiendeshwa na meneja wa kampuni yake aitwaye Petit Man.

ATEMBEZWA KWA MIGUU
Julai 17, asubuhi Wema alirudi kituoni hapo na kuwekwa chini ya ulinzi kwa ajili ya kupelekwa mahakamani kusomewa mashitaka yake.
Katika hatua ya kushangaza, staa huyo alitembezwa kwa miguu umbali wa mita 200 kutoka kituo cha polisi hadi Mahakama ya Mwanzo ya Kawe.
APANDISHWA KIZIMBANI
Wema alipandishwa kizimbani na kusomewa mashitaka yake na Mh. Hakimu, Bernice Ikanda na kudaiwa kufanya vurugu, kushambulia kwa kumpiga makofi na kumtukana Kayumbu.
Mbele ya hakimu, Wema alikana mashitaka na hakimu aliiahirisha kesi hiyo mpaka Julai 31, mwaka huu.

IKO SIKU WEMA ATAFUNGWA GEREZANI
Kumbukumbu kutoka kwenye makabrasha yetu zinaonesha kuwa, mrembo huyo ni mtu wa majanga, mara kwa mara amekuwa akifikishwa polisi na mahakamani kutokana na ugomvi.
ALIVUNJA KIOO CHA GARI LA KANUMBA
Mwaka 2009, Wema alidakwa na Polisi Kituo cha Magomeni na baadaye kupandishwa katika Mahakama ya Kinondoni, Dar kwa Hakimu Emilius Mchalu kwa kosa la kuvunja kioo cha gari la aliyekuwa staa wa filamu za Kibongo, Marehemu Steven Kanumba chenye thamani ya shilingi milioni moja. Hata hivyo, Kanumba aliifuta kesi hiyo.

ALIMTISHIA MAISHA BOB JUNIOR
Kama vile haitoshi, mwaka 2011, Wema huyohuyo alikamatwa na Polisi wa Oysterbay jijini Dar na kufikishwa Mahakama ya Mwanzo, Kinondoni kwa kosa la kumtusi na kumtishia maisha mwanamuziki wa Bongo Fleva, Rahem Nanji ‘Bob Junior’.
Katika kesi hiyo, Hakimu Mariam Masamalo alimtia hatiani Wema kwenda jela miezi sita au kulipa faini ya shilingi 40,000 ambapo alilipa fedha hizo.
ALIMTUSI REHEMA FABIAN
Aidha, mara baada ya Wema kuachiwa huru mahakamani hapo alikamatwa tena na polisi kwa kile kilichodaiwa kumtusi Miss Kiswahili 2008, Rehema Fabian. Wema alipelekwa Kituo cha Polisi cha Oysterbay jijini Dar kwa maelezo zaidi.

ALIMTUKANA MSANII
Aidha, Wema amewahi kulala kituo cha Polisi Oysterbay, Dar akiwa na mashoga zake, Kajala na Dida kwa madai ya kumshambulia mwigizaji mmoja wa Bongo, kwenye pati iliyofanyika Ukumbi wa Bwalo la Polisi, Oysterbay, Dar. Kesi hiyo iliisha kwa mazungumzo nje ya polisi.
Imeandikwa na Musa Mateja, Mwaija Salum, Makongoro Oging’ na Shakoor Jongo.

mercredi 17 juillet 2013

SERIKALII YA BONGO YATAKIWA KULIFUNGIA MAISHA KUNDI LA BAIKOKO! NA MAKUNDI YOTE YA AINA HII

Mmoja wa cheza show kama anavyoonekan akiwa akimchezea uchi mteja.
 
Mcheza show wa kundi la Bikoko akionesha manjonjo yake mbele ya wateja.
 
Laanakhum kama hii haikubariki Serikali inatakiwa kuyasambaratisha makundi kama haya ili kukomesha uposhwaji wa maadili ya mtanzania na kushawishi vitendo vya ngono.
 
 

Serikali ya Tanzania kupita wizara ya michezo utamaduni imeshauriwa kuyasambatisha makundi yote yanayojihusicha na kucheza uchi kwenye kumbi za burudani ili kukomesha hamasa  za ngono na udhalilishaji.

 Wakiongea na Xdeejayz baadhi ya wanchi waliyalalamikia makundi ya Khanga Moja " Laki Si pesa, Baikoko, Kitu Tigo K nyumbani kwako,Tako Camp lililopo Mwanyamala mchangaji watu hao walisema kushindwa kwa Serikali kuyazuia makundi hayo ni kuonesha udhaifu kwani yamekuwa yakidhalilisha heshima ya mwanamke wa Tanzania pamoja na kihamisha ngono.


DIAMOND AFUTURU NA KIMADA !

HIVI karibuni mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’ amenaswa akifuturu na hawara yake, Penniel Mungilwa ‘Penny’, kitendo ambacho kimewashangaza wengi na baadhi kufikia hatua ya kumponda kuwa anakwenda kinyume na Uislam.
Tukio hilo lilijiri nyumbani kwa Diamond maeneo ya Sinza- Mori jijini Dar ambapo mbali na mastaa hao, pia walikuwepo waumini wengine wa dini hiyo walioalikwa katika chakula hicho kitakatifu.

Waumini wamponda
Wakizungumza na gazeti hili mara baada ya kumuona Penny ambaye ni demu wa Diamond akiwa eneo hilo, baadhi ya waumini walisema walishangazwa na uwepo wake kwani sheria ya dini ya Kiislam hairuhusu kuwa karibu na kimada hasa katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Walisema, Diamond hatakiwi kuwa karibu na Penny si kwa kipindi hiki tu bali hata baada, mpaka pale ambapo atatoa mahari na kuozeshwa kwa kufuata misingi ya dini ya Kiislam.
“Huyu kijana kafanya jambo zuri la kuwafuturisha wenzake ila amekosea kumualika yule mwanamke wake, yule kwake ni kimada na kwa sheria za dini yetu huruhusiwi kabisa kumkaribia, sasa ona wanafuturu pamoja na wanashikanashikana, ile siyo sawa,” alisema muumini mmoja aliyeomba hifadhi ya jina lake.
Mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Swaleh alisema: “Diamond anatakiwa aambiwe kuwa anafanya makosa sana kuwa karibu na yule Penny.
“Kihalali kwanza anatakiwa amsilimishe kisha amlipie mahari ndipo amuoe lakini kinyume na hapo atakuwa anaishi na hawara na kuwa naye karibu ni kujichumia dhambi anazoweza kuziepuka.”

Mashehe nao wacharuka
Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti, baadhi ya mashehe wenye heshima kubwa Tanzania nao walionesha kukerwa na kitendo alichokifanya Diamond na kusema kinakiuka maadili ya dini yao.
Walisema, mwanamke ambaye hajaolewa anayeishi au kuwa karibu na mwanaume na wakati mwingine kuzini, huyo ni kimada na hana nafasi kwenye Uislam.

Shehe Khamisi Mataka
Huyu ni Katibu Mkuu wa Taasisi ya Mashehe na Wanazuoni Tanzania anasema: “Lengo la swaumu ni kumfanya mtu kuwa Mchamungu na Mchamungu ni yule anayefanya yale aliyoamrishwa na Mwenyezi Mungu na kuacha aliyokatazwa.
“Katika Uislam kuwa na hawara inakatazwa, si kwa kipindi hiki tu cha Mwezi Mtukufu bali hata baada. Kwa hiyo kufuturu na hawara ni kinyume na Uislam na unapata dhambi.”

Maalim Hassan Yahya
Ni Mnajimu maarufu nchini. Yeye anasema kuwa, hawara hakubaliki kidini hivyo hatakiwi kupika futari wala kuwa naye karibu kwa namna yoyote, kufanya hivyo ni kwenda kinyume na taratibu za funga na maadili ya Uislam.

Shekh Alhad Musa Salum
Huyu ni Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam. Kuhusiana na hili la Diamond la kufuturu na Penny anasema kuwa, uhawara hauruhusiwi katika Uislam na wanaoendekeza hilo waache mara moja ili waweze kupata radhi za Mwenyezi Mungu.
Shehe Mkuu wa Tanzania, Mufti Shaaban Simba hivi karibuni aliwasihi Waislam kutimiza nguzo hiyo muhimu ya Uislam na kuwataka wahakikishe wanafuata sheria na taratibu zilizowekwa ili waweze kufikia lengo la kufunga

Source:GLP

vendredi 12 juillet 2013